Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Miss world ni binti mdogo aliyezaliwa masafa ya mbali na Tanzania. Alipofika Tanzania miaka minne iliyopita alitembelea Arusha na kukuta familia zisizo na uwezo wa mlo wa siku wala malazi. Watoto wengi zaidi ya asilimia 20 walibainika kutokwenda shule. Wawapo shuleni wanakosa chakula huku wakitumia muda wa zaidi ya masaa manne kwenda na manne kurejea majumbani kwao.
Binti huyu alishiriki kujenga shule na akajitolea kufundisha. Alijitolea chakula na malazi ikiwemo kuwanunua wanafunzi mavazi. Stori hii imerushwa live na inasambaa mitandaoni. Wanaojadili wanaona kama fedhea kwa watawala wetu huku watawala wakijinadi kwamba inatangaza utalii na kuitangaza nchi yetu.
Kwa maana nyingine watawala tatizo la watoto kukosa shule siyo big deal bali kwao wao wanaona kama video hii inatangaza utalii. Nimesoma comment ya waziri mmoja akisifia video ile akidai imesaidia wengi kuifahamu Tanzania.
Mimi nikawa na Mtizamo tofauti; nilipoona video hii nimejiuuliza Mama Salma Kikwete anakosa nini hadi achukue fedha za wananchi maskini ziwe zake na familia yake kupitia sheria mpya aliyopenyeza bungeni ya mafao ya wenza wa viongozi?
Hao wenza wa viongozi wana umaskini gani hadi wajione wao wanafaa kulipwa mabilioni ya kodi za umma for years huku wananchi wakikosa mlo mmoja?
Huyu binti Miss Worl hana pensheni lakini ana moyo wa Mungu na upendo. Huyu binti siyo Mtanzania ila ameonyesha kujali na kuthamini uhai wa watoto wetu. Huyu binti siyo mweusi bali ametambua kila binadamu anahitaji haki ya elimu na kuishi.
Natambua wenza walio wengi ni wanawake kuliko wanaume. Natambua waliopigania kulipwa mabilioni haya ni wanawake na siyo wanaume. Natambua wanawake wote waliopigania hii hoja wamezaliwa familia bora. Natambua wanawake hawa hawajawahi kuwaza wala kufikia kusaidia yeyote kwa fedha zao kama alivyofanya huyu binti. Wengi wao utumia fedha za umma kuzifanya mali yao na kutumia miradi ya umma kama fadhila kwa jamii.
Wanawake weusi jitafakarini, waume zenu walipopata madaraka walijilimbikiza mali za umma. Mwenyenzi Mungu akakasirika na sasa wakimaliza muda wa huduma wanachokiona mbele yao ni magonjwa na hivyo vile walivyochuma kwa dhulma vimeoza na kuishia kuwatibu kuliko kuvisaza.
Naona wanawake nao wameamua kujilimbikizia mali za maskini kwa msingi wa sheria. Wanawake viongozi wa Tanzania wamewakwa tamaa na nafsi zao zinawaza kuishi kwa anasa pale wenzao wao wanapoostaafu.
Amini Amin nawaambia......kwa kuwa pensheni hii italipwa mkiwa hai na ili msilipwe pensheni hii kwa muda mrefu na kunyonya maskini , Mwenyenzi Mungu anakwenda kuwapa maisha mafupi sana. Kisheria mtalipwa ila kiroho mtalipwa kwa muda mfupi sana.
Haiwezekani binti wa miaka 24 aje kwenye nchi yenye kila kitu akasaidie kulisha watoto wetu huku ninyi mkijilimbikizia mabilioni msiyoyafanyia kazi
Hongera miss world kwakuwainua wanetu.
Binti huyu alishiriki kujenga shule na akajitolea kufundisha. Alijitolea chakula na malazi ikiwemo kuwanunua wanafunzi mavazi. Stori hii imerushwa live na inasambaa mitandaoni. Wanaojadili wanaona kama fedhea kwa watawala wetu huku watawala wakijinadi kwamba inatangaza utalii na kuitangaza nchi yetu.
Kwa maana nyingine watawala tatizo la watoto kukosa shule siyo big deal bali kwao wao wanaona kama video hii inatangaza utalii. Nimesoma comment ya waziri mmoja akisifia video ile akidai imesaidia wengi kuifahamu Tanzania.
Mimi nikawa na Mtizamo tofauti; nilipoona video hii nimejiuuliza Mama Salma Kikwete anakosa nini hadi achukue fedha za wananchi maskini ziwe zake na familia yake kupitia sheria mpya aliyopenyeza bungeni ya mafao ya wenza wa viongozi?
Hao wenza wa viongozi wana umaskini gani hadi wajione wao wanafaa kulipwa mabilioni ya kodi za umma for years huku wananchi wakikosa mlo mmoja?
Huyu binti Miss Worl hana pensheni lakini ana moyo wa Mungu na upendo. Huyu binti siyo Mtanzania ila ameonyesha kujali na kuthamini uhai wa watoto wetu. Huyu binti siyo mweusi bali ametambua kila binadamu anahitaji haki ya elimu na kuishi.
Natambua wenza walio wengi ni wanawake kuliko wanaume. Natambua waliopigania kulipwa mabilioni haya ni wanawake na siyo wanaume. Natambua wanawake wote waliopigania hii hoja wamezaliwa familia bora. Natambua wanawake hawa hawajawahi kuwaza wala kufikia kusaidia yeyote kwa fedha zao kama alivyofanya huyu binti. Wengi wao utumia fedha za umma kuzifanya mali yao na kutumia miradi ya umma kama fadhila kwa jamii.
Wanawake weusi jitafakarini, waume zenu walipopata madaraka walijilimbikiza mali za umma. Mwenyenzi Mungu akakasirika na sasa wakimaliza muda wa huduma wanachokiona mbele yao ni magonjwa na hivyo vile walivyochuma kwa dhulma vimeoza na kuishia kuwatibu kuliko kuvisaza.
Naona wanawake nao wameamua kujilimbikizia mali za maskini kwa msingi wa sheria. Wanawake viongozi wa Tanzania wamewakwa tamaa na nafsi zao zinawaza kuishi kwa anasa pale wenzao wao wanapoostaafu.
Amini Amin nawaambia......kwa kuwa pensheni hii italipwa mkiwa hai na ili msilipwe pensheni hii kwa muda mrefu na kunyonya maskini , Mwenyenzi Mungu anakwenda kuwapa maisha mafupi sana. Kisheria mtalipwa ila kiroho mtalipwa kwa muda mfupi sana.
Haiwezekani binti wa miaka 24 aje kwenye nchi yenye kila kitu akasaidie kulisha watoto wetu huku ninyi mkijilimbikizia mabilioni msiyoyafanyia kazi
Hongera miss world kwakuwainua wanetu.