Dr. Isaack Ndodi: Hisia mchanganyiko

Nafikiri kuna mambo muhimu yanayohitajika kujadili hapa na kutangaza biashara za watu hapa.
 
Nafikiri kuna mambo muhimu yanayohitajika kujadiliwa hapa siyo kutangaza biashara za watu hapa.
 
Nafikiri kuna mambo muhimu yanayohitajika kujadiliwa hapa siyo kutangaza biashara za watu hapa.

hakuna mtu anayetangaza biashara ya mtu, ni mawazo yako tu. akijadiliwa lwakatare, mengi, n.k tunawatangazia biashara zao? changia hoja mkuu
 
Management ya JF ina mipango gani kuwaalika watu kama hawa jamvini kwa manufaa ya wanajamvi wengine? anaweza kuruhusu haki zake kama video kutumika hapa kuelemisha wengine ambayo wanayohitaji elimu zaidi.
Mie nashauri JF kuwa na utaratibu wa kuwapa mwaliko kutoa mada hapa kama wageni waalikwa, si lazima wawe memba.
 
Management ya JF ina mipango gani kuwaalika watu kama hawa jamvini kwa manufaa ya wanamvi wengine? anaweza kuruhusu haki zake kama video kutumika hapa kuelemisha wengine ambayo wanayohitaji elimu zaidi.
Mie nashauri JF kuwa na utaratibu wa kuwapa mwaliko kutoa mada hapa kama wageni waalikwa, si lazima wawe memba.

umenena mkuu. wakuu wa meza walitazame hili
 
Star Tv ina ofisi zake Dar, sio lazima aende Mwanza. Ni kweli ni ghali na kwa mwananchi wa kawaida ni vigumu kupata service zake. Kama mtumishi angetakiwa afanye matibabu asilia kwa bei nafuu, lakini ni ghali hata kuliko virutubisho vya GNLD n.k.
 
Star Tv ina ofisi zake Dar, sio lazima aende Mwanza. Ni kweli ni ghali na kwa mwananchi wa kawaida ni vigumu kupata service zake. Kama mtumishi angetakiwa afanye matibabu asilia kwa bei nafuu, lakini ni ghali hata kuliko virutubisho vya GNLD n.k.

ni kweli kwani ukiangalia star TV asubuhi huwa wanawasiliana mwanza na Dar. Hope hizo safari zake huko MZ ni za kimaslahi zaidi hadi zinapelekea bei za huduma zake kupanda. he is extremely expensive
 
umeongea pwent. Huyu Dr. ni public speaker mzuri sana. Kwa wenzetu huko nje angekuwa mtu muhim sana. Na usemavyo kuhusu kujiunga humu lingekuwa jambo la busara. Labda yupo ila ni kwa vile hatujuani

Pwent? au pont, Any way sio kitu, mtoa mada amesema huyu bwana ni ghali sana, ukitaka kumuona ni Tsh 50,000/= hapo matibabu bado,

Ni vyema tukamuomba akaangalia kipato cha watanzania akapunguza kidogo.
 
Wana JF,Ukitaka kujua thamani ya afya lazima uwe umeugua.Huyu bwana natoa ushuhuda ambao watu wa Hospitali zetu kubwa waliishamtema mgonjwa ambaye hapo zamani alichanjwa katikati ya kifua,ika develop shimo linalotoa usahaa na mwingine unatokea puani. Option ilikuwa kumpeleka India-gharama ilikuwa karibu USD 4600 au kujaribu kwa Ndondi,mimi nikajitolea kujaribu kwa gharama yangu. Ndodi akala 1.6M na huyu mgonjwa akapona na akarudi hizo hosp. kupigwa X-ray mara 5 lile tobo limezibika.Je huyu ni bora angekufa au kwenda India?gharama zake na Ujuzi wake ni sawa na Engineers,Dr's.wapiga boxes nchi za nje,etc etc wanaolipwa thousands of US$/mon kuwaona. Shujaa kwao huwa .....
 
Kwani cha ajabu yeye kuja na kuchangia ni nini? Kwani unadhani wanaochangia humu hawana bei? Si ni kujitolea tu na hata yeye mbona anaalikwa sehemu mbalimbali kama makanisani kuzungumza na halipwi?[/QUOTE]

Huko japo halipwi, huwa anatafuta wateja kama nyie hamfahamu hilo.
 
Binafsi nimekuwa mfuatiliaje wa Vipindi vya Dr Isaack Ndondi kuanzia vile Channel 10 mpaka StarTv. Ukweli ni kwamba kuna baadhi ya mambo ya msingi katika jamii ambayo uwepo wake kwenye screen kumewasaidia wengi. Vipindi vyote hivyo anavifanya kwa gharama zake mwenyewe, kwa hiyo hata gharama zake kimatibabu lazima ziwe juu. Laiti kama watanzania wasingeendelea kuifanya mioyo kuwa migumu na kumsaidia huyu bwana kama basi angekuwa msaada mkubwa jamii

Binafsi huwa napata burudani saaaaafi napokuwa naangalia kipindi chake. Ni zaidi ya comedy . Pamoja na kujaliwa kipaji cha kuongea haraka haraka, pia huwa anajaribu kutumia lugha ambayo inaweza kueleweke kwa kila mtu.

hapo umenenna ni Ze KOMEDI !, hasa kwa wanaoweza kuchambua na kuchagua yanayofaa, kumbuka watanzania walio wengi wanachukua na kuamini yote anayoyasema Ndodi.
 
hapo umenenna ni Ze KOMEDI !, hasa kwa wanaoweza kuchambua na kuchagua yanayofaa, kumbuka watanzania walio wengi wanachukua na kuamini yote anayoyasema Ndodi.

Huyo bwana kwa wasiomfahamu utamuona ni mujuzi. Lakini kwa taarifa huyo bwana hajasomea taaluma ya utabibu. Ukifuatilia mada zake utagundua kuwa anaongea mambo ambayo hana ujuzi nayo. Kwa taarifa halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilimpiga marufuku kuendesha Kliniki yake iliyokuwa magomeni Kagera na kumpiga marufuku kuendesha biashara ya Kliniki eneo lolote la Manispaa hiyo kwa sababu nilizozitaja hapo awali.

Jamani kuweni makini na watu kama hawa ambao wanajiita "Doctor" Wakati hawakuusomea hata hiyo kozi ya 'Rural Medical Aid' nako hawakupita.

Kwa hiyo suala si kujua kuongea au kuwa na ushawishi; Suala hapa je ana taaluma inayotambulika? au ni comedian!!!!!!!
 
Acha kabisa LIBIDOZY kwani tofauti kati ya Buberwa na Dr. Ndondi ni sawa na tofauti kati ya Farao na Musa.

Buberwa ni member wa group ya anti-Christ na nina sema hivi kutokana na hotuba zake ambazo hazina hadhi ya kuitwa mahubiri bali KEJELI zinazosababishwa na UPOFU WA KIROHO.

Dr. Ndondi anakusaidia si lazima ukanunue dawa lakini vipindi vyake ni dawa tosha. ni kweli ni mtu muhimu mno katika jamii ya watanzania ingawaje hawa madaktari wetu wa kuchonga wamemkataza kujitangaza kwa kigezo eti SI RUKSA KIMAADILI YA UTABIBU DAKTARI KUJINADI KWA WAGONJWA. Huyu dokta hata kma hana doctorate ya Darasani lakini ni zaidi sana kuliko hawa wanaozeeka au kufa na utaalam wao bila kmnufaisha mtu zaidi ya familia zao.

Ndondi ni kweli ni public speaker mzuri mwenye mvuto na asiyechosha anapokalia kipindi chake sawasawa. Tunahitaji watu kama hawa katika huu mtandao watusaidie kukaza nati zilizolegea.
 
Ni ujinga kwa kila mganga wa kienyeji kujiingiza katika mambo ya kiuchungaji ili watu wawakubali!Alianza Yahaya Hussein,akaja Ndodi sasa Joseph Kalokola Buberwa wa JKB international nae eti anatoa neno la mungu!Acheni kukufuru mungu kwa kutaka ufalme wa hapa duniani.Kalokola mke kamshinda na wametengana kwa kupigana magumi pale ubungo plaza mimi pamoja na wafanyakazi wake akina Vick,Mrutu na Ndutu ndio tulioamulia hizo ngumi leo nae anafundisha watu jinsi ya kuishi katika ndoa!Aibu.Hawa ni wafanyabiashara tuu wala hawatendi mambo ya mungu,achaneni nao.

Jamani ni shetani aka ibilisi aliwapitia tu hadi wakazipiga za bure ila maandiko yanasema samehe mara 7 sabini! Kwahiyo ameamua kumrudia Mungu wake na kutubu madhambi yake yote :)
 
Kwani Dr Ndondi akija hapa hata kama halipwi hatapata wateja? ninaamini kwa ushuhuda uliotolewa na katabazi, na Dr Ndondi mwenyewe akija kama mgeni mualikwa wa JF wateja watapatikana tu japo lengo la kumualika JF halitakuwa kutafuta wateja. jamani kizuri chajiuza kibaya.....!
 
Huyo bwana kwa wasiomfahamu utamuona ni mujuzi. Lakini kwa taarifa huyo bwana hajasomea taaluma ya utabibu. Ukifuatilia mada zake utagundua kuwa anaongea mambo ambayo hana ujuzi nayo. Kwa taarifa halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ilimpiga marufuku kuendesha Kliniki yake iliyokuwa magomeni Kagera na kumpiga marufuku kuendesha biashara ya Kliniki eneo lolote la Manispaa hiyo kwa sababu nilizozitaja hapo awali.

Jamani kuweni makini na watu kama hawa ambao wanajiita "Doctor" Wakati hawakuusomea hata hiyo kozi ya 'Rural Medical Aid' nako hawakupita.

Kwa hiyo suala si kujua kuongea au kuwa na ushawishi; Suala hapa je ana taaluma inayotambulika? au ni comedian!!!!!!!

sikatai, ila mbona anapewa air time ya kutosha tu pamoja na kutoa mihadhara kibao ttena yenye tija kwa jamii yetu hii? pia bado anaoperate hapo sanitariam magomeni. sioni sababu ya mtu huyu kupigwa vita hivyo ila mamlaka zihakikishe anakuwa fair.
 
hapo umenenna ni Ze KOMEDI !, hasa kwa wanaoweza kuchambua na kuchagua yanayofaa, kumbuka watanzania walio wengi wanachukua na kuamini yote anayoyasema Ndodi.


kaka sioni ubaya kwa hawa waja wakichukua kila kitu kwani hana sumu kiivyo. ni bora huyu kuliko kakobe anayewaambia waumini wake wakae mbali na dhahabu na mapambo, kwamba ni ya miungu!!
 
Huyu bwana anajiita Dr, hakuna lolote. Ufahamu wake wa kutibu maradhi mbalimbali kwa kutumia lishe, kwa mfano mtu ana matatizo ya macho anamwambia kula sana matunda na mboga za majani, hakikisha mboga huzichemshi sana na kama una mafuta ya mawese weka. Jamani ni daktari gani wa muhimbili au hospital yoyote asiyejua umuhimu wa matunda na mboga za majani? Nakumbuka hata shule za msingi wanafundishwa haya. Sasa unatwambia tulipe Tshs. 50,000 kumuona huyu bwana!!! Wizi mtupu.

Mimi nimemuona mara nyingi kupitia star TV na channel ten, sijaona ujuzi wake zaidi ya kuchomoa pesa za watanzania. Nilikuwa nataraji kama wanavyofanya wachungaji wengine kama kakobe, mzee wa upako n.k atowe huduma hiyo bure kwa kondoo wa bwana.
 
Huyu bwana anajiita Dr, hakuna lolote. Ufahamu wake wa kutibu maradhi mbalimbali kwa kutumia lishe, kwa mfano mtu ana matatizo ya macho anamwambia kula sana matunda na mboga za majani, hakikisha mboga huzichemshi sana na kama una mafuta ya mawese weka. Jamani ni daktari gani wa muhimbili au hospital yoyote asiyejua umuhimu wa matunda na mboga za majani? Nakumbuka hata shule za msingi wanafundishwa haya. Sasa unatwambia tulipe Tshs. 50,000 kumuona huyu bwana!!! Wizi mtupu.

Mimi nimemuona mara nyingi kupitia star TV na channel ten, sijaona ujuzi wake zaidi ya kuchomoa pesa za watanzania. Nilikuwa nataraji kama wanavyofanya wachungaji wengine kama kakobe, mzee wa upako n.k atowe huduma hiyo bure kwa kondoo wa bwana.

hapo umetuacha. kwani kakobe na lusekelo wanatoa huduma zao bure?
 
wajameni jana nimemsikiliza tena Dr. ndodi. shuhuda za wagonjwa zinamuweka huru. pia nimegundua kuwa ile gharama yake kubwa inaenda kwa watu fulani kwa vile wale wanaopata ile elimu ya mtandao wanaipata kwa bure na kufaidika nayo. kama watu wangemchangia vya kutosha hapo ingebidi tumhukumu kwa gharama zake. otherwise, the guy is great!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom