Patashika

feyzal

JF-Expert Member
Apr 20, 2016
6,805
12,669
Kabla hujasoma Riwaya hii Nzuri na tamu niweke wazi hapa mimi sio muandishi wa hii riwaya na wala sijawahi kuandika hii riwaya hata neno moja.Pia nitoe angalizo iwapo mwandishi asipomalizia nisipewe lawama.

Nimeileta huku baada ya kuona nzuri na muandishi wa hii riwaya kuhitaji wasomaji wake wa riwaya kuishea sehemu mbali mbali ili kumuongezea umaarufu na urahisi wa kuuza vitabu vyake.Kwakuwa nimeisoma bure bila kuchangia hata senti moja nimeona niilete hapa zipo 3 nitaanza PATASHIKA,SAA 72 KISHA OPERESHENI PANAMA.

Haya kazi kwako kuisoma nakuahidi hutajutia.

Mwandishi:Japhet Sudi Nyang'oro
Simu:0762204166

PATASHIKA: 01

ALISHTUKA TOKA USINGIZINI. Akajituliza pale kitandani kwa sekunde kadhaa, masikio yake yaliweza kusikia moyo wake ulivyokuwa ukidunda kwa kasi. Naam! Baada ya kujituliza kwa muda, sasa akaweza kusikia dhahiri kuwa mlango wa sebuleni ulikuwa unagongwa na hicho ndicho kilichomkatisha usingizi wake mtamu. Kwa kukereka kidogo, alijiinua pale kitandani kisha kivivuvivu alinyoosha mkono wake kuelekea ilipokuwa swichi akawasha taa.
Baada ya kuwasha taa na mwanga kuwa umelishinda giza kwa kutawala kile chumba alichokuwemo, alipepesa macho yake ambayo wakati huu yalikuwa yakijitahidi kuuzoea mwanga. Hii hutokea mara zote mtu anapokuwa kwenye giza kwa muda mrefu au anapokuwa ametoka usingizini kisha akakutana na mwanga mkali kama hivi. Baada ya sekunde kadhaa tayari macho yake yalikuwa yameshauzoea mwanga wa taa, hapo aliyaelekeza hadi ilipokuwa saa iliyokuwa imesimama kama boksi juu ya meza ya kitanda. Saa ilimwonyesha majira kuwa ilikuwa saa nane na dakika kumi usiku. Alishangaa nani angekuwa anagonga usiku wote ule ambao mvua kubwa iliyoambana na radi za ajabu ilikuwa bado inanyesha? Ulikuwa ni msimu wa masika katika eneo hili la Katunguru wilayani Sengerema mkoani Mwanza. Hivyo wakazi wa eneo hilo walikuwa kwenye wakati wa kilimo, kilimo cha mpunga ndicho hasa kilichokuwa kikifanywa na watu wengi. Alitembea hadi sebuleni, hapo akaelekea ulipokuwa mlango wa kutokea nje. Kabla hajafanya lolote mlango huo uligongwa tena, ikabidi achungulie kwanza kwenye tundu la mlango. Mwanga wa taa ya kibarazani ukamwezesha kumwona mtu aliyekuwa anagonga.
“Milka mdogo wangu pole, kuna shida gani usiku wote huu? Ona ulivyonyeshewa na mvua!” Hatimaye Maganga alisema kwa mshangao baada ya kumwona mdogo wake wa damu akiwa amejikunyata pale nje huku akiwa ameloa chepechepe, nguo zikiwa zimemng'ang'ania mwilini kama manyoya ya kuku aliyeloa maji. Badala ya kujibu, Milka aliingia ndani huku akiwa anatetemeka kwa baridi iliyotokana na mvua iliyokuwa imemnyeshea.
“Kaka Maganga…” Milka alianza kuongea kwa shida huku sauti yake ikitetemeka pia.
"Naam, Milka mdogo wangu!” Maganga aliitika.
“Nimeficha kwa muda mrefu sana.” Milka akasita huku akiwa anamwangalia Maganga ambaye wakati huu alikuwa amekwisha ufunga mlango na kuuegemea. Alikuwa na hamu ya kujua nini kilikuwa kimemsibu mdogo wake yule. Badala ya kuendelea, kwikwi ya kilio ilisikika toka kwa Milka. Kusikia hivyo Maganga alimsogelea mdogo wake na kumshika mabegani.
"Niambie Milka, nini kinakutatiza?. Najua umekuja hapa kuniambia, niambie sasa!” Maganga aliongea kwa sauti ya huruma, msisitizo na iliyokuwa na mashaka. Alijua kuna jambo kubwa limemfika mdogo wake huyo.
“Maganga!” Milka aliita na kusita.
"Weee, Milka, hebu acha kufanya hivyo, niambie kuna tatizo gani?” Badala ya kuitika Maganga sasa aliongea kwa sauti ya kufoka kidogo.
"Unanipenda?” Milka alihoji huku akiwa bado kajikunyata huku sakafu aliyokuwa amesimama juu yake ikiwa imeloa maji yaliyokuwa yakiteremka toka mwilini mwake. Maganga hakuweza kuona hilo, kwani muda wote huo walikuwa gizani, taa ya sebuleni haikuwa imewashwa. Mwanga wa taa ya barazani ndiyo iliyokuwa ikipenyeza miale yake kupitia dirishani, miale ambayo hata hivyo haikuwa ya kutosha kuwawezesha kuona vema kila kitu. Mshtuko aliokuwa nao haukumpa nafasi Maganga ya kuwasha taa.
“Swali gani hilo wewe? Wewe wajua!”
“Acha kujibu ki-kasisi, nataka kujua Maganga!” Milka alisema huku akiinua mikono yake kushika viganja vya Maganga ambaye alikuwa amesimama nyuma yake na mikono yake ikiwa imeshika mabega ya Milka huku na huku.
“Unamaanisha nini Milka? Nitaachaje kukupenda na wewe ni ndugu yangu? Kama maandiko yanasema umpende adui, je si sana ndugu yako wa damu?!!
"Simaanishi hivyo Maganga. Oooh! Nasikia baridi. Una chai hapa?” Milka alisema huku akijitoa mikononi mwa Maganga kaka yake.
Japo Maganga alikuwa na hamu ya kujua nini hasa kilikuwa kimemsibu mdogo wake lakini pia hakushindwa kuona jinsi mdogo wake huyo alivyokuwa akiteseka kwa baridi ambayo ilimfanya atetemeke mwili na sauti. Hivyo ombi la Milka kuhusu chai alilipokea kwa uzito uliostahili. Alitembea kuelekea chumbani kwake. Aliingia na kuucha mlango wa chumba hicho wazi. Wakati mkono wa Maganga ukiwa unaifikia chupa ya chai iliyokuwa pembeni mwa kitanda chake chini ya meza ndogo ya kujisomea, alihisi kama kuna nyayo za mtu nyuma yake.
Akiwa bado ameinama pale ilipokuwa chupa ya chai, alitupia macho yake nyuma kupitia katikati ya miguu yake na aliweza kuona miguu. Macho yake yalipanda taratibu toka miguuni mwa Milka kwenda juu, alipofika juu kidogo ya mapaja Maganga alishtuka.
"Milka!” Aliinuka mara huku akipiga kelele. Wala hakuichukua tena ile chupa ya chai. Aligeuka, macho yalimtoka pima.
“Hivi wewe, umechanyikiwa nini? Hiki ndiyo kimekufanya uje usiku wote huu hapa kwangu?” Maganga aling'aka.
“Kaka Maganga, acha kujifanya hutaki. Najua unataka sana usiniambie mafunzo ya Utawa uliyonayo ndiyo yamekufanya usiwe mwanaume kamili...” Milka alisema huku ile sauti ya kutetemeka sasa ikiwa haipo tena. Maganga akabaki amesimama kwa shangao akimwangali Milka.
"Maganga, najua una kiu na unanipenda kama ulivyosema. Hivyo basi, kilichonileta hapa usiku wote huu ni kukwambia kuwa nakupenda sana, na nataka tufanye walau mara hii moja tu kiu yangu ikatike, naomba." Milka aliendelea kusema huku akiwa anatetemeka japo wakati huu sauti yake haikuwa ikitetemeka. Wakati akiongea akawa anamalizia kuvua blauzi toka mwilini mwake. Maganga akajishika kiuno huku macho yake yakiwa yanauangalia mwili mbichi wa mdogo wake. Japo alikuwa haamini kinachotokea lakini, aliendelea kuutalii mwili wa mdogo wake. Alijikuta yuko katikati ya maamuzi. Milka alikuwa amebaki kama alivyozaliwa, akaanza kumsogelea kaka yake, Maganga akaingiwa na huruma iliyochanganyika na tamaa. Wazo kuwa yuko ndotoni likamjia, hakutaka kuamini kuwa jambo lilokuwa linatokea mbele yake lilikuwa ni kweli. Akajaribu kujifinya ili aamke, lakini akajikuta kuwa Milka yuko karibu yake zaidi, wakati huu akaanza kuisikia harufu ya mwili wa Milka. Damu ya mwili wake ikaanza kukimbia kwa kasi mwilini. Mawazo kuwa alikuwa ni Padri mtarajiwa na wakati huu alikuwa kwenye nyumba ya kanisa kama Padri mwanafunzi yalishaondoka kichwani mwake. Lakini hata hivyo ghafula akamudu kusema,“Milka, hebu subiri kwanza mdogo wangu!” Alisema kwa hadhari huku akipepesa macho.
“Kaka Maganga, najua si halali, lakini sina namna nyingine ila kufanya hivi.”
“Unakosea mdogo wangu na kamwe siwezi kukubaliana na hili.” Maganga alisema.
“Sogea hapa ili unione vizuri.” Milka alisema kama anayenong’ona.
“Kaka Maganga, kwani nina kasoro gani au upungufu gani kwenye huu mwili wangu?” Milka alihoji huku safari hii machozi yakiwa yanamtoka tena.


Punde sehemu ya Pili itakujia




PATASHIKA: 02

Milka na...” kauli ya Maganga ilikatishwa na sauti ya mlango wa nje kugongwa. Mara ukagongwa tena!
Hakuna aliyeitikia, walitazamana. Mlango ulipogongwa mara ya tatu, wote wakatazamana tena. Akili ya Maganga ikafanya kazi harakaharaka, hakuwa na hakika mgongaji angekuwa nani na alikuwa anataka nini. Hivyo alimsogelea Milka, akamnong’oneza, “Baki hapa, sina hakika atakuwa nani. Haitakuwa picha nzuri akikukuta hapa ukiwa katika hali kama hiyo. Unajua miye ni nani na kanisa linanichukuliaje. Mbona wanifanyia hivi Milka mdogo wangu? Halafu usisahau wewe ni mdogo wangu pia.”
Wakati Maganga ananong’ona alikuwa jirani sana na Milka, zile pumzi za Maganga sikioni kwa Milka, na ile hisia ya ukaribu ikamfanya Milka amkumbatie Maganga. Miili yao ikakutana. Maganga akaweza kusikia jinsi mwili wa Milka ulivyokuwa wa moto utadhani hakuwa amenyeshewa mvua. Vitu kama umeme viliamsha mishipa yake ya mwili. Wakati akiwa amechanganyikiwa hajui nini cha kufanya, huku Milka akiwa anafanya vitu ambavyo Maganga hakuelewa vina lengo gani, mlango wa sebuleni uligongwa tena, safari hii kwa fujo zaidi.
Maganga akatumia nguvu zilizobaki mwilini, kumsukuma Milka. Milka akaangukia kitandani, Maganga akatoka chumbani kuelekea sebuleni. Milka akabaki kitandani, ameduwaa. Sasa mgongaji alikuwa amekazana kugonga.
“Nani na unataka nini usiku huu?” Hatimaye Maganga aliuliza.
“Paul.” Sauti nzito ilijibu. Maganga mara moja akaitambua sauti hiyo kuwa ni ya baba yake mzazi. Kwanza alichanganyikiwa, lakini akajipa moyo kuwa hakuna baya lilikuwa limefanyika. Ila akajiuliza baba alikuwa anatafuta nini pale usiku huo.
“Ooooh! baba karibu sana. Kuna nini mbona usiku sana kiasi hiki?” Alitoa karibu iliyoambatana na swali huku akifungua lango. Alijitahidi kuweka akili yake sawa.
“Imebidi nije tu, maana nimeona asubuhi ni mbali sana.” Alisema Mzee Paul baba kwa sauti nzito iliyojaa kitu kama ghadhabu huku akiwa anaketi kitini.
“Kuna nini baba?” Maganga alihoji. Maganga aliwasha taa ya sebuleni ambayo hakuwa ameiwasha kipindi Milka alipokuwa amekuja. Mzee Paul alianza kuzungusha macho pale sebuleni baada ya kuwa ameweka pembeni mwamvuli aliokuwa ametumia kujikinga mvua ambayo bado ilikuwa ikiendelea kunyesha. Macho ya Mzee Paul yaliweza kuona alama za miguu pale sebuleni, tena uzoefu wake ulimwambia kuwa ilikuwa alama ya miguu ya kike. Hakutaka kuuliza wala kufuatilia sana, hakutaka kugombana na Maganga, maana aliweza kuona zile nyayo zikiwa zimelekea chumbani. Aliweza kuona kwa vile mwenye nyayo alikuwa ameloana. Si hivyo tu aliweza pia kuona khanga na sketi vilivyokuwa vemelala pale sakafuni. Moyo ulimwenda mbio. Hakutegemea mwanawe ameshaanza mambo ya wanawake. Maganga alikuwa mtu mzima sasa lakini kwa jinsi alivyolelewa kidini na ambavyo Paul amekuwa akihakikisha anakuwa Padri, ilikuwa hakika Maganga hakuwa mtu wa wanawake. Hali hii sasa ilikuwa inampa ujumbe mpya.
“Sikiliza Maganga, nimegombana sana na mama yako, nimemwacha huko nyumbani akiwa katika hali mbaya…”
“Tatizo nini baba?”
“Tatizo ni lile lile Maganga.”
“Lipi hilo? Maana kama ni kuhusu mimi na Milka nadhani tulishakubaliana na limekwisha.”
“Halijaisha mwanangu, mama yako bado hajakubali wewe kuwa Padri na Milka kuwa Sista wa kanisa. Madai yake ni kuwa anataka awe na wajukuu. Yuko radhi mmoja wenu aendelee na wito wa kanisa lakini si nyote…”
“Lakini baba sijaelewa hilo limesababishaje ninyi mpigane usiku huu?” Maganga alizidi kuhoji.
“Kama ujuavyo dada yako Milka yuko hapa kwa mapumziko toka kwenye shule ya Utawa. Tangu amefika kuna mambo yamekuwa yakifanyika kati ya Milka na mama yako ambayo kwa kweli miye siyaelewi au kama nayaelewa basi siko radhi nayo. Ni wazi kuwa mama yako yuko tayari Milka aolewe wakati wowote. Hivi ninavyoongea na wewe Milka hayupo nyumbani, na ugomvi wetu ndiyo umeanzia hapo. Tangu saa tatu usiku nimekuwa nikimuuliza mama yako ili nijue mahali alipokuwa Milka, akawa ananiambia yuko kwa rafiki ake hapa Kijijini. Imeendelea hivyo hadi ilipofika saa saba usiku huu, nilipomuuliza mama yako, akaniambia Milka ni mtu mzima ana uhuru wa kufanya aonalo jema. Hapo ndipo ugomvi wetu ulipoanzia.” Mzee Paul alisema huku akionyesha hasira kuu.
“Baba, umesema mama ana hali mbaya nadhani, twende tukamwone kwanza, tumpeleke hospitali halafu haya mengine tutaongea kesho.”
“Maganga, naomba uongee na mama yako, ajue kuwa siwezi kubadili msimamo wangu na kwa hili niko tayari kulipa gharama yoyote.” Alisema mzee Paul huku akiwa anainuka toka kitini alipokuwa ameketi. Maganga aliingia chumbani akavaa shati kisha akatoka akiwa na ile ile Kaptula aliyokuwa nayo alipompokea Milka. Mwamvuli mkononi, hakutaka kupoteza muda zaidi. Wakatoka nje na safari ya kuelekea nyumbani ikaanza huku mvua ikiendelea kunyesha.
Walipofika nyumbani Maganga aliingia ndani na kupitiliza hadi chumbani ambako mzee Paul alikuwa amemwacha mkewe akiwa hajiwezi kwa kipigo. Kwa mshangao, hakukuta mtu yeyote chumbani humo. Walijaribu kuangalia kila kona.
“Mama ni miye mwanao Maganga, nimekuja, usijifiche, nataka nikupeleke hospitali.” Maganga alipiga kelele akihofia kuwa huenda mama yake alikuwa amejificha kwa woga wa kipigo. Dakika kadhaa zilipita wakiwa wanatafuta bila mafanikio.
Dakika thelathini zilizofuata zikawa za kutafuta na kuuliza kwa majirani kama mke wa Mzee Paul alikuwa huko. Saa nzima ilipita na walikuwa wameshazunguka kijiji kizima bila mafanikio.
“Mwanangu, nenda kapumzike, usije pata matatizo hapa nikashindwa namna ya kumjibu baba Askofu, kumbuka wewe sasa ni Padri mtarajiwa na sherehe yako ya upadirisho ni mwezi ujao.” Mzee Paul alimwambia Maganga kwa sauti nzito ya kubembeleza. Lakini sauti hiyo ilikuwa kama radi masikioni kwa Maganga na mkuki wa moto katika moyo wake. Hakutegemea baba yake angeongea hivyo katika wakati huo ambao mama yake mzazi ambaye ni majeruhi kwa kipigo ikiwa haijulikani alipo. Maneno hayo yalimuumiza moyo wake. Alitembea taratibu kuelekea ilipokuwa nyumba yake ambayo alikuwa amepewa na Kanisa. Moyo wake ulikuwa umekufa ganzi kwa simanzi, na akili yake ilikuwa imejaa wasiwasi. Aliomba kimoyo moyo kuwa Mungu amlinde mama yake popote alipo.
Alipofika nyumbani kwake, alifungua mlango akaingia. Mara hii ndiyo akakumbuka kuwa alikuwa amelowa chepechepe, hakukumbuka mwamvuli wake alikuwa ameuacha wapi. Alipoingia chumbani ndipo tena alipokumbuka kisa cha Milka baada ya kuona mtu amelala kitandani akiwa amejifunika blanketi. Alimwangalia kwa sekunde kadhaa bila kusema neno. Alifikiria kuwa kwa hali ilivyo isingekuwa busara kumwambia Milka aende nyumbani. Hivyo alikata shauri kumwacha Milka alale hapo kwake kwa ajili ya usalama. Maana kama Milka angetokea mbele ya Mzee Paul saa hizi, angemfanya kitu kibaya sana.
“Milka, umesikia habari ya mama na baba?” Maganga aliuliza kwa sauti iliyotoka kwenye koo lililokuwa limeshambuliwa na baridi.
“Nimesikia yote.” Milka alijibu huku akijinyonga nyonga ndani ya blanketi.
“Umesikia?” Maganga alishangaa.
“Ndiyo!”
“Mbona huonekani hata kushtuka Milka.” Maganga alihoji kwa sauti ya mshangao.
“Nilishituka wakati baba anaongea kukutaarifu, ila kwa sasa najua mama yuko salama sina shida.”
“Yuko salama! Kivipi wakati tumetafuta kijiji kizima hatujafankiwa kumpata?”
“Baba alivyosema amempiga mama, mara moja niliwasiliana na Vivian, yule rafiki yangu anayesomea utabibu Ujerumani, ambaye kwa sasa yuko likizo, kama mimi, akaenda kumchukua mama na amempa huduma tayari kwa hivyo mama yuko salama.”
“Nadhani tulale sasa Maganga, acha kujikunyata hapo baridi.” Milka aliongea kisha ghafla akaruka toka kitandani akamrukia Maganga.

Punde nitakuweke sehemu ya 3.

Enjoy, kimya kimya


PATASHIKA: 03

Maganga hakutarajia, hivyo mwili wake ukawa himaya ya Milka kwa sekunde kadhaa kabla hajatumia nguvu kujinasua na kumsukuma Milka pembeni.
“Hivi Milka umeingiwa na nini?” Maganga alihoji kwa hasira, “Huko kwenye mafunzo ya Utawa ndiyo mnafundishwa hivyo?” Aliongeza swali ambalo lilijibiwa kwa tabasamu tu toka kwa Milka. Maganga alimwangalia Milka kwa upya tena safari hii akawa kama anayekiona kwa upya kila kiungo cha mdogo wake, kisha akakumbuka ule mwili wa moto uliomkumbatia kwa sekunde chache kabla hajausukumia mbali. Akainamisha macho chini kukwepa macho ya Milka ambayo safari hii yalikuwa kama yanamsoma baada ya kugundua jinsi alivyokuwa anauangalia mwili wake.
* * *
Katika Maisha yake yote, Maganga hakuwahi kukutana na mtihani kama huu uliokuwa mbele yake. Akiwa na umri wa miaka takribani ishirini na tisa, Maganga alikuwa muadilifu mno kuweza kumtongoza msichana na alikuwa mwaminifu sana kuweza kufikiria kitu kama hicho. Wakati huu sasa, kufuatia vituko alivyokuwa amefanyiwa na Milka mbele ya macho yake, aliweza kuhisi dhahiri jinsi moyo ulivyokuwa ukimwenda mbio. Kadiri alivyokuwa akiungalia mwili wa dada yake macho yake yakawa kama yanakosa nguvu zake za kawaida. Alisikia kama nguvu zinaongezeka mishipani na damu inakimbia kwa kasi. Mambo mengi yakamjaa akilini mwake. Uwezo wa kutafakari mambo kwa kina ukaanza kupungua. Ni kweli ilikuwa imebakia mwezi mmoja tu apate upadirisho, kitu ambacho si tu kuwa alikuwa anakipenda sana, ila anajua fika hiyo ndiyo zawadi pekee ambayo angeweza kumpa baba yake katika maisha yake. Baba yake, Mzee Paul, hakuna kitu alikuwa anasubiri kama kuona mwanae amekuwa Padri. Alishamsikia baba yake akisema mara kadhaa kuwa siku mwanawe akiwa Padri na yeye akishuhudia tukio hilo kwa macho yake, basi ni siku ambayo atakuwa tayari kusubiri kifo chake.

*******
Riwaya hii imetungwa na kuandikwa na Japhet Nyang’oro Sudi ambaye anapatikana kwa namba 0762204166

**********
Si kwamba Maganga alipenda kuwa Padri, ila alijikuta akichukua njia hiyo kwa shinikizo la baba yake ambaye amekuwa Kateskista kwa muda mrefu sasa. Kazi yake ya uanajeshi aliyoifanya akiwa kijana na kuicha katika mazingira ya kutatanisha haikumfanya asahau kuwa karibu na kanisa. Maganga alimwangalia Milka, safari hii ile hali ya kuwa ni dada yake ikawa inaanza kufifia, kikubwa ikawa anafikiria kuwa hajawahi kufanya jambo lile. Hivyo akawa anajiuliza atafanyaje. Tofauti na Mzee Paul alivyokuwa akimdhania Maganga kuwa hakuwa mpenda wasichana, jaribu kubwa la Maganga siku zote ni pale anapokutana na wasichana wazuri. Mwili wake umekuwa ukimpeleka kasi sana na mara kadhaa amekuwa akijiridhisha mwenye kitandani. Hivyo huu ulikuwa ni zaidi ya mtihani kwake, hakuwahi kuwa karibu na msichana chumbani namna hii.
Milka akawa amemsoma kaka yake, maana kwake hayo mambo hayakuwa mageni. Kama kaka yake, Milka alishinikizwa na Mzee Paul awe mtawa, jambo ambalo si kwamba lilipingwa na yeye tu bali hata mama yake hakuafikiana nalo. Hivyo akajikuta ameingia kwenye mafunzo ya utawa bila ridhaa yake. Lakini kwa vile haikuwa hiari yake, Milka akajikuta mchezo wa kutembea na wanaume umeshamkolea mwilini na akilini.
Milka alisimama taratibu akasogea pale alipokuwa amesimama kaka yake. Akasogeza mkono wake akaushika ule wa kaka yake ambaye wakati huu alikuwa anatetemeka.
“Milka kwa nini unafanya hivi?” Maganga alihoji kikondoo kwa sauti ya kutetemeka, huku akishindwa kupinga mkono wake usinyanyuliwe na Milka.
“Maganga na….” Milka hakumalizia, kengele ya saa iliyokuwa juu ya meza pembeni mwa kitanda cha Maganga ililia, hiyo iliashiria kuwa saa kumi na moja alfajiri. Wakati huo huo wakasikia mlango ukigongwa. Maganga alichomoa mkono wake toka kwa Milka, akapiga hatua kuelekea mlango wa kutoka chumbani. Huku moyo wake ukiwa unapingana vikali na uamuzi wa akili yake kuamua kuachanisha mkono wake na ule wa Milka, ilikuwa burudani jinsi joto la Milka lilivyokuwa likipenya kupitia kwenye ule mkono. “Miye ni mwanaume, natakiwa kuitii akili zaidi kuliko moyo, we always use logic rather than feelings.” Maganga alijiwazia kuipa nguvu akili yake katika maamuzi yake yaliyokuwa yakipingwa na moyo.
“Karibu!” Alijibu huku akifungua mlango, safari hii hakuuliza kujua mgongaji alikuwa nani. Maana ilikuwa alfajiri tayari.
“Aaaaah Vivian, karibu ndani.” Maganga alisema.
“Mmmmh asante, miye naogopa kuingia nyumba ya Padri mtarajiwa akiwa pake yake nisije nikamtia majaribuni.” Vivian alisema kwa kutania lakini uso wake haukuonyesha hivyo.
“Maganga hali ya mama yako si nzuri, hivyo amenituma nije nikuite uende haraka.” Vivian alibadili mada haraka na ujumbe ulithibitisha kile uso wake ulikuwa ukionyesha. Maganga hakutaka kusubiri, alitoka nje na kufuatana na Vivian. Hakukumbuka kufunga mlango wala kumuaga Milka ambaye wakati huo alikuwa bado ndani.
“Vivian kwanza nashukuru kwa kukubali kumhudumia mama yangu. Unataka kuniambia mama ameumia sana?” Maganga alihoji baada ya kushukuru.
“Maganga, siwezi amini kama baba yako ndiye aliyefanya kitendo kile, labda kwa vile aliwahi kuwa mwanajeshi. Amempiga mama kama mtu aliyekuwa anapiga nyoka aliyeingia ndani!” Vivian alisema kwa sauti ya mshangao. Wakati huo walikuwa wameshafika nyumbani kwa akina Vivian. Vivian ni binti anayetoka katika moja ya familia zenye uwezo pale kijijini, kwa kifupi ndiyo familia tajiri zaidi. Haikuwa ajabu kwa Vivian kuwa anasoma Ujerumani. Wakati huu wazazi wake walikuwa wamekwenda mapumzikoni Brazil, alitakiwa awepo kwenye msafara, ila alikataa. Sababu kubwa ya kukataa aliwaambia wazazi wake kuwa amewakumbuka rafiki zake pale kijijini na angejisikia vema kama Krismas angekula akiwa pale nyumbani. Hivyo wakamwachia nyumba wakaenda zao Brazil.
Vivian na Milka ni marafiki tangu utotoni wakiwa majirani Dar es salaam, wakati huo wazazi wao wote wakiwa wanajeshi kwenye kambi ya Ruvu. Urafiki wao ulichangiwa na mambo mengi. Wakiwa wadogo Vivian na Milka walikuwa wakicheza pamoja. Ki-umri wote walikuwa sawa, Milka alikuwa pacha wa Maganga, japo Maganga ndiye Kulwa. Kingine ni kuwa watu hawa walizaliwa siku moja katika hospitali ya Bugando mjini Mwanza. Japo wakati wanazaliwa wazazi wao walikuwa ni Askari jeshi katika chuo maalumu cha kijeshi Monduli. Ambapo baadaye wote walihamishiwa Ruvu na kibahati-bahati wote sasa wanaishi katika kijiji hiki. Hili limekuwa likiwashangaza lakini wamekuwa hawana majibu kwa nini imewezakana wao kuwa wakihamia sehemu moja kila mara. Tofauti yao kubwa kimaisha ilitoka na ukweli kuwa baba yake Vivian alikuwa ni Daktari Mwanajeshi, hivyo amekuwa akijipatia hela nyingi kwa kazi ya utabibu ambapo kiinua mgongo chake alitumia kufungua hospitali binafsi. Hata walipoanza shule, Vivian alipelekwa shule ya misheni ambayo walikwenda watoto wa watu waliokuwa na uwezo pale kijijini ambao pia walichanganyika na watoto wa kizungu wa wamisionari waliokuwa katika kanisa Katoliki pale kijijini.
Walipoanza kukua, licha ya kumpenda Milka, Viviana alijikuta anaanza kuvutiwa na kaka yake Milka yaani Maganga. Hilo likawa limetia mafuta katika urafiki wao, nyumbani kwao na Milka kukawa na harufu nzuri kwa Vivian kama ile ya ua zuri puani kwa nyuki. Kila mara Vivian alijikuta akiwa nyumbani kwa akina Milka ili walau awe anamwona tu Maganga, hata kama asingeweza kuongea naye. Hii ilidhihirisha kuwa Mbegu haichagui pa kuota
“Karibu ndani Maganga, tafadhali usivue ndala, kuna baridi sana wakati huu haifai kukanyaga sakafu, simenti ni ya baridi sana.” Vivian aliongea kwa sauti iliyojaa ukarimu, ndala za Maganga zilikuwa na matope hivyo hakukubaliana na wazo la yeye kuingia na ndala. Akazivua mlangoni na kuingia ndani. Wakaingia chumba alichokuwa mama yake.
“Oooooh mama yangu!” Maganga alisema baada ya kuuona uso wa mama yake. Uso wake ulikuwa umeharibika vibaya kama vile gari ndogo iliyogongana na gari kubwa ya mizigo. Pua yake ilikuwa imevimba vibaya kama gari iliyofunguliwa boneti yake ya mbele. Macho yake yalikuwa yamevimba kiasi kuwa hakuwa anaweza kuyafungua.
“Siwezi amini kama baba yangu ndiyo amemfanyia mke wake kitu kama hiki...” Maganga alisema huku akiwa ameinama kumkumbatia mama yake ambaye alisikika akipumua kwa shida.
“Maganga, nadhani tumpeleke mama hospital ya Wilaya Sengerema huko anaweza kupatiwa matibabu zaidi maana hali yake inatia shaka sana, gari ina mafuta ya kutosha. Tusipoteze muda zaidi.” Vivian alisema huku akitoka na kuelekea chumbani kwake. Kwa Vivian ilikuwa ni huzuni lakini pia ilikuwa ni nafasi ya kumwonyesha Maganga ni kiasi gani alivyo msichana anayejali. Alikusudia kutumia nafasi hiyo kujiweka jirani na Maganga na ikiwezekana kupata muda wa kuwa naye na kumzoea.
“Haya tusipoteze nafasi tumbebe, tumpeleke kwenye gari.” Vivia alisema wakati huu alirudi toka chumbani akiwa tayari kwa safari.
“Sawa.” Maganga alisema kwa sauti ambayo alijishangaa kama ilikuwa yake. Wakati wanambeba ndipo mama yake Maganga alijaribu kusema kitu, alipokufungua mdomo wake ndipo Maganga akaweza kuona jinsi kinywa chake kilivyokuwa kimeharibiwa vibaya. Maganga nguvu zikamwishia chozi likamdondoka. Vivian alimkaribia Maganga, akamshika mabegani na kumpigapiga katika ile hali ya kumbembeleza.
“Jikaze Maganga wewe mtoto wa kiume, mama yako anakuhitaji sasa, fanya tumpeleke hospitali.” Sijui kama ndo maneno ya Vivian yalifanya kazi au Maganga alijikaza tu, maana aliinuka wakambeba mama yake kwenda nje. Walimwingiza kwenye gari, wakaingia kisha Vivian akalitia gari moto. Ni wakati wanataka kuondoka, waliona mkono unagonga kioo cha dirisha la nyuma. Wote wakageuka kuangalia. Mzee Paul alikuwa amesimama nje ya gari, macho yamemtoka huku akitetemeka kwa hasira. Maganga akafungua mlango ili kumkabili baba yake ambaye tayari alikuwa ameanza kutukana pale nje ya gari.
“Maganga, unaonaje kama tukienda tu, najua hawezi kufukuzana na gari.” Vivian alisema huku mkono wake wa kushoto ukiwa shingoni kwa Maganga unamminyaminya katika hali ya kumtuliza.
“No, this is too much Vivian, its unacceptable…” Maganga alisema huku akifungua mlango. Kabla hajamaliza kufungua mlango, sauti ilisikika toka kiti cha nyuma walikokuwa wamemlaza mama yake Maganga.
“Maganga mwa mwa mwa ma ….na nangu, nyu..nyu....nyumbani, chi…chi….chi…..oooh aaaah…chini…..ya…..ya…ya…..mtungi…..wa…..maji……chimba……usome siri…Zingatia sana…. Kauli ya mama yake na Maganga haikwisha mlango wa upande wa dereva ulivutwa. Mzee Paul alimvuta Vivian na kumsukumia kofi kali la usoni. Kuona hivyo Maganga alitoka nje ya gari kama Swala aliyekurupushwa mafichoni na mwindaji. Alienda ule upande aliokuwa Mzee Paul na Vivian. Vivian alikuwa akilia kwa sauti wakati huo.
“Baba huwezi kufanya hivyo, hivi wewe ni mtu wa namna gani usiyekuwa na hisia. Mbona una moyo wa shaba na akili za gundi?”






PATASHIKA: 04

Maganga alisema huku akimvuta baba yake amwachie Vivian. Kweli alifanikiwa. Vivian alikurupuka, akakimbilia kwenye gari na kuliondoa kwa kishindo huku akiacha watu wakiwa wanakimbilia eneo la tukio. Vivian hakusimama akatokomea. Mzee Paul alijizoa zoa pale chini, akamwangalia Maganga kwa jicho kali huku mikono, midomo na pua zikitetemeka kwa hasira. Maganga alimwangalia baba yake kwa jicho la kukata tamaa na uso ulioshuka. Wakiwa wanatazamana hivyo mara Milka akatokea.
“Na wewe mjinga utaniambia ulikuwa wapi, muda wote huo…wewe ndiye chanzo cha haya yote.” Mzee Paul alisema huku akimfuata Milka. Milka alisimama huku akitetemeka kwa hofu, alishahisi hatari mbele yake, lakini kwa wakati huo hakuwa na namna ya kujitetea, alikuwa kama Kinyonga aliye katikati ya barabara mbele ya gari lijalo kwa kasi. Aliuanda mwili wake kupokea kipigo. Mzee Paul alimfikia Milka, wakati anajiandaa kutoa kipigo mara akasikia sauti inaita.
“Mzee Paul!” Ilikuwa ni sauti anayoifahamu na kuiheshimu kuliko sauti ya mtu yeyote pale kijijini. Nguvu za kupiga zikaisha, akatamani yale mambo yasingekuwa yanatokea muda ule ambapo Askofu alikuwa ameingia eneo lile.
“Naam baba askofu!” Alijibu kwa heshima zote kama si yule aliyekuwa anakwenda kutoa kipigo kwa manawe wa kike na aliyekuwa ametoa kipigo kikali kwa mke wake usiku. Watu walikuwa wameshajaa aneo la tukio, wakubwa kwa wadogo, wanawake kwa wanaume. Baridi ilikuwa kali sana. Maganga alipomwona Askofu Alphonso ndipo alipokumbuka kuwa kumbe alikuwa amevaa kaptula na miguu yake ilikuwa imechafuka kwa tope huku shati lake likiwa lina matone ya damu yaliyosalia wakati anambeba mama yake. Alijiona kama yuko uchi, familia iliyotakiwa kuwa mfano sasa ilikuwa balaa. Alimwangalia dada yake akamwonea huruma kwa jinsi alivyokuwa amesimama. Alienda hadi alipokuwa amesimama akamkumbatia. Milka akaangusha kilio cha uchungu.
**********
MKONO WAKE WA KULIA ulikuwa ukichezea kifua cha msichana huyu ambacho wakati huu kilikuwa wazi na kufanya mwonekano mzuri uliodhihirisha kuwa alikuwa bado ni msichana mdogo sana na aliyejaaliwa uzuri wa kutosha, lakini mkono wa kushoto wa mwanaume huyu ulikuwa umeshikilia sigara ambayo ilikuwa ikiteketea taratibu bila kuvutwa. Wote walikuwa wameridhika na kitu walichokuwa wamekifanya hapo kwa masaa kadhaa. Wakati huu kila mmoja alikuwa kwenye ulimwengu wake baada ya kutoka kwenye ule wa pamoja ambao, Hellen alikuwa akilia kwa raha aliyokuwa akiipata na Machumu alikuwa akigugumia kwa sauti yake ya kiume kutokana na utamu aliokuwa akihisi. Walikuwa wameingia katika hoteli hiyo iliyoko uswahilini kabisa mwa jiji la Dar es salaam maeneo ya Sinza Kumekucha, majira ya saa tatu asubuhi. Walifanya kile walichotaka na sasa walikuwa wanapumzika huku kila mmoja akiwa anawaza lake.
Siku nne zilizopita Hellen alikuwa ametimiza umri wa miaka ishirini na moja. Hakuwa mwanafunzi, hakuwa mfanyakazi, hakuwa anaishi na wazazi, hivyo mishemishe za mjini zisizo na majina wala mahali maalum ndiyo ilikuwa mpango wake. Kwa kifupi alikuwa akifanya kazi zisizo maalum ila na watu maalum. Tofauti na wasichana wengine waliokuwa wakijiuza kwa bei chee maeneo hayo ya Sinza kumekucha, yeye alikuwa wa watu maalum. Uzuri wake, umri wake na dalali wake vyote kwa pamoja vilimfanya asiwe wa bei nafuu.
Maisha yake haya yalianza siku ile aliposikia mama yake na baba yake kwa mara ya kwanza wakigombana chumbani. Mwanzoni hakujua chanzo cha ugomvi lakini baadae alikuja kugundua kuwa chanzo ilikuwa ni yeye. Maana alisikia baba yake akisisitiza kuwa kama kweli yeye ni mwanae basi waende wakapime vinasaba na ijulikane. Hilo ndilo lilopelekea yeye na mama yake kufukuzwa nyumbani na mtu ambaye yeye aliamini kuwa alikuwa ni baba yake.
Maisha yao mtaani hayakuwa rahisi, mama yake alifanya kila awezalo ili kunusuru maisha yao. Lakini katika kufanya kila awezalo akajikuta anaishia kwenye UKIMWI na kumfanya Hellen abaki peke yake. Baada ya kifo cha mama yake, Hellen hakuwa na namna ya kuishi hivyo akajikuta analazimika kutafuta namna. Kazi pekee aliyokuwa anaifahamu ni ile aliyomwona mama yake akiwa anafanya ni kuuza mwili wake. Na yeye akaanza. Huyu ndiye Hellen ambaye alikuwa amejilaza kwenye chumba cha hoteli hii ya Gwama iliyoko Sinza Kumekucha.
“Machumu nadhani wakati umefika wa mimi kwenda Mwanza na kuujua ukweli kunihusu.” Hellen alisema huku akichezea misuli iliyokuwa imefungamana kifuani kwa Machumu.
“Mbona kama maamuzi yako hayo yamekuja ghafla sana, kuna tatizo lolote?” Machumu aliuliza huku akiachia kipande kifupi cha sigara iliyokuwa bado inateketea mkononi kidondokee kwenye sahani ya sigara iliyokuwa jirani na kitanda walichokuwa wamelalia.
“Wiki hii nimekuwa nikiota ndoto za ajabu ajabu tu na moyo wangu umekuwa mzito sana, nadhani natakiwa niende nikajue ukweli kuhusu mimi. Mama alinisisitiza sana katika dakika zake za mwisho kuwa lazima niende katika Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza kuna mtu nikaonane naye.” Alisema Hellen huku akijiinua toka pale kitandani. Alielekea bafuni huku nyuma macho ya Machumu yalikuwa yakimsindikiza na kuhusudu jinsi msichana huyo alivyokuwa ameumbika. Machumu alimeza mate, huku hamu ya kufanya tena ikiwa imeshamjaa. Alimfuata Hellen bafuni huko wakaanza tena. Kwa vile wote walikuwa mafundi, wote walikuwa na uwezo, mchezo wao ulikwenda vema. Vilio na miguno ya raha na utamu vikasikika tokea bafuni.

* * *

Saa kumi na mbili na dakika tano ya siku iliyofuata ilimkuta Hellen akiwa ameshakaa kwenye kiti cha basi la Zuberi tayari kwa safari ya kuelekea Mwanza. Kiu ya kutaka kujua chimbuko lake ilimzidi na hivyo kuyashinikiza maamuzi yake, maamuzi yalitii na akakata shauri aende.
Walifika Mwanza kituo cha mabasi Nyegezi majira ya saa tatu na robo usiku. Hapo alikodi taxi iliyompeleka hadi hoteli Lakairo maeneo ya Kirumba. Siku iliyofuata majira ya saa kumi na mbili na nusu tayari alikuwa ameshafika kwenye kivuko cha Kamanga Feri, huku akiwa ameshakata tiketi kweye basi la Nyehunge Express. Kutoka Kamanga Feri upande wa Mwanza mjini hadi Kamanga Feri upande mwingine iliwachukua kama dakika kumi na tano wakiwa majini. Ambapo safari ya kwenda Wilaya ya Sengerema ilianza.
“Konda, miye siyo mwenyeji sana maeneo haya ila nashukia sehemu inaitwa Katunguru.” Hellen alimwambia konda wakati basi likiwa limeshatoka kwenye kivuko na kuanza safari. Safari yao ilichukua saa moja na nusu hadi pale konda alipomwambia Hellen kuwa sehemu aliyotakiwa kushuka ilikuwa ni kituo kinachofuata. Kwa vile mabasi yalikuwa yanafukuzana, ilitakiwa asogee mlangoni ili wasipoteze muda mwingi kituoni.
Aliposhuka kituoni ilikuwa tayari saa tatu kasoro dakika ishirini na moja.
“Habari za leo kaka?” Hellen alisabahi.
“Nsuri tu dadayango, pole na safali!” Alijibu kijana huyo kwa ile lafudhi ya Kisukuma ambapo kwenye 'r' wao huweka 'l' huku wakiwa wanakandamiza maneno.
“ Samahani, nahitaji kwenda sehemu inaitwa madukani.” Hellen alisema baada ya kuwa amesoma maelekezo toka kwenye kitabu chake cha kumbukumbu.
“Aaaha, haina shida tu, nenda pale, chukua baiskeli mwambie akupeleke, ni kama nusu saa hivi kufika kule”.
“Haya asante!” Hellen alisema huku akijifunika mtandio, mvua ilikuwa ikinyesha sana tangu walipotoka Mwanza. Alishukuru kwani hapo mvua likuwa imeshaacha kunyesha japo kulikuwa na tope jingi.
Alipofika madukani, Hellen aliulizia kwa Mzee Paul, akaelekezwa. Hapo tena akachukua mtu wa baiskeli ampeleke. Haikuwa mbali sana toka madukani.
“Hapa ndiyo kwa Mzee Paul.” Mwendesha baiskeli alisema walipokuwa wamefika kwenye nyumba moja iliyokuwa imezungukwa na michungwa mingi. Hellen alishukuru baada ya kuwa amelipa. Hapo aliusogelea mlango wa hiyo nyumba, aligonga kwa muda mrefu bila majibu mpaka pale mtu mmoja alipopita na kumwambia Mzee Paul alikuwa nyumba ya tano toka hapo japo kulikuwa na ugomvi.
“Ugomvi wa nini tena?”Hellen alihoji.




PATASHIKA: 05

“Ugomvi wa kifamilia wewe nenda ukaone.” Alisema huyo mzee huku akionyesha kutotaka kuongelea zaidi habari hiyo. Alimwelekeza sehemu ambayo angempata Mzee Paul, nyumbani kwa akina Vivian. Alipofika umati wa watu ndiyo ulikuwa unatawanyika, huku Maganga na Milka nao wakiwa wanaondoka eneo hilo. Njia aliyokuwa anakuja nayo Hellen ndiyo njia ambayo Maganga na Milka walikuwa wakija wanatembea taratibu wakiwa wamejaa majonzi yaliyochanganyika na hasira kufuatia vitendo vilivyoonyeshwa na baba yao. Walikutana na Hellen, mara ya kwanza walipomwona wote walidhani ni Vivian. Maana msichana aliyekuwa hatua chache akija mbele yao alifanana kila kitu na Vivian ambaye waliongea naye dakika chache zilizopita akawahakikishia kuwa alikuwa amefika salama hospitali na kuwa mama yao alikuwa ameshaanza kutibiwa. Wote wakashikwa na bumbuwazi jinsi msichana huyo alivyofanana na Vivian. Walipokaribiana, wakasalimiana huku kila mmoja akiwa kajikunyata.
“Habarini za asubuhi?” Hellen alisabahi.
“Nzuri.” Maganga na Milka wakajibu.
“Je tunaweza kukusaidia, maana unaonekana mgeni hapa kijijini?” Maganga aliongeza huku akijilazimisha kutabasamu.
“Ndiyo, naitwa Hellen, namuulizia bwana mmoja anaitwa Paul, nimepita nyumbani kwake kuna mtu akaniambia yuko upande huu...na ....halafu...” Hellen akasita huku akijaribu kutafuta maneno.
“Oooh wala usijali, bila shaka Mzee Paul utampata tu dada yangu. Miye naitwa Maganga....”
“Na miye naitwa Milka...” Milka akadakia kwa sauti ya kutetemeka kutokana na baridi. Ilikuwa inaelekea saa sita mchana, lakini kutokana na hali ya mawingu na mvua iliyokuwa imenyesha usiku na mapema asubuhi ungedhani bado ni saa moja asubuhi.
“Siye ni watoto wa huyo Mzee Paul unayemtafuta...” Maganga akasita kisha akaendelea.
“...kwa sasa ametoka na nadhani atachelewa kurudi, basi karibu ukapumzike wakati tukimsubiri.” Maganga alisema huku akijitoa kwenye mkono wa Milka uliokuwa umemshika kwapani na kuomba mzigo wa Hellen. Hellen alimkabidhi Maganga begi lake dogo alilokuwa amekuja nalo. Walitembea kimyakimya hadi walipofika nyumbani kwa Maganga. Wote wakaingia ndani.
“Karibu sana Hellen hapa ni nyumbani kwangu, jisikie uko nyumbani. Karibu kiti ukae...” Maganga alisita, wakati anamwonyesha Hellen akae kwenye kochi upande wa kulia mwa sebule, ndipo macho yake yalipogongana na ushungi ukiwa sakafuni jirani na kochi hilo.
Wote watatu waliviangalia, Milka akajikausha maana alitambua kuwa ile ilikuwa nguo yake, alisahau kuichukua alipotoka. Jukumu likabaki kwa Maganga.
“Daaah!, jamani wamama wa kazi hawa, sasa ndiyo mambo gani haya inamaana alivyomaliza usafi hakuweza kuona hii kitu yake...” Maganga alijitia kudanganya, alidanganya kijinga, hakuwa amezoea kudanganya. Milka na Hellen waligundua jinsi Maganga alivyobabaika.
“Aaah!, huwa hawako makini wale..ha ha ha.” Hellen alisema huku akijilazimisha kucheka. Milka alichukua zile nguo na kuzipeleka bafuni.
Kila alipokuwa akiwaangalia vijana wenzake hawa Hellen akawa anapata hisia mchanganyiko. Kama kweli yeye ni mtoto wa Mzee Paul kama mama yake alivyomwambia kabla ya kufa, basi inamaana hapo yuko na kaka yake na dada yake, kama si kweli basi angependa kuwa rafiki wa hawa vijana maana walioneka wacheshi na wenye upendo. Milka alionekana mtulivu, Maganga alionekana mcheshi na alikuwa na mvuto pia, kila macho yao yalipogongana na yale ya Maganga kuna kitu alihisi kinaruka ndani yake.
"Ndiyo mgeni wetu, karibu sana kwa mara nyingine. Hatukuwa tumepata kifungua kinywa. Hivyo karibu mezani ujumuike nasi.” Maganga alisema huku kwa mikono miwili akimwonyesha Hellen meza ilipokuwa. Kwa kawaida chai hundaliwa sehemu moja na kusambazwa kwenye nyumba za Watawa. Hivyo Maganga aliikuta imeshaandaliwa mezani. Ilikuwa ni viazi vya kuchemshwa na chai ya maziwa.
“Asanteni sana...” Hellen alisema huku akijiinua kuelekea mezani.
Wakiwa wanapata kifungua kinywa japo walikuwa wamechelewa, waliongea mengi ikiwa ni pamoja na kutambulisha, mambo ya shule na mengineyo.
“Kwa hiyo kilichokufanya ufunge safari toka Dar hadi hapa Mwanza halafu Katunguru ni kuja kumwona Mzee Paul ambaye umeambiwa ni mganga wa kienyeji maarufu?” Maganga alihoji kwa mshangao baada ya Hellen kuwadanganya kuwa alikuwa amekuja kwa sababu za kitabibu.
“Haswaa!” Hellen alijibu huku akiangalia pembeni.
“Basi ngoja tumsubiri huyo Mzee Paul bila shaka anaweza kuwa na namna ya kukusaidia.” Maganga alisema huku akibetua midomo. Hakuwahi kusikia wala kumwona baba yake akitibu watu kwa uganga wa kienyeji. Hilo lilimshangaza.
“Hellen umefanana na rafiki yangu mmoja anaitwa Vivian, yaani mmefanana sana kwa kweli, ngoja akija utamwona...'”Milka alisema huku akitabasamu.
“Kweli?”Hellen alijitia kushangaa.
“Saana!” Milka alisisitiza.
“Basi safari hii itakuwa bahati yangu kwani sijawahi fananishwa na mtu yeyote wakati wowote huko nyuma. Nina hamu nimwone huyo mtu ninayefanana naye ili nijione nilivyo.” Hellen alisema wote wakacheka.

* * *

“Ndiyo binti, Maganga amenielezea kuwa kilichokuleta hapa ni kutafuta tabibu wa afya yako je, ni kweli?” Mzee Paul alihoji kwa sauti mzito iliyojaa wasiwasi.
“Hapana, si kweli baba, mimi naitwa Hellen Tino....” Helleni alijieleza kwa kirefu yeye ni nani na alikuwa ametoka wapi!
“Hivyo kabla mama yangu hajafariki siku moja alinielezea kuwa anaona ni haki yangu kujua ukweli kuhusu mimi...akasema siyo rahisi kunielezea nikaelewa ila akasema katika maisha yangu nijitahidi kuja hapa Kijijini nikutafute maana wewe ndiwe baba yangu mzazi.” Hellen alisema huku akijitahidi kumwangalia Mzee Paul usoni. Kumbukumbu nyingi zilimjia kichwani lakini Mzee Paul alijua kukubaliana na hilo ni kujivunjia heshima yake kijijini pale. Alikuwa anaelekea kuwa baba wa mtu ambaye ni Padri, kisha mwanawe mwingine angekuwa Mtawa muda si mrefu, habari kuwa alikuwa na mtoto wa nje ingemvurugia maisha yake. Ni kweli alimkumbuka Theresia, mama wa msichana aliyekuwa mbele yake.
“Inawezekana usemalo, ila ili kuhakiki kuwa wewe kweli ni mwanangu inabidi nikathibitishe hilo. Jioni hii itabidi twende wote kuna shamba langu liko Kasomeko, huko kuna waheshimiwa tutawauliza na watatuambia ukweli. Kama ni kweli itakuwa shangwe na vifijo kwelikweli.” Alisema Mzee Paul huku akitabasamu kinafiki. Hellen alikubaliana na mpango huo.
Ilipogonga saa kumi na mbili na nusu jioni Mzee Paul na Hellen walikuwa wameshafika kwenye shamba alilosema Mzee Paul.
“Hii ni njia ya kiutamaduni ya kujua kama mtoto ni wako au la. Wewe utasimama hapa chini ya mti miye nitapanda juu. Ukihisi kuna kitu kinakugusa kichwani tulia tu, ukiona kina zunguka shingoni na kukubana ujue wewe kweli ni mwanangu, basi utasubiri hivyo na miye kitakuja kunibana nitajua u mwanangu.” Alisema Mzee Paul huku akiwa anamwangalia Hellen usoni.
Hellen aliafikiana na utaratibu, akafumba macho, dakika chache baadae akasikia kitu kinamgusa kichwani, baadae akashitukia kinamzunguka shingoni kilipombana alisikia maumivu. Wakati bado anasikilizia, akashangaa anakabwa na kunyanyuliwa juu akafumbua macho wakati kitu hicho kikimnyanyua. Alipoangalia vizuri na kupapasa kwa mikono ndipo akagundua kuwa kamba ilikuwa imemzunguka shingoni. Alikuwa ananyongwa. Alitamani kusema kitu hakuweza, alitaka kupiga kelele akashindwa pumzi zikaanza kumbana.
“Karibu nyumbani Hellen!” Ilikuwa sauti iliyojaa dhihaka ya Mzee Paul, mtu aliyeamini kuwa ni baba yake. Wakati huo huo akamwona Mzee Paul akikimbia na kupotelea kichakani. Alianza kupigapiga miguu huku pumzi zikianza kumtupa mkono.

***************************
Macho yalimtoka pima, Maganga hakuamini kitu ambacho baba yake alikuwa anafanya. Mwanzo alitetemeka kwa woga, lakini mwishoni alipomwona Hellen ananing’inia kwenye kamba, Maganga alitetemeka kwa hasira. Alitaka kukurupuka aende lakini kuna kitu kilimzuia akasita. Mzee Paul alipoanza kukimbia kuondoka eneo la tukio alipita jirani na kichaka ambacho Maganga alikuwa amejificha.

Haya sasa msomaji wangu;

Maganga atamfanyaje baba yake?
Kwa nini Paul kaamua kumuua Hellen?
Nini kitatokea?
Mama yake na Maganga kule hospitali anaendeleaje?




PATASHIKA: 06

MACHO YALIMTOKA PIMA, Maganga hakuamini kitu ambacho baba yake alikuwa anafanya. Mwanzo alitetemeka kwa woga, lakini mwishoni alipomwona Hellen ananing’inia kwenye kamba, Maganga alitetemeka kwa hasira. Alitaka kukurupuka aende lakini kuna kitu kilimzuia akasita. Mzee Paul alipoanza kukimbia kuondoka eneo la tukio alipita jirani na kichaka ambacho Maganga alikuwa amejificha. Macho ya Maganga yalimsindikiza baba yake hadi alipopotelea kwenye miti ya mihogo shamba la jirani na pale alipowakuta Hellen na baba yake mzazi.
Aliporudisha macho kuelekea kwenye mti ambao Hellen alikuwa ananing’inia alishangaa kuona Mzee mmoja akiwa anahangaika namna ya kumshusha Hellen. Hapo tena akapigwa na bumbuwazi. Mzee huyo makamu yake yalionekana kutotofautiana sana na Mzee Paul, baba yake. Hakuwa anamjua Mzee huyo. Baada ya dakika chache yule Mzee alifanikiwa kumtoa Hellen katika kile kitanzi, japo mwili wa Hellen ulionekana kuwa umetulia kabisa. Maganga alitilia shaka kama bado uhai ulikuwemo ndani ya mwili huo. Mzee huyo alimbeba Hellen na kuanza kuondoka naye.
Maganga alimfuata Mzee huyo kwa siri hadi safari yao ilipoishia kwenye nyumba moja nzuri iliyokuwa mbali kiasi toka sehemu ambayo tukio lilikuwa limetokea. Nyumba hiyo ilikuwa nzuri ukilinganisha na nyumba nyingine kijijini pale huku ikiwa imezungushiwa ukuta wa matofali. Mzee huyo alipofika getini aligonga, geti likafunguliwa akaingia ndani. Hapo Maganga hakuweza kujua nini kiliendelea. Alikaa kwenye kichaka takribani nusu saa huku akiwa amejawa na mawazo tele. Wazo la kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi lilikuja lakini alilipinga haraka sana. Hakuna mwanajamii yeyote pale kijijini ambaye angemuelewa pindi angesikia kuwa amekwenda kumshitaki baba yake kwa mauaji. Maganga alijikuta akiishangaa siku hiyo, ilikuwa siku ambayo ilianza kwa visa na vituko tangu saa nane usiku alipoamshwa na Milka mdogo wake. Maganga hakuwahi kumwona wala kujua kuwa baba yake ni mganga wa kienyeji. Hilo lilimfanya awe na hamu ya kujua ukweli. Hivyo kwa siri sana alikuwa akifuatilia nyendo za Paul na Hellen. Hicho ndicho kilichomfanya aandamane nao kwa siri walipokuwa wakielekea kule shambani.
Alitaka kuondoka eneo la hiyo nyumba aliyoingia yule mzee akiwa amembeba Hellen, lakini sauti nyingine ikamwambia si vema kuondoka bila kujua hali ya Hellen. Pia, akajikumbusha kuwa Hellen alikuwa ni mgeni wao. Huruma ilimjaa, ikamsukuma kufanya kitu, akatoka kichakani alipokuwa amejificha huku akiwa amejawa na wasiwasi akapiga hatua taratibu kuelekea lilipokuwa lango kuu la nyumba hiyo. Alipofika langoni akangonga kama alivyofanya yule Mzee. Aligonga mara ya pili na ya tatu lakini hakukuwa na dalili ya mtu kuja kumfungulia. Aliendelea kubisha namna hiyo kwa dakika ishirini nyingine bila mafanikio. Ndipo wazo la kujaribu kuingia likamjia. Akaanza kuungalia ukuta wa nyumba hiyo, katika kuhangaika huko mara akaona mawe yaliyokuwa yamekusanywa kuegemea ukutani. Alikwenda hadi mahali pale, akasimama juu ya rundo la mawe hayo, akachungulia ndani. Mbwa wakubwa kama ndama wakawa wamemwona wakaanza kubweka kwa fujo na kufanya eneo hilo kulipuka kwa kelele. Alijua kuwa haingekuwa rahisi kwa yeye kuingia ndani bila mwenyeji kumruhusu kufanya hivyo.
Wakati anaondoka sehemu hiyo yenye mawe mara simu yake ya kiganjani ikaita.
“Hallo Milka!”Alisema baada ya kuminya kitufe cha kupokelea.
“Maganga uko wapi, nimekutafuta kila mahali hupatikani.” Milka alisema kwa sauti iliyokuwa na jazba iliyochanganyika na wasiwasi.
“Kuna nini Milka? Nipo nakuja.” Maganga alisema kwa sauti ya kichovu.
“Usiniambie uko na yule msichana mgeni.” Milka alisema tena.
“Sikiliza Maganga, baba ameteguka mguu, watu wamemleta hapa nyumbani baada ya kumkuta huko akiwa amelala hajiwezi. Halafu Vivian kanipigia simu, kasema hali ya mama imebadilika usiku huu.” Milka alisema huku akipumua kwa kuchanganyikiwa kama mtoto wa ndama ambaye hajamwona mama yake wakati kundi la Ng’ombe likiwa limerejea toka malishoni.
“Heeeh, Milka niko njiani nakuja!” Maganga alisema huku akiwa anaondoka eneo hilo. Kwa kifupi alikuwa amechanganyikiwa. Taarifa kuwa baba yake ameteguka, mama yake hali imekuwa mbaya, Hellen yuko ndani ya jumba lile ambalo ameshindwa kuingia, zote zilikuwa kama ndoto tu kwake. Akiwa ameshapiga kama hatua kumi na tano toka kwenye lango kuu la nyumba ile mara akasikia mlango wa chuma ukitoa mlio wa kufunguliwa. Alisimama akageuka kuona kama kuna mtu anatoka. Mara akamwona yule mtu aliyekuwa amembeba Hellen akiwa anachungulia. Maganga aligeuka akatembea haraka kuelekea kwenye lile lango.
“Shikamoo Mzee wangu!” Maganga alisema alipokuwa amefika pale langoni. Hakujibiwa. Yule Mzee alibaki anamwangalia tu Maganga kama mtu aliyeona kichwa cha nyoka nje kupitia dirishani mwa chumba cha kulala.
“Shikamoo Mzee wangu!” Maganga alirudia tena.
“Nani Mzee wako?” Hatimaye huyo mwanaume alisema kwa sauti ya kukwama kwama. Maganga alimwangali huyo mtu kuanzia juu hadi chini. Kisha akajikuta anakosa la kusema. Kama nilivivyosema, alikuwa mtu wa makamo, kati ya miaka arobaini na nane hadi hamsini na tano. Alikuwa na nyewle nyingi huku chache zikionekana kuwa na weupe. Alikuwa na mwili uliojengeka vema na kimo cha kupendeza. Si mweusi si mweupe.
“Una shida gani hapa kwangu usiku huu?” Alihoji, tayari ilishatimia saa mbili kasoro dakika kumi na saba. Kiza kilikuwa kimeshatanda kote, huku ndege aina ya Popo wakisikika kushangilia asubuhi yao. Maganga akakosa la kujibu.
“Ahh….ha..ha..nilikuwa nataka kujua kuhusu yule msichana uliyemchukua kule shambani.” Maganga alisema kwa kubabaika kiasi.
“Ahhhhh! kumbe wewe ndiyo uliyetaka kumuua?”
“Haya mikono juu na ingia ndani!” Yule Mzee alisema huku mdomo wa bastola aliyokuwa ameishikilia ukiwa unatazama paji la uso wa Maganga. Kwanza Maganga alisikia kizungu zungu, halafu akasikia kama damu imekauka mwilini halafu mwili umekuwa wa baridi, halafu mwishowe akahisi kama suruali yake imelowana, huku miguu ikiwa inagongana. Katika maisha yake hakuwa amewahi kuona bastola na hakuwa na mpango wa kuja kuwa nayo.
“Siyo mimi Mzee wangu, haki ya Mungu vile!” Alipomaliza kuapa ndipo akakumbuka kuwa kuapa ni dhambi tena hasa kwa yeye kama Padri mtarajiwa.
“Nimesema ingia ndani!” Alisisitiza yule Mzee. Maganga hakuwa na namna, alitii. Alipoingia yale majibwa yalianza kumnusanusa huku yakitoa miguno ya uchu.
“Tafadhali kijana usijifanye mjuaji hata kidogo.” Mzee alionya huku wakiwa wanatembea kuelekea ulipo mlango wa kuingilia ndani. Wakati huo huo mvua ilikuwa imeshaanza kunyesha.
“Haya niambie vizuri nini kimekuleta hapa?” Alihoji huku akiwa anakaa kwenye kiti na kumwacha Maganga akiwa bado amesimama. Alimimina mvinyo akanywa mafunda mawili, kisha akamkazia macho Maganga.
“Nilikuwa maeneo ya shambani kwako…”
“Ulikuwa unafanya nini kule peke yako jioni yote ile?” Mzee alimkatisha Maganga kwa swali. Hilo swali lilimkera Maganga.
“Kwani wewe ulikuwa unafanya nini? Nadhani hilo si swali la kuniuliza, kama wewe ulikuwa kule basi na mimi naweza kuwa kule. Cha msingi hapa nataka kujua kama yule dada yuko salama au la?” Maganga alijibu kwa ukali kiasi.
“Unajitia mbogo siyo, haya twende huku ukamsubiri huyo mwenzio.” Alisema yule Mzee kwa sauti yake iliyokuwa imekauka. Alisimama na akamwonyesha Maganga ishara kuwa atangulie. Walitembea wakapita vyumba kadhaa kabla ya kufika kwenye chumba kilichokuwa mwisho wa ukuta kwenye kona upande wa kulia.
“Ingia ndani!” Iliamuru sauti ya yule Mzee. Maganga akatii.
“Utakaa humu!” Alisema kisha akafunga mlango. Maganga aliangalia mule ndani kisha akakaa juu ya boksi la vitabu. Jambo moja lilikuwa dhahiri akilini mwa Maganga, huyu Mzee alikuwa ni msomi. Aliangaza macho yake huku na huko humo chumbani, chumba kilikuwa kimejaa vitabu vya aina mbali mbali, huku asilimia kubwa vikiwa katika lugha ya kiingereza. Alitembeza macho yake taratibu huku akisanifu namna chumba kile kilivyokuwa kimepangiliwa vema, kulikuwa na vitabu vya sayansi, vitabu vya hadithi, vitabu ya maarifa mbali mbali. Macho ya Maganga yaliendelea na safari yake hadi yalipogota kwenye vyeti vilivyokuwa ukutani. Havikuwa vyeti halisi bali nakala za vyeti halisi. Maganga alisoma kimoja baada ya kingine, vyote vilikuwa vya mtu mmoja. Kisha macho yake yakafika sehemu ambayo kulikuwa na picha mbalimbali huku nyingi zikiwa za Mzee aliyekuwa amemweka humo ndani. Zilionyesha tangu akiwa kijana, akiwa kwenye majoho mbalimbali ya kuhitimu elimu za juu. Alipomaliza macho yake yakahamia ukuta mwingine. Hapo ndipo akabaki kinywa wazi. Aliona nakala ya cheti cha kuhitimu mafunzo ya kijeshi. Kisha pembeni Maganga akaona picha ya mama yake mzazi akiwa bado msichna,amabaye wakati huu alikuwa hospitali. Anaoneka akiwa na mtu ambaye anafanana na huyo Mzee. Hapo akajikuta udadisi unaongezeka na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu huyo Mzee inaongezeka.
Akaanza kupekua, kabla hata hajafika mbali mara chumba chote kikawa giza. Hakujua kama ni umeme ulikuwa umekatika au taa ilikuwa imezimwa. Lakini baada ya sekunde chache wazo la kuwa umeme ulikatika lilitoweka pale alipoona mwanga ukiwa unatokea dirishani. Hakuwa na jingine la kufanya zaidi ya kutulia na kungoja majaaliwa yake. Mawazo yalirudi kwa baba yake na mama yake. Mlolongo wa matukio ulimfanya Maganga ahisi kuwa labda alikuwa anaota.
* * *
Hadi jogoo wa asubuhi walipoanza kuwika, Maganga alikuwa hajapata hata lepe la usingizi. Alikuwa amejaa mawazo mengi kiasi kuwa akili yake haikuruhusu usingizi hata kidogo. Ilipotimia saa moja na nusu, chumba tayari kilishakuwa na mwanga wa kutosha. Alisimama, wakati anasimama alipepesuka, ndipo alipogundua kuwa tangu juzi usiku alipoanza kusumbuana na mdogo wake Milka, alikuwa amepata mlo mmoja tu, wakati ule Hellen alipokuwa amewasili kijijini na wakawa wamepata naye kifungua kinywa. Tofauti na hicho hakuwa ametia kitu chochote tumboni. Lakini hata hivyo alijikaza kiume, akajinyosha kama mtu aliyekuwa ametoka kulala ili hali haikuwa hivyo. Akaendelea na zoezi lake la kupekua ndani ya kile chumba hadi ilipotimia saa mbili na dakika ishirini na moja wakati mlango wa kile chumba ulipofunguliwa taratibu. Yule mwanaume aliingiza kichwa chake huku kiwiliwili chake kikiwa nje kama wafanyavyo makonda wa daladala. Macho ya Mzee yule yalimwangalia kwa muda wa dakika nzima bila kusema neno lolote. Maganga naye alimwangalia hivyo kisha akapiga hatua kuelekea pale mlangoni.
“Hivi Mzee unajua kuwa ufanyavyo ni uhalifu mkubwa, sijajua kosa langu kwa nini umenifanya mateka wako?” Maganga alisema akiwa ameshafika pale mlangoni. Yule Mzee hakusema kitu, ila safari hii macho yake yalilegea na akawa kama analengwalengwa na machozi.
“Sikiliza Maganga.” Yule Mzee alianza kuongea. Kitendo cha kumtaja jina kilimshtusha sana Maganga.
“Umejuaje jina langu?” Maganga alihoji kwa namna ya kushangaa .
“Maganga, mimi nililijua jina lako hata kabla wewe mwenyewe hujalijua…”
“Kivipi?” Maganga alihoji huku macho yake yakipepeswa na kuusoma uso wa yule Mzee ambaye wakati huu alikuwa analengwa lengwa na machozi.
“Halafu nimeona picha ya mama yangu imefikaje humu ndani?” Maganga alizidi kuhoji.
“ Naitwa Mwasumbi, Luten Mwasumbi. Jana nilikuwa nakuja nyumbani kwako kuongea na wewe, lakini nilipokuwa jirani na kwako nikakuona unatoka kwa mwendo ambao nilihisi kulikuwa na shida. Hivyo nikakufuata kwa kuvizia hadi ulipofika kwenu. Kilichonishangaza hukuingia ndani na wewe ulijificha mahali. Nikajua kuna kitu kisicho cha kawaida kilikuwa kikiendelea. Baba yako alipotoka na Hellen nilimwona. Lakini nilishangaa Hellen alifikaje hapa kijijini, sikutegemea yeye kufika huku…”
“Kwani wewe unamjua Hellen kama nani, na kwa nini hukutegemea yeye kuja huku kijijini?”
“Tulia nikuelezee ili uelewe, nitakuja huko maana ndilo lililokuwa linanileta kwako.” Alisema yule Mzee na kumfanya Maganga akae chini.
“Baada ya hapo nikaona ulichokiona ila miye nilikuwa mwepesi kwenda kumwokoa Hellen.” Alisema yule Mzee. Wakati anataka kuendelea mlango wa kile chumba uligongwa, maana wakati huu yule Mzee naye alikuwa ameshaingia ndani.
“Subiri kidogo Grace.” Alisema yule Mzee huku akiwa anamwangalia Maganga kama anayemsoma vile.
“Unaonaje kama tukienda kuongelea kwenye chumba kizuri ili hali tukiwa tunapata kifungua kinywa?” Alihoji kwa sauti tulivu kiasi safari hii, bila shaka hiyo ilitokana na jinsi Maganga alivyokuwa ameanza kunywea.
“Mmmmmh!” Maganga alishusha pumzi kisha akainamisha kichwa chini. Hakuwa na sababu ya kukataa.
“Okay, twende. Hellen yuko wapi?” Hatimaye alikumbuka kuuliza.
“Yupo utamwona tu, baada ya tukio la jana, usiku ule ule nilimwita daktari wangu maalum akaja kumwangalia na kumpa huduma ifaayo.” Alisema yule Mzee akiwa anageuka na kufungua mlango. Waliongozana wakafika sebuleni.
“Hapa hapatatufaa kwa maongezi yetu, twende huku.” Alisema yule Mzee na kuongoza upande wa kushoto wa sebule, hapo alifunua pazia na kufungua mlango. Wakajikuta wako kwenye chumba kingine cha wastani tu. Kulikuwa na meza kubwa iliyokuwa imezungukwa na viti sita, kisha pembeni kulikuwa na sehemu ya kunawia mikono. Meza ilikuwa imeshaandaliwa tayari kwa kifungua kinywa, baada ya kuona vilivyokuwa mezani, Maganga akahisi kama njaa aliyokuwa nayo iliongezeka mara dufu.
“Karibu, utanawa pale halafu tutapata kifungua kinywa.” Alisema yule Mzee kwa sauti iliyokuwa na kitu ndani yake, japo Maganga alishindwa kupambanua kitu hicho ni kitu gani. Wakaanza kushambulia chakula, baada ya dakika kama ishirini hivi walikuwa wameshamaliza.
“Haya sasa tuna…” Maganga hakumalizia kuongea kwani macho yake yalitua ukutani na kuganda hapo.
“Baba!?” Maganga alishangaa huku akisimama kuisogelea ile picha.
“Ndiyo huyo ni rafiki yangu Paul, hapo tulikuwa jeshini mafinga, tulikuwa ni marafiki tulioshibana. Urafiki wetu ulianza tangu tulipokuwa wadogo sana, maana tulikuwa majirani. Baaada ya kumaliza shule wote tukaenda kujiunga na jeshi kwa ajili ya mpango maalum. Tulifanya mafunzo yetu na kumaliza kwa mafanikio makubwa sana. Wakuu wa jeshi wakapendekeza twende tukapate elimu ya juu, hivyo wote wawili tukajiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam.” Alipofika hapo Mzee huyo alinyamaza kuruhusu koo lake kupitisha mate. Maganga alikuwa ametulia tuli akimsikiliza huyo Mzee huku macho yake yakiwa hayabanduki usoni kwake.
“Jiji la Dar es salaam lilitupokea, japo miaka hiyo hailkuwa kama lilivyo sasa. Paul alikuwa mkorofi sana, japo alikuwa na akili sana. Mimi nilikuwa mcheshi sana, hiyo ilinifanya kuwa na wasichana wa kutosha hadi wa ziada. Wasichana wengi walikuwa wanamkataa Paul. Ikafikia wakati alipokuwa akihitaji wasichana ilibidi apitie kwangu ili nimfanyie mpango. Katika wasichana wote niliowafanyia mpango kwa Paul, Paul alifanikiwa kujenga urafiki na msichana aitwaye Elizabeth. Japo mara kwa mara nilikuwa nikiingilia kati kuamua ugomvi baina yao. Tulipokuwa mwaka wa mwisho pale chuoni, urafiki kati ya Paul na Elizabeth ulikuwa umefifia sana. Mara nyingi Elizabeth alipenda kuja chumbani kwangu kuongea, na mara kwa mara Paul alipotukuta ulizuka ugomvi mkubwa sana. Hatukuwa na sababu ya kujitetea maana tungekuwa tunachukua masomo yanayofanana tungesingizia kuwa tulikuwa tunajisome, lakini tofauti na sisi ambao wote wawili tulikuwa tunasomea uhandisi, Elizabeth alikuwa anasomea ualimu.
Kitendo cha kusingiziwa kuwa anatembea na miye kilimchukiza sana Elizabeth, mwishowe akajikuta anaanza kunishawishi tufanye kweli ili hata Paul akiwa anatulaumu iwe kweli. Mimi ni mgonjwa, ni mgonjwa kwa kweli, linapokuja suala la kiumbe wa kike. Hivyo sikuwa na nguvu za kupinga. Tukaanza kuwa tunafanya na Elizabeth.
Paul alipokuja kugundua, hapo urafiki wetu ukafa kabisa. Tulipomaliza chuo tukapangiwa kazi maalum, yeye alipelekwa Kagera wakati mimi nilipelekwa Ruvuma.
Miaka sita baadaye nikahamishiwa Arusha, kwa bahati nzuri au mbaya na yeye akahamishiwa Arusha. Hivyo wote tukawa Chuo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi Monduli. Hapo Paul akaamua kuoa, mimi bado nilikuwa sijaamua bado. Urafiki wetu ulipata uhai kidogo, japo mara zote Paul alikuwa akinitaja kama mlafi wa wanawake…”
“Ila wewe unaona ni kweli au si kweli?” Maganga alimkatiza kwa swali. Yule Mzee hakujibu, alitabasamu, huku akiuruhusu ulimi wake uyafute meno ya mbele juu na chini.




PATASHIKA: 07

“Sijui kwa kweli, jipe jibu mwenyewe. Basi ndani ya miaka mitatu Paul na mke wake hawakuwa wamefanikiwa kupata mtoto. Hii ilianza kuleta ugomvi kati ya Paul na mkewe ambaye alikuwa akiitwa Agatha. Kila mara Paul alipokuwa akilewa, alikuwa anampiga sana mkewe sababu ikiwa ni kushindwa kumzalia mtoto. Paul alidai kuwa dada zake na mama yake walikuwa wakimsumbua kuwa wanataka mtoto.
Basi siku moja kulikuwa na sherehe ya kuhitimu mafunzo ya kijeshi, kwa kawaidi viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Rais walikuwa wakija wakati wa mahafali hayo. Baada ya mahafali kufanyika mchana, usiku zilikuwa sherehe , watu kula, kunywa na kufanya anasa za kila aina.
Siku hiyo Paul kama kawaida baada ya kunywa na kulewa akaanzisha fujo na kuanza kumpiga mkewe. Kwa vile wengi walikuwa wamechoka na vitendo vyake hivyo vya kumyanyasa mkewe, walijitokeza wanaume wachache kumtuliza, lakini akataka kupigana nao, hapo ndipo walipompa Paul kipigo kikali sana, hakuna mtu aliyejitolea kumsaidia, ila miye nikaona nimsaidie kumwondoa mke wake maeneo hayo. Tulipoondoka eneo la tukio, mke wake akagoma kwenda nyumbani kwao usiku huo kwa kuhofia usalama wake. Hapo tena nikaona nimsaidie, nikamchukua mke wake hadi nyumbani kwangu tukalala naye. Alikuwa na mke mzuri, na nadhani unajua ugonjwa wangu...”
“Nimeshakuelewa Mzee, isingekuwa rahisi ugonjwa usipande wakati uko kwenye mazingira hatarishi kama yale!” Maganga alisema huku akionyesha kufurahia simulizi ya huyo Mzee. Kisha akakumbuka kisa chake na Milka usiku wa juzi.
“Eti, Mzee vipi kama una dada yako mzuri halafu akajipendekeza?” Maganga alihoji huku kwa mara ya kwanza katika maisha yake akijisikia huru kuongea hayo mambo. Alijikuta ile hofu aliyokuwa nayo mwanzo imemtoka.
“Maganga, sijajua unamaanisha nini lakini huwa kuna mazingira tata ambayo akili inakuwa na nafasi ndogo sana ya kuweza kupambanua mambo. Na hapo kama una ule ugonjwa kama mimi, utajikuta umeanza kupembua jema au baya wakati ukiwa unapumzika baada ya kumaliza kitendo.” Alisema yule Mzee, tabasamu likiwa limechanua usoni.
“Ha ha ha ha! We Mzee unanifurahisha.” Maganga alicheka.
“Basi asubuhi nikamwambia aamkie kwa mkuu wa kambi na amweleze kilichotokea na akiulizwa alilala wapi aseme kanisani. Basi mkuu wa kambi aliwasuluhisha huku Paul akipewa onyo kali juu ya tabia yake ya kupiga na kumdhalilisha mke wake. Baada ya miezi kadhaa habari zikavuma kuwa mke wa Paul alikuwa na uja uzito. Hatimaye Paul na mke wake wakafanikiwa kupata watoto mapacha wa kiume na wakike. Mke wake Paul alikuwa mwenyeji wa Mwanza, hivyo alikwenda kujifungulia Mwanza katika Hospital ya Bugando. Paul alifurahi sana.
Siku moja nikiwa katika pitapita zangu, nikakutana na mke wa Paul, alinisalimia kwa furaha sana. Lakini pia, akaniambia kuwa anatamani ile siku ingejirudia. Alinisisitiza sana niende nikawaone watoto. Nilijua uhusiano wangu na Paul haukuwa mzuri sana, hasa ambapo angegundua kuwa safari hii tena nimeanza kuwa jirani na mke wake, angeweza hata kunitia risasi. Nilimshukuru mke wake lakini nikamwambia ingekuwa vigumu kwenda nyumbani.
Siku nyingine tulipokutana naye aliniomba tupange tukutane naye mahali ili niwaone na kumsalimia watoto, msisitizo wake ulianza kunipa wasiwasi. Maana ilikuwa wazi alikuwa akijisikia raha zaidi kuwa na mimi na pia ilikuwa wazi kuwa alitaka sana niwe na ukaribu na watoto.
Baadaye ikawa tabia kuwa kila mwezi ilikuwa lazima tukutane na mke wa Paul mara mbili au tatu kwa ajili ya kuhudumiana. Muda ukafika na miye nikaamua kuoa, siku ya harusi yangu ndipo mambo yalipoharibika. Takribani ndugu zangu wote walikuwa wamekuja kwenye harusi yangu. Tukiwa katikati ya sherehe, ndipo bomu lilipolipuka, na kusababisha vifo vingi vya papo hapo huku wengi wakiwa na majeraha ya kutisha.
Kwa kifupi, katika tukio lile nilipoteza ukoo wangu wote wa karibu huku mwenyewe nikiwa na hali mbaya ya majeraha. Ni katika tukio hilo pia nilipoteza uwezo wa kulala na mwanamke kama mwanaume rijali.” Mzee alipofika hapo alinyamaza. Akaangalia chini huku akiminya minya mikono yake ambayo ilikuwa imeanza kutetemeka. Maganga alijikuta akianza kumuhurumia huyo Mzee.
“Bora ningekatwa miguu, lakini ningebaki na burudani yangu.” Alisema yule Mzee kwa masikitiko
“Pole Mzee wangu yote ni mapenzi ya Mungu…”
“Hapana Maganga, siamini kama hayo ni mapenzi ya Mungu….Mungu kweli anapenda kiumbe wake aishi bila furaha!?” Alisema huyo Mzee kwa sauti ya kulalamika. Alitia huruma.
“Basi kwa vile mkuu wa kambi alikuwa rafiki yangu nilipelekwa Urusi kwa matibabu. Nilipomaliza matibabu nilipitiliza huko huko kwa mafunzo mengine maalum. Baada ya miaka mitatu nilirudi, nikapelekwa Makao Makuu ya Jeshi. Baadae, nilipata mawasiliano na Paul, alikuwa ameshahamishiwa Dar es salaam. Kwa kuwa alikuwa amejua nini kimenipata hivyo hakuwa na hofu nami tena. Alianza kunikaribisha kwake, pale kambi ya Ruvu. Wakati mwingine aliniita ili nikashinde pale wakati wa mwisho wa wiki.” Alipofika hapo Mzee huyo alimwangalia Maganga kisha akainuka. Aliporejea, akaja na juisi ya Parachichi.
“Najua unapenda sana hii juisi.” Alisema huku akimkabidhi glasi moja.
“Umejuaje kuwa napenda, japo ni kweli napenda sana juisi ya Parachichi?”
“Wewe jua tu kuwa najua.” Alijibu yule Mzee.
“Najua hata hizi habari ninazokupa hasa za mambo ya wanawake unazipenda sana, maana ndiyo asili yako na siyo huo upadri unaoung’ang’aniza.” Alisema huku akiinua glasi ili anywe juisi.
“Jumamosi moja nikiwa kwa Paul huku yeye mwenyewe akiwa amesafiri kikazi, mwanae aligongwa na gari. Kwa vile alivuja damu nyingi ilitakiwa mtu ajitolee kumwongezea. Kwa vile nilikuwa pale ilibidi utaratibu ufanyike nitolewe damu. Mke wa Paul pia alikuwa akisisitiza kuwa lazima nimsaidie mwanae. Nilimweleza kuwa inategemea kama makundi ya damu zetu yanawiana, lakini yeye alisisitiza tu kuwa lazima yatawiana.
Hilo lilinishangaza mimi na kunipa wasi wasi, Daktari aliyekuwa anamhudumia yule binti, mtoto wa Paul naye akaingiwa na wasiwasi juu ya tabia aliyoonyesha mke wa Paul. Hivyo walipokuta damu yangu inafanana na ya mtoto waliichukua na kumwongezea mtoto. Lakini tukafanya kitu cha zaidi tukapima vinasaba vya damu ya mtoto na yangu. Cha kushangaza, ilibainika kuwa yule mtoto alikuwa wangu. Nilishikwa na mshangao uliochanganyika na furaha.” Hapo alitengeneza koo lake kisha akaendelea.
“Duniani hakuna siri, habari zikamfikia Paul, ikabidi aende kupima damu yake na ya watoto kuona ukweli wa mambo. Alishangaa kukuta ni kweli. Siku moja nikiwa natoka matembezi jioni, ilikuwa ni miezi kadhaa baadae, nilivamiwa na watu ambao naweza kusema walikuwa maalum, kwani pamoja na utaalamu wangu katika kupigana, lakini nilikuta watu hao wananizidi kila idara. Watu hao waliniambia wazi kuwa nimeingilia maisha ya watu na kwa hivyo nilikuwa nakwenda kufa, ili kuondoa ushahidi wowote kuwa nimeuawa, watu hao wakaishia kunitupa katikati ya bahari ili nifie huko. Lakini kwa kudra za mwenyezi Mungu nikiwa katika hatua za mwisho, kama ilivyokuwa kwa Hellen jana, wavuvi waliniokoa baada ya mtego wao wa samaki kunikokota toka vilindi vya Bahari. Sikurudi kambini, niliwasiliana na mkuu wangu wa kazi, akanikubalia kujiuzulu. Na kama zawadi ya jeshi kwangu, ndiyo wakanijengea nyumba hii na kuniwekea vitu vyote unavyoviona humu ndani.
Uchunguzi juu ya kifo changu, ulifanyika, maana hakuna aliyekuwa anajua kuwa bado naishi. Tulikubaliana na mkuu wangu kuwa kwa usalama wangu bora ijulikane kuwa nimekufa. Lakini pia baada ya uchunguzi, Paul aliachishwa kazi huku akipoteza haki zote za msingi. Kufuatia ombi langu, mkuu wa kambi alijitolea kumnunulia Paul mashamba katika kijiji hiki. Lengo ni kuwa pamoja na kuwa nimekufa lakini niwe na uwezo wa kuwaona wanangu.” Alipofika hapo Maganga alishituka.
“Unamaanisha nini? Paul unayemwongelea ni yupi?”
“Paul ninayemwongelea ni baba yako, watoto ninao waongelea ni wewe na Milka.” Alipofika hapo, Maganga akawa kama aliyekufa ganzi. Alishindwa kufikiri, akili yake iligoma kuamini, aliona kama ni hadithi ya kutungwa na kuwa hayakuwa mambo halisi. Alimwangalia yule Mzee katika hali ya bumbuwazi. Mzee alisimama kisha akatoka nje. Akili ya Maganga ilizunguka ikasimama, ikaruka, ikachuchumaa, ikalala kwa muda, ilipokuja kuanza kuzunguka tena. Alijikuta anaongea kwa sauti.
“Haiwezekani, unajaribu kunirubuni tu! Nooooo !” Alipiga ngumi juu ya meza.
Mlango ulifunguliwa, Hellen aliingia huku akiwa na tabasamu usoni. Maganga alipomwona Hellen alisimama, alisikia kama kuna vitu vinamtembea mwilini japo hakujua ni nini hasa.
“Pole Hellen! Maganga alisema huku akiwa ameshamfikia Hellen ili amkumbatie.
“Don’t!” Hellen aling’aka.
“Wewe na baba yako lenu moja, na mtajuta kwa mliyonitendea.” Hellen alisema huku machozi yakimlengalenga. Maganga alijikuta anashindwa namna ya kujitetea.
 
PATASHIKA: 8

WAKATI Maganga akiwa anafungiwa kwenye kile chumba kilichojaa vitabu na maandiko mbalimbali jioni ile, Milka yeye alikuwa akihangaika na baba yake, mzee Paul, ambaye mguu wake ulikuwa umefura vibaya sana baada ya kuanguka wakati akikimbia toka shambani ambako alikuwa amemning’iniza Hellen kwa nia ya kumnyonga.
Baada ya kumpigia simu Maganga kumwelezea yaliyokuwa yamemkuta baba yao, Milka alikuwa katika harakati za kumpeleka baba yake, mzee Paul hospitalini. Kwa msaada wa watu wengine pale kijijini, alifanikiwa kumpeleka hospitali ya misheni, Katunguru.
“Dokta naomba umsaidie baba yangu jamani, mkimwacha akae kwenye foleni wakati ana maumivu kiasi hiki itakuwa ni utesaji,” Milka alimwambia daktari aliyekuwa anapita kwenda upande kulikokuwa na kinamama waliotoka kujifungua.
Wakati huu mzee Paul alikuwa akigugumia kwa maumivu makali, japo mguu ulionekana wa kawaida tu.
"Bila shaka atakuwa amevunjika huyu," daktari alisema mara baada ya kuwa ameuangalia mguu wa mzee Paul kwa muda.
“Neema, hebu mleteni huyo mzee huku ndani,” daktari alimwambia muuguzi aliyekuwa amebeba dawa. Kauli ya Daktari ilionesha kuwa alikuwa ameafikiana na maelezo ya Milka.
“Oooh... mguu wangu, ooooooh God!” mzee Paul alipiga kelele kwa uchungu wakati alipokuwa anainuliwa kupelekwa kwenye chumba cha vipimo.
“Pole baba, ngoja wakuhudumie hali itakuwa nzuri,” Milka alisema kwa huruma, alishaweka pembeni ugomvi mkubwa waliokuwa nao asubuhi ya siku hiyo. Muda huu ilikuwa ni saa tatu na nusu usiku, ni siku ile ambayo Maganga alikuwa ametekwa na yule mzee kule shambani.
“Kutokana na hali ilivyo huyu mzee inabidi apelekwe hospitali ya Wilaya Sengerema, ni dhahiri kuwa kavunjika mguu. Kule ndiyo wapo wataamua ama kuunga au kuukata inategemea na jinsi watakavyoona,” daktari alimwambia Milka.
Maelezo hayo yalimchanganya sana Milka. Alichukua simu yake ili kuuliza Maganga alikuwa amefika wapi, maana tangu alipokuwa amemtaarifu muda ulikuwa umeshapita. Aliijaribu simu ya Maganga lakini haikuwa inapatikana.
“Najaribu, kumpigia Maganga lakini simu yake haipatikani,” Milka alimwambia baba yake katika hali ya kuchanganyikiwa.
“Inawezekana yuko kwenye mambo ya kanisa, haina shida maadam anafanya mambo ya Mungu,” mzee Paul alisema huku akiwa anauma meno, ishara kuwa alikuwa anapambana na uchungu wa maumivu.
“Sidhani kama hiyo ni sababu ya msingi baba,” Milka alisema kwa hisia kali. “Hawezi kukuacha wewe unateseka hapa halafu akasema kuwa yuko kwenye kazi za kanisa. Hata hiyo jamii anayoihudumia sidhani kama atakuwa anaifundisha kwa vitendo. Maana hii ni sawa na wale wanaosema fuata maneno yangu na si matendo yangu. Maganga hawezi kufanya hivyo, nadhani kutakuwa na tatizo limempata maana hata nilivyoongea naye, haikuwa sauti ya Maganga ninayemfahamu.”
Milka alikuwa na wasiwasi uliochanganyika na kuchanganyikiwa. Alikuwa anamfahamu Maganga tangu wakiwa wadogo, hakuwa mtu wa kuambiwa baba kaumia halafu awe hajaonekana hadi muda ule. Alijua ingekuwa vigumu kwa yeye Milka, kumsamehe baba yao kwa yote aliyomfanyia mama yao lakini si kwa Maganga. Maganga ni mtu aliyejaa upendo na msamaha na ndiyo maana alimpenda kaka yake huyo.
* * *

Saa sita kasoro dakika mbili usiku, kwa msaada wa gari la AIC misheni ya Katunguru, mzee Paul na Milka ndiyo walikuwa wamefika Hospitali ya Wilaya Sengerema. Wataalamu waliamuru mzee Paul apelekwe moja kwa moja chumba cha upasuaji.
Wakati wakiwa wanampeleka huko, mara Milka akakutana na Vivian. Vivian alikuwa anatokwa na machozi. Alipomwona Milka ndiyo machozi yakazidi kububujika.
“Milka, mbona mmechelewa sana kuja mpenzi, hali ya mama ni mbaya sana. Amekuwa akilalamika kuwa anataka awaone, ni hakika kuwa uwezekano wa yeye kupona ni mdogo sana. Najaribu kumpigia Maganga lakini simu yake haipatikani, je, una taarifa zozote kuwa yuko wapi na ana mpango gani?” Vivian alisema kwa uchungu, huku tayari akiwa ameshamkumbatia Milka.
“Saa mbili kasoro nilimpigia simu Maganga,” Milka alisema. “Nilimpata na nikamwambia juu ya maendeleo ya mama kama ulivyoniambia lakini pia, nikamwambia kuwa baba amepata ajali na kuvunjika mguu. Nimejaribu kumpigia tena wakati tulipoambiwa kuwa tunatakiwa kumleta huku baba, lakini simu yake haikuwa inapatikana. Muda ule nilipoongea naye, nilipata wasiwasi kidogo, maana sauti ya Maganga haikuwa ile yake ya siku zote.”
“Ilikuwaje?” Vivian alisema kwa kushtuka kama mtu aliyetoneshwa kidonda kilichovunda.
“Alionekana kuwa na wasiwasi halafu ni kama mtu aliyekuwa anataka nimalize kuongea haraka!” Milka alisema huku akiwa anatengeneza sketi yake.
“Unadhani anaweza kuwa wapi?” Vivian alihoji.
“Sijui kwa kweli.” Milka alijibu.
“Duh! Mbona haya mambo yanatokea kama vile kuna mkono wa mtu?” Vivian alisema huku akiwa anamvuta mkono Milka kuashiria kuwa amfuate.
“Ni vyema twende ukamwone mama sasa hivi!” Vivian alisema huku akiwa anamwongoza Milka kuelekea ilipo wodi ya wagonjwa walio katika hali mbaya. Walipokuwa wanatazamana na mlango wa chumba walichokuwa wanakwenda, mara nesi alitoka huku akiwa anakimbia. Kuona hivyo, Vivian na Milka nao wakakimbia kuharakisha kuingia kwenye kile chumba. Walipoingia walikwenda moja kwa moja kwenye kitanda alichokuwepo mama Milka. Walipomwangalia kila mmoja hakungoja utaalamu wa daktari kumwambia kuwa mgonjwa wao alikuwa katika dakika zake za mwisho.
Milka alimshika mkono mama yake, kisha akainama na kumwambia, “Mama, tafadhali usituache, bado tunakuhitaji mama!”
Bila shaka mama Milka aliitambua sauti ya mwanaye. Alifumbua macho kisha akatabasamu. Akaushika mkono wa Milka kwa mikono yake yote miwili. Alitaka kusema kitu akashindwa maana sauti yake ilikuwa kama anayekoroma vile.
“Milka, mwa... mwa... mwanangu, ni…i…n i…i..samehe mimi mama yako. Mwambie Ma... ma... Maganga naye anisamehe…mwambieni asisahau kuangalia chini ya mtungi. Nimemsamehe baba yenu….kwa vile…a.a.a.a.a.a.linifichi..ia.siri yangu... Kwa..a...a...a...a...a...a...aher… ....aaaaggggrrrih. Mwasumbi Mwasumbiiiiii...Mwasumbiiii.” Hilo ndilo lilikuwa neno la mwisho la mama yao. Mwasumbi.
Akaendelea kukoroma huku macho yake yakigeuka na kuwa meupe. Kilichofuata hapo ni kilio toka kwa Milka na Vivian.

* * *

Wakati Agatha mama yake akiwa anapigania uhai wake katika hospitali ya Wilaya Sengerema, Maganga alikuwa kwenye wakati mgumu mbele ya Hellen. Hellen hakuishia tu kukataa kukumbatiwa na Maganga, akaendelea kumshambulia kwa maneno. Bado walikuwa kwenye ile nyumba ya yule Mzee aliyemkomboa Hellen kitanzini, Mzee Mwasumbi.
“Baba yako Mzee Paul ameshaniua, naishi lakini kwenye akili zake miye ni mfu. Amefanya haya yote kwa ajili yako na Milka, anaona nyie mkijua kuwa miye ni mtoto wake hadhi yake kwenu itashuka...”
“Kwa ajili yangu na Milka?” Maganga alihoji kwa hamaki na kumkatisha Hellen ambaye bado alikuwa anaongea
“Ndiyo, anajua kuwa miye ni mwanae!” Hellen alisema huku akijimwaga kitini. Kwa vile alikuwa amevaa khanga moja tu, macho ya Maganga yalibaki yanaangalia mtetemeko wa viungo vya msichana huyo. Alipomwangalia Mzee Mwasumbi, alikutana na macho yaliyokuwa yakimsoma Maganga wakati akiwa anamwangalia Helleni kwa matamanio. Ugonjwa!
“Ina maana wewe ni mtoto wa Mzee Paul!?” Maganga alisema kwa mshangao mkubwa.
“Ndiyo Maganga, na inavyoonekana baba anajua hilo, ila hataki nyie na jamii ijue kwa sababu ya kulinda heshima yake.” Hellen alisema kwa uchungu huku akifuta kamasi ambazo zilikuwa zinachuruzika kwa wingi.
“Heshima, kwani mtu kuwa na mtoto ni kosa? Kwa nini hataki siye tujue? Je, mama anajua hilo? Wewe umejuaje kuwa baba anajua na hataki siye tujue?” Maganga aliuliza maswali mfululizo bila kutoa nafasi kwa Hellen kujibu. Alikuwa amechanganyikiwa na taarifa hizo, si kuwa hakutaka Hellen kuwa ndugu yake, ila ni vile haya mambo yalivyojifunua kwa muda mfupi bila kumpa nafasi ya kufikiria na kuyapokea.
“Jana niliongea na Mzee Paul, na kumweleza kile kilichonifanya nifunge safari toka Dar es Salaam kuja huku Katunguru katika Wilaya ya Sengerema.
Ni kufuatia mama yangu kunisisitiza kuwa nije kumtafuta baba yangu katika kijiji hiki cha Katunguru. Mzee Paul hakuoneka kushtuka, na pia aliweza hata kukumbuka jina la mama yangu mzazi kuwa anaitwa Theresia. Lakini akaniambia kuwa ili yeye kuthibitisha kuwa mimi ndiye yule mtoto aliyekuwa amezaa na Theresia inabidi taratibu za kimila zifuatwe. Ndipo akaniambia kuwa twende kule shambani chini ya mti, na nifumbe macho wakati mizimu ya mababu itakapokuwa inanihakiki kama miye ni mwanae kweli au la. Hapo ndipo akaishia kunitundika, kabla huyu Mzee Mwasumbi hajatokea na kuniokoa.” Hellen alielezea huku kilio cha kwikwi kikiwa kinasikika. Maganga alisogeza kiti chake na kukaa jirani na Hellen. Baada ya dakika kadhaa za kubembelezana hatimaye Hellen alinyamaza.
Baada ya Hellen kutulia, Mzee Mwasumbi alikaribia na kuwaambia,“Ukweli ni kwamba miaka ishirini iliyopita Paul alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Theresia ambaye ndiye mama wa Hellen. Nayaita mahusiano kwa vile wawili hawa walitumia kitanda kimoja katika kutafuta mtoto. Haikuwa hiari ya Theresia, lakini kwa Paul ilikuwa ni hiari yake. Kama nilivyokusimulia Maganga, baada ya kugundua kuwa watoto wote aliokuwa nao si wake, Mzee Paul alitafuta chanzo cha tatizo. Ndipo wataalamu walipomwambia kuwa shida ilikuwepo kwa sababu ya muundo wa chembe chembe hai za Paul na mkewe Agatha zilikuwa haziingiliani. Ambapo kutokana na aina ya chembe chembe za uhai alizonazo baba na mama hawawezi kwa pamoja kutengeneza mtoto, hata kama wakitengeneza mtoto hataweza kuishi maana atakufa akiwa mdogo. Paul akaambiwa kuwa anaweza kuzaa na mwanamke mwingine. Hivyo akaamua kwa siri sana kutembea na msichana wake wa ndani, ambaye ndiye Theresia mama yake Hellen. Hapo ndipo ulipopatikana Hellen.” Alisema huyo Mzee huku akiwa amebeba glasi mbili za mvinyo, moja alimpa Hellen na moja akampa Maganga.
“Sasa kwa nini baba hataki kukubali kuwa huyu ni mwanae?” Maganga alihoji.
“Hilo pia ni suala la kihistoria Maganga! Baada ya kugundua kuwa ana uwezo wa kuzaa na mwanamke mwingine, Paul alikusudia kulipiza kisasi kwa mama yenu. Jambo hili alilifanya hata kabla hajafanya jaribio la kuniua. Hivyo alipanga kuzaa na Theresia kisha, angefanya utaratibu wa kutaka mpimwe hadharani kisha angewakataa ninyi. Mpango huu alimwambia mmoja wa marafiki zake wakiwa kwenye baa, bila kujua kuwa rafiki yake huyo ana uhusiano wa kimapenzi na msichana, ambaye ni mdogo wake na mama yenu.
Taarifa zikamfikia mama yenu, ambaye naye aliwashirikisha baadhi ya ndugu zake wa karibu ambao wangeweza kumsaidia pindi angefukuzwa na watoto.”
“Je, mama hakuwasiliana na wewe kama baba wa watoto?” Maganga alimkatiza yule Mwasumbi kwa swali.
“Alinitaarifu maana wakati huo ilikuwa bado sijafanyiwa jaribio la mauaji, nami nikamwambia si mpango wangu wala furaha yangu kuona ndoa yake inavunjika, hivyo nilimwambia ningeingilia kati pale tu ambapo ningeona kuwa sasa msaada wangu unahitajika kwa ajili ya kuwanusuru watoto wangu. Mzee Paul alikuwa akitaka mtoto wa kiume, hivyo hakufurahi pale Theresia alipojifungua mtoto wa kike ambaye ndiye huyu Hellen. Ili kuondoa utata tena, ndipo akaamua kuwaona madaktari ili wampe namna ya kufanya ili apate mtoto wa kiume. Hapo ndipo kaka yake mama yenu, yeye akiwa kama daktari alipotumia mwanya huo kama kutaka kumsaidia Mzee Paul. Ni katika kumsaidia huko ndipo alipomfanyia ‘testosterone injections’ kwa kiwango kikubwa. Hiyo iliondoa kabisa uwezo wa Mzee Paul kupata mtoto, hilo likamkumbusha ule usemi wa waswahili kuwa, usiache mbachao kwa msala upitao. Ili asiharibu heshima yake mbele ya jamii kuwa hana mtoto wa kiume, maana kwake mtoto wa kiume ndiyo mtoto. Akaamua kumfukuza Theresia na kumpa vitisho vizito kuwa asije thubutu kutoa siri. Lakini pia, alimwonya kuwa asimfuatefuate maishani mwake. Miye niliweza kuyajua hayo kwa sababu Theresia alinijia siku moja kuomba msaada na ndipo aliponisimulia yote hayo kwa masharti kuwa nisimsimulie mtu yeyote. Pia, akaniambia kuwa lolote likitokea niwe tayari kumwonyesha Hellen alipo mzazi wake halisi.” Alisema Mzee huyo na kuweka tuo. Wakati wote huo Maganga na Hellen walikuwa wakisikiliza kwa makini sana. “Hellen na Maganga, nadhani tumeongea mengi, tumeulizana mengi na tumejibizana mengi, binafsi naona kama nimetua mzigo niliokuwa nimeubeba kwa siku nyingi sana.” Alisema Mzee huyo.
* * *
Hii ilikuwa siku ya tano tangu siku ile Mzee Mwasumbi alipomwokoa Hellen katika tundu la kifo na kumteka nyara Maganga kwa nia njema kama yeye mwenyewe anavyosema.
“Kukuteka kwangu nyara, niliona ndiyo njia pekee ya mimi kupata muda wa kuongea na wewe mambo haya mazito, na wakati huohuo wewe ungeweza kunisikiliza.
Mnayo haki ya kuyafanyia uchunguzi mambo haya niliyowaambia ili kuthibitisha kama ni kweli au la.
Naomba mniache niendelee kuishi maisha yangu haya ila kama kwa kufanya hivyo mnaona siwadhulumu na kuwanyima haki zenu za msingi. Kwa hivi sasa niko tayari kwa lolote kwani baada ya kuyasema haya maisha yangu hayana thamani kama yalivyokuwa hapo kwanza. Nilikuwa naogopa sana kama ningekufa halafu nyuma yangu akakosekana mtu wa kuufunua ukweli huu. Lakini maadamu nimeshausema, hata nikifa hakuna jambo ambalo litanifanya nitamani kurudi Duniani.” Alisema Mwasumbi huku akiwa anajitengeneza kitini. Walikuwa wameshaongea mengi na ilivyokuwa kila mtu alikuwa ameridhika na hakukuwa na la kuongezea.
“Hivyo mimi leo nawaruhusu kuondoka hapa, ila msimwambie mtu kuhusu maisha yangu. Napenda niendelee kuishi hivi, msalimieni Milka na ningependa nionane naye pia.” Alisema Mwasumbi huku akisimama na kwenda kukumbatiana na Maganga na Hellen, ambao hata hivyo walioneka kana kwamba wamepigwa na bumbuwazi na walihitaji muda kutafakari na kupembua yote waliyokuwa wameyaona na kuyasikia hapo.
**********
UMATI MKUBWA ULIKUWA UMEKUSANYIKA kwa Mzee Paul kufuatia kifo cha Agatha, mke wa Mzee Paul. Msiba huo ulikuwa umebeba hisia tofauti-tofauti miongoni mwa wanakijiji waombolezaji. Wapo waliokuwa wanajua kuwa mke wa Mzee Paul alifariki kufuatia kipigo kikali toka kwa mumewe, Mzee Paul.
Mzee Paul mwenyewe hakuwa anaumizwa kichwa na kifo cha mke wake, sababu za kutoumizwa sana na kifo hicho ni nyingi na zilikuwa wazi kichwani mwake lakini kubwa ni kuwa Maganga alikuwa na umuhimu zaidi kuliko utu na mapenzi. Ni kweli Agatha mkewe walikuwa wameishi naye kwa muda mrefu lakini yeye hakuhesabu kuwa ni kitu kwani hawakuwahi kuwa na mtoto na mwanamke huyo. Kwa sasa kichwa chake kilikuwa kinaumizwa na kutoonekana kwa Maganga.
Katika hali halisi msiba huu ulikwa ‘msiba’ kwa Vivian na Milka. Walikuwa wameona jinsi Aghata mke wa Paul alivyokuwa amefariki. Lakini pia, walikuwa wanaujua ukweli kuwa kifo kile kilikuwa kinatokana na kipigo alichopata toka kwa Paul. Tatu ilikuwa haijulikani Maganga alikuwa wapi. Kingine kilichokuwa kinawaumiza ni kauli ya mwisho aliyokuwa ametoa mama yake Milka dakika za mwisho za uhai wake. Ile kauli kuwa wamsamehe na kuwa amemsamehe baba yao kwa vile amemfichia siri kwa muda mrefu. Ilikuwa inamuumiza Milka kutaka kujua ni ‘siri’ gani ambayo baba yake alikuwa amemfichia mama yake kiasi kuwa mama akawa tayari kumsamehe. Pili, ni kitu gani ambacho mama alitaka wamsamehe, maana hakuweza kukisema wazi.
Mzee Paul alikuwa amegoma mwili wa mke wake kuzikwa ikiwa Maganga hakuwepo.
“Haiwezekani mke wangu kuzikwa wakati mwanangu hayupo. Nimeshaomba hospitali watauchoma sindano mwili ili usiharibike” Alisema Mzee Paul ambaye sasa alikuwa anatembelea gongo.
Jioni hii siku ya tano watu wakiwa wamekaa, wangine wanacheza bao, wangine karata, wengine wako kwenye mabishano ya mpira, wamama washika dini wako wanaimba zile nyimbo za misibani na wengine wakiwa na habari zao za umbea tu, maana penye wengi pana mengi.
Mara kwa mbali wakaona watu wawili wanakuja. Wakiwa kwa mbali hakuna aliyeweza kutambua sura zao, ila ilikuwa dhahiri kuwa mmoja alikuwa mwanaume na mwingine ni mwanamke. Watu hao waliposogea karibu ndipo watu walipoweza kutambua kuwa walikuwa ni Maganga na Hellen. Wengi walimjua Maganga ila hawakuwa wanamjua Hellen. Kutokezea kwa Maganga kulisababisha msiba kuanza moja, watu walilia sana, lakini Milka alilia zaidi huku akionyesha dhahiri kutokumwelewa kaka yake. Katoweka kwa takribani wiki nzima halafu anarejea katikati ya msiba akiwa na msichana ambaye ni mgeni pale kijijini.
Maganga alipoambiwa kuwa ule msiba ulikuwa wa mama yake alikaa chini mavumbini, kisha akalia sana.
“Baba yuko wapi?” Alilia huku akiuliza watu wamuonyeshe baba yake.
 
PATASHIKA - 9

Huku akiwa anaomboleza kwa uchungu mkubwa Maganga alilia kuelekea kilipokuwa chumba cha baba yake. Kabla hata hajaingia ndani mara akasikia sauti inamwita kwa nyuma yake usawa wa mlango wa kutokea nje. Aliifahamu sauti hiyo, ilikuwa ya Askofu Alphonso, Maganga aligeuka na kumwangalia askofu kwa macho makali.
“Maganga, naomba tuonane ofisini kwangu, naelewa hali uliyonayo sasa, ila tafadhali sana naomba tuonane sasa hivi.” Askofu alisema huku akimshika na kumkumbatia Maganga.
“Nataka kumuona Mzee Paul kwanza halafu nitakuja baba Askofu.” Maganga alisema kwa jazba na uchungu mkubwa.
“Nakushauri tungeongea kwanza, ni maongezi muhimu sana ambayo yatakusaidia pia, kuonana na baba yako.” Askofu alisema huku akiwa anamwangalia Maganga machoni. Maganga alipoonyesha kutoafikiana na Askofu, ndipo Askofu akamnong’oneza
“Baba yako yuko kule kwangu.”
Kusikia hivyo, Maganga hakubisha tena waliongozana na Askofu kuelekea kanisani ambako pia, pembeni yake kulikuwa na nyumba ya Askofu na watawa wengine.
Maganga na Askofu walikuwa wameshaingia ndani ya nyumba ya Askofu wakati waliposikia mlio wa Bastola. Maganga alishtuka, askofu hakushtuka, alitabasamu. Maganga akainuka kwa haraka ili atoke nje lakini mara Askofu akamwita kwa sauti ya chini. Maganga alipogeuka kumwangalia Askofu akakuta ameshikilia bastola ameielekeza kifuani kwa Maganga. Maganga akabaki ameduwaa. Wakati hajui afanye nini maana hakutegemea kukabiliana na hali kama hiyo, Maganga alihisi anachomwa na kitu kama pini shingoni mwake. Alipotaka kushika sehemu aliyohisi yale maumivu, alishangaa alipohisi kuwa alikuwa amepoteza uwezo wa kunyanyua mkono wake. Wakati huo huo akahisi macho yake yamekuwa mazito kiasi kwamba uwezo wa kunyanyua kope ukamtoka. Giza likamvaa usoni na miguu yake ikashindwa kuubeba mwili. Akaanguka chini huku fahamu zikiwa zinamtoroka taratibu.
* * *
Fahamu zilipomrudia Maganga alijikuta amelala kitandani. Alizungusha macho pande zote, chumba kilikuwa nadhifu sana. Kila kitu ndani ya chumba hicho kilikuwa cheupe; mashuka, mapazia, viti na chochote kilichokuwepo. Ni sehemu chache ambazo vitu hivyo vyeupe vilikuwa vimewekewa alama ya msalaba mwekundu. Alijiinua taratiibu, akairuhusu miguu yake kutoka kitandani na kukanyaga chini. Miguu ikagusa chini, hilo likaruhusu yeye kuubebesha mwili wake kwenye hiyo miguu. Akasimama. Aliposimama ndipo akaona karatasi ndogo ikiangukia sakafuni toka pale kitandani. Inaonyesha karatasi hiyo ilikuwa juu ya mwili wake hivyo alipoinuka ikaanguka chini. Maganga aliiangalia karatasi hiyo ya njano iliyokuwa na maandishi meusi. Akainama kuichukua, wakati anaichukua ndipo alipogundua kuwa vidole vyake vilikuwa vikitetemeka. Hata hivyo aliichukua na macho yake yakakimbilia haraka kusoma maandishi ambayo yalisomeka hivi, ‘RELAX, IT IS FOR YOUR SAFETY. SAFE TRAINING. REV. ALPHONSO.’Kwa Kiswahili yakiwa na maana; ‘TULIA, NI KWA USALAMA WAKO. MAFUNZO MEMA.’ Ilikuwa wazi kuwa mwandishi wa Karatasi hiyo alikuwa ni Askofu Alphonso. Maganga alielewa maneno yale yanasomekaje, lakini hakuweza kuelewa lengo hasa la Askofu Alponso kusema vile. Aliiangalia ile karatasi kama mtu anayetaka kuuliza maelezo zaidi juu ya kile alichosoma. Lakini karatasi haikuwa na jipya. Akaikunja na kuiweka mfukoni. Wakati ameingiza mkono mfukoni ndipo alipohisi uwepo wa kitu kingine mfukoni mule. Vidole vyake vilikivuta kile kitu. Ilikuwa ni karatasi nyingine iliyokuwa chafu. Ndipo alipokumbuka kuwa kabla hajaondoka kumfuata askofu Alphonso siku ile pale nyumbani kwao alikuwa ameenda chini ya mtungi kama mama yake alivyokuwa amemhimiza asubuhi ile wakiwa ndani ya gari la Vivian muda mfupi kabla ya kupelekwa hospitali. Hapo tena Maganga akawa na hamu ya kujua kilichokuwa ndani ya karatasi hiyo. Hamu hiyo ilitokana na jinsi mama yake alivyokuwa ameificha ile karatasi na pia muda ambao mama yake aliamua kumwambia kuhusu hiyo karatasi. Alijua kwa vyovyote karatasi hiyo itakuwa na mambo muhimu ambayo mama yake angependa yeye ajue. Maganga aliifunua karatasi hiyo kisha macho yake yakaanza kutembea kwenye maandishi. Barua ilisomeka

Mwanangu, Maganga!

Sijui ni mazingira gani uliyonayo wakati unaisoma karatasi hii, ila ni dua yangu kuwa upate nafasi ya kuisoma maana ni muhimu sana kwako na kwa ndugu zako.
Maganga, leo siku ambayo tunakuaga hapa nyumbani kwa vile unasafiri kwenda shule kuanza mafunzo yako ya Ukasisi, nimegundua kuwa mbali ya kuwa mama na mwana lakini pia tumekuwa marafiki wakubwa sana. Najisikia furaha na fahari kubwa kuwa mama yako huku wewe ukionekana kuwa na furaha sana.
Lakini hata hivyo, kuna mambo ambayo siwezi kukuambia leo katika umri huu ulionao. Natamani ujumbe huu uupate miaka kumi au kumi na tano toka leo. Lengo langu ni kuwa upate haya ninayoandika humu siku ambayo utakuwa unapata upadirisho. Najua huo ndiyo utakuwa wakati muafaka. Ila kutokana na hali ya maisha niishiyo na Paul lolote linaweza tokea wakati wowote. Hivyo kwa kuwa sasa umeweza kuipata Karatasi hii ina maana nimeshindwa kusubiri hadi wakati huo ambao ningekuambia kwa mdomo wangu mwenyewe. Inawezekana wakati huu unaposoma karatasi hii mimi ni marehemu au ni taabani sijiwezi.
Maganga mwanangu, ningependa ujue haya mambo manne. Ningependa ujue majina yenu halisi kuwa mnaitwa;
1. Maganga Mwasumbi
2. Milka Mwenda
3. Vivian Mwasumbi
4. Hellen Paul
Maganga mwanangu, baada ya kuyajua mambo hayo manne, pia ningependa kukuambia machache ambayo yatakusaidia. Haya niyasemayo ni hisia zangu, naomba ufanye ambavyo hisia zako zitakuongoza na uonavyo kuwa ni vema.

Mwanangu, ni vema kuwa Padri, ila kwa mazingira yanayokuzunguka lazima ujifunze upande wa pili wa shilingi. Zingatia hili, Mwasumbi na Paul wako kazini. Ni mmoja tu kati yao aliye upande wako. Nasikitika kukuambia kuwa kwa kweli sijui ni yupi aliye upande wako. Nimejitahidi sana kwa miaka yote tangu umezaliwa hadi leo ninavyoandika ujumbe huu kutaka kujua nani hasa yuko upande wako lakini sijafanikiwa. Ninachojua ni kuwa wewe ni mtu uliyejaaliwa sana na unahitajika sana. Na kati ya hao niliowataja hawajuani kuwa wako kazini na mlengwa wao ni mmoja.
Nijuavyo ni kuwa ukimaliza mafunzo ya Upadri utakuwa umehitimu nusu ya kile unatakiwa kujifunza. Utakuwa umemaliza nusu ya safari ya mafunzo yako. Itakuja awamu ya pili.
Naomba ushike hii namba kichwani siku ukiona kuwa umefikia sehemu huwezi kuendelea mbele piga hii namba kwa msaada +255762204166.
Maganga, nakupenda sana mwanangu. Naamini utashinda yote yaliyoko mbele yako. Pia, utawasaidia wenzio kujua ukweli.
Umalizapo kusoma karatasi hii, tafadhali sana iharibu kwa kuichoma moto au kuitumbukiza chooni. Mtu yeyote akiiona itakuwa hatari sana, kwa maisha yako na ndugu zako.

Tafadhali kariri sana hiyo namba ya simu.
Akupendaye milele,

Agatha wa Mwasumbi na Paul.

Maganga alibaki akiwa ameiangalia ile karatasi kama Pusi aliyeona shimo la Panya. Wakati anaanza kusoma alikuwa amesimama lakini pindi alipomaliza alijikuta akiwa ameketi kitandani. Barua ile iligusa roho, nafsi na mwili wake. Mambo mengi yaliujaza ubongo wake. Alimtafakari Askofu Alphonso akamuacha, aliwaza mazungumzo yake na Mzee Mwasumbi, alimtafakari Milka akamwacha, aliwaza ujio wa Hellen kijijini kwao na jinsi mtu ambaye yeye alikuwa anajua ni baba yake alivyotaka kumuua binti yule. Alipomuwaza Mzee Paul na visa vyake vyote, Maganga akajikuta anajawa na hasira. Aliwaza namna Milka, Hellen na Vivian ambavyo wangekuwa wanamfikiria wakati huu ambapo yeye ametoweka katikati ya msiba wa mama yake na kuugua kwa baba yake. Wakati akiwa anawaza mara akasikia vishindo vya mtu aliyekuwa akitembea. Vishindo vya hatua za huyo mtu vilionyesha kuwa mtembeaji alikuwa akija upande wa chumba alichokuwa kwani sasa aliweza kuvisikia kwa karibu zaidi. Aliingalia ile barua ya mama yake, haraka haraka akaifutika mfukoni.
 
PATASHIKA - 10

Mlango wa chumba alichokuwemo ulifunguliwa. Aliingia binti mmoja mrembo sana, alimtazama kwa nukta chache kisha akaurudisha mlango nyuma yake.
“Naitwa Maganga. Unaitwa nani na hapa ni wapi?” Maganga aliongea kwa haraka haraka. Badala ya kujibu yule msichana alitembea taratibu hadi pembeni ya chumba sehemu iliyokuwa na meza. Akaweka kitu kama daftari lakini kilifanana hasa na kadi za harusi sambamba na hicho akaweka saa ya mkononi iliyotengenezwa kwa plastic. Alipomaliza akageuka na kutoka kwa kupitia sehemu aliyoingilia bila kuaga wala kuongea lolote.
Maganga akabaki anashangaa. Akaenda pale vilipowekwa vile vitu, akachukua ile karatasi na kuisoma. Alishangaa kwa jinsi ilivyokuwa imeandikwa. Ilikwa na kichwa kilichoandikwa, ‘RATIBA YA MAFUNZO’, halafu kikafuatiwa na ratiba ya siku nzima ambayo ilijaa matukio ambayo alitakiwa kuyafanya huku yeye akitajwa kama mwanafunzi. Katika ratiba hiyo hakukuwa na majina ya waalimu wala majina ya mahali alipotakiwa kuwa kwa mafunzo. Kulikuwa na muda kwa kila tukio huku muda wa kulala ukiwa ni saa nne tu kwa siku. Akaichukua ile saa akaangali, ilisomeka 6:05pm, hapo akajua kuwa ilikuwa ni saa kumi na mbili na dakika tano jioni. Kwa ratiba iliyokuwa mbele yake ilikuwa ni muda wa kula na kujiandaa kwa mazoezi ambayo yangeanza saa moja na nusu jioni.
Saa moja ilipofika, Maganga alikuwa amejipumzisha kwenye kitanda mle mle chumbani. Alikuwa amekula chakula katika hali ya kutatanisha baada ya kuletewa na mtu ambaye alikuwa haongei. Alipomaliza aligundua kuwa ndani ya chumba kile kulikuwa na kabati la nguo, bafu na choo. Hivyo tofauti na chakula, kila kitu angeweza kukipata ndani ya kile chumba. Mara taa ya chumbani humo ilizimika, giza likachukua nafasi. Akashtuka kiasi. Ukweli ni kuwa akili yake na hisia vilikuwa vimeshakufa ganzi, mambo yalivyokuwa yametokea kwa siku takribani saba mfululizo yalifanya awe mvivu wa kufikiri na hisia zake zilishamalizwa makali yake. Hivyo alijiona kuwa yuko tayari kwa lolote. Hakuwa anajali tena, aliona maisha yake hayakuwa na maana tena. Yangekuwaje na maana kama ameshindwa hata kumzika mama yake kipenzi, yatakuwaje na maana kama mtu aliyekuwa anatamani kuwa kama yeye ndiye aliyemteka na kumleta hapo. Yatakuwaje na maana kama muda wote amekuwa akiishi bila kumjua baba yake huku akiishi na mtu katili kama Mzee Paul. Yatakuwaje na maana.
“Njoo nifuate!” Sauti iliamuru tokea sehemu ambayo kulikuwa na mlango wa kutokea nje ya chumba kile. “Mbona hunielezi nikaelewa, wewe nani?”
“Njoo!” Ile sauti ilisema kwa ukali kidogo.
“Nieleweshe kwanza.” Maganga alisisitiza.
Hakupewa jibu, alishangaa tu anapokea kofi kali la usoni ambalo lilimpeleka hadi chini, kwa vile wakati aliposikia ile sauti alikuwa amesimama.
“Jesus!”Maganga aligugumia kwa maumivu.
“Njoo!” Ile sauti ilisema tena.
Maganga akatii. Alijikuta anafuata hatua za huyo mtu aliyekuwa mbele yake. Walipita milango kadhaa kabla ya kutokezea nje. Alishangaa kukutana na msitu mkubwa wa miti mikubwa na midogo.
“Hakikisha unanifuata kila ninakokwenda na kwa kasi ninayotumia. Ukishindwa unajua nini kitakupata.” Sauti ilisema. Maganga hakuwa na la kujibu wala hakupata nafasi ya kufanya hivyo kwani alikiona kivuli cha mtu aliyekuwa anamsemesha kilianza kukimbia kuingia kwenye lile pori.
Maganga akaanza kufuata. Sehemu walizopita zilikuwa za taabu na vichaka vilivyojaa miiba, lakini kila alipotaka kupumzika au kupunguza mwendo alishushiwa kipigo ambacho aliona heri kujilazimisha kukimbia kama alivyoamriwa. Hiyo ndio ikawa siku ya kwanza ya mafunzo ya Maganga. Aliporudi kwenye chumba chake alikuwa hoi huku akiwa na majeraha mengi mwilini.

************

SIKU ILE AMBAYO MAGANGA NA HELLEN waliruhusiwa kuondoka kwa Mzee Mwasumbi, na Maganga alipofika nyumbani kwao kisha akaanza kumtafuta Mzee Paul huku akilia kwa uchungu. Dakika chache kabla ya kuwasili kwa Maganga na Hellen nyumbani hapo Mzee Paul alikuwa shimoni kwenye nyumba yake hiyo. Watu wakiwa wamejaa nyumbani kwake kufuatia kifo cha mke wake. Mzee Paul aliingia ndani kwake kwenye chumba cha kulala akiwa anatembea kwa taabu sana kwa vile mguu bado ulikuwa umefungiwa muhogo. Lakini baada ya kuwa amejifungia chumbani kwake. Haraka sana aliufungua ule muhogo. Baadaye aliinua kitanda chake cha miti na kukisukumia pembeni. Ule uigizaji wake kuwa mguu umevunjika akawa ameshaachana nao. Aliyekuwa akishughulika sasa ni Mzee Paul kamili ambaye alionekana kuwa alikuwa akiharakisha kutaka kufanya kitu. Baada ya kuwa amekisukumia kile kitanda pembeni, alisogea sehemu moja ya ukutani karibia na sakafu akapapasa kisha akashika kitu kilichokuwa kama kisiki, akakivuta kama anayetaka kuking’oa. Kikabanduka kama kifuniko. Baada ya kufunuka likaonekana kufuli dogo likiwa limeshikamanisha vyuma viwili bapa. Haraka, Mzee Paul kwa kutumia funguo alizochukua mfukoni mwake alifungua lile kufuli. Alichukua upanga uliokuwa chumbani humo na kuuingiza katikati ya vile vyuma viwili vilivyokuwa vimeshikanishwa na kufuli akaanza kupindua mithili ya mtu afunguaye mfuniko wa ndoo ya plastiki ya maji. Mfuniko ulipofunguka, kukawa na shimo kubwa kiasi cha kuweza kumtumbukiza mbuzi wa miezi tisa. Mzee Paul kabla ya kutumbukia ndani alipanga vitu mle chumbani na kuwa kama hapo awali. Baada ya kujiridhisha, aliingia uvunguni mwa kitanda chake kilichokuwa kimechoka na kuchakaa, uvunguni alikutana na shimo likiwa linamwangalia, alitumbukia kwa kutumia kamba aliyoukuwa imefungwa kwenye chuma cha mviringo kilichofanya ukingo wa lile shimo.
Wakati Maganga anachukuliwa na Askofu Alphonso, kamba ilimpeleka Mzee Paul hadi tumboni mwa lile shimo, sakafu ikampokea huku mlio wa nyayo ukionyesha kuwa kulikuwa na uwazi wa kutosha. Alitembea taratiibu hadi sehemu ambayo alijikwaa kwenye kengele, mlio wa kengele hiyo ulifanya taa kuwaka. Mwanga wa taa ukafanya macho yake yaweze kuona kila kitu kilichokuwa ndani ya kile chumba.
Kilikuwa chumba kizuri cha wastani. Kulikuwa na viti viwili na meza moja ambayo juu yake kulikuwa na computer laptop. Kwenye kona moja ya chumba hicho ambacho kuta zake zilioneka kuwa zimejengwa kwa matofali mazito kulikuwa na kabati moja ndogo ya chuma, ambayo ilionekana kuwa ya miaka mingi. Mzee Paul alielekea ilipokuwa ile kabati, katika rundo la funguo alizokuwa nazo ambazo katika hizo moja aliitumia kufungua kufuli lililokuwa kwenye mlango wa kwenda kwenye chumba hicho.
Kwa muda wa saa moja na kama dakika arobaini, Mzee Paul alifungua na kusoma mafaili mbali mbali yaliyokuwa kwenye compyuta iliyokuwa kwenye hicho chumba. Betri moja kubwa ya kisasa iliyokuwa chumbani humo ambayo ilikuwa imeunganishwa kwenye mlango wa mabati wa kuingilia nyumbani kwa Mzee Paul, iliwezesha utoaji wa umeme kwa vifaa vichache vilivyokuwa chumbani humo. Mlango wa kuingilia nyumbani kwa Mzee Paul, ambao ni wa bati ulikuwa ni mashine maalum ya kukusanya nguvu za jua na kuzifanya kuwa umeme. Mtu yeyote angeiona nyumba ya Mzee Paul, ambayo ilikuwa imeezekwa kwa nyasi asingeweza kudhani kuwa mlango ule mbovu ulikuwa na kazi maalum kama hiyo. Mzee Paul, mara kwa mara alikuwa akigombana na mkewe juu ya kuhakikisha anaezeka vizuri sehemu ya mlangoni maana ilikuwa wazi kiasi kuwa wakati wa mvua maji ya mvua yaliweza kupitia sehemu ile na wakati wa jua, basi mionzi ya jua iliweza kulifikia barabara eneo lile. Mzee Paul, alikuwa akitoa visingizio mbalimbali ili mradi asiezeke lile eneo, alifanya makusudi maana alihitaji mionzi ya jua iweze kuufikia mlango ambao ulikuwa na kazi maalum. Mlango huo wa bati kwa usiri sana ulikuwa umeunganishwa na waya mmoja ambao ulikwenda moja kwa moja kwenye betri iliyokuwa kule shimoni. Hivyo betri hiyo ilikuwa ikipata nguvu kila siku.
Wakati huu Paul alipokuwa kwenye shimo, hakuwa na wasi wasi juu ya umeme, ile betri ilifanya kazi. Kwa jinsi Mzee Paul alivyokuwa akifungua na kufunga mafaili mbalimbali ndani ya ile kompyuta na jinsi alivyokuwa akitumia keyboard kwa ustadi mkubwa usingeweza amini kuwa ndiye yule Mzee aliyeonekana wa kawaida tu pale kijijini. Sehemu nyingi alizotembelea ndani ya ile kompyuta, mafaili mengi aliyofungua yalihitaji neno la siri, lakini ilikuwa ajabu namna ambavyo aliweza kukumbuka maneno mengi ya siri, ya aina tofauti na mafaili kwa kasi na usahihi mkubwa.
Aliporidhika na alichokuwa amefanya na kuona kwenye ile compyuta, Paul aliizima kisha akabaki amekaa kimya kama mtu anayesubiri kuingia kwa Daktari.
Baadaye kama aliekurupushwa, alisimama na kuelekea upande mwingine wa shimo. Alifikia kwenye ukuta wa upande huu, hapo kulikuwa na kibuyu kilichokuwa kinaning’inia kwenye kamba moja iliyokuwa imefungwa toka darini mwa lile shimo. Alikichukua kile kibuyu, ndani yake alitoa kitu kama simu, simu ya upepo ambayo askari polisi hupenda kuzitumia wanapokuwa kwenye operesheni mbalimbali.
Aliifungua ile simu, akaiwekea kitu kama betri, baada ya kuifunga akaifutafuta kisha, akaminya kitufe cha kuiwasha. Baada ya sekunde kadhaa, simu iliwaka na makelele mengi kusikika. Alirudi kwenye kile kiti kilichokuwa pembeni ya meza yenye compyuta. Makelele yalipopungua sasa alisikia sauti kama ya radio ambayo kituo cha matangazo kimewekwa hewani.
“Hallo, Mr M hapa wa oparesheni TAFUTA, Over!” Mzee Paul alisema huku akiwa anasubiri majibu toka upande wa pili.
“Ooooh! Mr. M, long time men, Captain hapa naongea, over!” Ulijibu upande wa pili.
“Always on time Captain, najua leo jioni ndiyo siku ambayo mzigo unahitajika, Over!’ Mzee Paul alisema.
 
PATASHIKA: 11

“Ndiyo ndiyo, tumekusubiri sana kuanza kwa hii operesheni, hasahasa kuwasili kwa huo mzigo maana shughuli nzima inategemea uwepo wake.” Upande wa pili ulisema.
“Vipi umeshatuma wasafirishaji, over?” Mzee Paul alihoji.
“Wameingia tangu juzi, walipowasili walinitaarifu na nikawaambia wawe maeneo hayo kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa maana mara nyingi mambo huharibika dakika za mwishoni kama umakini usipokuwepo, wapo hapo kijijini, nitawasiliana nao muda mfupi ujao ili ifikapo saa kumi na nusu jioni hii wafike hapo nyumbani kwako kuchukua mzigo na kuondoka, over.” Upande wa pili ulijibu.
“Safi sana Captain, hata mimi nimechoka pia, nimekuwa hapa kwa miaka mingi sasa, nimekuwa kama mfungwa, ningejua hii kazi ingekuwa ndefu kiasi hiki wala nisingeichukua. Mzigo uko kwenye hali nzuri sana, utafurahi pindi utakapouona, haujaingiziwa uchafu wowote kichwani, bado uko safi. Over.” Mzee Paul alisema kwa sauti ya mtu aaliyetua mzigo mzito mabegani.
“Hamna shida Mr. M, baada ya leo utakuwa huru kwa muda wakati ukisubiri hatua ya mwisho ya oparesheni hii. Baada ya kazi hii, nchi itakuhitaji kwa ajili ya kuandaa vijana wetu ambao watachukua nafasi zenu. Ila hilo tutaliongea baadae. Over.” Ulisema upande wa pili kwa sauti iliyoonyesha furaha.
“Maagizo mengine Captain?” Mzee Paul aliuliza.
“Maagizo mengine na njia za mawasiliano utazikuta sehemu ya mapokezi ya Hoteli Tilapia Mwanza. Ukifika sema unatoka kwa Captain, utahudumiwa. Hela ya kutosha wewe kwenda nchi yoyote na pia, Diplomatic Passport ya kukupa uwezo wa kwenda nchi yoyote. Hapo vipi Mr M? Over.” Upande wa pili ulisema kwa sauti ya kujigamba kidogo.
“Imekaa vizuri sana Captain, hawakukosea waliokupa kuendesha hii oparesheni. Over!”
“Asante Mr M”
“Asante Captain.”
“Over.”
“Over.”
Dakika ishirini baadaye, Mzee Paul alitokea ndani ya nyumba yake huku akichechemea kama mtu aliyekuwa na maumivu makali sana. Watu waliokuwa wamekusanyika pale mbele ya nyumba yake walimwangalia. Wapo waliomuonea huruma na wapo waliomuona yeye kama mdogo wake shetani. Alipofika chini ya mti waliokuwa wamekaa wazee wenzie aliketi. Wazee wengine ambao walikuwa bado hawajaonana naye waliendelea kumpa pole kwa msiba. Baada ya dakika kadhaa viongozi wa kijiji walimwita kutaka kuwa na maongezi naye.
Walimweleza nia yao ya kutaka mazishi yafanyike siku hiyo, kwani isingekuwa busara kuendelea kuweka ndani ule mwili. Mzee Paul aliafikiana nao hasa ikizingatiwa kuwa alishaambiwa kuwa Maganga alikuwa ameshaonekana. Kusikia kuwa Maganga ameondoka na Askofu Alphonso kwa maongezi kulimfanya Mzee Paul afarijike. Alikubaliana na wazo la wazee wa kijiji. Mara moja vijana wakaelekezwa sehemu ya kuchimba kaburi.
Kaburi lilipokuwa tayari, mjira ya jioni, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tayari kwa mazishi. Watu wote walikuwa wameshakuwa eneo la tukio isipokuwa Maganga, Vivian, Hellen na Askofu Alfonso.
* * *
Vivian na Hellen walikuwa wanatoka nyumbani kwa Askofu Alphonso. Walimwona wakati Askofu Alphonso anamchukua Maganga. Kutokana na hali aliyotoka nayo Maganga pale nyumbani na muda aliokaa kwa Askofu Alphonso viliwapa wasiwasi hivyo kwa pamoja wakajikuta wanakubaliana kwenda kuangalia kulikoni.
Walipofika walipokelewa vizuri na Askofu Alphonso ambaye alianza nao maongezi. Walishangaa kutomkuta Maganga eneo lile.
“Kutokana na hali aliyokuwa nayo Maganga, nimemwambia afanye sala maalum. Ila itakwisha muda si mrefu kutoka sasa. Inaonekana ana hasira sana juu ya baba yake, hilo si jambo zuri, ni kweli Mzee Paul anaweza kuwa amekosea lakini yeye kama mwanaye na pia, mtumishi wa Bwana anatakiwa kuwa na moyo mstahimilivu na wa kusamehe.” Aliongea Askofu huku macho yake yakiwa mapajani kwa Vivian.
“Vivian ulifanyaje hapo?” Askofu Alphonso alihoji huku macho yake akiwa ameyaelekeza kwenye paja la mguu wa kushoto wa Vivian.
“Wapi?” Viviani alijibu kwa aibu kiasi huku akijaribu kuivuta khanga iliyokuwa imeacha wazi sehemu ya paja lake. Alikuwa amevaa sketi fupi sana lakini kwa sababu ya msiba alikuwa amevaa khanga kwa juu. Kwa Vivian kuvaa nguo fupi ilikuwa jambo la kawaida japo wazee kijijini pale walijaribu kupiga kelele dhidi ya tabia yake hiyo lakini, hawakufanikiwa kumbadilisha. Mazingira ya watu aliyokuwa akiishi wakati akiwa shuleni huko Ulaya yalikuwa yameshambadilisha kwa kiasi kikubwa.
“Unajua hiyo alama imenikumbusha kitu.” Alisema Askofu Alphonso huku akiwa anameza mate.
“Kitu gani?” Vivian aliuliza kwa mshangao. Hakutegemea Askofu angeendeleza mazungumzo yale. Vivian alimwangalia Hellen usoni na kukutana na mshangao usoni kwa binti huyo kadhalika.
“Ulizaliwa Hospitali gani?” Askofu alihoji huku akiwa anamwangalia Vivian usoni.
“Bugando Mwanza.” Vivian alijibu kwa sauti ya kukereka kidogo.
“Aiseee!, umewahi kumuuliza mama yako kama kuna kisa chochote cha kushangaza kiliwahi kutokea wakati wa kuzaliwa kwako?” Askofu Alphonso alizidi kuwashangaza wale mabinti kwa maswali yake.
“Mmmmmmh! hapana, ila siku moja niliwahi kutembelea hospital ya Bugando kutaka kujua sehemu niliyozaliwa. Nilipotaja tarehe niliyozaliwa, nilielekezwa kumuona Daktari mmoja mzee. Yule Daktari aliponiona na nilipomweleza shida yangu aliangalia paja langu la mguu wa kushoto. Alipoangalia akasema, sitoweza kuangalia wodi niliyozaliwa kwa vile, asubuhi iliyofuata baada ya kuzaliwa kwangu, kulitokea mlipuko kwenye ile wodi, na Daktari wa kiyahudi ambaye ndiye alikuwa daktari pekee aliyekuwa amebaki katika hospital ya Bugando inasemekana aliuawa katika mlipuko huo. Mwili wa Daktari huyo haukuwahi kuonekana hadi sasa, hivyo serikali ya Israel ikaiomba serikali ya Tanzania kuifunga ile wodi hadi watakapo kamilisha uchunguzi wao. Ni miaka mingi sasa, hicho chumba kimefungwa na hairuhusiwi mtu kuingia wala kutoka.” Vivian aliema huku sasa ile hali ya kukereka ikiwa imeondoka usoni na badala yake mshangao ulichukua nafasi.
“Sasa, na wewe nini kimekufanya uunganishe hii alama yangu na siku yangu ya kuzaliwa. Maana yule Daktari naye aliunganisha kuzaliwa kwangu na alama pajani.” Vivian alihoji.
“Ndiyo maana nimekwambia hiyo alama imenikumbusha kitu. Any way, tutaongea kwa mapana zaidi siku nyingine. Ila nadhani kwa sasa twende msibani. Tangulieni mimi nitakuja na Maganga.” Askofu Alphonso alisema huku akiwa anasimama. Vivian na Hellen nao walisimama. Macho ya askofu Alphonso yalikuwa mwilini mwa Vivian muda wote.
Walipofika nje ya mlango, Alphonso aliita.
“Vivian!”
“Bee!, Baba Askofu!
“Naomba nikuone kidogo.” Alphonso alisema huku akiminya jicho la kushoto.
“Makubwaaaa!” Hellen alinong’ona.
Vivian alirudi ndani.
“Vivian tutaongea zaidi msiba ukiisha, hakikisha unaniona ili nikupe habari vizuri. Ila ukifanikiwa kuingia ndani na kufunua ile maiti ya mama yake Maganga, na ukaona ana alama kama yako pajani, ujue ni mama yako pia. Baadae.” Askofu alisema kwa kunong’ona. Kauli hii ilimchanganya sana Vivian. Lakini alijua wazi hakuwa na muda wa kuuliza zaidi. Ila alidhamiria kufanya alichoambiwa na Askofu Alphonso.

Huyu Alponso ni nani?
Mzee Paul yuko kwenye misheni gani?
 
PATASHIKA: 12

Kukosekana kwa Hellen, Maganga, Vivian na Askofu Alphonso kulifanya minong’ono kuzagaa eneo hilo. Toafauti na kawaida yake, Mzee Paul alikuwa mpole huku akisikilizia kilichokuwa kinaendelea.
“Jamani, naomba tutulie. Nimepewa taarifa hapa kuwa Maganga alichukuliwa na Askofu Alphonso wakaelekea nyumbani kwa askofu. Baadaye Vivian na Binti mwingine wameenda kuwaita.” Alisema Mwenyekiti wa Kijiji katika hali ya kupooza minong’ono iliyokuwa ikiendelea.
Wakati watu bado wakiwa katika ile sintofahamu, mara ulisikika muungurumo wa gari. Haukuwa muungurumo mpya, wengi walishauzoea, ulikuwa wa gari la Askofu Alphonso. Na kweli, gari lilitokezea, lakini tofauti na matarajio ya wengi hailikuwa limetokea upande yaliko majengo ya kanisa na nyumba za watawa. Lilitokea upande mwingine iliko barabara ya kuelekea madukani. Watu wakashikwa na mshangao.
Si watu waliokuwa kwenye eneo la kaburi tu, hata Vivian na Hellen walishikwa na mshangao. Walikuwa wanatoka nyumbani kwa Askofu Alphonso, walikuwa wamemwacha kwa makubaliano kuwa angekuja muda mfupi ujao baada ya Maganga kumaliza sala maalum. Sasa iweje wanamwona Askofu Alphonso akiwa anatokea upande mwingine. Walichanganyikiwa.
Askofu Alphonso alishuka kwenye gari na kuanza kutembea taratibu pale walipokuwa wanakijiji. Watu walizidi kushangaa. Alipofika kwa wanakijiji, alienda alipokwa Mzee Paul, alimkumbatia kwa upendo.
“Pole sana baba Maganga, habari ya msiba huu imenisikitisha sana. Nilikuwa Mwanza mjini lakini imebidi nije haraka ili kuhakikisha nahudhuria huu msiba…”
“Hebu acha mzaha Askofu, unasema ulikuwa Dar es salaam wakati tulikuwa hapa wote muda wote huu!?’ Mzee Paul aliongea kwa jazba na hamaki kubwa.
“Baba Maganga najua inawezekana labda umechanganyikiwa kwa msiba wa ghafula wa mkeo mpenzi. Tuliza akili. Mungu atakusaidia…” Kabla hata Askofu hajamaliza, Mzee Paul alirusha ngumi kali iliyompata.
“Haya niambie haraka sana Maganga yuko wapi?” Alifoka Mzee Paul kwa jazba, huku watu wakishangaa jinsi mtu aliyekuwa mgonjwa wa mguu akiwa anatembea sawa sawa.
“We! Askofu, hivi unataka kusema kweli siye wewe tuliyekuwa tukiongea wote kule nyumbani kwako sasa hivi?” Vivian aling’aka kwa hasira.
Hapo ikatokea taharuki kubwa sana. Ikabidi watu waelekee nyumbani kwa Askofu Alphonso. Walipofika walikuta mlango uko wazi. Kundi la watu likavamia ile nyumba, wakaanza kukagua sehemu zote mule ndani lakini hawakuona mtu.
“Mamaaaaa!” Sauti ya kike ilitokea upande ambako kulikuwa na jiko na bafu. Watu wote wakaelekea huko. Yule mama alitoka anakimbia.
“Vipi mama?” Askofu aliuliza kwa fujo.
“Hebu pisha huko!” Yule mama hata kabla hajajibu, Mzee Paul alielekea bafuni kwa kasi na kumsukuma Askofu Alphonso apishe njiani.
Mzee Paul alipofika kwenye mlango wa choo, aligutuka kidogo.
“Shiiiiiit!” Ilimtoka. Lakini wakati watu wakija alifaulu kuinama na kuchukua karatasi iliyokuwa sakafuni pale. Aliiangalia kwa mshangao kidogo. Karatasi ilikuwa imeandikwa “Operesheni TAFUTA imeanza, muulizeni Mzee Paul!” Mara moja Paul alielewa nini kilikuwa kikiendelea. Hakutaka kupoteza muda wake na wale watu wala Askofu. Alishaelewa kuwa amezidiwa hesabu na watu asiowajua. Hivyo wakati umati wa wanakijiji ukisukumana kuja pale ulipo mlango wa choo, Mzee Paul yeye alikuwa akisukuma watu wampishe ili atoke eneo lile. Hakuwa na makelele tena. Yule mama aliyekuwa ameona kitu kilichokuwa bafuni alizidi kupiga kelele kwa nguvu.
“Maiti za watu jamani, zimevimba, uuuuuuwi watu wana dhambi!”
“Wewe kweli…Askofu ndiyo kafanya hivyo au?” Walizidi kuropoka hili na lile. Askofu akajikuta kwenye wakati mgumu sana. Hakuwa anajua nini kilikuwa kikiendelea.
Hebu Vivian na yule msichana ninyi ndiyo mlikuwa wa mwisho kuonana na Askofu, tuelezeni kilichotokea.” Hatimaye Mwenyekiti wa Kijiji aliongea kwa hamaki.
“Yule msichana na Vivian mko wapi?” Mwenyekiti aliuliza kwa sauti ya kupaa.
“Niko hapa!” Hellen alijibu kwa hofu kubwa.
“Njoo hapa!” Mwenyekiti aliamuru. Umati wa watu ukatulia tuli. Hellen akajongea alipokuwa amesimama mwenyekiti.
“Vivian yuko wapi?” Mwenyekiti aliunguruma huku watu wakiwa wanageuza macho huku na kule katika kumtafuta Vivian.
Vivian hakuwepo eneo lile. Alijionea mambo yalivyokuwa yakienda kwa kasi, alishaona maji ya mto yalikuwa yakielekea wapi, hivyo hakutaka kuoegelea yalipokuwa yakitokea, akaona ni busara kuogelea yalipokuwa yakielekea huenda angeweza kuona mti wa kushika na kujiokoa. Alipoona watu wote wamekimbilia nyumbani kwa Askofu Alphonso, yeye aliona ndiyo mwanya wa kuangalia kile alichoambiwa na yule Askofu Alphonso mwingine. Maana hadi sasa ilikuwa dhahiri kichwani mwake kuwa kulikuwa na Askofu Alphonso wawili.
Haraka sana alielekea walipokuwa wameweka jeneza lililokuwa na mwili wa mke wa Mzee Paul, kiu ya kutaka kujua ilikuwa imemjaa kifua na kichwa chake kiasi kuwa hofu na kinyaa vikawa mbali sana na hisia zake. Alipekuwa, japo mwili ulikuwa umeshavimba. Alipofika kwenye sehemu ya paja la kushoto la ile maiti, macho yalimtoka. Aliona alama kama ile aliyokuwa nayo kwenye paja lake la mguu wa kushoto.
“Ina maana mama yake Maganga ni mama yangu? Ina maana Mzee Paul ni baba yangu? Na wazazi nilionao sasa, je?”
Maswali mengi yalifumuka kichwani mwa Vivian, akajikuta kichwa kinakuwa kizito. Mara akaona kama anga linazunguka kwa kasi. Akaona kiza usoni. Fahamu zikamtoka.
Paul alimwona Vivian akiwa anaanguka lakini hakuwa na muda wa kushughulika naye kwani aliweza kuliona gari moja la kifahari jeusi liliokuwa imeegeshwa mbele ya nyumba yake. Alielewa kuwa wale ndiyo wasafirishaji waliokuwa wametoka kwa CAPTAIN, mtu aliyekuwa ameongea naye shimoni chini ya nyumba yake.
“TAFUTA?” Mzee Paul alisema alipowafikia watu waliokuwa kwenye gari.
“TAFUTA.” Walisema huku wakimwangalia Mzee Paul kwa macho yao yaliyokuwa kama ya paka.
“Mzigo umetoweka, inabidi tufukue kila sehemu mradi upatikane. Mimi nitaenda kushugulika kule upande wa kanisa. Wewe utahakikisha kila nyumba inafukuliwa hapa kijijini. Wewe utahakikikisha hakuna mtu anatoka hapa kijijini. Sitaki makosa, tutapekua kila mahali ili mradi Maganga apatikane.” Alisema Mzee Paul kwa amri. Ile mipande ya watu ilitii amri na kuanza kushughulika.
 
PATASHIKA - 13


Paul alimwona Vivian akiwa anaanguka lakini hakuwa na muda wa kushughulika naye kwani aliweza kuliona gari moja la kifahari jeusi liliokuwa imeegeshwa mbele ya nyumba yake. Alielewa kuwa wale ndiyo wasafirishaji waliokuwa wametoka kwa CAPTAIN, mtu aliyekuwa ameongea naye shimoni chini ya nyumba yake.
“TAFUTA?” Mzee Paul alisema alipowafikia watu waliokuwa kwenye gari.
“TAFUTA.” Walisema huku wakimwangalia Mzee Paul kwa macho yao yaliyokuwa kama ya paka.
“Mzigo umetoweka, inabidi tufukue kila sehemu mradi upatikane. Mimi nitaenda kushugulika kule upande wa kanisa. Wewe utahakikisha kila nyumba inafukuliwa hapa kijijini. Wewe utahakikikisha hakuna mtu anatoka hapa kijijini. Sitaki makosa, tutapekua kila mahali ili mradi Maganga apatikane.” Alisema Mzee Paul kwa amri. Ile mipande ya watu ilitii amri na kuanza kushughulika.

***********
TILAPIA HOTEL, chumba namba nane kilikuwa kimewekwa picha ya samaki mlangoni. Juu ya kitanda kwenye chumba hicho Mzee Paul ndiyo kwanza alikuwa ameshtuka toka usingizini. Hakuamka, aliendelea kujigaragaza kwa muda juu ya kitanda hicho pasi kufungua macho. Mlio wa saa kuashiria ukamilifu wa wakati ulilia, Mzee Paul aliusikia lakini aliendelea kujigaragaza kwenye hicho kitanda kikubwa na kizuri. Baadaye huku akiwa amefumba macho alijivuta hadi kwenye ukingo wa kitanda hicho kwa juu upande wa kulia. Hapo kulikuwa na kimeza kidogo ambacho kilifanya sehemu ya kitanda hicho. Akiwa bado umefumba macho alinyanyua mkono wake kivivuvivu akauelekeza juu ya kile kimeza. Kiganja na vidole vikawa vinacheza kama vile ambavyo mtu aliye katika hatua za kukata roho ambaye yuko katika kuachia pumzi ya mwisho ya uhai wake hufanya. Akiwa amelala kifudifudi huku kichwa akiwa amekifukia kwenye mito miwili alipapasa hivyo kichovu hadi pale mlio wa saa iliyodondoka chini uliposikika. Alikuwa akitaka kuchukua saa, kivivu kivivu.
“Shiiit!” Ilimtoka aliposikia mlio wa saa kudondoka chini. Bila kufungua macho alijivuta zaidi hadi pale kichwa ckake sasa kikawa kinaning’inia kwenye ukingo wa kitanda. Akafungua jicho moja, alilifumbua kidogo sana, aliiangalia ile saa. Aliona uvivu kuiokota.
“Mmmmmh!, saa mbili tayari. Daaaah!” Alinong’ona kwa sauti ya kichovu. Akafumba jicho lake, akajisogeza katikati ya kitanda huku akiwa ameiacha ile saa pale chini. Akaendelea kujigaragaza kama chatu aliyemeza ndama. Safari hii alikuwa chali lakini akiwa bado amefumba macho yake. Alifanya hivyo kwa dakika kadhaa. Halafu taratibu akaanza kutulia. Mwishowe alitulia na kuyafungua macho yake taratibu. Aliliangalia dari, fikira zake zikiwa mbali toka chumbani humo. Aliyaruhusu macho yake kusafiri toka upande mmoja wa dari hadi upande mwingine kama ambaye alikuwa akisanifu namna fundi aliyetengeneza lile dari alikuwa amefanya kwa ubora kiasi gani. Macho yake yalipofika upande wa kushoto wa chumba kile ambamo pia, kulikuwa na dirisha kubwa, yalidakwa na mionzi michanga ya jua la mashariki ambalo lilikuwa likitoa uhai wake na kuvigawia viumbe mbalimbali vilivyohitaji mionzi hiyo. Mionzi hiyo ilimfanya afumbe tena macho yake kana kwamba yalikuwa yameshindwa vita na mionzi ya mwanga wa jua tamu la asubuhi. Dirisha lilikuwa limefunikwa na pazia zuri jeupe, lakini mionzi ya jua iliweza kupenya katikati ya muunganiko wa vipande viwili vya pazia hilo. Alifikicha macho yake huku akiwa anaupitisha ulimi wake juu ya meno ya juu na chini kinywani mwake kwa namna ya kuuzungusha ulimi huo. Ladha aliyoipata ilimfanya aone kuna umuhimu wa kuamka na kuianza siku yake alihitaji kuswaki. Kama aliyekurupushwa, alijibiringisha hadi upande wa chini wa kitanda sehemu ambayo alikuwa ameelekezea miguu yake wakati amelala. Huko alikisogeza kifua chake ukingoni mwa kitanda. Upande huo kulikuwa na meza ndogo ya mviringo.
Huku akiwa bado amefumbua macho safari hii aliunyoosha mkono wake hadi ilipokuwa meza ndogo ya mviringo. Meza hiyo pamoja na mambo mengine ilikuwa na simu ya mezani. Mzee Paul aliichukua ile simu kizembezembe tena. Aliitua kitandani, akanyanyua mkonga wa simu, akaminya namba kadhaa huku akiwa amefumba macho. Lakini ni ajabu ambavyo aliweza kuminya namba alizozitaka. Kwanza aliminya namba sifuri na kuongea na mapokezi.
“Nataka kupiga simu nje ya hoteli tafadhali.” Paul aliongea na mtu wa mapokezi.
“Hamna shida Mzee, bonyeza 472 ikifuatiwa na namba unayotaka kupiga. Kama ni nje ya nchi anza na 972 kisha endelea kama kawaida. Gharama utazikuta kwenye bili yako.” Alisema mtu wa mapokezi. Mzee Paul hakuwa na muda wa kujibu, aliuweka chini mkonga na kuminya namba nyingine huku akiwa bado amefumba macho.
“Hallo, je, hapo ni Katunguru hospitali ya misheni?” Mzee Paul alisema.
"Ndiyo penyewe, naongea na nani na nikusaidie nini?”Upande wa pili ulijibu.
“TAFUTA, naitwa TAFUTA. Nahitaji kuongea na Daktari Masaga tafadhali". Mzee Paul alisema.
“Subiri kidogo tafadhali nikuunganishe ofisini kwake kama atakuwepo.” Ulijibu upande wa pili. Mzee Paul alisubiri hivyo kwa sekunde kadhaa.
“ Hallo, naitwa Daktari Masaga, sijui mwenzangu?”
“TAFUTA.” Mzee Paul alisema.
“TAFUTA.” Upande wa pili ulisema.
“Sikiliza, mambo yameharibika kiasi. Maganga ametoweka, jana ilikuwa patashika pale kijijini. Tumeteketeza karibuni Kijiji chote katika jitihada za kumtafuta. Nadhani utakuwa umepata taarifa. Hadi dakika hii naongea na wewe bado hatujafanikiwa kumpata…” Mzee Paul alisema kabla kauli yake haijakatishwa
“Nimezipata, hivi hapa kuna askari kila kona ya Kijiji, unasakwa ile mbaya. Ila na nyie ni balaa watu watatu tu mmeweza kuteketeza kile Kijiji na raia bila kujali! Ama kweli!, hii ni Operesheni TAFUTA. Sasa nani atakuwa ameuchukua mzigo wetu, maana inauma sana baada ya kusubiri kwa miaka yote hiyo na mipango ya muda mrefu mambo yanataka kuharibika mwishoni jamani?” Ulisema upande wa pili.
“Hilo ndilo linatuumiza vichwa, wakuu bado wanasubiri tuupeleke mzigo ili awamu ya pili ya mpango ianze. Nina wasiwasi wakisikia hili limetokea wanaweza chukua kichwa changu. Unajua nimekuja kugundua kuwa inawezekana Mwasumbi bado yuko hai. Hii nimeipata jana, inasemekana Maganga na msichana mwingine ambaye ni damu yangu walishinda kwake kwa siku zaidi ya nne. Sasa wasiwasi wangu inawezekana Mwasumbi anahusika au kuna upande ambao hatuujui nao uko kwenye huu mpango…hapo ndiyo sijui na natakiwa nijue ndani ya saa chache zijazo kama kweli nayapenda maisha yangu...”
“Khaaaa! unamaanisha Mwasumbi yule Kipusa hatari…basi kazi ipo! Vipi Askofu huyu anajua lolote? Maana inasemekana anahojiwa hapa na Polisi lakini inasemekana hataki kusema chochote.” Ulisema upande wa pili wa simu.
“Hapana, inavyoonekana kuna mtu alikuja akajibadilisha na kujifanya Askofu Alphonso, cha kusikitisha alifanikiwa kunihadaa hata miye. Unajua kwa jinsi nilivyokuwa nimetengeneza mazingira sikutegemea ingekuja julikana na yeyote kuwa tuko kwenye operesheni. Na ndiyo maana nikachagua sehemu ya mbali na ya kijijini ili kuweka haya mambo. Hivyo huyo mtu alivyoingia na kuondoka na Maganga ni kama mzimu tu. Ila kwa gharama yeyote, ili mpango huu ufanikiwe lazima nimpate Maganga.” Alisema Mzee Paul huku akiwa bado amefumba macho pale kitandani.
“Nakuaminia Mr M. Wewe tena ukiamua hakuna la kushindikana. Nakumbuka siku ile umekuja hapa hospitali unajiliza mguu, tofauti na miye, hakuna mwingine aliyehisi kuwa ule ulikuwa mchezo kama michezo yetu mingi ambayo tuliwahi kuifanya pamoja…” Ulisema upande wa pili kabla kauli yake haijakatishwa.
“Hilo ndiyo limefanya nikupigie. Najua uchunguzi unaweza kufika mbali, hivyo si ajabu watu wakajiuliza nilipona muda gani na kuweza kufanya yale mambo. Kwa kifupi lazima watajua kuwa kuna namna nilidanganya kuwa nimevunjika mguu, na kwa jinsi ule uongo ulivyokuwa lazima watashawishika kuja kuulizia hospitali zote nilizopita…nadhani unajua. Itajulikana ulishiriki uongo. Hivyo nashauri utoweke hapo Kijijini. Unaweza kwenda popote kati ya vituo vyetu…” Alisema Mzee Paul kwa sauti yenye mkazo.
“Hilo ni kweli aisee, nitaondoka leo leo, sina haja ya kuchukua chochote. Nitaenda kujizika kokote kule, bila shaka akaunti yangu iko njema?”Ulihoji upande wa pili wa simu.
“Hilo usitie shaka. Wewe tu!” Paul alisema.
“Sawa, Mr M, nimefurahi kufanya kazi na wewe. Imekuwa kazi nzuri hadi hiyo jana na naamini ipo siku tutafanya kazi pamoja. Miye ninatoweka muda mfupi kuanzia sasa” Ulisema upande wa pili.
“TAFUTA.” Paul alisema.
“TAFUTA.” Upande wa pili ulijibu. Kisha, Paul akaweka simu chini kabla ya kuinyanyua tena. Safari hii akiwa amefumbua macho.
“Hallo, je, hapo ni Hospitali ya Wilaya Sengerema?”
“Ndiyo Mzee wangu, je, naongea na nani na nikusaidie nini?” Ulijibu upande wa pili.
“Sihitaji msaada, nahitaji kuongea na Daktari Hassan wa kitengo cha mifupa tafadhali. Mwambie Mr TAFUTA, ninashida naye ya muhimu sana.” Mzee Paul alisema.
“Sawa, subiri, usikate simu tafadhali nikuunganishe naye kama yuko ofisini.” Ulisema upande wa pili. Kisha ukafuata ule mlio wa simu inayounganishwa.
“Hallo! Asante kwa kusubiri. Tafadhali ongea na daktari yuko hewani.”
Ulisema upande wa pili.
“Naitwa Hassan, nani mwenzangu na nikusaidie nini?” Ulisema upande wa pili.
“Mr M hapa, TAFUTA!”
“TAFUTA!” Upande wa pili ulijibu mara baada ya utambulisho wa Mzee Paul.
“Sikiliza, mambo yameharibika, mzigo wetu ambao tumeuandaa kwa muda mrefu umetoweka. Sasa kazi ndiyo imeanza, badala ya kusonga mbele na hatua ya pili inabidi tuanze kuushughulikia mzigo ulipo. Maana kama ujuavyo bila Maganga mpango wetu kamwe hauwezi kutimia. Sasa kilichofanya nikupigie simu ni juu ya usalama wako. Unajua juzi nilikuja hapo, kwa hila na ukaniwekea ule mhogo. Sasa kwa hali ilivyo najua Polisi na watu wowote wa usalama watakufikia kuulizia kulikoni mgonjwa wako aonekane akifanya vitu kama vile nilivyofanya pale Kijijini. Hivyo unatakiwa utoweke muda wowote kuanzia sasa.” Mzee Paul alieleza huku akipiga mwayo.
“Nimekuelewa Mr M. Ila nadhani ushauri huu umpe na Masaga maana ulipitia pale kwake kabla huajaja huku.” Upande wa pili ulishauri.
“Unatilia mashaka utendaji wangu nini?” Mzee Paul alifoka. Alichukia pale alipogundua kuwa mtu wa upande wa pili alionyesha kuwa yeye hawezi kufikiria jambo dogo kama lile.
“Hapana Mzee!” Ulijibu upande wa pili kwa sauti iliyojaa hofu mara hii.
“Fanya kama nilivyokwambia, mengine niachie mimi.” Mzee Paul alisema kisha akaibamiza chini simu. Alipoweka simu chini alisikia mlango wa chumba alichokuwemo ukigongwa.
“Nani?” Aliuliza kwa sauti ya juu kiasi. Lakini hakupata jibu. Kwa vile alikuwa bado hajaamka, alisimama huku akiwa uchi wa mnyama. Alitembea hadi upande kulikokuwa na bafu, alivuta taulo moja jeupe. Akajizungusha kiunoni, kisha akatembea kuelekea mlango wa chumba.
“Nani wewe unayenikatisha usingizi wangu?” Aliuliza tena huku akiwa amekaribia mlango. Lakini mara akasita akaelekea kwenye kitanda alichokuwa akijigaragaza hapo awali. Alinyanyua mto mmoja na kuchomoa Bastola yake ya automatic.
“Room service!” Sauti ya kike ilisikika mlangoni. Mzee Paul alivyosikia hivyo. Aliirudisha ile Bastola alipokuwa ameitoa. Kisha akauendea mlango. Alizungusha ufunguo, akaufungua malango. Akatoa kichwa nje ili amwangalie mhudumu aliyekuwa akibisha mlango. Hapo ndipo mara akajikuta amerushwa ndani chumbani kwa teke kali lililokuwa limetolewa na mtu tokea mlangoni. Kabla hata hajainuka, mara akaingia Kijana mmoja mwembamba akiwa amevalia sare za jeshi.
 
PATASHIKA: 14

“Room service!” Sauti ya kike ilisikika mlangoni. Mzee Paul alivyosikia hivyo. Aliirudisha ile Bastola alipokuwa ameitoa. Kisha akauendea mlango. Alizungusha ufunguo, akaufungua malango. Akatoa kichwa nje ili amwangalie mhudumu aliyekuwa akibisha mlango. Hapo ndipo mara akajikuta amerushwa ndani chumbani kwa teke kali lililokuwa limetolewa na mtu tokea mlangoni. Kabla hata hajainuka, mara akaingia Kijana mmoja mwembamba akiwa amevalia sare za jeshi.

Huyo ndiye aliyekuwa amepiga lile teke. Mzee Paul hakutaka kuamini kuwa uzito wa lile teke ulitoka kwa yule Kijana. Hivyo akasimama ili akabiliane naye, akashangaa kuona yule Kijana akiwa anamngoja tu. Mzee Paul kwa kasi sana alilivuta taulo na kulirusha kwa yule Kijana halafu akalifuata lile taulo. Wakati yule Kijana anatafuta namna ya kulikwepa lile taulo, alipokea teke zito la shingo akapepesuka. Baadaye alisikia kitu kama nyundo kinatua kichwani mara baada ya kichwa cha karibu kilichopigwa na Mzee Paul kutua upande wa sikioni. Kijana akajaribu kujiweka sawa, lakini Mzee Paul hakumpa hiyo nafasi. Alimwandama kwa vipigo vikali, halafu teke la paji la uso likawa limechukua uhai wa yule kijana. Wakati Mzee Paul hajakaa sawa aliingia binti mmoja mdogo tu na yeye alikuwa na sare za jeshi. Alikuwa akitabasamu huku akimwangalia Mzee Paul. Mzee Paul alimwangalia akamfananisha lakini hakuwa na muda wa kukumbuka alimwona wapi. Yule binti alikuwa ameshika ua jekundu mkononi. Alimrushia Mzee Paul.
“Binti Ua Jekundu, kuna nini mbona mnanifanyia hivi?” Mzee Paul alisema baada ya kumbu kumbu kumjia
“Unahitajika!” Yule binti alijibu huku tabasamu bado likiwa usoni.
“Sasa kwa nini mnanijia namna hii?” Mzee Paul alihoji.
“Shiiii!, sina muda wa kujibu maswali yako. Ama unakwenda na mimi kwa hiari au nakupeleka kwa nguvu.” Alisema yule binti huku akiangalia maiti ya yule mwenzie. Mzee Paul kuona, yule binti ameelekeza macho pembeni akataka ajaribu bahati yake. Akarusha mateke mawili makali, lakini akaambulia patupu, kisha akapokea vipigo vitatu tatanishi sana.
“Naona umenisahau baada ya kuwa likizo ya muda mrefu siyo Mr M?” Yule binti alisema.
“Unajua kawaida yangu, huwa naweka ua la heshima kwa mtu kabla hajafa ili aone kile nilichoweka kwenye maiti yake akiwa bado hai…” Kabla yule binti hajamalizia, Mzee Paul alirusha taulo lake tena kama alivyomfanyia yule Kijana mwingine ambaye sasa alikuwa marehemu.
Yule binti kwa kasi ya ajabu sana alitoa kitu kama cheni akalipiga lile taulo na kulizungusha kisha akalirudisha usoni kwa Mzee Paul. Mzee Paul ambaye mara baada ya kurusha lile taulo akawa anamfuata yule binti huku akiwa ameshajiandaa kutoa kipigo alishangaa lile taulo linatua usoni kwake kisha mvua ya vipigo ikafuata.
“Haya Ua Jekundu, nimekubali twende!” Mzee Paul alisema kwa sauti ya kusalimu amri. Lakini hilo halikumfanya yule binti aache kushusha kipigo. Yule binti alikuwa fundi wa kupiga. Baada ya muda, Mzee Paul alikuwa chini hoi hajitambui.
“Nasikitika sana kuwa sitokuua, si kawaida yangu na unajua hilo, nikishamrushia mtu ua jekundu hakuna namna anaweza pona. Wewe unanijua vizuri.” Yule binti alisema. Lakini Mzee Paul hakuweza kujibu maana hakuweza hata kusikia sauti, alikuwa ameshazimia. Kuona vile yule binti alitoa simu yake ya upepo. Akaiwasha na kuminya kitufe.
“Kapteni, Ua Jekundu hapa, Over!”
“TAFUTA.” Upande wa pili ulisema.
“TAFUTA.” Yule binti alisema.
“Mr M tumempata ila wakati tunaingia kumuona kamuua Mika. Mr M, bado yuko vizuri sana huwezi amini. Vipi bado unamhitaji au nimalize? Over!” Yule binti alisema.
“Mwache hapo nitatuma watu wamhifadhi, nahitaji ufanye kila namna uwatafute Vivian na Hellen. Maana kwa taarifa nilizo nazo hao wana habari ambazo zinaweza kuvuruga mambo yetu. Mwasumbi niachie mimi mwenyewe maana huyo hahitajiki haraka kiasi hicho. Ukiweza kuwapata hao watu wawili utakuwa umetuliza hali ya mambo wakati tukiendelea kujua mzigo uko wapi na kutafuta harufu ya Mwasumbi. Over!” Ulisema upande wa pili.
“Nimekuelewa Kapten, Over!
“TAFUTA, Over!” Ulisema upande wa pili.
“TAFUTA, Over!” Alisema yule binti. Kisha akazima ile simu. Akatengeneza vizuri mavazi yake. Kisha akatoka mle chumbani tayari kwa kuanza msako wa Hellen na Vivian.
********
VIVIAN ALIPOZINDUKA alijikuta amekaa ndani ya gari ambalo lilikuwa kwenye mwendo wa kasi sana. Alikuwa amekalishwa kwenye kiti cha abiria pembeni ya dereva. Aligeuza shingo na kumuangalia dereva ambaye alikuwa akiendesha gari kwa kasi sana.
“Askofu unanipeleka wapi? Tunaenda wapi? Mazishi yameshaisha? Tuko wapi? Ile alama uliyosema niingalie kwenye maiti ya mama Maganga niliiona je, inamaanisha nini? Mbona hunijibu, na kwa nini unaendesha gari langu kwa fujo kiasi hiki?” Maswali mengi mfululizo yalimtoka Vivian pasi kumpa nafasi muulizwa kujibu.
Dereva aliendelea kuendesha huku akiwa kama mtu ambaye hajamsikia Vivian. Vivian akaanza kushikwa na mshangao juu ya hali hiyo ya Askofu Alphonso.
“Sikiliza Vivian, unatakiwa utulie kwa usalama wako na wengine ambao maisha yao yanakutegemea wewe.” Alisema yule dereva huku akiendelea kukanyaga moto ili gari iongeze mwendo zaidi.
“Mazishi yaliisha jana jioni na nitakueleze vizuri tukifika mahali pazuri na salama. Ila kwa sasa nakuomba tulia, hapo kwenye kiti cha nyuma kuna mfuko, ndani yake kuna boksi mbili za juice, chukua unywe maana hujala tangu jana ulivyoanguka na kuzimia.”
“Ennnhe! ilikuwaje maana ninachokumbuka mara ya mwisho nilikuwa kwenye jeneza nikikagua mwili wa mama Maganga?” Vivian alihoji kwa shauku.
“Nitakueleza yote, nitakueleza wewe ni nani, hiyo alama inamaanisha nini. Pia, nitakueleza kwa nini niliihusisha na yule daktari wa Kiyahudi kule kwenye Hospitali ya Bugando. Ila kwa sasa tuko hatarini, lazima tufanye namna ya kujiokoa kama kweli tunapenda maisha yetu na ya wale tuwapendao. Najua unampenda Maganga, lazima tumsaidie katika mazingira magumu aliyonayo.” Alisema Askofu Alphonso huku akijaribu kukwepa korongo moja lililokuwa mbele yao.
Vivian aliangalia vijiji vilivyokuwa pembeni ya barabara na kugundua kuwa walikuwa kwenye barabara itokayo Kijiji cha Katunguru kwenda kilipo kivuko cha Kamanga. Aligundua kuwa walikuwa kwenye Kijiji cha Nyamatongo. Dereva alishindwa kukwepa korongo na wakawa wameliingia, gari ikayumba lakini kwa namna ya ajabu sana dereva alifanikiwa kulitoa gari na kuendelea na safari.
Walipofika kijiji fulani, dereva alikatisha gari na kuingia nyumba za ndani Kijijini hapo. Kijiji hicho kilikuwa upande wa kushoto mwa barabara. Aliendesha gari hadi jirani na shamba moja lililokuwa na miwa.
“Haya shuka!” Dereva aliamuru.
“Ndiyo tumefika? Hapa ni wapi? Kwani hapa ndiyo kuna usalama sasa? Miye nilidhani tunaenda Kituo cha Polisi Kamanga?” Maswali yalimtoka Vivian. Alipomwangalia dereva usoni na kukutana na lile jicho akashituka.
“Wewe ni Askofu Alphonso kweli, mbona macho yako yako tofauti.” Vivian aling’aka kwa sauti iliyojaa wasiwasi, mshituko na hofu.
“Macho yangu yakoje?” Dereva aliuliza.
“Yako kama ya ndama wa mwezi mmoja.” Vivian alisema huku safari hii akiwa hana hamu ya kumwangalia tena yule dereva.
“Shuka!” Sauti ilisema tena, ila safari hii ikiwa na chembechembe za amri.
“Mmmhhh!” Alipumua huku akiwa ameshafungua mlango wa gari na kushuka. Alikuwa ameshikilia boksi la juisi mkononi.
“Simama pale!” Aliamuru tena.
“Wewe ni mwanajeshi?” Vivian alihoji huku akichukua ujasiri wa kumwangalia usoni.
“Simama pale binti, hatuna muda wa kupeana majibu hapa!” Aliamuru yule dereva kwa sauti ya hadhari.
Vivian alipoenda sehemu aliyoambiwa asimame, yule dereva alikanyanga mafuta na kuiingiza ile gari kwenye shamba la miwa. Aliendesha hivyo hadi alipopotelea kwenye msitu wa miwa. Baada ya dakika kadhaa akaja akiwa anatembea.
“Gari lako utapewa nyingine, ila kwa sasa sahau.” Alisema yule dereva huku akiwa anatembea kurudi upande wa barabarani. Wakati huu na yeye alikuwa na boksi la juisi mkononi.
“Nifuate!” Alisema mara baada ya kugeuka na kukuta Vivian bado akiwa amesimama pale mahala pa kwanza kwa bumbuwazi. Alivyosema hivyo hakugeuka aliendelea kutembea, kuona hivyo, Vivian alianza kumfuata. Hakuwa na hiari maana hakuwa na mbadala wa yale maamuzi.
 
Kuna namba hapo juu ya Muandishi mcheki whatsapp akuunge group mimi nilijitoa so kuna jamaa ndo huwa ananitumia
 
Back
Top Bottom