Hii ya wake wa viongozi wastaafu kuanza kulipwa ni zaidi ya too much

Nikisema bila machafuko au mapinduzi ya kijeshi huu ujinga hauwezi kuisha huwa sieleweki, lakini bila hayo kutokea utasikia hadi wapenzi wa waliokuwa mawaziri wanalipwa pensheni, na wote wanawekewa kinga ya kutoshtakiwa maisha yao yote.
 
Nikisema bila machafuko au mapinduzi ya kijeshi huu ujinga hauwezi kuisha huwa sieleweki, lakini bila hayo kutokea utasikia hadi wapenzi wa waliokuwa mawaziri wanalipwa pensheni, na wote wanawekewa kinga ya kutoshtakiwa maisha yao yote.
Yaani Nchi iingie kwny zilzala ya vurugu, machafuko na ghasia kwa kuwa tu wake wa Viongozi wanalipwa pensheni ? yaani tuharibu mifumo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kimahusiano kiwepesi wepesi tu?

kwanza tusaidie Nchi iliyoondoa hayo unayotaka yaondolewe kwa njia za ghasia?

kuna watu mna msongo wa mawazo sana Nchi hii, Serikali ianzishe Clinic za ku deal na watu wa aina yako
 
Vituko haviishi kwenye hii nchi iliyo laaniwa kua na viongozi wa hovyo kushinda wengine wote duniani, sasa wanalipwa kwa kazi gani waliyo ifanyia serikali au wananchi 🤔🤔 yani wanakopa Kila siku ili waje kuchezea pesa kwa upumbavu namna hiyo, lile tetemeko lililo tokea Morocco lipite na huku liondoshe hawa wapumbavu nchi ipumue kidogo 😡😡
 
Mbona kama vile nchi hii ina Ufa mkubwa sana wa kujali raia wake?

Yaani mwanajeshi mstaafu kapigana vita Uganda na kaponea chupuchupu mara kadhaa vitani, daktari aliyestaafu miaka ya 1990 na Mungu amempa maisha mpaka leo au Mwalimu aliyekuwa anatumika kwa moyo wote miaka hiyo bahati mbaya kwa serikali HAJAFA hadi leo anapokea kutoka HAZINA shs laki moja kama pension kila mwezi lakini eti wake wa viongozi nao wawe wanalipwa mamilioni 25% ya mishahara waliyokuwa wanalipwa waume zao?

Basi nchi hii ni tajiri sana! Lakini kwa nini haiwakumbuki basi hata hawa wazee waliolitumikia taifa kwa moyo mmoja enzi hizo.

Kumbukeni nazungumzia wastaafu walio staafu zamani 1998 kwenda nyuma kabla ya mifuko ya jamii haijaanza na wanalipwa na Hazina.
Kwanza sidhani kama wastaafu hawa wanazidi 5000 nchi nzima maana wengi wametangulia mbele ya haki waliobaki ni mateso tuu.

Mara ya mwisho kiwango hiki kupanda na kuwa laki moja ni miaka 10 iliyopita wakati wa JK. Waoneeni huruma acheni uchoyo.
Mbona kama vile nchi hii ina Ufa mkubwa sana wa kujali raia wake?

Yaani mwanajeshi mstaafu kapigana vita Uganda na kaponea chupuchupu mara kadhaa vitani, daktari aliyestaafu miaka ya 1990 na Mungu amempa maisha mpaka leo au Mwalimu aliyekuwa anatumika kwa moyo wote miaka hiyo bahati mbaya kwa serikali HAJAFA hadi leo anapokea kutoka HAZINA shs laki moja kama pension kila mwezi lakini eti wake wa viongozi nao wawe wanalipwa mamilioni 25% ya mishahara waliyokuwa wanalipwa waume zao?

Basi nchi hii ni tajiri sana! Lakini kwa nini haiwakumbuki basi hata hawa wazee waliolitumikia taifa kwa moyo mmoja enzi hizo.

Kumbukeni nazungumzia wastaafu walio staafu zamani 1998 kwenda nyuma kabla ya mifuko ya jamii haijaanza na wanalipwa na Hazina.
Kwanza sidhani kama wastaafu hawa wanazidi 5000 nchi nzima maana wengi wametangulia mbele ya haki waliobaki ni mateso tuu.

Mara ya mwisho kiwango hiki kupanda na kuwa laki moja ni miaka 10 iliyopita wakati wa JK. Waoneeni huruma acheni uchoyo.

View attachment 2744590View attachment 2744592
Ccm wabinafsi sana yaan kodi zetu zipo kwa ajili ya kuwalipa watoto wa vigogo waliojazana serikalini na wazazi wao tunahitaji katiba mpya haraka sana tuwez kuleta usawa
 
Mkitaka haya yasitokee ipigeni chini ccm.
Wa tz tuna tatizo moja maovu tunayaona ila zile 10k kipindi cha uchaguzi zinachanganya watu wanasahau hata upewe millioni uchaguzi ukiisha nanhela imeiaha unateeka tena miaka mitano
Kwanini tunawaza suluhisho la kutatua matatizo na serikali ni uchaguzi tu? Hii inafanya ccm nao kujiimarisha zaidi huko na hatuna la kufanya, sio kila tatizo tufikiri kuitoa ccm madarakani ndio suluhu. Ccm washajua hawa wajamaa hakuna wanachoweza kufanya zaidi ya kuwaza uchaguzi tu na huko kwenye uchaguzi wamejipanga vizuri kivyovyote kuhakikisha wanaendelea kubaki madarakani.
 
CCM inatumia utulivu na amani iliyopo nchini KUJIKWAPULIA mali na ukwasi isivyo haki.

Amani na Utulivu ni nyenzo ya maendeleo kwa Umma na siyo kuwasadiia watawala kuwanyonya Watanzania.

Wamelileta hili jambo ili kutututoa kwenye ishu ya bandari

Hii fhambi itawatafuna.
Huku kujisifia amani na utulivu utafikiri Africa nzima ni sisi tu pekee ndio tuna amani na utulivu kwengine kote kuna vita na machafuko. Maana hiyo amani utafikiri kama mlima wa kilimanjaro kwamba tunao pekee yetu.
 
na bado waume zao wameshaiba sana.wana migodi,wana majumba.wana mashamba,mabiashara makubwa,benk kuna hela za kutosha,haya sio matusi kweli?
Nyie si mnasubiri hadi muwatoe madarakani na wao wanakula kwa urefu wa kamba zao hadi muda wao ukiisha wasibaki kizembe.
 
Hizo pesa mara kumi mmngewapa mayatima au kuboresha huduma za kijamii. Yaani mtu kastaafu kapewa pension yake ila bado mkewe naye anahitaji pesa za pensheni mbona wanatamaa sana hawa hivi wanadhani hizo ela watazikwa nazo.

Pesa za upigaji wao wanabeba
Pesa za mikopo na misaada wanabeba
Mishahara wanachukua
Pensheni za waume zao waliostaafu wanabeba
Ajira wanapeana wao kwa wao
Ila bado mengine wanataka

Kweli wa Afrika tumelaaniwa. Viongozi ni wabinafsi wanajali maslahi yao kwanza. Nasemaje mtakufa na hizo pesa mtaziacha mtatueleza siku ya hukumu tuliwapa dhamani ya uongozi na hakuna mlichofanya ee Mwenyezi Mungu tupe subira
 
Kwanini tunawaza suluhisho la kutatua matatizo na serikali ni uchaguzi tu? Hii inafanya ccm nao kujiimarisha zaidi huko na hatuna la kufanya, sio kila tatizo tufikiri kuitoa ccm madarakani ndio suluhu. Ccm washajua hawa wajamaa hakuna wanachoweza kufanya zaidi ya kuwaza uchaguzi tu na huko kwenye uchaguzi wamejipanga vizuri kivyovyote kuhakikisha wanaendelea kubaki madarakani.
Upo sahihi sana mkuu ila hebu tuambie wanabadilishikaje hawa viongozi wetu maana nia ni kuwa na nchi yenye wananchi wenye ustawi
 
Kodi yangu inaenda kwa mchepuko wa fulani.

Sasa nikikwepa mtanilaumu ndugu zangu wana JF?
 
Back
Top Bottom