Dr. Ulimboka: Damu yangu iliyomwagika ikawe chachu

huwezi kuamini kamaTanzania inaweza kuwa na mashujaa wa namna hii.hapa naanza kuelewa kwa nini ulimboka alitekwa na kupigwa kinyama.
Niambieni shujaa mwingine aliyewahi kutokea hapa Tanzania.mwili hauna nguvu lakini msimamo uko palepale!

...Ulimboka anaweza akawa Mpiganaji lakini katika hili kwa sababu anachopigania hakina sifa ya kumpa "ushujaa" kwa sababu amesimama upande wa "maslahi"tofauti na upande wa wananchi maskini wanaokufa sasa kwa kukosa matibabu waliokuwa wanayapata kwa sababu madaktari hawapo kazini....

....Kama angewakumbuka wananchi hawa japo kidogo basi angeungana nao hospitalini bila kupata huduma za Madaktari ili ayasikie machungu wanayoyapata,ila kwa kuwa hayupo tayari kuyaonja machungu hayo kwa sababu hayajali na anajali zaidi uahi wake,amsehindwa kuungana nao naye kukimbilia nje kwenye huduma nzuri zaidi,wananchi hawa maskini hawana pa kukimbia,huua ni Usaliti....

...Ndugu yangu,uhai haununuliwi,hawa wananchi maskini uhai wao hautarudi, machungu watakayoyapata ndugu zao wa karibu hayaelezeki,kushiriki kufanya hicho hakuweza kukufanya kuwa Shujaa bali kunakufanya kuwa Msaliti na Muuaji....
 
Ziada ya kipato kukipata kupitia roho za watu huu ni ufreemasons,najiuliza kama mlikuwa hivyo mmefuata nini huko afya,iko wapi kujitolea kwenu kwa ajili ya afya zetu,politcs in profesionals is more harmful than expired medics,
lol drs
nenda hospitali ukaangalie vitoto vinvyokufa kwa kuwa hakuna mitungi ya hewa ya oksijeni.bei ya mtungi mmoja ni kama Tsh 150000 hivi,je tunashindwa kununua au hatuna nia ya dhati ya kufanya hivyo.kimsingi ulimboka anatetea afya bora hata kwa viongozi wetu wa nchi ambao mara zote wanahisi watatibiwa india wakati matibabu ya dharura yanaanzia kwenye zahanati au kituo cha afya au hospitali ya mkoa.
Ni kweli nchi hii imekosa fedha za kututibu au ni mzaha tu?
Kwa nini tusiseme asilimia
0.5 ya mapato ya madini au kodi za wafanyakazi zitarudi kwenye afya?leo hii marekani wakichukia basi ujue wagonjwa wa ukimwi watakosa dawa.kwa nini utegemee hisani kuendesha sekta muhimu kama ya afya?
 
Uungwana unaanzia kwako,madaktari damu yao iwe ya ukombozi,yetu iwe ya kusahulika!kunya anye kuku,akinya bata kaharisha,hata raia ni watu
 
Pamoja na mapungufu ya kibinadamu ila dokta ulimboka anahitaji maombi ya wapenda maendeleo wote mbona viongozi wa serikali wanaingia mikataba mibovu inayogharimu maisha yetu sote lakini tupo kimya kwa nini mbunge awekewe mazingira mazuri halafu dokta anayetibu watu asahaulike?

TK!
U r the GT indeed....

Japo kwa udogo watu wetu wangekuwa wanaliangalia hili Saga kwa jicho hili kama ulivyoeleza!
Drs wangekuwa na mzigo mwepesi na serikali ingefyata.....

Ila kwa bahati mbaya sana mambo hapa kwetu yapo kinyume!

HAKI tunayoichelewesha kwa drs ni haki tunayoipoteza kwetu na vizazi vijavyo.....

Na tutaendelea kuwa taifa la hovyo lenye watu wenye afya mbovu ajabu........
 
...ulimboka anaweza akawa mpiganaji lakini katika hili amepigania "course" ambayo haitaweza kumfanya aitwe shujaa kwa sababu amesimama upande tofauti na upande wa wananchi maskini wanaokufa sasa kwa kukosa matibabu waliokuwa wanayapata kwa sababu madaktari hawapo kazini,kama angekuwa shujaa kweli basi angeungana na wananchi hao na kugoma kupata huduma ili ayasikie machungu wanayoyapata,ila kwa kuwa hayupo tayari kuyaonj machungu wanayoyaonja wananchi maskini kwa sababu ya mgomo,yeye kakimbilia nje kwenye hudum nzuri,wakati hawa maskini hawana pa kukimbia,huo ni usaliti....

...ndugu yangu,uhai haununuliwi,hawa wananchi maskini uhai wao hautarudi, machungu watakayoyapata ndugu zao wa karibu hayaelezeki,kushiriki kufanya hicho hakuweza kukufanya kuwa shujaa bali kunakufanya kuwa msaliti na muuaji....
ila serikali yako ndo shujaa , kwa kuzima midomo kwa kudai haki, ninyi wanachi ndo wajinga kama matababu ni mazuri mbona mlikuwa mnakimbilia kwa babu...loliondo. Au mbona hao mafisadi wenu hawatibiwi hapo....fikiri kabla hujasema
 
Pamoja na kwamba sim-support kupigwa kwake...

Lakini si-support mgomo anaousimamia...

Yeye=waliompiga=wote wauaji.
 
Without vision, people perish...Na wapendao kumwaga damu humchukia mtu asiye na hatia,lakini watu wema huyalinda maisha yake...Mithali 29:10
 
Huwezi kutetea uovu kwa uovu hata siku moja. Kwanza huo ni uzushi, ukitetea haki ya matibabu usiingize madai ya mafao na mapato yako, inakuwa hujafanya kitu. Sasa wewe udai mafao zaidi na gas zaidi? wacheni hayo, kuweni wakweli.
zomba kuwa mkweli!njia ya mazungumzo imechukua muda gani?
Kuna swali mnalikwepa sana...hebu elezea njia ambayo ni effective ya kufikisha ujumbe wa madaktari kwa serikali!
 
Shida yetu watz huwa tunadiscuss mambo juu juu tu. Mfano, hili la madaktari inaonekana wengi hawajaelewa nini madaktari wanataka! Kwa kifupi sana, madaktari wanadai huduma za afya ziboreshwe ili matibabu ya hao mnawaita maskini ziwe bora zaidi. Watz wengi ni wagumu kuelewa sijui kwa nini!!
 
mmefilisika fikra zenu, mmeshiba rushwa hata fikira zenu zinatokea tumboni...shame on you...

Yeyote anaeweka rehani maisha ya watu na kutishia uhai na usalama wao ni gaidi. Huyu Ulimboka ni gaidi "terrorist" wa hali ya juu.
 
kwani kabla ya mgomo walikuwa hawafi? Nini sababu ya vifo vyao....fikiri kabla ya kusema

Well said, kwa sababu hiyo uwepo wa madaktari hauna effect yoyote kwani wogome wasogome watu wanakufa. Nadhani wewe ndiye unatakiwa ufikirie kabla ya kuandika. Kwa ulichokiandika tafsri ni kwamba madaktari hawaponyi kwahiyo hata madai yao hayana msingi. Kitu kingine siyo sahihi kutumia uhai wa watu to procure your personal end hii haina justification katika hali yoyote. Tutumie bongo zetu jamani.
 
zomba kuwa mkweli!njia ya mazungumzo imechukua muda gani?
Kuna swali mnalikwepa sana...hebu elezea njia ambayo ni effective ya kufikisha ujumbe wa madaktari kwa serikali!

Niia ya mazungumzo hata ichukuwe miaka 2, Jee ndio uwe gaidi na kuweka rehani na kuwaweka roho juu wagonjwa wasio na hatia. Wewe leo utafanikiwa kupatiwa mafao yako, na wale wagonjwa wanaotoka roho zao ambao ungeweza kuwatibu.

Huu simply ni ugaidi tu, na jinsi mnayowanyanyasa na kupokea t=rushwa kwenye mahospitali ndiyo maana hamuendelei na kila anaejiweza anakwenda kutibiwa nje. Nyinyi ni magaidi tu na kubwa lenu ndio hilo, sasa lijuwe maana ya kuumwa nini.
 
huwezi kuamini kamaTanzania inaweza kuwa na mashujaa wa namna hii.hapa naanza kuelewa kwa nini ulimboka alitekwa na kupigwa kinyama.
Niambieni shujaa mwingine aliyewahi kutokea hapa Tanzania.mwili hauna nguvu lakini msimamo uko palepale!

Mkuu kwa kweli nimemsikiliza Dr Ulimboka kupitia ITV,nimeumia sana moyoni,ila nimefarijika kuona ya kwamba watanzania wazalendo,wapigania haki wapo tulikuwa hatuwjui tu au walikuwa hajajitokeza,imagine mwili hauna nguvu kweli,bado afya yake haijatengemaa,bado anakumbukumbu za mateso aliyopata,maumivu ya kipigo bado anayo lakini msimamo wake na kauli yake ya kuwaaga wanataaluma wenzie iko pale pale,na kwa kweli kama madaktari mtasaliti maneno aliyowaasa Dr ulimboka wakati anaondoka basi mjue laana itawapata.
Kila la heri Dr ulimboka nami nasema kwa kauli yako sina sababu ya kuogopa kufa kwa kutetea haki,kukataa unyanyasaji na dhuluma dhidi ya fikra mbadala kwa mstakabli wa nchi yetu.
Shime wakuu tuzidi kumuombea na huku tukiendela na mapambano
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom