TITAN
JF-Expert Member
- Dec 13, 2010
- 308
- 47
JK ni mwanaume. Amefanya kile ambacho hata nyerere alikuwa hawezi kukiruhusu wala kukivumilia. Enzi za Nyerere leo hii watu kama Slaa wangekuwa ukimbizini. Kikwete anasoma alama za nyakati. anataka kujenga Tanzania ya watu majasiri wanaoamua nani awe kiongozi wao na nani asiwe.
Wengi sana na hasa ndani ya ccm hili linawauma sana. Wanapigwa mawe. Wanazomewa. wanafanywa chochote na wananchi, lakini Jk hana habari. Katulia tuli na Salma. Kikwete ni mwanamapinduzi kwa maana ya kuruhusu wananchi wajiamulie aina ya watu wanaotaka kuongozwa nao.
JK nakuomba sana. Popote pale ulipo, ruhusu maandamano, ruhusu watu kuzungumza na kukusanyika, agiza vyombo vya usalama kulinda raia bila ubaguzi wa kiitikadi, waache watanzania wajikomboe wanavyotaka wao.
CCM imejaa mizee yenye misimamo ya kinyonyaji. JK mwenyewe anajua, lakini anakosa la kufanya. Anachoona ni busara ni kunyamaza. Safi!
Long live JK.
Mkuu umezungumza ukweli kabisa,