Innocent Killer (The Revenge)

JIJI LA KAMALI ( GAMBLING CITY)

INTRO...........
Usiku wa kiza kinene ambacho kilikuwa kinasindikizwa na mvua ambazo hazikuwa na mpaka wa kuweza kuzielezea vyema, alionekana mwanaume mmoja akiwa ndani ya nguo zake nyeusi tii na begi jeusi usiku huo huku mwili wake ukiwa umefunikwa na koti kubwa jeusi pia ambalo lilikuwa refu kiasi kwamba lilivuka mpaka magotini.

Mikono yake ilifunikwa na gloves nzito nyeusi pia ambapo mkono wake wa kulia ndio ambao alikuwa ameutumia kuweza kushika begi lake mkononi akiwa anatembea kwa mwendo wa haraka sana huku akiwa makini mno kuonyesha wazi kwamba alikuwa anatakiwa kulifikisha begi hilo salama kabisa sehemu ambapo lilikuwa linahitajika kuweza kufika.

Akiwa kwenye mwendo wake huo wa haraka, wakati amefika katikati ya barabara ndogo ambayo ilikuwa imezungukwa na majengo marefu sana na pembeni yake kukiwa na vichochoro vingi, alihisi kwamba eneo hilo ni kama lilikuwa na mtu au watu wengine ukiacha yeye hivyo alizidisha hali ya umakini sana kwa hapo ambapo alikuwa amesimama.

Masikio yake yalimtekenya vizuri mithili ya funguo zinapokuwa zinazamishwa kwenye kufuli na kumpa taarifa hiyo, alikuwa ni mtu wa kuutumia sana mlango wake wa sita wa fahamu huo wa hisia hivyo alikuwa na uhakika kwamba hisia zake zisingeweza kumsaliti kamwe kwani alikuwa akijiamini sana kwenye jambo hilo hivyo akawa na uhakika kwamba kulikuwa na ugeni ndani ya hilo eneo.

Alisimama na kutulia ili kuweza kujua kwamba huyo mgeni alikuwa anatokea upande upi huku akiwa ameyafumba macho yake kuweza kujipa hali ya utulivu zaidi kwenye masikio yake. Akiwa bado amesimama hapo alihisi kama kuna kitu kilikuwa kinakuja kwa kasi sana sehemu ambayo alikuwa amesimama hivyo aliinama kwa kasi mno mithili ya radi ya mvua.

Wakati anainama alipishana na shoka ambalo lilienda kukita kwenye ukuta mmoja wa jengo la pembeni. Aligeuka haraka sana ila wakati anageuka alitumia muda mrefu ambao ulimpa nafasi mtu ambaye alikuwa ameingia hapo kufanya kile ambacho alikuwa anakitaka.

Alihisi kifua kinamuwasha mithili ya mtu aliye tafuna pilipili kichaa maana spidi ambayo mvamizi aliitumia kumkita hapo kifuani haikuwa ya binadamu mwenye mifupa ya kawaida bali alikuwa ni mashine haswa kama namna umeme unavyo safari kwenye zile njia zake. Alipokea mishindo ya haraka na mabuti makali na kumfanya begi kumtoka mkononi huku ikionekana wazi kwamba mabuti hayo yalitokea kwa mtu ambaye alidhamiria kabisa kumuua ndiyo maana hakumpa hata nafasi ya kuweza kumtazama maana mvamizi huyo uso wake ulifunikwa kwa kitambaa cheusi na hata mvamiwaji hakupata hiyo nafasi ya kumtazama kwa ukaribu.

Mwanaume huyo licha ya kurushwa mbali na mabuti hayo hali ambayo ingemfanya auvunje mgongo wake kwa kujibamiza kwenye kuta za mawe mazito za majengo ambayo yalikuwa pembeni, hakuwa fala kufa kijinga namna hiyo. Mkono wake ndio ambao aliutumia kukita kwenye kuta hizo na sio mgongo ambao ulitua ukutani kwa nguvu sana.

Kasi ambayo alitua nayo kwa mkono wake ililifanya koti lake kujivuta kidogo na kwenye mkono wake ikaonekana alama ya tatoo (tatuu) ambayo ilisomeka kama 001. Baada ya kujichomoa hapo ndipo aligeuka na kumuangalia mtu ambaye alionekana alihitaji kumuua, mtu huyo alikuwa kwenye mavazi meusi kama yeye na koti kama lake, yaani kiufupi wote walikuwa wamevaa sawa ila utofauti wao ni kwamba mvamiwaji alivaa kofia aina ya pama kichwani ila mvamiaji alikuwa amejifunika tu kitambaa kwenye uso wake hivyo sura yake haikuwa ikionekana kabisa.

Baada ya hapo ulipigwa mkono wa hatari mno mpaka umeme ulipo katika ghafla sana ndipo mvamiwaji alitulia akiwa makini sana maana hakuwa akimuona mtu ambaye alitakiwa kumshambulia huku akiwa amepigwa vibaya sana na umeme huo kukatika alishukuru sana japo ilikuwa ni hatari maana angeweza kuuawa bila kujua mhusika yuko wapi ila aliamini kwamba angepata dakika chache za kupumzika maana bila hivyo ni lazima angekufa.

Akiwa anaangaza kwa umakini huku na huko umeme ulirudi tena ghafla sana na ndipo alipo gundua kwamba ndani ya eneo hilo hapakuwa na mtu mwingine zaidi yake, mvamizi alikuwa ameondoka muda mrefu sana ila chini palikuwa na karatasi nyeupe ambayo ilikuwa imesainiwa kwa damu huku ikiendelea kunyeshewa na mvua.

Aligeuka na kuangalia pale ambapo begi lilikuwa limedondokea ili kujua usalama wake ila kwa bahati mbaya sana begi halikuwepo kabisa eneo hilo, alishtuka sana akionyesha hofu ya wazi moyoni na kwenye uso wake hivyo hakuwa na namna zaidi ya kuisogelea ile karatasi ili aweze kusoma kile ambacho kilikuwa kimeandikwa.

“KAMALI YANGU YA MWISHO, NDIYO KAMALI YAKO YA KWANZA” hayo ndiyo maneno ambayo yalikuwa yameandikwa hapo. Aliogopa sana baada ya kuisoma huku akionekana wazi kwamba mikono yake ilikuwa inatetemeka wakati huo. Hiyo ilikuwa ni kauli ambayo alikuwa anaitumia mwanaume mmoja ambaye alimuua yeye mwenyewe kwa mkono wake miaka kadhaa ambayo ilikuwa imepita huko nyuma, huku begi ambalo lilionekana kuwa na nyaraka mhimu mno likiwa limepotea kizembe sana.

Inawezekanaje mwanaume ambaye alimuua kwa mkono wake mwenyewe bado awe hai? Hilo begi lina nini mpaka mtu ambaye alisemekana kwamba alikufa aweze kupotea nalo? Nini maana halisi ya JIJI LA KAMALI na jiji hilo lina mambo yapi na siri zipi labda?

Unategemea kukutana na nini humu ndani? Mimi nashika kalamu yangu sasa nakaa mezani, kazi yako wewe ni kuhakikisha unaenda nayo nukta kwa nukta ili uweze kuifunua kila kurasa kuweza kuzisoma serikali tatu kwa wakati mmoja ndani ya JIJI LA KAMALI.

Simulizi hii inasomwa kwenye group la WhatsApp tu pekee na haitapostiwa mahali pengine popote hivyo nicheki haraka nikuunge kwenye group langu la WhatsApp uanze kusoma simulizi hatari sana ya watu wenye jiji lao la KAMALI (ni hatari sana).

Kujiunga bei yake ni shilingi 3000 tu, yaani ukilipia 3000 nakuunga kwenye group haraka sana.

Usikae kinyonge wakati naingia kujifungia ili ufurahi na kwenda kuisherehekea vyema likizo yako ndefu. Maandishi yapo yanakusubiri wewe tu, usijibane ukataka kukosa simulizi hii bora ya kusisimua eti kisa 3000 tu.

Lipia kupitia namba

0621567672 ( WhatsApp)

0745982347

Zote FEBIANI BABUYA

Nataka watu 30 tu wa mwanzo nianze nao haraka sana, unaweza kuwahi kabla nafasi hazijajaa ili usije ukaikosa

Niwatakieni asubuhi njema.

Kalamu ni yangu mwenyewe;

FEBIANI BABUYA.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Boom.....kesho inaanza kwa group
Gambling%20City2.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Tumebakiwa na episodes 38 ili kumalizana na simulizi hii mpaka mwisho sehemu ya 135.

Natoa ofa kubwa. Malizia hizo episodes zote kwa shilingi 1000 tu.

1000 yako inakufanya umalizane na hii simulizi leo leo.

Lipia kwa namba

0621567672 (WhatsApp)

0745982347

Zote jina FEBIANI BABUYA.

Wasalaam.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)-Simulizi mpya na bora sana ya kipelelezi/kijasusi imetoka rasmi kwa mfumo wa softcopy (nakala laini)

Hii ni moja kati ya movie bora sana iliyopo kwenye maandishi ambayo utaisoma mwaka huu....Kuna mwanaume alipigwa zaidi ya risasi sita kwenye mwili wake kisha akaenda kuzikwa akiwa hai.......Alizikwa porini ambako hakukuwa na binadamu yeyote yule anayeishi LAKINI cha kushangaza mwanaume huyo alikutwa anaishi na yupo hai miaka kumi na mbili iliyo fuatia baadae.....Walichanganyikiwa na ndipo alitumwa BEAST mmoja kwenda kumtafuta ili kujua mtu aliyezikwa anakutwa vipi mtaani! Ni bonge moja la simulizi NICHEKI UJIPATIE NAKALA YAKO LAINI uendelee kufurahi.....

Softcopy yake inapatikana kwa shilingi 5000 tu.

Nicheki WhatsApp kwa namba 0621567672 uweze kuipata yako.

Kama unalipia namba za malipo ni hizi hapa

0621567672

0745982347

FEBIANI BABUYA.

Karibu tuyafurahie maandishi, ndipo chanzo kikubwa cha akili na maarifa kilipo jificha.
FB_IMG_1701864748679.jpg


Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)-Simulizi mpya na bora sana ya kipelelezi/kijasusi imetoka rasmi kwa mfumo wa softcopy (nakala laini)

Hii ni moja kati ya movie bora sana iliyopo kwenye maandishi ambayo utaisoma mwaka huu....Kuna mwanaume alipigwa zaidi ya risasi sita kwenye mwili wake kisha akaenda kuzikwa akiwa hai.......Alizikwa porini ambako hakukuwa na binadamu yeyote yule anayeishi LAKINI cha kushangaza mwanaume huyo alikutwa anaishi na yupo hai miaka kumi na mbili iliyo fuatia baadae.....Walichanganyikiwa na ndipo alitumwa BEAST mmoja kwenda kumtafuta ili kujua mtu aliyezikwa anakutwa vipi mtaani! Ni bonge moja la simulizi NICHEKI UJIPATIE NAKALA YAKO LAINI uendelee kufurahi.....

Softcopy yake inapatikana kwa shilingi 5000 tu.

Nicheki WhatsApp kwa namba 0621567672 uweze kuipata yako.

Kama unalipia namba za malipo ni hizi hapa

0621567672

0745982347

FEBIANI BABUYA.

Karibu tuyafurahie maandishi, ndipo chanzo kikubwa cha akili na maarifa kilipo jificha.View attachment 2835386

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Imalizie kwanza hii boss
 
Huyu jamaa sijui vipi. Mahadithi kibao hayana hata mwisho.
Ni hadithi ngapi ambazo hazina mwisho?

Nimeleta ULIMWENGU WA WATU WABAYA...nilimaliza mpaka mwisho.

Nikaleta I WANT TO DIE JUDGE.....Nikamaliza mpaka mwisho.

Nikaleta GEREZA LA HAZWA.....Nilimaliza mpaka mwisho.


INNOCENT KILLER pekee ndo niliishia 100...
Sikumaliza kwa sababu zangu maalumu.


Now DOCUMENT NUMBER 72 inaendelea.


Kwa hayo maelezo yako ya mahadithi kibao hayana hata mwisho unajiona upo sahihi?


Kuna muda wasapotini waandishi hata kama sio mimi, wengine wasapoti tu. Waandishi wengi wanaandikia kwenye mazingira magumu sana na kuna watu wanatumia muda wao mwingi sana kwenye uandishi.

Kuna watu wanaandika kama burudani (hawa mara nyingi ni watu ambao hawana shida ndogo ndogo), kuna waandishi Wanaandika kama kazi, yaani ni sawa na wewe unavyo amka kwenda kwenye kampuni au ofisi unayo fanyia kazi. So kama unavyokuwa unafeel kuhusu kazi yako kuna waandishi nao wanafeel maandishi hivyo hivyo.

Ni vyema tupunguze kuwabeza sana waandishi kwa kuhisi ni wapoteza muda kuandika na kuanza kuwasapoti.

Uwe na siku njema.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ni hadithi ngapi ambazo hazina mwisho?

Nimeleta ULIMWENGU WA WATU WABAYA...nilimaliza mpaka mwisho.

Nikaleta I WANT TO DIE JUDGE.....Nikamaliza mpaka mwisho.

Nikaleta GEREZA LA HAZWA.....Nilimaliza mpaka mwisho.


INNOCENT KILLER pekee ndo niliishia 100...
Sikumaliza kwa sababu zangu maalumu.


Now DOCUMENT NUMBER 72 inaendelea.


Kwa hayo maelezo yako ya mahadithi kibao hayana hata mwisho unajiona upo sahihi?


Kuna muda wasapotini waandishi hata kama sio mimi, wengine wasapoti tu. Waandishi wengi wanaandikia kwenye mazingira magumu sana na kuna watu wanatumia muda wao mwingi sana kwenye uandishi.

Kuna watu wanaandika kama burudani (hawa mara nyingi ni watu ambao hawana shida ndogo ndogo), kuna waandishi Wanaandika kama kazi, yaani ni sawa na wewe unavyo amka kwenda kwenye kampuni au ofisi unayo fanyia kazi. So kama unavyokuwa unafeel kuhusu kazi yako kuna waandishi nao wanafeel maandishi hivyo hivyo.

Ni vyema tupunguze kuwabeza sana waandishi kwa kuhisi ni wapoteza muda kuandika na kuanza kuwasapoti.

Uwe na siku njema.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
You said it all. Pamoja sana mkuu
 
Stori: Innocent Killer (The Revenge)
Msimuliaji: Bux the story teller
Umri: 18+
Sehemu ya Kwanza:

NB: Hadithi hii ni ya kubuni na kufikirika haihusiani na maisha ya mtu yeyote, wala taasisi yoyote wala mamlaka yoyote ile, lengo lake ni kuburudisha na kutoa burudani kwa wasomaji wangu.

ANZA NAYO.........................

Saa 6:59 za usiku kukiwa na kiza kinene na mvua kali sana nje kukisindikizwa na radi zisizo isha pamoja na upepo mkali wakati huo wa usiku kwenye chumba kimoja kidogo cha vitabu ambacho ndani yake anaonekana mwanaume mmoja akiwa kwenye meza ndogo ambayo alikuwa akiitumia kusomea anapokuwa ndani ya hicho chumba mbele yake palikuwa na vitabu kumi ambapo saba alikuwa ameviweka pembeni kuonyesha alikuwa amevisoma vilibakia vitatu ambavyo navyo ilikuwa ni lazima avimalize usiku huo huo kabla hakuja pambazuka. Vitabu vyote kumi vilikuwa ni vitabu vya sheria ya nchi ya Tanzania, aliangalia saa yake mkononi muda ulikuwa umeenda sana lakini hakuwa na namna ya kufanya ilikuwa ni lazima atimize kile ambacho kilikuwa mbele yake alipiga miayo na kuiweka vizuri miwani yake usoni akainama kinyonge sana kwenye kitabu huku akiwa na mawazo lukuki kwenye kichwa chake.

"Sina uhakika wa maisha yangu kuwa marefu baada ya kesho kwa maamuzi nitakayo yaamua najiona kuwa na maisha mafupi mno lakini mimi siwezi kuipindisha sheria ambayo nimeisomea kwa muda mrefu na naijua vizuri kuliko hata herufi za jina langu eeh MUNGU naomba unisaidie na kuniongoza katika hili" alitoka kwenye mawazo na kuivuta pumzi ndefu sana kisha akatulia na kuinamia chini kukipitia kitabu cha nane kati ya vile kumi ambavyo ilikuwa ni lazima amalize kuvisoma usiku huo.

Markvelous Japhary jaji mkuu wa nchi ya Tanzania ndilo lilikuwa jina la huyu mwanaume ambaye alikuwa ndani ya makataba yake ndogo nyumbani kwake akiwa anaendelea kujisomea vitabu vya sheria ambazo alizijua kiundani kuliko binadamu yeyote kwenye nchi yake. Kesho yake alikuwa na kesi kubwa sana ya kuitolea hukumu mbele ya mahakama ambayo ilikuwa inasubiriwa na taifa zima na ni tukio ambalo lilikuwa linaenda kurushwa na kushuhudiwa moja kwa moja mbele ya watu wote ndani ya nchi hii, alikuwa anaenda kuifanyia maamuzi kesi moja ya gaidi mmoja ambaye alikuwa na shutuma mbaya za kuweza kumuua mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania kwa kumpiga risasi tano kwenye kichwa chake.

Alivuta kumbukumbu zake vizuri siku mbili zilizopita akiwa ndani ya ofisi yake maeneo ya posta simu yake ya mfukoni iliita aliiangalia alikuwa ni mheshimiwa makamu wa raisi aliipokea na kupokea taarifa nzito ambazo zilimfanya aache kila alichokuwa anakifanya aliambiwa kwamba raisi wa nchi ya Tanzania alikuwa amefariki dunia kwa kuuawa msako ulikuwa unafanyika kuweza kumpata mhusika na tayari kuna watu wamekamatwa kwa ajili ya mahojiano, hakuendelea na kazi tena siku hiyo alibeba kila ambacho kilikuwa ni cha kwake na kupanda gari yake ambayo aliiendesha kwa kasi sana bila kujali kama kuna tatizo zito linaweza kutokea kama angepata ajali na hilo gari lake, alikuwa amechanganyikiwa mwanaume ambaye alikuwa amekufa kwake hakuwa raisi wake tu alikuwa ni rafiki yake mkubwa ambaye walikua wote tangu wakiwa wadogo na kusoma pamoja alikuwa zaidi ya ndugu kwake aliumia mno aliitoa miwani yake na kufuta machozi yake akiwa yupo makini barabarani, alifika nyumbani kwake alimpita mkewe kama hamjui na kwenda chumbani ambako alikaa kwa dakika tano tu na kutoka akiwa amebadilika sura yake alijitahidi kujificha ila ilikuwa inatoa machozi muda wote.

"Who did this to my friend, oooh noooooo it's definitely impossible how can they let this happen?" Alikuwa amepanda kwenye gari yake alitoa simu mfukoni na kuipiga mahali.

"Nitakuwa hapo kwa dakika thelathini zijazo" aliongea kwa uchungu na kukata simu yake alitoka kwake kwa spidi mpaka mlinzi wa getini alibaki anamshangaa sana bosi wake alikuwa ni mtu mpole na alimjua vyema hakuwa mtu wa pombe kabisa kwenye maisha yake leo alikuwa kama mtu aliye lewa kama sio kupandwa na wazimu hata mkewe ambaye alikuwa amesimama juu ya nyumba hiyo ya ghorofa alibaki anamshangaa mumewe kwa hali ambayo alikuwa nayo jioni hiyo. Safari yake ilienda kuishia nje ya nyumba moja kubwa maeneo ya Makongo juu hapo palikuwa nyumbani kwa CDF mkuu wa majeshi wa nchi ya Tanzania mheshimiwa Jaiwelo mkupi makubilo, alikuwa anajulikana sana hapo ila alishangaa leo anavyotaka kuingia alizuiliwa mlangoni na kuulizwa kama alikuwa na miadi ya mtu huyo alimpiga jicho kali sana huyo mlinzi ambaye alimzuia bila shaka alikuwa ni mwanajeshi.

"We mjinga hivi unajua unaongea na nani ambaye unanizuia leo kuingia humu ndani?" Aliongea macho yake yakiwa mekundu wakati huo alikuwa amemkunja mwanajeshi huyo shingoni ilikuwa ni dharau sana kijana mdogo kama huyo kumsimamia jaji mkuu wa serikali na kumzuia kirahisi sana namna hiyo
"Najua lakini tumeambiwa tusimruhusu mtu yeyot....." Kabla hajaongea maneno yake yote simu yake ya mfukoni iliita, aliipokea na kuitikia mara moja tu.

"Nisamehe mkuu" kisha akasogea pembeni kumuacha jaji huyo apite kuonyesha kwamba aliipokea amri ya upande wa pili kumuacha mwanaume huyo aingie ndani bila kupata kizuizi chochote kile.

"We mjinga kwa hiki ulicho kifanya baada ya hapa nitakurudia uelewe namna ya kuishi na watu wakubwa kwenye nchi hii" mheshimiwa jaji mkuu alikuwa kama amechanganyikiwa usoni kwake kulikuwa na machozi mengi kama mtoto mdogo, alinyoosha moja kwa moja mpaka juu kabisa sehemu ya makutano ni wazi alikuwa mwenyeji sana kwenye nyumba hiyo alimkuta mtu ambaye alikuwa amemjia hapo.

"Unajua kilicho tokea?" Alisahau hata kusalimia alimuuliza mtu huyo huku akiwa amemkazia macho kwa hasira sana
"Ndiyo"

"Nina imani utakuwa umejua nani aliye husika na hili kupitia jeshi lako"?" Jaiwelo mkupi makubilo hakuongea chochote alitembea mpaka kwenye droo moja ndogo sana akatoa frashi ndogo na laptop akaja nayo mpaka pale alipokuwa amekaa mheshimiwa jaji mkuu, aliichomeka hiyo frash kwenye hiyo laptop na kuifungua ilionekana video moja tu humo ndani akairuhusu iweze kuanza kisha akaigeuzia kwa mheshimiwa jaji mkuu.

"Yuko wapi huyu shetani" aliuliza kwa hasira sana akifuta machozi yake baada ya kuweza kushuhudia namna mheshimiwa raisi alivyoweza kuuawa.

"Tayari yupo kwenye mikono yetu amekamatwa muda sio mrefu baada tu ya kutenda hili tukio"
"Amewekwa wapi muda huu namhitaji kwenye mkono wangu".

"Mark relax this is not easy as you may think, aliye uawa ni raisi wa nchi sio raia wa kawaida tu mtaani"
"No matter what I'm going to kill this idiot".

"Please don't do that kwa usalama wako na wa familia yako nisikilize kwa sasa tu tafadhali sana usifanye chochote" hakumjibu kitu mkuu wa majeshi zaidi ya kuibeba frash hiyo ambayo ilikuwa na ushahidi wote kisha akarudi zake nyumbani kwake akiwa amechanganyikiwa sana, kumbukumbu zake ziliishia hapo.


**********************
Raia wengi walilaani sana hicho kitendo cha mtu huyo kufanya hilo jambo walitaka auawe mpaka kunyongwa mbele ya mahakama wakiwa wanaona iwe kama fundisho kwa watu wengine, ushahidi kwa asilimia zaidi ya miamoja ulikuwa ukionyesha kwamba ni kweli mtu huyo alihusika moja kwa moja na hayo mauaji lakini mheshimiwa jaji mkuu alikuwa amepokea simu nyingi sana za kumtaka afanye namna yoyote ya kuipindisha hiyo kesi na kutengeneza ushahidi wa uongo ambao ungemuweka salama mtuhumiwa huyo ambaye mpaka muda huo hakuwa akijulikana ni nani. Akiwa ameanza kusoma kitabu chake hicho cha nane ghafla sana radi kali ilipiga umeme ukazima alihema kwa wasiwasi akianza kutokwa na jasho jingi usoni kwake mara simu yake ikaanza kuita kwenye hicho kiza kinene aliangalia namba ilikuwa ngeni kabisa hakuwahi kuiona kabla alisita kuipokea iliita mpaka ikakata. Sekunde kama kumi tu uliingia ujumbe ambao alisita sana kuufungua lakini hakuwa na namna.

"ANGALIA DIRISHANI KWAKO HAPO KWA NJE UTAONA MTU, KAMA KESHO UKIFANYA UJINGA WOWOTE ULE BASI FAMILIA YAKO ITAINGIA KWENYE KUNDI LA WANADAMU AMBAO WALIWAHI KUFA KIKATILI SANA ZINGATIA NILICHO KWAMBIA KESHO SAA NNE ASUBUHI MAAMUZI YAKO NDIYO YATAKAYO AMUA HATIMA YA MAISHA YA FAMILIA YAKO" ni ujumbe ambao ulimfanya aanze kutetemeka sana alitoa kitambaa mfukoni na kujifuta jasho lililokuwa linamtiririka usoni, aliiwasha tochi yake kubwa na kusogea dirishani kukiwa bado kuna kiza cha kutisha nje alifungua dirisha taratibu na kuchungulia nje alimulika tochi alishangaa baada ya kumuona ninja mmoja akiwa na mapanga yake mawili mgongoni amesimama pale chini, alionekana ni muda mrefu sana alikuwa ananyeshewa na mvua muda wote pale aliogopa mno.

Aligeuka nyuma baada ya kusikia kama kuna hatua za mtu lakini akahisi ni kichwa chake hakipo sawa aliyarudisha macho yake pale chini hakuona kitu chochote wala hapakuwa na alama ya uwepo wa mtu alianza kurudi nyuma taratibu kwa uoga aligeuka na kuchomoa bastola yake akainyooshea sehemu ambayo alihisi kuna mtu anakuja ghafla sana umeme ulirudi alishangaa mkewe amesimama mbele yake akimshangaa mumewe ameshika bastola tena ameelekezea kwake, aliishusha na kuiweka mfukoni haraka huku akiwa anatokwa na jasho jingi mno, mkewe alimfuata pale na kumkumbatia akiwa ana mpiga piga mgongoni.

"Punguza mawazo mume wangu najua siku ya kesho inakuumiza sana akili muachie MUNGU ila hakikisha unaamua kile kilicho bora mimi siku zote nipo nyuma yako kwa kila jambo" sauti moja ya kinanda mrembo sana ilimfanya atabasamu kwa mara ya kwanza tangu kuingia kwenye hicho chumba, huyu ndiye binadamu pekee ambaye alikuwa anamjua kuanzia unyayo wake mpaka nukta ya mwisho ya unywele wake kichwani, akiwa mbele ya huyu mwanamke alikuwa anapata amani sana ya moyo aliinama na kumbusu mkewe tumboni ambapo palikuwa pametuna kuonyesha ilikuwa ni mimba kubwa tu.

"Is my son wonderful?" Aliuliza akichekelea kuonyesha wazi aliifurahia mimba hiyo kuwa ya mtoto wa kiume japo moyoni hakuwa na furaha yoyote ile.

"Hahahaha ananipiga mateke tu nafikiri dada yake atafurahia sana akizaliwa maana alikuwa anatamani sana kuwa na kaka yake pale anapokuwa anaonewa" mkewe alijibu huku akijitoa mwilini na kusogea pale mumewe alipokuwa anasomea.

"Jitahidi basi mume wangu uwe unapata muda wa kupumzika na leo usichelewe sana kulala kesho ni siku mhimu sana" alitabasamu baada ya kuisikia sauti ya mwanamke aliye mpenda sana, alimfuata na kumbusu kwenye paji lake la uso.

"Nakuja baada ya nusu saa tu mke wangu" alijibu kiunyenyekevu hakuhitaji kumuudhi mama kijacho wake alitabasamu na kuanza kuelekea mlangoni lakini aligeuka kabla hajatoka.

"Jason umempigia simu kumueleza hichi kinacho endelea?" Swali la mkewe lilimshtua kidogo mwanaume ambaye alikuwa anauliziwa hapo alikuwa ni mdogo wake wa damu kabisa ambaye alikuwa nje kimasomo jina lake alifahamika kama Jason Japhary na walizaliwa wawili tu.

"Anapenda mno kulala yule nitampigia simu baada ya kumaliza kesi kesho usijali" aliongea kikakamavu ila mwili wake ulikuwa unamsaliti alikuwa akitetemeka sana mkewe alimuonea huruma sana mume wake alikuwa kwenye wakati mgumu sana hakuwa na namna aliondoka na kwenda kulala. Jaji mkuu alibaki kwenye hicho chumba lakini hakuwa na mood ya kusoma tena alibaki akiiwazia ile meseji aliyotumiwa pamoja na alicho kishuhudia nje alijikuta akiogopa mno.

Ndo kwanza tunaifungua sehemu ya kwanza kabisa ya hadithi yetu mpya ya INNOCENT KILLER (THE REVENGE), the magic finger mwenyewe nipo na kalamu yangu....Bux the story teller.

TWENDE PAMOJA MPAKA MWISHOView attachment 2396804

Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Mmmh mkuu hii umetisha sana daah 🙏🙏🙏♥️♥️♥️
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 9

SONGA NAYO............
Jason kitu alicho kiona baada ya kuuona mwili wa kaka yake kilimfanya aume meno kwa hasira sana, aliuangalia kwa dakika kumi bila kukwepesha macho yake. Mwili huo ulikuwa na tobo la risasi kwenye paji la uso wa kaka yake, alisogelea sehemu ambapo lilikuwa limeandikwa jina la shemeji yake napo aliangalia kwa umakini sana na kuona kitu kile kile risasi ilipita kwenye paji la uso.

Alikumbuka vizuri kwamba shemeji yake alichomwa na kisu maeneo ya tumboni aliyafumba macho yake akijaribu kuvuta hisia kwa mtu kukosa huruma mpaka kufikia hatu ya kuweza kumchoma kisu mwanamke mjamzito namna hiyo, inahitajika mtu kuwa na roho ngumu sana.

Alienda kumalizia kwenye jokofu lililokuwa na jina la mtoto ambaye alikuwa anapenda sana alivyokuwa anamuita baba mdogo, huyo ndiye pekee aliwahi kumfanya naye ajihisi ni baba kwenye hii dunia, alivuta taratibu sana kuonyesha kwamba hakuwa tayari kuona kilichokuwa mbele yake ila hakukuwa na namna alihitaji kujihakikishia mwenyewe kile ambacho kilikuwa kimetokea, mtoto alikuwa ameyafumba macho kama vile alilala na angeamka ila ni kitu ambacho kilikuwa ni ndoto tu na isingewezekana kuwa kweli hata kama ungekuwaje.

Kama alivyokuwa ametegemea hata huo mwili pia ulikuwa una risasi kwenye paji la uso, aliinama na kumbusu mtoto huyu kwa dakika nzima akiwa ameinamisha uso wake hapo alinyanyuka na kuanza kuzunguka humo ndani kama mtu aliye changanyikiwa mpaka akaenda kukaa kwenye kona ya hicho chumba cha kuhifadhia maiti licha ya kuwepo kwa baridi kali sana humo ndani ila kwake haikuwa sababu ya msingi sana ya kumfanya kutoka haraka.

Yaliisha masaa mawili mazima ndipo mlango huo ulipo funguliwa na mwanaume huyo akatoka na kuurudishia mlango kama ulivyokuwa, alitembea taratibu mpaka kwenye ile ofisi ambayo kwa mara ya kwanza alipelekwa na IGP, aliingia bila hata kugonga na kumfanya IGP na daktari huyo kushtuka sana hawakujiandaa na ujio wake humo ndani.

“Nina maongezi nawewe nifuate” aliongea na IGP kisha akatoka nje kumsubiria mtu wake huyo, IGP alibaki anaangaliana na daktari tu mle ndani

“Hivi huyu ndiye mfiwa kweli? Mbona hana hata wasiwasi wala dalili za kuonyesha kwamba ni mtu mwenye majuto kupotelewa na familia yake? Halafu mbona kama anakuchukulia kawaida sana kwamba hajui kama wewe ni kiongozi mkubwa kwenye nchi hii” daktari alimuuliza IGP akiwa anajiandaa kutoka Kwenda kuongea na mtu wake huyo, IGP aligeuka na kulazimisha tabasamu

“Jambo usilo lijua ni sawa na usiku wa giza hivyo kuna mambo usilazimishe kuyajua yatakuja kuhatarisha maisha yako, kuhusu familia hakuna binadamu ambaye anafiwa na familia anayo ipenda sana halafu akafurahia au kuwa kawaida sema kuna watu wamefunzwa kuwa wanaume unaweza ukamuona anacheka sana ila moyo wake unalia kuliko unavyo fikiria wewe shida yako umezoea sana hizo kazi za kubembelezana na wagonjwa hivyo hata kulia kwako ni rahisi sana yule hayupo vile mpaka unamuona yupo siriasi sana jua ni mtu ambaye anatokwa machozi kila dakika ila hayo machozi wewe hapo huwezi kuyaona kwa sababu umechagua kuyaamini sana macho yako kuliko hisia” IGP alijibu kwa mafumbo na kumuacha daktari huyo kwenye njia panda wakati huo aliubamiza mlango huo na kutoka nje ambapo alikohoa kidogo baada ya kumkaribia Jason ili kumpa taarifa kwamba alikuwa amefika.

“Kwanini unanipa taarifa nusu nusu?” swali la Jason lilimshtua kidogo mheshimiwa

“Una maanisha nini kusema hivyo?”
“Unajua wale waliokufa ni akina nani kwangu?
“Ni familia yako”

“Sasa mbona unanipa taarifa kama vile nimefiwa na jirani yangu au mtumishi mwenzengu?”
“Taarifa ipi hiyo ambayo wewe unaihitaji na haujaipata kama ulivyokuwa umetarajia?”

“Umenipa maelezo mengi sana lakini hakuna sehemu ambayo umenielezea kwamba familia yangu imekufaje na hicho ndicho nilichokuwa nakihitaji”

“Bado sijakuelewa”

“Una kichwa Kizito sana sijui ulipewaje hiyo nafasi”

“Sasa nafasi yangu inahusiana vipi na swali lako?”
“Nimekuuliza walikufaje? Mbona hujanambia kama miili yote ilimuwa na risasi kwenye kichwa”

“Daaah nilikuwa mbali sana haya majukumu naona kabisa kwamba yananizidi sasa ndiyo maana hata sikuwaza huko kwa sababu nilijua utayapata kwenye ripoti ya madaktari wanavyokupatia taarifa ya vifo vyao”

“Mhhhhhhh kiwepesi tu namna hiyo”

“Yes, imegundulika kwamba wote mpaka walinzi walipigwa risasi za kwenye paji la uso ndiyo maana nilisema kwamba muuaji ni mmoja tu na sio wengi kwa sababu aina ya mauaji iliyotumika ilikuwa ni moja tu basi”

“Sijajua kwamba ni kwanini kiwepesi tu namna hiyo ulininyima hizo taarifa ila kwa sasa nahitaji niandaliwe hiyo ripoti na daktari nitakuja kuichukua na huyo daktari mwenyewe nitahitaji kukutana naye, pia utanipa namba ya nyumba ya huyo askari ambaye alifika pale mapema sana kuja kufanya uchunguzi baada ya tukio, hivyo sivihitaji saivi labda tu namba ya nyumba ya huyo askari nitumiwe ndani ya muda mfupi ila ripoti ya daktari naihitaji siku moja baada ya msiba”

“Kwa muda huu hapa nina vitu viwili, kitu cha kwanza naihitaji hiyo video ambayo inaonyesha mheshimiwa raisi akishambuliwa na huyo mtu mpaka kufa na kingine nataka kujua kwanini ulinambia uongo” ishu ya video IGP hakushtuka sana japo alisita ni kama alitarajia mtu huyo angeiomba tu kwa namna yoyote ile ila kilicho mshtua sana ile ya kusema kwanini alimwambia uongo, alibaki anawaza uongo upi wakati asilimia zote alikuwa anatoa maelezo ya kitu ambacho anakijua? Ilimbidi alijibu ili asije akashtukiwa.

“Uongo upi huo ambao unausema?” Jason alimwangalia sana mzee huyo

“Najua kwenye ile simu hakukuwa tu na zile sms tatu kama ulivyosema wewe, kuna sms uliamua kuzimezea na sijajua kwanini na kwa sababu zipi, hilo utaenda kujitafakari mwenyewe kisha tutaongea vizuri siku nyingine kwa sasa nionyesha hiyo video ya kuuawa kwa raisi” Aliongea bila kitetemeshi chochote kile, IGP hakuongea kitu chochote zaidi alinyoosha kwenye njia ambayo ilikuwa inawapeleka kwenye lifti, walishuka mpka chini na kuelekea kwenye gari yake ambapo waliingia na kufunga milango yote, alitoa simu kwenye droo yake na kumpatia Jason ambaye aliifungua na kuangalia kwa dakika tano video hiyo fupi ambayo ilikuwa inajirudia rudia.

“Pumbavuu, inawezekana vipi raisi wa nchi auawe kirahisi sana namna hii?” aliongea kwa hasira sana akiwa amemkazia macho IGP ambaye alibaki ameinama tu

“Si nakuuliza wewe hapo au haunisikii? Nitajibu vipi hili suala kwa watu ambao mliaminika mtamlinda huyu mtu ndo mkaacha afe kizembe sana namna hii, shiiiiiiit this is lunatic” alifoka kwa hasira sana Jason na mzee huyo ambaye kwa umri alikuwa mkubwa sana alikuwa ametulia tu akimsikiliza kijana huyo hakutaka kabisa kumuingilia kwenye hizo hasira zake.

“Ok kama huwezi kunijibu hilo kwanini mmeruhusu ahukumiwe mtu ambaye siyo muuaji? Ina maana huu ulikuwa ni mpango endelevu wa kumuua na kaka yangu sio?” hayo maswali ya Jason yalimshtua mzee huyo baada ya kusikia kwamba walikuwa wamemhukumu mtu ambaye alikuwa hahusiki na chochote kabisa

“Mbona sijakuelewa”
“Mzee ujue nakuheshimu sana na nadhani unajua miongoni mwa vijana ambao huwa wanakupenda sana namimi nipo na unalijua hilo ila usitake tuende kuwa maadui hapo mbeleni nitakusahau kama sijawahi kukuona kwenye maisha yangu. Ni nani ambaye alimkamata huyo mtu ambaye amenyongwa kama muuaji? Nani alifanya huo uchunguzi?”

“Tulipewa taarifa kwamba huyo muuaji alikamatwa na jeshi la wananchi hivyo sisi hatukuwa na namna zaidi ya kufuata mamlaka zilizokuwa zimemshikilia kwa sababu walituambia itabaki kuwa hivyo na hapo ndipo tulipo ingilia kati kuanza kufanya uchunguzi lakini tulizuiliwa na kuambiwa kwamba watu wa ikulu watahusika na hilo na sisi tutashughulika na mengine ambayo yataendelea mbele” IGP alijibu jibu ambalo ni kama mtu huyo lilimuacha njiapanda sana kwa namna alivyo jibiwa kiwepesi sana

“Huyo aliyewapa hiyo amri ni nani?”
“CDF alitupatia hiyo taarifa kwamba imeamuliwa iwe hivyo”

“Huyo CDF anahusika nini na mheshimiwa raisi mpaka yeye ndiye atoe amri ya taarifa ya uchunguzi? Na yeye anahusika nini na ikulu? Sasa naomba umpe taarifa kwamba leo usiku nataka nikutane naye tukiwa wawili tu, akiukuuliza nani mwambie mdogo wake jaji anakuhitaji sana kuliko hata maisha yake nadhani yeye ndiye aje anipe hayo majibu sahihi”

“Sawa hilo nalifanyia kazi lakini sijakuelewa ulivyosema kwamba amehukumiwa mtu ambaye hahusiki” IGP alihitaji sana kuzijua hizo taarifa

“Kaka amekufa baada ya hukumu na yule mtu kunyongwa sio?”

“Ndiyo”

“Umeona namna raisi alivyokufa”

“Ndiyo alipigwa risasi”

“Ya wapi?”

“kwenye paji la uso”

“Na familia yangu imeuliwa vipi?”

“Kwa risasi za paji la uso” hapo sasa hata IGP akili yake ilifunguka, alijiona kuwa ni mzembe sana kushindwa kung’amua hicho kitu mapema ni mchezo mdogo sana ambao hata mtoto mdogo anaweza kuutegua bila hata kutumia nguvu.

“Muuaji hapa ni mmoja, maana yake mtu aliyeweza kumuua mheshimiwa raisi ni yule yule ambaye aliiua familia yangu, sasa kama alikamatwa na kunyongwa kivipi aue familia yangu baada ya kufa? ni kitu ambacho hakiwezekani inamaanisha huyo mtu yupo hai ila kuna mchezo tu wa akili ndogo wameamua kuucheza sasa naingia mimi mwenyewe kwenye huu mchezo nikacheze nao hilo draft ambalo wamelichora wao wenyewe na sheria wamezitunga wao wenyewe” aliongea kwa msisitizo sana Jason akiwa anaufungua mlango ili atoke humo ndani.

“CDF nimwambie mkutane saa ngapi?”

“Mwambie saa 6 kamili usiku nitakuwa nje ya nyumba yake na unitumie namba ya nyumba ya huyo askari wako muda huu” mwanaume aliongea hivyo na kuondoka IGP alibaki anashangaa jasho likiwa linamtoka, kwa muda mfupi sana aliona mambo yanaenda kuwa mabaya kuliko hata ilivyokuwa imekadiriwa, alichukua simu yake na kuitafuta namba ambayo alikuwa ameisevu Jaiwelo Mkupi Makubilo huyu ndiye ambaye alikuwa CDF mwenyewe mkuu wa majeshi, aliruhusu simu hiyo iweze kupiga, iliita kidogo na kupokelewa.

“Nakuja kwako ndani ya dakika thelathini zijazo” hakusubiri hata kujibiwa alikata simu na kuwasha gari yake kisha akaondoka kwa kasi sana hilo eneo.

Jason Japhary ni nani huyu kijana mpaka anajiamini sana namna hii mbele ya watu wakubwa sana serikalini kama hawa wakati kuna watu wanamjua kama ni kijana laini sana asiye na makuu na mtu waweza kumuita mtoto wa mama? ……. bado tupo taratibu twende pamoja michezo ya akili imeanza tukaitafutie majibu halisia.

Bux the storyteller.
Ndo kwanza aaaa kimenuka🤣🤣🤣🤣
 
STORY: INNOCENT KILLER (THE REVENGE)
STORY WRITER: BUX THE STORYTELLER
WHATSAPP : 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+
SEHEMU YA 25

SONGA NAYO............
Saa 6 kamili usiku ndio muda ambao Jason alikuwa anatoka kwenye nyumba ya akina Nayrah, alitumia muda mrefu sana kumwelewesha binti huyo mpaka kumuelewa kile ambacho alikuwa amekifanya kitu kikubwa ambacho alimsisitiza sana binti huyo ni kwamba hakutakiwa kabisa kukatika hewani kwenye simu yake ahakikishe muda wote inakuwa hewani kwa gharama yoyote ile na alihitaji usiku huo huo akitoka tu hapo basi wafunge milango yote kuna watu watakuja sio muda sana na asimfungulie mtu yeyote yule mpaka yeye mwenyewe ampigie simu kumruhusu afungue, hiyo ndiyo sababu mwanaume aliweza kuondoka akiwa pekeake kabisa hiyo sehemu hakuhitaji watu hao wamsindikize hata hivyo hakufanikiwa kumuona baba yake pamoja na wadogo zake ila aliahidi kwamba kuanzia siku hiyo hawatabahatika kumuona tena mpaka pale itakapo isha miezi sita.

Aliinyanyua simu yake na kuiweka sikioni, iliita kwa muda kidogo kisha ikawa imepokelewa upande wa pili.

“Umeiona hiyo namba ambayo nimekutumia” aliongea kwa sauti nzito sana baada ya kuhakikisha upande wa pili simu imepokelewa

“Ndiyo bosi”
“Nendeni mpaka namba hiyo inapo onyesha ipo, mkifika hapo kuna familia inatakiwa muichukue na kuondoka nayo na kuipeleka Kigamboni kwenye nyumba ya baharini kule, mtakuja na IGP na kujifanya nyie ni miongoni mwa maaskari na kuna askari nitampa maagizo mtaungana naye yeye yupo Mbagala ila baada ya nyie kufika hapo na hiyo familia ikimuona yeye atabaki na nyie mkiondoka hapo IGP atawaacha wenyewe mkiondoka, mimi sitakuwepo kwa miezi sita hivyo jukumu la kuilea hiyo familia nakukabidhi wewe hapo na wenzako hakikisheni hiyo familia inakuwa salama kwa gharama yoyote ile, kuna watoto wawili wa kiume hakikisha unawatafutia moja ya shule bora na za gharama sana hapa mjini wasome kwa amani na walindwe sana. lakini pia kuna mama ana matatizo ya moyo atibiwe kama mama yangu mzazi na kwa gharama yoyote ile mpaka apone na kuna mzee ni mgonjwa wa akili ambaye ni mume wa huyo mama atibiwe kama ni Tanzania au nje IGP atakupa maelekezo zaidi kama atahitajika kupelekwa nje ya nchi ila hakikisha ninavyorudi awe amepona” aliongea kwa msisitizo na kuweka kituo baada ya mwili wake kumsisimka sana alihisi hilo eneo lilikuwa na usalama mdogo sana mpaka wakati huo, alisikitika kisha akaendelea kuongea.

“Halafu kuna huyo mwanamke ambaye utamkuta hapo ni mtoto mkubwa wa huyo mzee na huyo mama huyo keshokutwa anatakiwa kuanza kazi mhimbili pale hilo atalimaliza IGP kwamba anaendaje pale ila wewe hapo nakupa kazi ya kumlinda wewe mwenyewe hakikisha hakuna binadamu anamgusa hata kidole chake wala sehemu yoyote ya mwili na kama nikija kupata hizo taarifa basi mimi nitakuua wewe hapo, nina imani hivi ninavyo ongea nawewe nadhani sio zaidi ya dakika kumi utakuwa hapa na wenzako” aliongea kwa msisitizo sana tena kwa sauti nzito na kukata simu akiwa anatembea haraka haraka, hakusimama tena bali alibonyeza tarakimu kadhaa kwenye simu yake na kupiga Kwenda namba ya IGP


“Mhhhh kuna nini kijana wangu mpaka unanipigia na usiku wote huu?” IGP aliipokea hiyo simu akiwa anaonekana kama alitoka kuamka mida hiyo ni wazi alikuwa amepitiwa na usingizi.

“Nisikilize kwa umakini hivi ninavyo ongea nawewe nipo mbagala, kuna namba nakutumia hapo sasa hivi itrack kwenye simu yako na sehemu ilipo ndipo wewe unatakiwa kuwepo ndani ya muda mfupi ujao ila kabla ya wewe kufika mpigie simu yule ASP mwambie awahi kwa akina Nayrah akae nje kuwasubiri vijana wangu yeye ataelewa nadhani nawewe ukifika nitamruhusu huyo binti kuufungua mlango wa kwao, familia yake itatolewa na yeye mwenyewe Kwenda Kigamboni muda huu eneo ambalo ni salama zaidi na wewe kazi yako hapo ni kuhakikisha wameondoka salama kisha huyo binti ambaye anaitwa Nayrah hakikisha kesho unafanya lolote pale mhimbili anapata kazi na keshokutwa anaingia kazini kwa sababu amesomea udaktari hayo mengine tutaongea tukikutana mimi na wewe wakati mwingine” aliongea akiwa anajiandaa kukata simu hiyo lakini IGP alimuwahi kabla hajafanya hivyo.

“Hey mbona unanichanganya umesema Mbagala kuna familia? wewe Mbagala una ndugu gani na umefika saa ngapi huko wakati ulipaswa kuwa Ikulu?”

“Mzee sio muda wa kuanza kuulizana maswali saivi fanya hicho nilicho kwambia halafu hayo mengine tutayaongea mimi nawewe tukionana, hiyo ni familia yangu mpya hivyo hawa watu wasiguswe na mtu yeyote ambaye anaishi kwa kuutegemea moyo wake ili awe hai wapewe kila kitu maelekezo utayapata kwa vijana wangu kwamba ni kitu gani kinahitajika nimesha waambia nadhani sina muda sana”aliongea akionyesha wazi kwamba alikereka sana na kilicho kuwa kinaulizwa hakuhitaji maswali mengi sana yalikuwa yanamboa mno.

“Mhhhh sawa ndani ya dakika ishirini nitakuwa hapo lakini umeona tukio linalo endelea saivi kwenye vyombo vya habari?” hilo swali lilimshtua sana Jason licha ya hivyo aliikata simu hiyo na kuingia kwenye mtandao wa kijamii ili kuweza kujua kwamba ni nini hicho ambacho alikuwa ameambiwa na kilikuwa kinaendelea, alijua fika kwamba hayo maeneo kulikuwa na watu hata hivyo hakujali sana hilo alikuwa anatembea kwa mwendo wa haraka sana mpaka pale alipokaribia kufika kwenye kona moja ya uwanja wa ile sehemu ambayo alikutana kwa mara ya kwanza na Nayrah alisimama.

Kwenye mitandao ya kijamii kulikuwa na taarifa ya kushtua sana kuhusu mdada mmoja ambaye alikuwa mwanasheria alijirekodi video kwa kudai kwamba kesi ya mauaji ya mheshimiwa raisi pamoja na jaji mkuu wa nchi ya Tanzania yeye alikuwa ana ushahidi wa kutosha juu ya hicho kitu ambacho kilikuwa kinaendelea na aliweka wazi kwamba hao ambao walikuwa wamehusika na hilo jambo kuna uzembe mkubwa sana waliufanya ambao ulimsaidia yeye kuupata huo ushahidi hivyo alitaka kuutumia ushahidi huo kuweka wazi mambo yote mbele ya mahakama na kila aliye husika kutenda hilo jambo akutane na mkono wa sheria na kuadhibiwa kama inavyo stahili. Hiyo video ndani ya saa moja tu tangu iachiwe ilikuwa imetazamwa na watu milioni kumi na kuvunja rekodi ya nchi kwa kuwa video ambayo ilikuwa imetazamwa na watu wengi zaidi kwa muda mfupi kwenye historia ya nchi ya Tanzania, watanzania wengi sana walikuwa wanatoa maoni kwamba kama mwanasheria huyo alikuwa ana ushahidi basi serikali ilitakiwa kumlinda kwa gharama yoyote ile ili kuhakikisha kwamba anawaumbua watu wote ambao walikuwa wanahusika kuutenda huo unyama ndani ya nchi yao huku wengine walikuwa wakikomenti kumuonea huruma mwanamke huyo kwa kudai kwamba anaweza kuwa na maisha mafupi sana kwani huenda watu ambao alikuwa anaenda kuwaripoti ndio hao hao viongozi wakubwa wa nchi hivyo wasingekuwa tayari kuweza kuruhusu afichue maovu yao mbele ya jamii lazima wangemuua tu, Jason akiwa anaendelea kuirudia video hiyo alihisi mvumo wa kitu ukiwa unakuja upande ambao alikuwepo alibinya batani ya kuiweka simu off kuupoteza mwanga kwenye skirini ghafla sana na kuinama kidogo tu, ilipita shoka moja ambayo ilikuwa inang’aa sana kwa taa ambazo zilikuwa zinamlika kwa mbali sana na kwenye kukita kwenye mti mmoja ambao ulikuwa upo mbele, alisimama vizuri na kugeukia upande ambao ilitokea shoka hiyo walikuwa wanaume watano ambao wote walikuwa wameziba sura zao kwa vitambaa vyeusi huku vichwa vyao vikiwa wazi, mmoja alipita karibu yake na kupitiliza mpaka kwenye ule mti na Kwenda kuichomoa shoka kwenye ule mti kisha akawa anarudi taratibu mwanaume hakuwa ametikisika wala kuongea chochote alikuwa anasubiri wageni wake hao waongee chochote.

“Mchukueni tuondoke naye” mmoja wao aliongea kwa sauti ambayo ilikuwa kavu kana kwamba hakuwa mtu ambaye maji yalikuwa sehemu ya maisha yake zaidi ya sigara ambayo mpaka wakati huo ilikuwa ipo kwenye mdomo wake kitambaa yeye akiwa amekishusha kidogo.

“Mtu dhaifu kama wewe hapo ndo unawaambia wenzako wanichukue mimi?” Jason aliuliza akiwa anawasogelea pale walipokuwepo mpaka wenyewe wakabaki wametaharuki mtu gani huyo ambaye alikuwa anajiamini sana kiasi cha kuwa na ujasiri huo wa kuwafuata mpaka hapo walipokuwa wamesimama? Hakuna ambaye alikuwa ana jibu la hilo swali lao.

“Mhhhhh kijana mdogo kama wewe na udhaifu wote huo unajiaminia nini mpaka huogopi hata kutusogelea watu kama sisi?" aliongea kwa msisitizo sana mwanaume huyo ambaye paji lake la uso lilikomaa sana kuonyesha hata umri haukuwa rafiki sana kwake tofauti na wenzake, Jason alitabasamu mara moja tu kwenye uso wake

“Mimi huwa nacheka mara chache sana ninapokuwa mbele ya wanaume wenzangu, ok tuachane na hayo mna muda gani mnanifuatilia na huyo ambaye amewatuma watu walaini kama nyie kuja kunifuata hapa ni nani na mnahitaji mnichukue ili twende wapi?”

“Mchukueni mbwa huy……..” kauli yake ilikatishwa na ngumi ya moyo, alipigwa ngumi nzito sana mithili ya jiwe kwa namna mkono huo ulivyokuwa umekomaa alibaki amesimama hivyo hivyo na sigara yake mdomoni, iliongezwa ngumi nyingine pale pale kwenye moyo alishuka chini kama anahitaji kukaa chini ila safari yake ndiyo ilikuwa imetimia ya Kwenda kujitetetea mbele ya muumba kwa madhambi ambayo alikuwa ameyafanya, vijana watatu ambao walikuwa wapo mbele yake walikuwa bado wameduwaa sana ni jambo ambalo lilitendeka kwa muda mfupi mno tena na mwanaume ambaye wao walidai kwamba alikuwa ni mlaini sana, aliyekuwa nyuma na shoka alizinduka kutoka kwenye hiyo simanzi alirusha shoka lake tena kwa nguvu huku akiwa anasogea kwa kasi, shoka Jason aliipisha kidogo ikampita kisha aliuchomoa mkono wake kwa nguvu sana akalidaka hilo shoka, yule kijana wakati anakaribia pale shoka lilirudishwa nyuma na kutua kwenye kifua chake, ilisikika sauti ndogo tu

“Mhhhhhhhh” hiyo ndiyo sauti pekee ambayo ilisikika kutoka kwenye kinywa chake, kifua kilipasuliwa kama mtu ananapasua kuni na shoka namna kuni inavyo chakazwa na ule uzito wa shoka ndicho kilichokuwa kimemkuta mtu huyo, damu ilikuwa inamtoka mdomoni kwake pamoja na kifuani huku hata kuhema kwake kukiwa kwa shida sana alishuka shini na shoka lake likiwa kifuani mwake lilikuwa ni miongoni mwa matukio ya mauaji ya kutisha sana miongoni mwa wanadamu ambao waliwahi kutokea kuishi ulimwenguni. Waliokuwa wapo mbele yake alikuwa amewakazia macho sana licha ya kiza totoro ambacho kilikuwa kimetawala ila walimuona vyema, mikononi mwao wote walikuwa na vishoka vidogo tofauti na yule ambaye alikuwa amepasuliwa na shoka lake mwenyewe yeye shoka lake lilikuwa ni kubwa kiasi walianza kusogea nyuma taratibu mwanaume aliitoa bastola kwenye kiuno chake na kuvichakaza vichwa viwili vya miongoni mwa hao vijana ambao walikuwa mbele yake na ubaya risasi hizo zilitolewa kwenye bastola ambayo haikuwa hata na kiwambo cha kuzuia sauti za risasi hizo hivyo hiyo sauti ilisikika mbali sana kitu kilicho pelekea ndani ya sekunde za kuhesabu mtaa kubaki kimya sana kana kwamba hakukuwa na watu ambao walikuwa wanaishi.

“Hautakiwi kubahatika kukutana namimi nikiwa namna hii utakufa kifo kibaya sana ambacho utatamani hata ni heri ungejiua mwenyewe, kwanini unaacha kutafuta mwanamke mrembo majira haya ya usiku akakupa burudani unahangaika kuwinda roho za watu ambao hata hauwajui?” alikuwa anaongea na huyo kijana mmoja ambaye ndiye pekee alikuwa amebaki hapo, alikuwa akisogea nyuma akitetemeka huku kishoka chake akiwa amekiweka kwa juu kama ishara ya kujitetea.

“Hapana Hapana naomba usiniue”

“Ok kawatuma nani kuja kunifuatilia mpaka huku?”
“Hapana Hapana mimi simju….” Alipigwa risasi mbili za mguu alianza kulia sana akiwa amedondoka chini

“Kwahiyo unaona hapa unaongea na mtoto mdogo sio, ok kama hilo ni tatizo kubwa sana kwako basi ngoja nikupunguze viungo kadhaa kwenye mwili wako” Jason aliongea huku akiichomoa lile shoka kubwa kwa yule mwanaume ambaye alimpasua nalo kwa mara ya kwanza kifuani.

“Nasema nasema usinifanyie hivyo tafadhali”

“Tumetumwa na Oden”

“Oden ni nani?”

“Mtoto wa CDF”
“Amewatuma ili mfanye nini na mimi?”
“Alikuwa anakuhitaji kwa gharama yoyote ile uwe hai au umekufa, maelekezo yake alikuwa anatamani ufike kwake ukiwa hai ila kama ingeshindikana basi alitupa maagizo kwamba tukuue”

“Waambie na wenzako walio tangulia huko wasilete mazoea na binadamu wasio wajua” alimaliza kuongea hivyo huku akishusha shoka hilo kwenye shingo ya kijana huyo kisha akalitupa hilo shoka pembeni na kutoweka hilo eneo haraka sana baada ya kusikia muungurumo wa magari yakiwa yanafika eneo la kwenye huo uwanja, waliokuwa wamefika alikuwa anajua ni akina nani ila hakutaka kabisa wamkute hilo eneo ndiyo maana alipotea kwa kasi sana kuelekea kwenye vichochoro ambavyo vilikuwa mtaani hapo.

Tumeanza kumfunua taratibu huyu mwanaume ili tumjue kwamba yeye ni nani hasa kwenye maisha yake mpaka baadhi ya watu wanamuogopa sana, kwa haya mauaji unahisi jamaa kweli ni mlaini kama baadhi ya watu walivyokuwa wanasema au ni maneno tu ya wale ambao hawaijui hata ncha ya maisha yake ya kweli?

25 sina la ziada niseme tu kwanza inafika tamati.

Wasalaam

Bux the storyteller.
Mmmh hadi nmeogola 😌😌😌😌😌
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom