Kuhusu Hayati Magufuli, Tafakari Inanipeleka Hatupo Sahihi

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,075
Hili linaweza lisiwahusu wote bali waishio kwa imani.

Kristo alitukanwa, alikashifiwa, alidhalilishwa (fikiria mpaka kuvuliwa nguo), alitemewa mate, na mwishowe aliuawa. Yesu, akiwa katika mateso makali katika safari yake kuelekea kuuawa, akijua kabisa hawa wanaomtesa, mwishowe watamwua, alisema, "Baba uwasamehe kwa sababu hawajui walitendalo"

Kristo alijifanya mtu, akauvaa ubinadamu, ili atuoneshe tunavyostahili kuenenda. Kuitwa mkristo maana yake ni kufuata maisha ya Kristo. Japo kwa nguvu zetu, hatuwezi, lakini kwa msaada na neema yake, tunaweza kujaribu kuyafuata maisha ya mfano aliyotuachia.

Papa John Paulo II, alishambuliwa kwa risasi na mturuki Mehmet Ali Agka. Akafanyiwa surgery iliyochukua masaa 10, alipopata tu fahamu, kauli yake ya kwanza ilikuwa:

"Kwanza namsamehe aliyetaka kuniua. Nayaunganisha mateso yangu na ya Kristo Bwana wetu. Nawapa pole waliojeruhiwa pamoja nami". Hivyo ndivyo watu wenye imani tunavyostahili kuwa. Lakini siyo jambo rahisi.

Baadaye Rais Sadat wa Misri akamwandikia barua ya wazi Papa akimwomba msamaha Papa. Barua ile ilikuwa na kichwa cha habari, "NAOMBA MSAMAHA KWA KUTAKA KUMWUA PAPA". Maelezo yake ya ndani, Rais Sadat wa Misri akasema kwamba anamwomba msamaha kwa kutaka kumwua Papa kwa sababu Mehmet ni muislam kama yeye, hivyo waislam wamediriki kutaka kumwua Papa. Japo kiuhalisia, Mehmet hakuwa ametumwa na waislam, na wala hakuwahi kutamka kuwa ni imani yake ndiyo iliyompelekea kutaka kumwua Papa. Bali alisema alifanya jambo lile akiamini baada ya kufanya hivyo, Dunia nzima itamfahamu.

Kauli hizi mbili, ya Kristo na ya Papa John Paulo II, itufikirishe sisi tunaoona tulionewa sana wakati wa utawala wa marehemu. Kuna baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Katika maovu, uovu mkubwa kabisa ni kumwua mtu. Na mtu akitaka kukuua halafu ukanusurika, kumsamehe mtu huyu, na ikiwezekana ukamfanya kuwa rafiki yako, hakika inahitaji neema ya Mungu. Lakini Kristo aliwasamehe wauaji wake. Hii ndiyo tafsiri ya lile neno lake, 'njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na kuelemewa na mizigo ya dhambi, nami nitawapumzisha, hata kama dhambi zenu zitakuwa nyekundu kama damu".

Sijaanzisha mada kwaajili ya kumsema marehemu. Na nawaomba wengine pia mkiweza msifanye hivyo, baki kuwakumbusha ndugu zangu kuwa kuna neema na baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Mandela alikuwa mtu maarufu sana, na watu wote Duniani walimstaajabia sana, kwa sababu ya kuwasamehe makaburu, watu waliomfanya karibia maisha yake yote amalizie gerezani. Waafrika ndani ya chama chake hawakutegemea. Waliamini baada ya Mandela kuwa Rais ulikuwa muda sahihi kwao kulipiza kisasi. Lakini Mandela aliwaambia,

"Kama ubaguzi wa kaburu dhidi ya mtu mweusi haukuwa mzuri, basi pia ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya mzungu hauwezi kuwa mzuri".

Nami nasema, kama tunaamini marehemu alikuwa na kauli mbaya dhidi yetu, nasi tukiwa na kauki mbaya dhidi yake au wale tunaoamini ni watu waliokuwa wake, tutakuwa na tofauti gani na yeye? Tutakuwa na haki gani ya kudai sisi ni bora kuliko yeye? Kama tunaamini kuwa yeye alikuwa mbaguzi au alikuwa na upendeleo, nasi tukafanya jambo lolote la kuwatenga tunaoamini walikuwa ni watu wake, na sisi si tutakuwa pia ni wabaguzi? Tutakuwa na haki gani ya kusema kuwa marehemu alikuwa mbaguzi?

Kwa upande mwingine, kama kuna ukweli wowote wa jambo lolote tunalojua marehemu alilitenda ambalo halikuwa sawa, basi wale waliokuwa karibu sana na marehemu, japo si lazima, wanaweza kuwaomba msamaha hao walioumizwa sana na marehemu. Lakini hata wasipofanya hivyo, haiwi sababu ya wale walioumizwa sana kutosamehe.

Lisu, familia ya Ben Sanane, Azory, Rugemarila, Mbowe, n.k; kwa neema ya Mungu, siku moja wafike Chato, wakafanye ibada na kutamka kusamehe yote. Na tangu siku hiyo, ikawe mwisho kumnena kwa mabaya marehemu, maana ukishasamehe, unakuwa mwisho wa uadui.
 
Hakuna kiongozi anayeingia kwa kusudi la kuua au kuumiza. Hata boko haram wanaumiza na kupambana ili wafikie kutawala na wakifanikiwa hutosikia wameingia sehemu tu na kuua labda kwa sababu maalum.

Magu kama kiongozi alikuwa na nia njema na TZ na wote ni mashuhuda. Kuna wakati baadhi ya wabunge wa chadema walikiri kuwa wakikaa pembeni wanaikubali kazi ya JPM.

Magu alihakikisha anafanya kila jambo ili kuleta ustawi wa watu wake. Kuna vifo vilitokea kwa sababu maalum na vingine vilitokea tu kama vifo vingine.

Enzi za JK albino walikufa sana na wala hawakuuliwa na JK. Hata Daud Mwangosi aliuawa ila hakuuliwa na JK. Lakini kulikuwa na mauaji ya wafanyabiashara wa madini na kuna watu kama kina said kubenea walimwagiwa tindikali.

Hata sasa kuna watu wanakufa pengine sababu sio maarufu. Kuna dada kauawa na wasiojulikana, kuna vijana watano walipotea hadi sasa haijulikani walipo.
 
Tanzania siyo nchi ya kwanza duniani ambayo watawala wake wamevunja haki za binadamu na kuumiza raia. Karibia mataifa yote makubwa yana nakala chafu kuhusu haki za binadamu, ila raia wake wameamua kuyaacha, kukomaa kihisia na kiakili, mwishowe kusonga mbele. Ndiyo, kuna watanzania walifanyiwa vibaya mno, lakini wasipoufahamu ukweli kwamba Magufuli ameshaondoka ila wao wamebaki na maisha yao ambayo inabidi wayaishi vizuri, watachelewa sana.

Wachina walifanyiwa vibaya mno na Mao, mamilioni walikufa huku maelfu wakiingia kwenye lindi kubwa la umasikini. Ila leo hii huwezi kuwakuta wachina wakimtwika lawama marehemu kama kisingizio cha wao kushindwa maisha. Familia za Deng Xiaoping na Xi Jinping, ni miongoni mwa familia ziliozoteswa sana na Mao, lakini hata baada ya Deng na Xi kuukwaa uraisi huwezi kukuta wanamtukana Mao hata siku moja.

Kule ulaya, wayahudi walichinjwa katika idadi ya mamilioni na wajerumani. Leo huwezi kukuta myahudi anamtwika zigo la lawama Hitler, akasahau kuishi maisha yake. Waliyofanyiwa wameyageuza kuwa somo kwao na dunia nzima. Ila sisi Waafrika, ndiyo tumemumizwa kuliko binadamu wengine wote, hivyo lazima tupige kelele dunia ituonee huruma na itulipe kwasababu sisi ni jamii muhimu zaidi. Kinachokera ni kwamba unakuta upumbavu wa hivi unashabikiwa na watu waliobahatika kwenda shule.
 
Wewe umeongea kama Mandela..

Tatizo wala sio Magufuli...since Magufuli kama binadaamu kashamaliza ya kwake ..
Tatizo ni wapambe wanaotaka kuhalalisha maovu yake na kukejeli walioteswa na maamuzi yake..

Hakuna anaemkejeli marehemu wala kumkashifu....
Watu wanawakashifu wafuasi wake wanaondeleza kejeli Kwa walioumizwa na yeye
 
Wewe umeongea kama Mandela..

Tatizo wala sio Magufuli...since Magufuli kama binadaamu kashamaliza ya kwake ..
Tatizo ni wapambe wanaotaka kuhalalisha maovu yake na kukejeli walioteswa na maamuzi yake..

Hakuna anaemkejeli marehemu wala kumkashifu....
Watu wanawakashifu wafuasi wake wanaondeleza kejeli Kwa walioumizwa na yeye

Kabisa, kuna wajinga wanakingia uovu wake kwa kusema eti alileta maendeleo, kana kwamba ili tupate maendeleo ni lazima rais aumize wananchi wake, kisa hawakubaliani na falsafa zake. Kama kuleta maendeleo kunahalalisha ukatili, tulienda kuwasaidia weusi wa Afrika kusini ili iwe nini wakati makaburu walifanya maendeleo kama Ulaya? Magufuli alikuwa rais muovu wala hilo halina mjadala, ni wakati sasa wote walioshirikiana naye kufanya uovu wachukuliwe hatua kali ili tuweze kusamehe, ama watajwe wote na uovu wao kisha waombe msamaha ili tusameheane. Kinyume na hapo hatutanyamazia uovu wa Magufuli hadi tuondoke hapa duniani.
 
Haya Matusi anayorushiwa Magufuli mitandaoni na baadhi ya watu wachache na Rais anayaona na hakemei basi itakua anayafurahia.

Anatengeneza precedent mbaya sana.

Kinachompata Magufuli kitampata na yeye it is just a matter of time.
Wakati musiba anatukana watu Magu alimkemea?

Wakati Ally hapi anawatukana wazee na kuwambia wakae kimya Magu alimkemea?

Au mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu.
 
Haya Matusi anayorushiwa Magufuli mitandaoni na baadhi ya watu wachache na Rais anayaona na hakemei basi itakua anayafurahia.

Anatengeneza precedent mbaya sana.

Kinachompata Magufuli kitampata na yeye it is just a matter of time.
Kipi hicho kilichompata Magu kitampata na yeye?
 
Hili linaweza lisiwahusu wote bali waishio kwa imani.

Kristo alitukanwa, alikashifiwa, alidhalilishwa (fikiria mpaka kuvuliwa nguo), alitemewa mate, na mwishowe aliuawa. Yesu, akiwa katika mateso makali katika safari yake kuelekea kuuawa, akijua kabisa hawa wanaomtesa, mwishowe watamwua, alisema, "Baba uwasamehe kwa sababu hawajui walitendalo"

Kristo alijifanya mtu, akauvaa ubinadamu, ili atuoneshe tunavyostahili kuenenda. Kuitwa mkristo maana yake ni kufuata maisha ya Kristo. Japo kwa nguvu zetu, hatuwezi, lakini kwa msaada na neema yake, tunaweza kujaribu kuyafuata maisha ya mfano aliyotuachia.

Papa John Paulo II, alishambuliwa kwa risasi na mturuki Mehmet Ali Agka. Akafanyiwa surgery iliyochukua masaa 10, alipopata tu fahamu, kauli yake ya kwanza ilikuwa:

"Kwanza namsamehe aliyetaka kuniua. Nayaunganisha mateso yangu na ya Kristo Bwana wetu. Nawapa pole waliojeruhiwa pamoja nami". Hivyo ndivyo watu wenye imani tunavyostahili kuwa. Lakini siyo jambo rahisi.

Baadaye Rais Sadat wa Misri akamwandikia barua ya wazi Papa akimwomba msamaha Papa. Barua ile ilikuwa na kichwa cha habari, "NAOMBA MSAMAHA KWA KUTAKA KUMWUA PAPA". Maelezo yake ya ndani, Rais Sadat wa Misri akasema kwamba anamwomba msamaha kwa kutaka kumwua Papa kwa sababu Mehmet ni muislam kama yeye, hivyo waislam wamediriki kutaka kumwua Papa. Japo kiuhalisia, Mehmet hakuwa ametumwa na waislam, na wala hakuwahi kutamka kuwa ni imani yake ndiyo iliyompelekea kutaka kumwua Papa. Bali alisema alifanya jambo lile akiamini baada ya kufanya hivyo, Dunia nzima itamfahamu.

Kauli hizi mbili, ya Kristo na ya Papa John Paulo II, itufikirishe sisi tunaoona tulionewa sana wakati wa utawala wa marehemu. Kuna baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Katika maovu, uovu mkubwa kabisa ni kumwua mtu. Na mtu akitaka kukuua halafu ukanusurika, kumsamehe mtu huyu, na ikiwezekana ukamfanya kuwa rafiki yako, hakika inahitaji neema ya Mungu. Lakini Kristo aliwasamehe wauaji wake. Hii ndiyo tafsiri ya lile neno lake, 'njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na kuelemewa na mizigo ya dhambi, nami nitawapumzisha, hata kama dhambi zenu zitakuwa nyekundu kama damu".

Sijaanzisha mada kwaajili ya kumsema marehemu. Na nawaomba wengine pia mkiweza msifanye hivyo, baki kuwakumbusha ndugu zangu kuwa kuna neema na baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Mandela alikuwa mtu maarufu sana, na watu wote Duniani walimstaajabia sana, kwa sababu ya kuwasamehe makaburu, watu waliomfanya karibia maisha yake yote amalizie gerezani. Waafrika ndani ya chama chake hawakutegemea. Waliamini baada ya Mandela kuwa Rais ulikuwa muda sahihi kwao kulipiza kisasi. Lakini Mandela aliwaambia,

"Kama ubaguzi wa kaburu dhidi ya mtu mweusi haukuwa mzuri, basi pia ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya mzungu hauwezi kuwa mzuri".

Nami nasema, kama tunaamini marehemu alikuwa na kauli mbaya dhidi yetu, nasi tukiwa na kauki mbaya dhidi yake au wale tunaoamini ni watu waliokuwa wake, tutakuwa na tofauti gani na yeye? Tutakuwa na haki gani ya kudai sisi ni bora kuliko yeye? Kama tunaamini kuwa yeye alikuwa mbaguzi au alikuwa na upendeleo, nasi tukafanya jambo lolote la kuwatenga tunaoamini walikuwa ni watu wake, na sisi si tutakuwa pia ni wabaguzi? Tutakuwa na haki gani ya kusema kuwa marehemu alikuwa mbaguzi?

Kwa upande mwingine, kama kuna ukweli wowote wa jambo lolote tunalojua marehemu alilitenda ambalo halikuwa sawa, basi wale waliokuwa karibu sana na marehemu, japo si lazima, wanaweza kuwaomba msamaha hao walioumizwa sana na marehemu. Lakini hata wasipofanya hivyo, haiwi sababu ya wale walioumizwa sana kutosamehe.

Lisu, familia ya Ben Sanane, Azory, Rugemarila, Mbowe, n.k; kwa neema ya Mungu, siku moja wafike Chato, wakafanye ibada na kutamka kusamehe yote. Na tangu siku hiyo, ikawe mwisho kumnena kwa mabaya marehemu, maana ukishasamehe, unakuwa mwisho wa uadui.
Mkuu, nipitie kesho twende kanisani
 
Lissu na Mbowe walijitutumua kupitiliza


Mbowe kama 'mtoto wa mjini' alitaka kutingisha dola.... kwa sababu zake binafsi, ila kwasababu yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama cha Upinzani akaleta nyodo kisiasa badala ya kutafuta suluhishi la kiutu uzima, ikiwa ni pamoja na kutumia mila na desturi zetu za kutumia wazee...Alishindwa na aombe msamaha.

Kufedhehesha serikali halikubaliki katika nchi yeyote ile. Utoto wake wa mjini ikifuatiwa na vita baridi ya matabaka Nchini na kisasi binafsi cha mjengo wa Familia ndio kilichompeleka kuwa limbukeni wa dola, sio yeye tu hata wengine waliowahi kuwa na madaraka Nchini. Hayo, yakiunganishwa na vita ya kiuchumi ambayo Raisi yeyote yuke Afrika anapambana nayo, kwa maoni yangu yalitengeneza mazingira ya Hayati na Serikali yake kuwa on the defensive....hakika huwezi kupambana na simba aliyepo konani, dhuruba yake ndio aliyopata Mbowe


Lissu kwa kujitutumua na ujuaji pamoja na kudanganywa na Wevi wa Rasilimali, alitengeneza mazingira ya kutokuwepo kwa Usalama. Yaliyomkuta ana massage kila kukicha naye aje atubu, aombe msamaha kwa Watanzania kwa kutengeneza mazingira.
Hatahivyo...Uchunguzi ufanyike, tena wa Wazi.


Taasisi za serikali zilifanya shuguli zake kama taasisi zingine zezote Duniani, ila zilishindwa kumlinda Raisi. They failed! either by design or by negligence. Zitubu, ziwaombe msamaha Watanzania.

Hayati hakuwa muovu kama mnavyotaka kuaminisha umma....ulimbukeni wake wa madaraka makubwa na kutojisitiri kwa kauli unaweza kuwa ni changio kubwa la maadui kutumia mianya inayoachwa na kauli za Wakuu wa nchi, kutumiwa kufanya Uasi wa hali ya juu. Yesu alishabeba dhambi zetu.
Amani ziwafikie.
 
Mpaka iletwe tume ya ukweli na maridhiano, watu waeleze walivyofanyiwa udhalimu na serikali yake hapo kidogo tunaweza kufunga chapter hii ya udhalimu wake lakini Dhalimu yule kaumiza watu sana, tena sana.

1. Mtu anachungulia account ya mtu, akiona ina vimilioni kadhaa anaipiga pini mpaka mgawane pasu kwa pasu

2. Mtu anaiba uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu bila haya.

3. Mtu anabambikizia watu kodi ili kuwatia njaa, kwa malengo maalum ya kisiasa.

4. Mtu anaendesha magenge ya utekaji na kupoteza watu, binafsi nilinusurika sababu ya comments za kawaida tu facebook.

5. Mtu haheshimu katiba, anaichezeachezea tu anavyotaka.

6. Mtu anabambikizia watu kesi, makia ya watu walifungwa jela kwa kesi za kubambikiza sababu ya uchaguzi mkuu etc.

7. Unapiga mbunge risasi mchana kweupe.

8. Unawalinda akina Sabaya, Mnyeti na Makonda wanaumiza watu na kufanya ukatili mkubwa ajabu.

9. Unapora korosho za wananchi kwa mtutu wa bunduki.

10. Unavunja nyumba za wananchi wakati kuna zuio la mahakama. Ulitaka wakimbilie wapi kama hata mahakama nayo hauiiheshimu?.

Aisee usinikumbushe machungu ya yule muovu hafai.
 
Mpaka iletwe tume ya ukweli na maridhiano, watu waeleze walivyofanyiwa udhalimu na serikali yake hapo kidogo tunaweza kufunga chapter hii ya udhalimu wake lakini Dhalimu yule kaumiza watu sana, tena sana.

1. Mtu anachungulia account ya mtu, ukiona ina vimilioni kadhaa anaipiga pini mpaka mgawane pasu kwa pasu

2. Mtu anaiba uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu bila haya.

3. Mtu ansbambikizia watu kodi ili kuwatia njaa, kwa malengo maalum ya kisiasa

4. Mtu anaendesha magenge ya utekaji ba kupoteza watu, binafsi nilinusurika sababu ya comments za kawaida tu facebook.

5. Mtu haheshimu katiba, anaichezeachezea tu anavyotaka.

6. Mtu anabambikizia watu kesi, makia ya watu walifungwa jela kwa kesi za kubambikiza sababu ya uchaguzi mkuu etc

7. Unapiga mbunge risasi mchana kweupe

8. Unawalinda akina Sabaya, Mnyeti na Makonda wanaumiza watu na kufanya ukatili mkubwa ajabu.

9. Unapora korosho za wananchi kwa mtutu wa bunduki.

10. Unavunja nyumba za wananchi wakati kuna zuio la mahakama. Ulitaka wakimbilie wapi kama hata mahakama nayo hauiiheshimu?

Aisee usinikumbushe machungu ya yule muovu hafai.
Mtu mmoja tu huyo,aaaah wacha weee!
 
Hili linaweza lisiwahusu wote bali waishio kwa imani.

Kristo alitukanwa, alikashifiwa, alidhalilishwa (fikiria mpaka kuvuliwa nguo), alitemewa mate, na mwishowe aliuawa. Yesu, akiwa katika mateso makali katika safari yake kuelekea kuuawa, akijua kabisa hawa wanaomtesa, mwishowe watamwua, alisema, "Baba uwasamehe kwa sababu hawajui walitendalo"

Kristo alijifanya mtu, akauvaa ubinadamu, ili atuoneshe tunavyostahili kuenenda. Kuitwa mkristo maana yake ni kufuata maisha ya Kristo. Japo kwa nguvu zetu, hatuwezi, lakini kwa msaada na neema yake, tunaweza kujaribu kuyafuata maisha ya mfano aliyotuachia.

Papa John Paulo II, alishambuliwa kwa risasi na mturuki Mehmet Ali Agka. Akafanyiwa surgery iliyochukua masaa 10, alipopata tu fahamu, kauli yake ya kwanza ilikuwa:

"Kwanza namsamehe aliyetaka kuniua. Nayaunganisha mateso yangu na ya Kristo Bwana wetu. Nawapa pole waliojeruhiwa pamoja nami". Hivyo ndivyo watu wenye imani tunavyostahili kuwa. Lakini siyo jambo rahisi.

Baadaye Rais Sadat wa Misri akamwandikia barua ya wazi Papa akimwomba msamaha Papa. Barua ile ilikuwa na kichwa cha habari, "NAOMBA MSAMAHA KWA KUTAKA KUMWUA PAPA". Maelezo yake ya ndani, Rais Sadat wa Misri akasema kwamba anamwomba msamaha kwa kutaka kumwua Papa kwa sababu Mehmet ni muislam kama yeye, hivyo waislam wamediriki kutaka kumwua Papa. Japo kiuhalisia, Mehmet hakuwa ametumwa na waislam, na wala hakuwahi kutamka kuwa ni imani yake ndiyo iliyompelekea kutaka kumwua Papa. Bali alisema alifanya jambo lile akiamini baada ya kufanya hivyo, Dunia nzima itamfahamu.

Kauli hizi mbili, ya Kristo na ya Papa John Paulo II, itufikirishe sisi tunaoona tulionewa sana wakati wa utawala wa marehemu. Kuna baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Katika maovu, uovu mkubwa kabisa ni kumwua mtu. Na mtu akitaka kukuua halafu ukanusurika, kumsamehe mtu huyu, na ikiwezekana ukamfanya kuwa rafiki yako, hakika inahitaji neema ya Mungu. Lakini Kristo aliwasamehe wauaji wake. Hii ndiyo tafsiri ya lile neno lake, 'njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na kuelemewa na mizigo ya dhambi, nami nitawapumzisha, hata kama dhambi zenu zitakuwa nyekundu kama damu".

Sijaanzisha mada kwaajili ya kumsema marehemu. Na nawaomba wengine pia mkiweza msifanye hivyo, baki kuwakumbusha ndugu zangu kuwa kuna neema na baraka nyingi katika kusamehe kuliko kulipa kisasi.

Mandela alikuwa mtu maarufu sana, na watu wote Duniani walimstaajabia sana, kwa sababu ya kuwasamehe makaburu, watu waliomfanya karibia maisha yake yote amalizie gerezani. Waafrika ndani ya chama chake hawakutegemea. Waliamini baada ya Mandela kuwa Rais ulikuwa muda sahihi kwao kulipiza kisasi. Lakini Mandela aliwaambia,

"Kama ubaguzi wa kaburu dhidi ya mtu mweusi haukuwa mzuri, basi pia ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya mzungu hauwezi kuwa mzuri".

Nami nasema, kama tunaamini marehemu alikuwa na kauli mbaya dhidi yetu, nasi tukiwa na kauki mbaya dhidi yake au wale tunaoamini ni watu waliokuwa wake, tutakuwa na tofauti gani na yeye? Tutakuwa na haki gani ya kudai sisi ni bora kuliko yeye? Kama tunaamini kuwa yeye alikuwa mbaguzi au alikuwa na upendeleo, nasi tukafanya jambo lolote la kuwatenga tunaoamini walikuwa ni watu wake, na sisi si tutakuwa pia ni wabaguzi? Tutakuwa na haki gani ya kusema kuwa marehemu alikuwa mbaguzi?

Kwa upande mwingine, kama kuna ukweli wowote wa jambo lolote tunalojua marehemu alilitenda ambalo halikuwa sawa, basi wale waliokuwa karibu sana na marehemu, japo si lazima, wanaweza kuwaomba msamaha hao walioumizwa sana na marehemu. Lakini hata wasipofanya hivyo, haiwi sababu ya wale walioumizwa sana kutosamehe.

Lisu, familia ya Ben Sanane, Azory, Rugemarila, Mbowe, n.k; kwa neema ya Mungu, siku moja wafike Chato, wakafanye ibada na kutamka kusamehe yote. Na tangu siku hiyo, ikawe mwisho kumnena kwa mabaya marehemu, maana ukishasamehe, unakuwa mwisho wa uadui.
Binafsi nakubaliana na wewe Mkuu, barikiwa Sana Kwa kutenga Muda wako kunena yatokayo Kwa Mungu. Najua si wewe Bali umetumika kama chombo kufikisha ujumbe Kwetu tunaosoma thread hii.
 
Wewe umeongea kama Mandela..

Tatizo wala sio Magufuli...since Magufuli kama binadaamu kashamaliza ya kwake ..
Tatizo ni wapambe wanaotaka kuhalalisha maovu yake na kukejeli walioteswa na maamuzi yake..

Hakuna anaemkejeli marehemu wala kumkashifu....
Watu wanawakashifu wafuasi wake wanaondeleza kejeli Kwa walioumizwa na yeye
Hapana mkuu,watu wanapambana na Magufuli siyo wapambe.
Na mapambano haya yalianza tangu akiwa hai.Sababu kubwa ni maslahi na wivu
 
Wewe umeongea kama Mandela..

Tatizo wala sio Magufuli...since Magufuli kama binadaamu kashamaliza ya kwake ..
Tatizo ni wapambe wanaotaka kuhalalisha maovu yake na kukejeli walioteswa na maamuzi yake..

Hakuna anaemkejeli marehemu wala kumkashifu....
Watu wanawakashifu wafuasi wake wanaondeleza kejeli Kwa walioumizwa na yeye
Maovu yapi?

Unaweza kunitajia maovu ya Magufuli?

Najua huwezi kutaja inabaki kua ni uzushi na uongo.
 
Back
Top Bottom