Vp shehe mtashiriki sensa?Kumbe bado WaTanzania walio wengi wanaipenda CUF , wananchi wanaimani ya kweli na CUF na wanaelewa majungu na njama za kukidhoofisha chama chao ambazo zimefanywa kwa awamu mbalimbali na wapinzani wao na hata wale wasio kitakia mema Chama hiki cha CUF.
CUf tofauti na vyama vingine kimekubalika kila pembe ya Tanzania kutokana na itikadi zake na sera ambazo zinatoa mwanga kwa kila anaezifahamu na hata kwa yule anaehadithiwa ,ni chama ambacho kama kisingehujumiwa basi leo hii waTanzania wangelikuwa mbali sana kimaendeleo.
Nguvu za CUF zimedumaa kutokana na dhoruba ilizopita na sasa imeanza kupata ahueni na kuanza kujipapatua ili kirudie katika hali yake ya zamani ili kufanikisha malengo yake ya kuliongoza Taifa hili la Tanzania.CUf inaamini kabisa nguvu za wanachama wake bado zipo kwani aliewahi kukipenda chama hiki basi hawezi kukiacha na ikionekana amekiacha basi bado ndani ya moyo wake ipo nafasi ya CUF ni kama wale askari wa akiba ,ambao wakati wowote vita ikitokea huwa wapo tayari kupambana.
Akiba hii ya wanachama ambao ndani yamioyo yao bado CUF imo na wapo tayari kwa lolote lile ,hawa ndio wale walio ngangari kinoma na ndio hazina ya CUF iliyo nyamaza na ipo kimya na ni hazina kubwa sana ,isiyomilikiwa na chama kingine.Karibu mbiu ya mgambo itaitishwa ili kuanza mapambano mepya ya kumrudisha na kuwarudisha maadui nyuma.