Watanzania wenzangu wanamikakati wote hapa tunakubaliana na ukweli kwamba Tanzania kuendelea kwa muda mrefu inahitaji elimu. Kuwapiga vita mafisadi ni swala muhimu sana kwa nchi lakini tukikaa chini na kufikiria je ni kitu gani tufanye ili nchi yetu iendelee na iwe na ushindani ni elimu. Hivyo mimi ningependekeza tuanze kumulika ufisadi wa elimu na tujiulize kama elimu ya msingi au ya kidado cha nne inatosha kwa madogo wetu. Shule mpya za sekondari zina hadhi ya chini kuliko shule za mkoloni! kama Kibara, Tambaza, Ilboru, Umbwe, Weruweru, n.k.Vilevile tutoe mawazo mfano mimi nafikiri bado serikali ingetakiwa kukuza shule ambazo zipo badaya ya kujenga shule mpya zenye hadhi ya chini mfano badala ya Ilboru kuchukuwa wanafunzi 800 basi ongeza mabweni na wanafunzi kwani wanafunzi wanahitaji vitu vya msingi kama Library na viwanja vya mpira. Vilevile sisi wote na watoto wa Kikwete wamesoma kwasababu ya imani kuwa elimu ni muhimu hivyo basi JF tuwe mstari wa mbele kuhimiza elimu ya juu. Vilevile tubadilishe mfumo kwa mwanafunzi kusoma miaka zaidi ya kumi na kumaliza shule bila kujua kutumia coputer au hata kusoma hatutafika. Mimi nabahati ya kuja USA na kusoma na kupata elimu nzuri lakini nasikitika na kuwaonea huruma Watanzania ambao hawajapata bahati kama mimi na elimu inafungua mambo sana.