FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,035
- 1,925
Stori: Innocent Killer (The Revenge)
Msimuliaji: Bux the story teller
Umri: 18+
Sehemu ya Kwanza:
NB: Hadithi hii ni ya kubuni na kufikirika haihusiani na maisha ya mtu yeyote, wala taasisi yoyote wala mamlaka yoyote ile, lengo lake ni kuburudisha na kutoa burudani kwa wasomaji wangu.
ANZA NAYO.........................
Saa 6:59 za usiku kukiwa na kiza kinene na mvua kali sana nje kukisindikizwa na radi zisizo isha pamoja na upepo mkali wakati huo wa usiku kwenye chumba kimoja kidogo cha vitabu ambacho ndani yake anaonekana mwanaume mmoja akiwa kwenye meza ndogo ambayo alikuwa akiitumia kusomea anapokuwa ndani ya hicho chumba mbele yake palikuwa na vitabu kumi ambapo saba alikuwa ameviweka pembeni kuonyesha alikuwa amevisoma vilibakia vitatu ambavyo navyo ilikuwa ni lazima avimalize usiku huo huo kabla hakuja pambazuka. Vitabu vyote kumi vilikuwa ni vitabu vya sheria ya nchi ya Tanzania, aliangalia saa yake mkononi muda ulikuwa umeenda sana lakini hakuwa na namna ya kufanya ilikuwa ni lazima atimize kile ambacho kilikuwa mbele yake alipiga miayo na kuiweka vizuri miwani yake usoni akainama kinyonge sana kwenye kitabu huku akiwa na mawazo lukuki kwenye kichwa chake.
"Sina uhakika wa maisha yangu kuwa marefu baada ya kesho kwa maamuzi nitakayo yaamua najiona kuwa na maisha mafupi mno lakini mimi siwezi kuipindisha sheria ambayo nimeisomea kwa muda mrefu na naijua vizuri kuliko hata herufi za jina langu eeh MUNGU naomba unisaidie na kuniongoza katika hili" alitoka kwenye mawazo na kuivuta pumzi ndefu sana kisha akatulia na kuinamia chini kukipitia kitabu cha nane kati ya vile kumi ambavyo ilikuwa ni lazima amalize kuvisoma usiku huo.
Markvelous Japhary jaji mkuu wa nchi ya Tanzania ndilo lilikuwa jina la huyu mwanaume ambaye alikuwa ndani ya makataba yake ndogo nyumbani kwake akiwa anaendelea kujisomea vitabu vya sheria ambazo alizijua kiundani kuliko binadamu yeyote kwenye nchi yake. Kesho yake alikuwa na kesi kubwa sana ya kuitolea hukumu mbele ya mahakama ambayo ilikuwa inasubiriwa na taifa zima na ni tukio ambalo lilikuwa linaenda kurushwa na kushuhudiwa moja kwa moja mbele ya watu wote ndani ya nchi hii, alikuwa anaenda kuifanyia maamuzi kesi moja ya gaidi mmoja ambaye alikuwa na shutuma mbaya za kuweza kumuua mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania kwa kumpiga risasi tano kwenye kichwa chake.
Alivuta kumbukumbu zake vizuri siku mbili zilizopita akiwa ndani ya ofisi yake maeneo ya posta simu yake ya mfukoni iliita aliiangalia alikuwa ni mheshimiwa makamu wa raisi aliipokea na kupokea taarifa nzito ambazo zilimfanya aache kila alichokuwa anakifanya aliambiwa kwamba raisi wa nchi ya Tanzania alikuwa amefariki dunia kwa kuuawa msako ulikuwa unafanyika kuweza kumpata mhusika na tayari kuna watu wamekamatwa kwa ajili ya mahojiano, hakuendelea na kazi tena siku hiyo alibeba kila ambacho kilikuwa ni cha kwake na kupanda gari yake ambayo aliiendesha kwa kasi sana bila kujali kama kuna tatizo zito linaweza kutokea kama angepata ajali na hilo gari lake, alikuwa amechanganyikiwa mwanaume ambaye alikuwa amekufa kwake hakuwa raisi wake tu alikuwa ni rafiki yake mkubwa ambaye walikua wote tangu wakiwa wadogo na kusoma pamoja alikuwa zaidi ya ndugu kwake aliumia mno aliitoa miwani yake na kufuta machozi yake akiwa yupo makini barabarani, alifika nyumbani kwake alimpita mkewe kama hamjui na kwenda chumbani ambako alikaa kwa dakika tano tu na kutoka akiwa amebadilika sura yake alijitahidi kujificha ila ilikuwa inatoa machozi muda wote.
"Who did this to my friend, oooh noooooo it's definitely impossible how can they let this happen?" Alikuwa amepanda kwenye gari yake alitoa simu mfukoni na kuipiga mahali.
"Nitakuwa hapo kwa dakika thelathini zijazo" aliongea kwa uchungu na kukata simu yake alitoka kwake kwa spidi mpaka mlinzi wa getini alibaki anamshangaa sana bosi wake alikuwa ni mtu mpole na alimjua vyema hakuwa mtu wa pombe kabisa kwenye maisha yake leo alikuwa kama mtu aliye lewa kama sio kupandwa na wazimu hata mkewe ambaye alikuwa amesimama juu ya nyumba hiyo ya ghorofa alibaki anamshangaa mumewe kwa hali ambayo alikuwa nayo jioni hiyo. Safari yake ilienda kuishia nje ya nyumba moja kubwa maeneo ya Makongo juu hapo palikuwa nyumbani kwa CDF mkuu wa majeshi wa nchi ya Tanzania mheshimiwa Jaiwelo mkupi makubilo, alikuwa anajulikana sana hapo ila alishangaa leo anavyotaka kuingia alizuiliwa mlangoni na kuulizwa kama alikuwa na miadi ya mtu huyo alimpiga jicho kali sana huyo mlinzi ambaye alimzuia bila shaka alikuwa ni mwanajeshi.
"We mjinga hivi unajua unaongea na nani ambaye unanizuia leo kuingia humu ndani?" Aliongea macho yake yakiwa mekundu wakati huo alikuwa amemkunja mwanajeshi huyo shingoni ilikuwa ni dharau sana kijana mdogo kama huyo kumsimamia jaji mkuu wa serikali na kumzuia kirahisi sana namna hiyo
"Najua lakini tumeambiwa tusimruhusu mtu yeyot....." Kabla hajaongea maneno yake yote simu yake ya mfukoni iliita, aliipokea na kuitikia mara moja tu.
"Nisamehe mkuu" kisha akasogea pembeni kumuacha jaji huyo apite kuonyesha kwamba aliipokea amri ya upande wa pili kumuacha mwanaume huyo aingie ndani bila kupata kizuizi chochote kile.
"We mjinga kwa hiki ulicho kifanya baada ya hapa nitakurudia uelewe namna ya kuishi na watu wakubwa kwenye nchi hii" mheshimiwa jaji mkuu alikuwa kama amechanganyikiwa usoni kwake kulikuwa na machozi mengi kama mtoto mdogo, alinyoosha moja kwa moja mpaka juu kabisa sehemu ya makutano ni wazi alikuwa mwenyeji sana kwenye nyumba hiyo alimkuta mtu ambaye alikuwa amemjia hapo.
"Unajua kilicho tokea?" Alisahau hata kusalimia alimuuliza mtu huyo huku akiwa amemkazia macho kwa hasira sana
"Ndiyo"
"Nina imani utakuwa umejua nani aliye husika na hili kupitia jeshi lako"?" Jaiwelo mkupi makubilo hakuongea chochote alitembea mpaka kwenye droo moja ndogo sana akatoa frashi ndogo na laptop akaja nayo mpaka pale alipokuwa amekaa mheshimiwa jaji mkuu, aliichomeka hiyo frash kwenye hiyo laptop na kuifungua ilionekana video moja tu humo ndani akairuhusu iweze kuanza kisha akaigeuzia kwa mheshimiwa jaji mkuu.
"Yuko wapi huyu shetani" aliuliza kwa hasira sana akifuta machozi yake baada ya kuweza kushuhudia namna mheshimiwa raisi alivyoweza kuuawa.
"Tayari yupo kwenye mikono yetu amekamatwa muda sio mrefu baada tu ya kutenda hili tukio"
"Amewekwa wapi muda huu namhitaji kwenye mkono wangu".
"Mark relax this is not easy as you may think, aliye uawa ni raisi wa nchi sio raia wa kawaida tu mtaani"
"No matter what I'm going to kill this idiot".
"Please don't do that kwa usalama wako na wa familia yako nisikilize kwa sasa tu tafadhali sana usifanye chochote" hakumjibu kitu mkuu wa majeshi zaidi ya kuibeba frash hiyo ambayo ilikuwa na ushahidi wote kisha akarudi zake nyumbani kwake akiwa amechanganyikiwa sana, kumbukumbu zake ziliishia hapo.
**********************
Raia wengi walilaani sana hicho kitendo cha mtu huyo kufanya hilo jambo walitaka auawe mpaka kunyongwa mbele ya mahakama wakiwa wanaona iwe kama fundisho kwa watu wengine, ushahidi kwa asilimia zaidi ya miamoja ulikuwa ukionyesha kwamba ni kweli mtu huyo alihusika moja kwa moja na hayo mauaji lakini mheshimiwa jaji mkuu alikuwa amepokea simu nyingi sana za kumtaka afanye namna yoyote ya kuipindisha hiyo kesi na kutengeneza ushahidi wa uongo ambao ungemuweka salama mtuhumiwa huyo ambaye mpaka muda huo hakuwa akijulikana ni nani. Akiwa ameanza kusoma kitabu chake hicho cha nane ghafla sana radi kali ilipiga umeme ukazima alihema kwa wasiwasi akianza kutokwa na jasho jingi usoni kwake mara simu yake ikaanza kuita kwenye hicho kiza kinene aliangalia namba ilikuwa ngeni kabisa hakuwahi kuiona kabla alisita kuipokea iliita mpaka ikakata. Sekunde kama kumi tu uliingia ujumbe ambao alisita sana kuufungua lakini hakuwa na namna.
"ANGALIA DIRISHANI KWAKO HAPO KWA NJE UTAONA MTU, KAMA KESHO UKIFANYA UJINGA WOWOTE ULE BASI FAMILIA YAKO ITAINGIA KWENYE KUNDI LA WANADAMU AMBAO WALIWAHI KUFA KIKATILI SANA ZINGATIA NILICHO KWAMBIA KESHO SAA NNE ASUBUHI MAAMUZI YAKO NDIYO YATAKAYO AMUA HATIMA YA MAISHA YA FAMILIA YAKO" ni ujumbe ambao ulimfanya aanze kutetemeka sana alitoa kitambaa mfukoni na kujifuta jasho lililokuwa linamtiririka usoni, aliiwasha tochi yake kubwa na kusogea dirishani kukiwa bado kuna kiza cha kutisha nje alifungua dirisha taratibu na kuchungulia nje alimulika tochi alishangaa baada ya kumuona ninja mmoja akiwa na mapanga yake mawili mgongoni amesimama pale chini, alionekana ni muda mrefu sana alikuwa ananyeshewa na mvua muda wote pale aliogopa mno.
Aligeuka nyuma baada ya kusikia kama kuna hatua za mtu lakini akahisi ni kichwa chake hakipo sawa aliyarudisha macho yake pale chini hakuona kitu chochote wala hapakuwa na alama ya uwepo wa mtu alianza kurudi nyuma taratibu kwa uoga aligeuka na kuchomoa bastola yake akainyooshea sehemu ambayo alihisi kuna mtu anakuja ghafla sana umeme ulirudi alishangaa mkewe amesimama mbele yake akimshangaa mumewe ameshika bastola tena ameelekezea kwake, aliishusha na kuiweka mfukoni haraka huku akiwa anatokwa na jasho jingi mno, mkewe alimfuata pale na kumkumbatia akiwa ana mpiga piga mgongoni.
"Punguza mawazo mume wangu najua siku ya kesho inakuumiza sana akili muachie MUNGU ila hakikisha unaamua kile kilicho bora mimi siku zote nipo nyuma yako kwa kila jambo" sauti moja ya kinanda mrembo sana ilimfanya atabasamu kwa mara ya kwanza tangu kuingia kwenye hicho chumba, huyu ndiye binadamu pekee ambaye alikuwa anamjua kuanzia unyayo wake mpaka nukta ya mwisho ya unywele wake kichwani, akiwa mbele ya huyu mwanamke alikuwa anapata amani sana ya moyo aliinama na kumbusu mkewe tumboni ambapo palikuwa pametuna kuonyesha ilikuwa ni mimba kubwa tu.
"Is my son wonderful?" Aliuliza akichekelea kuonyesha wazi aliifurahia mimba hiyo kuwa ya mtoto wa kiume japo moyoni hakuwa na furaha yoyote ile.
"Hahahaha ananipiga mateke tu nafikiri dada yake atafurahia sana akizaliwa maana alikuwa anatamani sana kuwa na kaka yake pale anapokuwa anaonewa" mkewe alijibu huku akijitoa mwilini na kusogea pale mumewe alipokuwa anasomea.
"Jitahidi basi mume wangu uwe unapata muda wa kupumzika na leo usichelewe sana kulala kesho ni siku mhimu sana" alitabasamu baada ya kuisikia sauti ya mwanamke aliye mpenda sana, alimfuata na kumbusu kwenye paji lake la uso.
"Nakuja baada ya nusu saa tu mke wangu" alijibu kiunyenyekevu hakuhitaji kumuudhi mama kijacho wake alitabasamu na kuanza kuelekea mlangoni lakini aligeuka kabla hajatoka.
"Jason umempigia simu kumueleza hichi kinacho endelea?" Swali la mkewe lilimshtua kidogo mwanaume ambaye alikuwa anauliziwa hapo alikuwa ni mdogo wake wa damu kabisa ambaye alikuwa nje kimasomo jina lake alifahamika kama Jason Japhary na walizaliwa wawili tu.
"Anapenda mno kulala yule nitampigia simu baada ya kumaliza kesi kesho usijali" aliongea kikakamavu ila mwili wake ulikuwa unamsaliti alikuwa akitetemeka sana mkewe alimuonea huruma sana mume wake alikuwa kwenye wakati mgumu sana hakuwa na namna aliondoka na kwenda kulala. Jaji mkuu alibaki kwenye hicho chumba lakini hakuwa na mood ya kusoma tena alibaki akiiwazia ile meseji aliyotumiwa pamoja na alicho kishuhudia nje alijikuta akiogopa mno.
Ndo kwanza tunaifungua sehemu ya kwanza kabisa ya hadithi yetu mpya ya INNOCENT KILLER (THE REVENGE), the magic finger mwenyewe nipo na kalamu yangu....Bux the story teller.
TWENDE PAMOJA MPAKA MWISHO
Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app
Msimuliaji: Bux the story teller
Umri: 18+
Sehemu ya Kwanza:
NB: Hadithi hii ni ya kubuni na kufikirika haihusiani na maisha ya mtu yeyote, wala taasisi yoyote wala mamlaka yoyote ile, lengo lake ni kuburudisha na kutoa burudani kwa wasomaji wangu.
ANZA NAYO.........................
Saa 6:59 za usiku kukiwa na kiza kinene na mvua kali sana nje kukisindikizwa na radi zisizo isha pamoja na upepo mkali wakati huo wa usiku kwenye chumba kimoja kidogo cha vitabu ambacho ndani yake anaonekana mwanaume mmoja akiwa kwenye meza ndogo ambayo alikuwa akiitumia kusomea anapokuwa ndani ya hicho chumba mbele yake palikuwa na vitabu kumi ambapo saba alikuwa ameviweka pembeni kuonyesha alikuwa amevisoma vilibakia vitatu ambavyo navyo ilikuwa ni lazima avimalize usiku huo huo kabla hakuja pambazuka. Vitabu vyote kumi vilikuwa ni vitabu vya sheria ya nchi ya Tanzania, aliangalia saa yake mkononi muda ulikuwa umeenda sana lakini hakuwa na namna ya kufanya ilikuwa ni lazima atimize kile ambacho kilikuwa mbele yake alipiga miayo na kuiweka vizuri miwani yake usoni akainama kinyonge sana kwenye kitabu huku akiwa na mawazo lukuki kwenye kichwa chake.
"Sina uhakika wa maisha yangu kuwa marefu baada ya kesho kwa maamuzi nitakayo yaamua najiona kuwa na maisha mafupi mno lakini mimi siwezi kuipindisha sheria ambayo nimeisomea kwa muda mrefu na naijua vizuri kuliko hata herufi za jina langu eeh MUNGU naomba unisaidie na kuniongoza katika hili" alitoka kwenye mawazo na kuivuta pumzi ndefu sana kisha akatulia na kuinamia chini kukipitia kitabu cha nane kati ya vile kumi ambavyo ilikuwa ni lazima amalize kuvisoma usiku huo.
Markvelous Japhary jaji mkuu wa nchi ya Tanzania ndilo lilikuwa jina la huyu mwanaume ambaye alikuwa ndani ya makataba yake ndogo nyumbani kwake akiwa anaendelea kujisomea vitabu vya sheria ambazo alizijua kiundani kuliko binadamu yeyote kwenye nchi yake. Kesho yake alikuwa na kesi kubwa sana ya kuitolea hukumu mbele ya mahakama ambayo ilikuwa inasubiriwa na taifa zima na ni tukio ambalo lilikuwa linaenda kurushwa na kushuhudiwa moja kwa moja mbele ya watu wote ndani ya nchi hii, alikuwa anaenda kuifanyia maamuzi kesi moja ya gaidi mmoja ambaye alikuwa na shutuma mbaya za kuweza kumuua mheshimiwa raisi wa nchi ya Tanzania kwa kumpiga risasi tano kwenye kichwa chake.
Alivuta kumbukumbu zake vizuri siku mbili zilizopita akiwa ndani ya ofisi yake maeneo ya posta simu yake ya mfukoni iliita aliiangalia alikuwa ni mheshimiwa makamu wa raisi aliipokea na kupokea taarifa nzito ambazo zilimfanya aache kila alichokuwa anakifanya aliambiwa kwamba raisi wa nchi ya Tanzania alikuwa amefariki dunia kwa kuuawa msako ulikuwa unafanyika kuweza kumpata mhusika na tayari kuna watu wamekamatwa kwa ajili ya mahojiano, hakuendelea na kazi tena siku hiyo alibeba kila ambacho kilikuwa ni cha kwake na kupanda gari yake ambayo aliiendesha kwa kasi sana bila kujali kama kuna tatizo zito linaweza kutokea kama angepata ajali na hilo gari lake, alikuwa amechanganyikiwa mwanaume ambaye alikuwa amekufa kwake hakuwa raisi wake tu alikuwa ni rafiki yake mkubwa ambaye walikua wote tangu wakiwa wadogo na kusoma pamoja alikuwa zaidi ya ndugu kwake aliumia mno aliitoa miwani yake na kufuta machozi yake akiwa yupo makini barabarani, alifika nyumbani kwake alimpita mkewe kama hamjui na kwenda chumbani ambako alikaa kwa dakika tano tu na kutoka akiwa amebadilika sura yake alijitahidi kujificha ila ilikuwa inatoa machozi muda wote.
"Who did this to my friend, oooh noooooo it's definitely impossible how can they let this happen?" Alikuwa amepanda kwenye gari yake alitoa simu mfukoni na kuipiga mahali.
"Nitakuwa hapo kwa dakika thelathini zijazo" aliongea kwa uchungu na kukata simu yake alitoka kwake kwa spidi mpaka mlinzi wa getini alibaki anamshangaa sana bosi wake alikuwa ni mtu mpole na alimjua vyema hakuwa mtu wa pombe kabisa kwenye maisha yake leo alikuwa kama mtu aliye lewa kama sio kupandwa na wazimu hata mkewe ambaye alikuwa amesimama juu ya nyumba hiyo ya ghorofa alibaki anamshangaa mumewe kwa hali ambayo alikuwa nayo jioni hiyo. Safari yake ilienda kuishia nje ya nyumba moja kubwa maeneo ya Makongo juu hapo palikuwa nyumbani kwa CDF mkuu wa majeshi wa nchi ya Tanzania mheshimiwa Jaiwelo mkupi makubilo, alikuwa anajulikana sana hapo ila alishangaa leo anavyotaka kuingia alizuiliwa mlangoni na kuulizwa kama alikuwa na miadi ya mtu huyo alimpiga jicho kali sana huyo mlinzi ambaye alimzuia bila shaka alikuwa ni mwanajeshi.
"We mjinga hivi unajua unaongea na nani ambaye unanizuia leo kuingia humu ndani?" Aliongea macho yake yakiwa mekundu wakati huo alikuwa amemkunja mwanajeshi huyo shingoni ilikuwa ni dharau sana kijana mdogo kama huyo kumsimamia jaji mkuu wa serikali na kumzuia kirahisi sana namna hiyo
"Najua lakini tumeambiwa tusimruhusu mtu yeyot....." Kabla hajaongea maneno yake yote simu yake ya mfukoni iliita, aliipokea na kuitikia mara moja tu.
"Nisamehe mkuu" kisha akasogea pembeni kumuacha jaji huyo apite kuonyesha kwamba aliipokea amri ya upande wa pili kumuacha mwanaume huyo aingie ndani bila kupata kizuizi chochote kile.
"We mjinga kwa hiki ulicho kifanya baada ya hapa nitakurudia uelewe namna ya kuishi na watu wakubwa kwenye nchi hii" mheshimiwa jaji mkuu alikuwa kama amechanganyikiwa usoni kwake kulikuwa na machozi mengi kama mtoto mdogo, alinyoosha moja kwa moja mpaka juu kabisa sehemu ya makutano ni wazi alikuwa mwenyeji sana kwenye nyumba hiyo alimkuta mtu ambaye alikuwa amemjia hapo.
"Unajua kilicho tokea?" Alisahau hata kusalimia alimuuliza mtu huyo huku akiwa amemkazia macho kwa hasira sana
"Ndiyo"
"Nina imani utakuwa umejua nani aliye husika na hili kupitia jeshi lako"?" Jaiwelo mkupi makubilo hakuongea chochote alitembea mpaka kwenye droo moja ndogo sana akatoa frashi ndogo na laptop akaja nayo mpaka pale alipokuwa amekaa mheshimiwa jaji mkuu, aliichomeka hiyo frash kwenye hiyo laptop na kuifungua ilionekana video moja tu humo ndani akairuhusu iweze kuanza kisha akaigeuzia kwa mheshimiwa jaji mkuu.
"Yuko wapi huyu shetani" aliuliza kwa hasira sana akifuta machozi yake baada ya kuweza kushuhudia namna mheshimiwa raisi alivyoweza kuuawa.
"Tayari yupo kwenye mikono yetu amekamatwa muda sio mrefu baada tu ya kutenda hili tukio"
"Amewekwa wapi muda huu namhitaji kwenye mkono wangu".
"Mark relax this is not easy as you may think, aliye uawa ni raisi wa nchi sio raia wa kawaida tu mtaani"
"No matter what I'm going to kill this idiot".
"Please don't do that kwa usalama wako na wa familia yako nisikilize kwa sasa tu tafadhali sana usifanye chochote" hakumjibu kitu mkuu wa majeshi zaidi ya kuibeba frash hiyo ambayo ilikuwa na ushahidi wote kisha akarudi zake nyumbani kwake akiwa amechanganyikiwa sana, kumbukumbu zake ziliishia hapo.
**********************
Raia wengi walilaani sana hicho kitendo cha mtu huyo kufanya hilo jambo walitaka auawe mpaka kunyongwa mbele ya mahakama wakiwa wanaona iwe kama fundisho kwa watu wengine, ushahidi kwa asilimia zaidi ya miamoja ulikuwa ukionyesha kwamba ni kweli mtu huyo alihusika moja kwa moja na hayo mauaji lakini mheshimiwa jaji mkuu alikuwa amepokea simu nyingi sana za kumtaka afanye namna yoyote ya kuipindisha hiyo kesi na kutengeneza ushahidi wa uongo ambao ungemuweka salama mtuhumiwa huyo ambaye mpaka muda huo hakuwa akijulikana ni nani. Akiwa ameanza kusoma kitabu chake hicho cha nane ghafla sana radi kali ilipiga umeme ukazima alihema kwa wasiwasi akianza kutokwa na jasho jingi usoni kwake mara simu yake ikaanza kuita kwenye hicho kiza kinene aliangalia namba ilikuwa ngeni kabisa hakuwahi kuiona kabla alisita kuipokea iliita mpaka ikakata. Sekunde kama kumi tu uliingia ujumbe ambao alisita sana kuufungua lakini hakuwa na namna.
"ANGALIA DIRISHANI KWAKO HAPO KWA NJE UTAONA MTU, KAMA KESHO UKIFANYA UJINGA WOWOTE ULE BASI FAMILIA YAKO ITAINGIA KWENYE KUNDI LA WANADAMU AMBAO WALIWAHI KUFA KIKATILI SANA ZINGATIA NILICHO KWAMBIA KESHO SAA NNE ASUBUHI MAAMUZI YAKO NDIYO YATAKAYO AMUA HATIMA YA MAISHA YA FAMILIA YAKO" ni ujumbe ambao ulimfanya aanze kutetemeka sana alitoa kitambaa mfukoni na kujifuta jasho lililokuwa linamtiririka usoni, aliiwasha tochi yake kubwa na kusogea dirishani kukiwa bado kuna kiza cha kutisha nje alifungua dirisha taratibu na kuchungulia nje alimulika tochi alishangaa baada ya kumuona ninja mmoja akiwa na mapanga yake mawili mgongoni amesimama pale chini, alionekana ni muda mrefu sana alikuwa ananyeshewa na mvua muda wote pale aliogopa mno.
Aligeuka nyuma baada ya kusikia kama kuna hatua za mtu lakini akahisi ni kichwa chake hakipo sawa aliyarudisha macho yake pale chini hakuona kitu chochote wala hapakuwa na alama ya uwepo wa mtu alianza kurudi nyuma taratibu kwa uoga aligeuka na kuchomoa bastola yake akainyooshea sehemu ambayo alihisi kuna mtu anakuja ghafla sana umeme ulirudi alishangaa mkewe amesimama mbele yake akimshangaa mumewe ameshika bastola tena ameelekezea kwake, aliishusha na kuiweka mfukoni haraka huku akiwa anatokwa na jasho jingi mno, mkewe alimfuata pale na kumkumbatia akiwa ana mpiga piga mgongoni.
"Punguza mawazo mume wangu najua siku ya kesho inakuumiza sana akili muachie MUNGU ila hakikisha unaamua kile kilicho bora mimi siku zote nipo nyuma yako kwa kila jambo" sauti moja ya kinanda mrembo sana ilimfanya atabasamu kwa mara ya kwanza tangu kuingia kwenye hicho chumba, huyu ndiye binadamu pekee ambaye alikuwa anamjua kuanzia unyayo wake mpaka nukta ya mwisho ya unywele wake kichwani, akiwa mbele ya huyu mwanamke alikuwa anapata amani sana ya moyo aliinama na kumbusu mkewe tumboni ambapo palikuwa pametuna kuonyesha ilikuwa ni mimba kubwa tu.
"Is my son wonderful?" Aliuliza akichekelea kuonyesha wazi aliifurahia mimba hiyo kuwa ya mtoto wa kiume japo moyoni hakuwa na furaha yoyote ile.
"Hahahaha ananipiga mateke tu nafikiri dada yake atafurahia sana akizaliwa maana alikuwa anatamani sana kuwa na kaka yake pale anapokuwa anaonewa" mkewe alijibu huku akijitoa mwilini na kusogea pale mumewe alipokuwa anasomea.
"Jitahidi basi mume wangu uwe unapata muda wa kupumzika na leo usichelewe sana kulala kesho ni siku mhimu sana" alitabasamu baada ya kuisikia sauti ya mwanamke aliye mpenda sana, alimfuata na kumbusu kwenye paji lake la uso.
"Nakuja baada ya nusu saa tu mke wangu" alijibu kiunyenyekevu hakuhitaji kumuudhi mama kijacho wake alitabasamu na kuanza kuelekea mlangoni lakini aligeuka kabla hajatoka.
"Jason umempigia simu kumueleza hichi kinacho endelea?" Swali la mkewe lilimshtua kidogo mwanaume ambaye alikuwa anauliziwa hapo alikuwa ni mdogo wake wa damu kabisa ambaye alikuwa nje kimasomo jina lake alifahamika kama Jason Japhary na walizaliwa wawili tu.
"Anapenda mno kulala yule nitampigia simu baada ya kumaliza kesi kesho usijali" aliongea kikakamavu ila mwili wake ulikuwa unamsaliti alikuwa akitetemeka sana mkewe alimuonea huruma sana mume wake alikuwa kwenye wakati mgumu sana hakuwa na namna aliondoka na kwenda kulala. Jaji mkuu alibaki kwenye hicho chumba lakini hakuwa na mood ya kusoma tena alibaki akiiwazia ile meseji aliyotumiwa pamoja na alicho kishuhudia nje alijikuta akiogopa mno.
Ndo kwanza tunaifungua sehemu ya kwanza kabisa ya hadithi yetu mpya ya INNOCENT KILLER (THE REVENGE), the magic finger mwenyewe nipo na kalamu yangu....Bux the story teller.
TWENDE PAMOJA MPAKA MWISHO
Sent from my TA-1053 using JamiiForums mobile app