Hawa wako wapi sasa?

Ktk ulowataja, Dela soul yupo NYC ana mke mtasha, Sindila yupo Cincinati, OH....Jump Around yupo Columbus, Rhymson mara ya mwisho kumwona ilikuwa Bongo safarini Canada, Y-thang nilimwacha Muhimbili akiwa mwaka wa nne, nadhani ni doctor somewhere...............................baadhi ya wengine nasikia mateja, waliovuta haya, lakini life goes on!!.

duu kolumba mwingira..mzee wa OILERS..maskani mikocheni ..TPDC..KUNA kipindi ali join pale muhimbili kusomea pharmacy..alikaa miezi sita tu ..mzee akaenda marekani..

mnawakumbuka LWP[LIVE WITH PURPOSE..kuna kale katoto kao sijui kako wapi sasa.kalikuwa kananata na mistari vizuri sana ]na concert zao pale ukumbi wa korea ..kipindi hicho 2 proud mshamba tu ndio anaingia kuitoka mbeya na raba zake za dh..du ila jamaa alikuwa commercial kichizi ..wakati wenzake wanapiga buru ..yeye alikuwa adaki mike hadi wamdakishe...

tery ..fanani..alioa halafu badaye akawa teja wa nguvu ile buuu..karibuni amere cover ..na alikuwa ana mpango wa kwenda canada..sijui amefikia wapi au kama tayari yupo canada..ila anamlaumu sana prof ..j kwa kuwamwaga ..hasa wanapooongelea kutoa album kama hard b..jamaa anangangania achukue pesa karibu yote..ndio wanashindwana..badala angalau angewavuta wenzake...
 
mhhh sijui lakini kwa jinsi anavyoongea inaonekana alikuwa mjanja mnja huyu halaf si unajua wengine safari zao zilikuwa za kukamatiwa na hivyo hawakuhanithiwa na majitu kama akina aally mrisho au ule upuuzi wa kupelekana Tanga kwenye kambi za kujifunza kufunga kamba

we acha tuuu

anywa you never know lakini watakuja tuu hapa

ebwana hivi uliwahi kuwa member wa USIS katika miaka ya early 90's unajua tena amabo ya TV bongo ilikuwa bado huku Mohammed Farah Aideen alikuwa akipelekana puta na wanyamwezi kule somalia basi USIS walikuwa wanaonyesha 30 minutes video za CBS NEWS ...kama hupajui basi ni pale Tanganyika motors juu ...nadhani mwanakijiji atakuwa anapajua maana yule mwenezu ni mtu wa KLM!


kuna dada mmoja mnene alikuwa pale USIS..mnene hivi ..jina limenitoka kidogo..she was so useful kwenye ile library ..sijui kama bado ipo...
 
Ile library ilikua bonge la source of info kwa watu waliokuwa wanatafuta issues za vyuo Marekani.Waliifunga baada ya 9/11 sijui kama wameihamisha au kuifunga kabisa.Pale ilikuwa funga kazi kuanzia mambo ya theoretical Physics mpaka Ebony.

Brazameni usione ajabu kuna watu walikuwa wanachanganya ujioni kisomo na "Yo Rap Bonanza" kuna mtu anakumbuka video ya "Dar Young Mob" wakati huo wako na "Too Proud"? Moja kati ya videos za kwanza kabisa za muziki wa bongoflava ITV.
 
Mie anga zangu zilikuwa Ilala flats, Kariakoo, Msasani, Migomigo...lakini muda mwingi nilikuwa boarding school mikoani( moro na arusha). Ilala flats pale kuna chizi mmoja anaitwa Nadi sijui unamjua?? Martin Kinguruwe, wakina MT na mob nyingine karibu yupo ipo reading!!!!. Mie nilikuwa na mix, mtaani kwa sana wakti wa likizo za zile break za kumaliza shule, lakini kwa ujumla nilikuwa joni kisomo!!.
Nilikuwa Visa ya Mnyamwezi Jo'burg,SA, wakti wa bomu la Osama!!!.
Nitaku-PM siku nikiwa natia timu kwa "wajameni" kuhusu hilo dili la petroli.

Dah! machizi mnajua nilipata mfadhili au sijui tusemeje jamaa alinunua ticket mbili za game ya ARSENAL lakini huyo mwenzie hakutokea hivyo nikachukuliwa basi nnilipotoka kwenye GAME nikaona bora nijimwage pale CAT & CANARY na ma gooners wangu na hivi ndio nimeingia hapa muda si mrefu...

Jana usiku mliniendesha ma ma story nikaishia kuchapia tuuuu

Ebwana lile bomu la 98 nakumbuka na watu kibao walienda kuchulkulia visa MALAWI na chi zingineza ...unajua ubalozi wa USA Dar kulikuwa na dada mmoja wa kidosi alikuwa mnoko ile mbaya lakini pesa alikuwa anakula anaitwa NAFISA yaani unajua ubalozi hata ulipohamishiwa kule kwa DEWJI kwa muda ikawa bado kuna noma lakini waliokwenda nchi za nje walitusua...


Talka about ILALA FLATS basi mie nilikuwa nafunga sana pale maana enzi hizo ndio CHALA BOY ndio karudi toka ITALY na kama DOLA LAKI MBILI na uchee...halafu 2PAC naye ndio kavuta basi sie tulikuwa tunasikiliza ME AGAINST THE WORLD all day

Ilala flats pale kulikuwa na vijiwe viwili, cha mwanzo ni kile kilicho kwenye magorofa ya kule mwisho kwa kama unataka kwenda hospitali au kwenye ile baa ya MNYALUKOLO...kijiwe kile kilikuwa ni cha watu wa safari za SOUTH AFRICA yaani machizi wale hata siye hatukutaka ku mess about nao

Kijiwe cha pili kilikuwa kile chini ya kwa akina brazameni FRANCIS...na pale kulikuwa na mabitozi wote AKINA MANI KUYAGA, JEY C, SAIDI MOLEL (nasikia kawa junky sikuhizi) na jamaa wengine

ebwana unamkumbuka ZAWIYA? ebwana nasikia ana watoto wawili halafu anazidi kuwa mzuri


Nyie Masela niliwahi kuwa uliza nani anamfahamu Fillipino... wa karibu na train station?... alikuwa na kiosk chake pale na bidhaa nyingi mle ndani zilikuwa zile za 'madili'... kama mnamfahamu, yuko wapi hivi sasa tafadhali nijulisheni..

SteveD.

Filipino kabla hajahamia kule upande wa RELI alikuwa huku pembeni ya HOTELI YA STEAK INN opposite na lile jengo la USALAM WA TAIFA huku stesheni enzi hizo tulikuwa tunapanda ma UDA tokea pale

Filipino nimemuuzia sana CD japo alikuwa ananidhulumu ile kinoma na zaidi ya hayo kama ukiibiwa redio au amplifier au chombo chohcote za muziki basi ukionana na yule mtu mfupi utapata tuu mali yake ...halafu ilikuwa kama dini JAMAA ALIKUWA HAFUNGUI SIKU YA ALHAMIS!

unataka nikupe zaidi za FILIPINO?

Umenikumbusha simu za muhimbili kule karibu na mabweni ya mademu wa nursing!!! mzee mtu ulikuwa uchelewi kuua ndege wawili kwa jiwe moja(maana unapiga simu na kama zali lako unaibuka na choposi ya kinesinesi).
Kwahiyo wewe mambo ya "longroom" kule docks hayakupanda kabisa eeenh!!??.
Unakumbuka vile vichochora vya somora vinavyokuunganisha na upande wa pili(sijui ndio indira ghandi ile, kwa uzazi na vifo na bills), vilikuwa na mageti upande mmoja........basi tumewaliza sana wakina "alphonsi" ktk yale mageti kwa kuwaacha solemba!!!.

SASA KABLA YA KWENDA MUHIMBILI MANENO ILIKUWA KWA BABU MTAMA MCHUNGU PALE OPPOSITE NA LANGO LA JIJI

jamaa alikuwa anatoa visa zaUSA kuliko state dept wenyewe, achilia mbali hizo za kwenda India. Na pale mle ndani kwake kabla hujaingia ilikuwa lazima ujieleze kwenye simu na marufuku kuingia na viatu japo pale nje kulikuwa na majunki wanayoyoma baada ya kupata vikete viwili vitatu

Nani hapa anaijua Mande Guest House?

nini mande guest house, how about UGWENO GEST HOUSE pale magomeni nyuma ya ya JABA MOTORS? au ile guest ya EXANADU kule mwananyamala?

Hamna noma wala nini masela wangu, nimekuelewa...Na kuhusu mabasi ya mashirika ya umma kwa ajili ya madenti vipi mnayakumbuka, kupandia pale Jangwani, pia kulikuwa na stop over sehemu kadhaa, yakifika Forodhani yamesha jaa, watoto soft wa Forodhani walikuwa hawawezi kuning'inia milangoni.. ... daah, ilikuwa vurugu kichizi... wengine tulikuwa tunazuga tu... kuvizia form 2 wa zanaki, maana ngamia walikuwa wanapenda wasongo toka Azania...

UDA tulikuwa tunapanda stesheni sasa baada ya kuondoka UDA ndio zikaja zile CHAI MAHARAGWE na nakumbuka watu wa MASAKI wakuwa wanakula dala dala lao la KABIBIII ambalo lilikuwa halifuati taa za bara barani kisa mwnye GARI alikuwa ni TRYPHON MAJI ambalo lilikuwa linapiga tripu za MASAKI STESHENI

na watu wa MIKOCHENI B akina quick mover walikuwa wana chai mahagwe lao linaitwa CHICAGO BULLS ambalo of course sie wengine tulikuwa tunalipanda kama STAFF japo ni madenti tena tunakaa mbele huku tunabadilisha zile tape zetu za CHROME...nakumbuka ARIS alitumia tapes from London nilizisahau mle moja ilikuwa ni ya MILLYVANILLY na nyingine ilikuwa ya LISA STANSFIELD halafu mika ile lile ngoma la BEEN AROUND THE WORLD AYAYAYAA I CANT FIND MY BABY lilikuwa ndio linatamba ile kinoma

then akaja NIKAS na mshikaji wake wakaja na MBASI WAO huoooo, jina limenitoka lakini kama mnavyomjua nikas, basi lake lilikuwa linapandisha madenti wa kule kwa kanali MASAWE FREE na pili lilikuwa na mziki bomba ile mbaya


Naikumbuka hiyo nikiwa form one Tambaza kabla ya kurushwa mkoani. Ikatokea na ile michango ya sijui umoja wa vijana ili kununua mabasi ya wanafunzi.......ule mradi sijui uliishiaga wapi??.
Kuna bar moja inaitwa "kwa kabila" ipo mtaa wa kiwanuka kwa ndanindani hivi sijui mnaijua?!.

Naijua sana ile baaa ...ebwana ule mradi wa basi unajua ulianshiwa na yule KHALID wa MAKONDEKO lakini naye alikuwa anatumiwa tuu na akina MARY CHIPUNGAHELO zaidi hii itabidi MASATU atakupeni midata zaidi ya ule mradi

Nyani,
Leo NY Jets wanakandamizwa pale gillete stadium. Lakini kuna snow ya kutosha, maana ni double punches(ya kwanza ilikuwa thursday na leo nyingine). Pats wana usongo nao sana, kwasababu jamaa walipakazia ile issue ya ku-spy wakiwa kwenye mazoezi....kama unakumbuka first week, mpaka belchick akawa fined. Mungu si Athumani, wamerudi kwenye chopping block bila ya kutaka!!!. Game itachezwa, rain, snow or shine na Pats watakuwa kidedea. Go Pats!!!.

talk about mamabo ya unyamwezini ebwana vipi umenunua ile DVD ya CRIMINALS GONE WILD? ninayo link hapa uanweza kuitazama BURE hapa niambie kama huna nikuwekeee link hapa?

zangu zilikuwa ilala kotaz......jioni lazima mazee nitie timu jangwani kupiga tizi....baadaye nikahamia zangu sinza uzuri nikajiunga na Abajalo....mazee nilikipiga sana pale na safari buti zangu (Bora made) mazoezini nayakati fulani za weekend nilikuwa nazuka kuangalia ngoma za kimakonde kule msasani (zilikuwepo kila jpili).....baadaye jioni nilikuwa najiunga pale nje ya Drive-Inn na washikaji tunapiga mihogo yetu ya kuchoma na pilipili huku tukicheck sinema bubu........wakati huo Julius Nyaisanga anatuburudisha na "Ring my Bell" izaa ya biashara RTD

eee bwana Nyani naikumbuka sana Mande Guest House.....................duuh mshikaji umenikumbusha mbali sana

haya sasa nani kati yenu alikuwa anaenda kwa wanawake wa kihaya kule uwanja wa fisi? mie sijawahi lakini najua wengi walikuwa wanaibuka kule kimya kimya...lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa sometimes nilikuwa nakamatia pale kwa macheni hali ikiwa ngumu si unajua tena, shilingi mia tano tuuuu...yaani mie mpaka leo mzima nashukuru mungu maana dah haya mambo ya kuokota okota nilikuwa noma maana wale wauza samaki uswahilini usiki mie twende ...ebwan Drive inn pale kulikuwa na hao wauza samaki usiku bwana loh! we acha tuuu

haya nani kati yeni anakumbuka lile jumba la sinema la EMPIRE? HALAFU PALE NJE KULIKUWA NA empire video YAANI RAHA TUPU MWANANGU MAANA ukisku mnaenda kucheki DJANGO STRIKES AGAIN halafu kesho yake mnakodisha video ya AMERICAN NINJA au MISSING IN ACTION....

sasa huyo JULIUS NYAISANGA kabla hajaja DAR toka kwao huko bara kulikuwa na EDA SANGA external service si nyimbo za diana ross hiziooo

halafu RTD walikuwa na mtangazaji wao mmoja alikuwa kiitwa ANGALIENI MPENDU na kipindi chake cha KIJARUPA now top that!

QUOTE=phillemon mikael;111728]duu kolumba mwingira..mzee wa OILERS..maskani mikocheni ..TPDC..KUNA kipindi ali join pale muhimbili kusomea pharmacy..alikaa miezi sita tu ..mzee akaenda marekani..[/QUOTE]

Kolumba nasikia alipata scholarship au sijui ndio GREEN CARD na sasa hivi ana heshima mtingio mmoja su unajua huyo Unyamwezini si mchezo

mnawakumbuka LWP[LIVE WITH PURPOSE ]na concert zao pale ukumbi wa korea ..kipindi hicho 2 proud mshamba tu ndio anaingia kuitoka mbeya na raba zake za dh..du ila jamaa alikuwa commercial kichizi ..wakati wenzake wanapiga buru ..yeye alikuwa adaki mike hadi wamdakishe...

mhhh wewe mbona huwelewi? 2 PROUD si kwamba alikuwa ni mshamba...2 proud bado ni MSHAMBA na hata alipobadilisha jina kaaanza kujiiita MR2 bado akawa ni mshamba na mbka hivi alipojilipua huko Leicester kama mrudi bado ni MSHAMBA, nadhani wajanja wao walikuwa EBONY MOALIM ambaye CD alikuwa ana zitengenezea Dubai na of course brazameni MR PAUL ambaye alitaka kujifanya RALF TRESVANT wetu Bongo

tery ..fanani..alioa halafu badaye akawa teja wa nguvu ile buuu..karibuni amere cover ..na alikuwa ana mpango wa kwenda canada..sijui amefikia wapi au kama tayari yupo canada..ila anamlaumu sana prof ..j kwa kuwamwaga ..hasa wanapooongelea kutoa album kama hard b..jamaa anangangania achukue pesa karibu yote..ndio wanashindwana..badala angalau angewavuta wenzake...

hao tena itakuwa watu wa late 90;s hao apart from Tery

kuna dada mmoja mnene alikuwa pale USIS..mnene hivi ..jina limenitoka kidogo..she was so useful kwenye ile library ..sijui kama bado ipo...

kulikuwa na sister mmoja black american alikuwa very helpful...wewe USIS uliwa unakuna mika ipi? maana mie nilichukua umember tangu walipokuwa AMERICAN LIBRARY sasa hivi imegeuzwa MAELEZO, I am talking about 89/90 then wakairebrand kama USAIS walipohamia kule Tanganyika motors

mkurugenzi pale alikuwa mzaramo mmoja aliyesoma anitwa somebody MWINYIGOHA

Ile library ilikua bonge la source of info kwa watu waliokuwa wanatafuta issues za vyuo Marekani.Waliifunga baada ya 9/11 sijui kama wameihamisha au kuifunga kabisa.Pale ilikuwa funga kazi kuanzia mambo ya theoretical Physics mpaka Ebony. Brazameni usione ajabu kuna watu walikuwa wanachanganya ujioni kisomo na "Yo Rap Bonanza" kuna mtu anakumbuka video ya "Dar Young Mob" wakati huo wako na "Too Proud"? Moja kati ya videos za kwanza kabisa za muziki wa bongoflava ITV.


Ebwana si unajua sie wengine tulikuwa na wazimu wa kwenda Unyamwezini lakini TOEFL tulitaka kuipigia denge matokeo yake tukawa tunaaply Michigan state au vyuo vya WICHITA FALLS halafu ukipata I-20 unashindwa kwenda ubalozini kwani huna Banks statement!

Pale magazeti ya WORD UP na RIGHT ON tulikuwa hayawekwi lakini mwanangu amambo ya WASHINGTON POST, NYTIMES, ES NEWS na BLACK ENTERPRISE ndipo palikuwa mahala pake pale...na kipindi hiko hiko hawa machizi walikuwa wanachana ile kinoma na YO MTV RAPS ndio maana sie wengine tulikuwa hatuko enthiastic saaana na mamabo ya kina 2 proud kwani tulikuwa tunapata vitu direct from Kitchen toka kwa Ed Lover and Doctor Dre kuitia ile mitambo ya TV YA MARINES wa USA ambayo kama antena zako ziko strong ulikuwa unaweza kuinasa

Puma&



of course around the same time ICE CUBE alitoa ile track the the day was a good day na unajua tena LA RIOTS nazo hazikuwa mbali sana

USIS ninavyojua mimi walifunga baada ya Ubalozi wao Dar kupigwa mabomu
 
ebwana ebony moalim mtu wangu kinoma..miaka hiyo ...tangu wakirap yoo..pale coco..ofisi yake[njenje grafix] ikiwa opposite na dtv..uchochoro wa uwani..na demu wake bonna...badaye akahamia mbele pale kitumbini mtaa wa CHAGGA ST..kama vipi ..badae akaingia kwenye ofisi ya kaka yake ilala,njenje records..siku hizi yupo kino..

jamaa ni artist mzuri tatizo kama waazilishi wote hakufanikiwa kutoka..hata ofisi yake alikuwa mtaalamu sana wa kanjanja documents..na watu wengi wasafiri lazima wanamjua...ukitaka namba yake nitakupa!!
 
ebwana naikumbuka hiyo ya jama kufa maji TX noma tupu unaambiwa mwenyewe nimechinga sana mihuri kwa wale vijana wa kichaga pale mbele

duh noma


ebwansi unajua opposite pale akina IPPY MALECELA,KINJE, NA ALBERT MARWA (nasikia kasilimu) walikuwa na ofisi opposite na kile kiji saluni alichoanzia maisha RITA MLAKI na enzi hizo yule binti yake NAMBUA likuwa bomba ile kinoma sema si unajua keshachoka na kuzeeka? yaani market ya watoto wazuri imekuwa saturated ile kinoma unambiwa

huyu kaslimu ili aweke jiko ndani(mtoto wa JK)..lile basi lao lilikuwa linaitwa Bullet Train.

Mwinyigoha yuko State Department, kuna dada mmoja alikuwa anaitwa Rhoda kama sikosei.

Alafu zile beach party za coco beach alhamis usiku usiku watoto wa Tandika wanaingizana saa kumi na moja na vihiace.

mnakumbuka kile kibanda cha kuuza kanda pale opposite na Tanganyika Meat karibia na Leather Land zamani lilikuwa duka la Electronics.

Iddi Janguo alikuwa na rafiki yake mmoja Mpoki(RIP) walikuwa wakikanyagwa kidogo wanaenda nyumbani kubadilisha nguo..

Alafu Kidongo chekundu pale karibia na kwa Hassan Afif kulikuwa na mechi za mchangani John Mwansasu akawa analeta wachezaji wenzake kuongezea majeshi, kulikuwa na timu ya vibaka inaitwa Marolabugi bila kumsahau mwizi wa meter za maji Michuzi.
Enzi hizo stendi ya mabasi ya mkoani hiko Mnazi Mmoja pale, basi watu walikuwa wanaingizwa mjini kila leo. Ukienda KAriakoo basi unamkuta JK, Ditto na RO pale Saigon au kwenye ile baa ya mtaa wa Nkurumah kwa mzee Makange.

Mabitozi wa Shaban Robert na Mzizima walikuwa wanasave pocket money ijumaa wanakweda Fosters.

Umenikumbusha mbali sana kuhusu Nafisa, hivi yule sista du wa Obay aliyekuwa ubalozi wa Uingereza yuko wapi?
 
Nyie Masela niliwahi kuwa uliza nani anamfahamu Fillipino... wa karibu na train station?... alikuwa na kiosk chake pale na bidhaa nyingi mle ndani zilikuwa zile za 'madili'... kama mnamfahamu, yuko wapi hivi sasa tafadhali nijulisheni..

SteveD.

Filipino, jamaa mlanguzi sana yule vitu vyenyewe vilikuwa vya dili lakini dah alikuwa anataka kukuuzia kwa bei ya dukani.
mara ya mwisho alikwua amehamia huku upande wa Station ya reli karibia na clock tower(karibia na ghorofa wanalokaa shemeji zake kusaga).
 
huyu kaslimu ili aweke jiko ndani(mtoto wa JK)..alafu unakumbuka lile basi lao la bullet train?

Tatizo naona niko too fast na watu mnakuwa hamsomi nilichoiandika

hebu ipitie tena post yangu ya mwisho utagundua jina la lile basi la akina NIKAS lilinitoka

tes lilinikuwa linaitwa BULLET TRAIN

mzee uko right kabisa

naona itabidi ni slow down kidogo duh!
 
Tatizo naona niko too fast na watu mnakuwa hamsomi nilichoiandika

hebu ipitie tena post yangu ya mwisho utagundua jina la lile basi la akina NIKAS lilinitoka

tes lilinikuwa linaitwa BULLET TRAIN

mzee uko right kabisa

naona itabidi ni slow down kidogo duh!

Vijana wa Mbagala walikuwa hawapandi basi lolote wanasubiria lile dubwana basi wasikilize mziki tu. Enzi hizo Njaidi anatangaza kipindi cha mziki ITV

Nikas alikuwa akitaka kukufungia mziki basi mfano anatumia wa kwenye basi, alafu akajaga mdosi mmoja anaitwa Intu naye ndio ikawa deal lake akamuingiza mjini Elisante na mziki wa bei rahisi kwenye ile Nissan Patrol yake.

Kuna yule jamaa mmoja wa Wu Tang anaitwa Ommy ana mshikaji wake mmoja anaitwa Njiti na Abdelle unawakumbuka?
 
Filipino alikuwa ananirekodia tracks kutoka CD kwenda kwenye tape wayyy back in the days.
 
hii thread itanipa meltdown...not sure if i can keep up

ha ha ha.... na bado brazameni, utakuwa vapourised kabisa baada ya muda!!

.....je, unakumbuka ujio wa Mv.Dallas (ile meli yenye maktaba), ujio wa papa, na ule ujio wa Mandela ambapo mvua ilinyesha kichizi lakini siye na uniform zetu tulienda mnazi mmoja kusubiria msafara wake tukiwa tumelowa chepechepe.... mara huyoooo akatokeza akiwa na Winnie wake na Mstaafu Rais Mwinyi kwenye lile Rolls Royce jeusi tii wanalolitundika makumbusho...
 
ha ha ha.... na bado brazameni, utakuwa vapourised kabisa baada ya muda!!

.....je, unakumbuka ujio wa Mv.Dallas (ile meli yenye maktaba), ujio wa papa, na ule ujio wa Mandela ambapo mvua ilinyesha kichizi lakini siye na uniform zetu tulienda mnazi mmoja kusubiria msafara wake tukiwa tumelowa chepechepe.... mara huyoooo akatokeza akiwa na Winnie wake na Mstaafu Rais Mwinyi kwenye lile Rolls Royce jeusi tii wanalolitundika makumbusho...

Ebanae lile Rolls Royce la wazi sijui bado linateembea maana nakumbuka kila rais akija lazima apandishwe alafu anapitishwa kutoka Airport/Buguruni/Shule ya Uhuru mpaka Ikulu alafu dhifa ya taifa inatangazwa RTD.

Kila Alhamis mambo ya kwenda kuangalia movie pale Marines ukirudi uswahilini unapambana na wale Polisi wanajiita Farasi weupe.Kulikuwa na watu wanakwenda American Chips?

Nilinunua vitabu kadhaa kwenye MV. Doulos
293488442.jpg
 
Ebana eehh humu lazima watu tunajuana humu maana hizi stori mnazomwaga na watu mnaowataja ni wa karibu sana. Walahi tena nikiwatajia jina langu wote mtanijua.....anybody wanna guess my name?
 
Ebana eehh humu lazima watu tunajuana humu maana hizi stori mnazomwaga na watu mnaowataja ni wa karibu sana. Walahi tena nikiwatajia jina langu wote mtanijua.....anybody wanna guess my name?

Nyani, hata kama nalijua jina lako ndugu yangu siwezi kulitaja hapa. Ni kukiuka masharti ya JF kinamna pamoja na kuwa umeomba kutajwa, naomba tuitane majine yetu tu tuliyo register nayo JF...

Na ni kweli ya kuwa, wengi hapa tunafahamiana. Wengine ni ndugu wa damu haswaa... ila maslahi ya nchi yetu na uhuru wa kuandika tukionacho kina tuchokonoa mioyoni mwetu, katika uficho wa kinamna wa mtandao wa internet, ndicho hicho kinatufanya tuwe tunatofautiana mara kwa mara hapa na pahala pengine ofkozi kukubaliana. Nina uhakika, tukikutana pahala- ile hali ya kuonana ana kwa ana tu itatufanya tufanye mengi katika hali sawia.

SteveD.
 
Icadon, ahsante kwa kunisahihisha katika kuiita hiyo meli jina, Mv. Doulous, nilichapia hapo mwanzo... :)
 
how about mambo ya FOOD EVENING kule SHALIMAR town na watoto wa FORODHANI?

unamkumbuka SINGITIRA? ROZI MLEKWA je?

ZAWADI dada yake MAKUSARO ( yule mix la kijerumani na kibongo) wote walikuwa wanaosma Forodhani
 
Duh page 7 stori karibu zote na wote waliotajwa humu ndani nawafahamu na zingine nimeshiriki, yep si utani wengi humu ndani tunafahamiana bila shaka...

Kifupi:
1. Rhymson sasa hivi anaitwa Zavara Mponjika anaishi Iringa na mkewe na watoto (4 boys)
2. OJ katulizwa kwenye "chuo cha mafunzo" huko Texas
3. KBC alikuwa somewhere in Alabama mara ya mwisho namsikia alikuwa amerekodi na "Fawty Acres and a mule" sijui matokeo
4. Heri Carlos nilikutana naye mwaka jana pale Salamander, anaendelea na biashara yake ila ndio vile
5. Carl Lewis huko hapo NYC
6. Duh kuhusu Tambaza, Pazi, Vijana, USIS, Clouds, coco beach, 7th Floor, Motel Agip, poolside, videos za ITV za rappers enzi hizo, dili za safari, upanga, obay, masaki, ursino, makongo, uswazi temeke wailesi, tandika davis corner, mwananyamala komakoma, yaani hata sijui nianzie wapi niishie wapi...tupo brazameni usione kimya tunalalamikia Buzwagi na siasa kwa saaana ukadhani ndio vile...
 
Lile Rolls Royce la wazi nimeliona mara ya kwanza alipokuja Malkia Elizabeth II hiyo 1979 tumekurupushwa primary tukajipanga pale posta ya zamani tunashangaa shangaa Nyerere anapita na Malkia wanapunga...
 
basi siku hizi kuna sehemu zinaitwa,kigilagila lumo,kiembe mbuzi,mwembe sindimba,kilamba nyoka,mtampwimpwi basi ni burudani tu ya meno na ulimi.
masakani yangu ilikuwapale empressi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom