CUF na CHADEMA waungane kuiondoa CCM madarakani - Mtatiro

Ahaaa!siwezi kutoa hukumu kwa matokeo haya......chadema kipambane mpaka tone la mwisho la damu mtatiro kawaeka mfano wa kata za lindi na mtwara ambako cuf na ccm waliweka mizizi kitambo chadema kimeweza kufinya kura kura nyingi tu...........mtatiro alipaswa kuongea hayo kabla ya uchaguzi na isitoshe wenyewe tayari ni washirika wa ccm yaani kimada
 
Mtatiro alivyo mnafiki amechukua zile kata ambazo CUF imepata kura nyingi ili ahalalishe hoja yake.Kwanini asiweke matokeo ya kata zote 29?

Kwa historia ya CUF na hoja hii ya Mtatiro ninawafananisha na chama cha UPND cha Zambia chini ya kiongozi wake Hakainde Hichilema

-Chadema tuna historia nzuri ya kufanya alliance mapema kabisa tulipoingia kwenye uchaguzi wa kwanza mwaka 1995 na hatukumsimamisha mgombea Urais na kumuachia Agustine Mrema wa NCCR-Mageuzi
Pia Mtatiro kama anaijua historia ya chama chake atakumbuka mwaka 2000 tulimuunga mkono Prof.Lipumba kwenye nafasi ya Urais
Pia yeye anajua alikataa kumuachia John Mnyika kugombea ubunge jimbo la Ubungo mwaka Juzi hata baada ya kuona kuna hatari ya kura kugawanyika kwa upande wa upinzani huku akijua tayari Mnyika alishajenga political base Ubungo.Anyways labda alijifunza in hard way baada ya matokeo ya Ubunge.Haya...

-Kama ilivyo Chama cha CUF,UPND hakijulikani kinasimamia ni.It has never been and will never be there a strong alliance based on opportunism,evasions or illusions and suspicion.

-UPND waliafanya Alliance na UNIP na chama Cha FDD baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2006 na baadae wakaungana na chama cha Patriotic Front cha Michael Sata(Slaa wa Zambia).Kwa kuwa walikua opportunist chama cha PF kikajiondoa kwenye alliance kama walivyofanya CHADEMA kujitoa kwenye ushirikiano na vyama vyenye usaliti na unafiki.

-Baadae kiongozi wa UPND akaungana na chama tawala NMD na hata akathubutu kupinga mapendekezo ya upinzani bungeni ya kubadili vipengele vya katiba kuhusu uchaguzi kwamba mshindi apatikane kwa zaidi ya asilimia 50(kitanzi walichotaka kumvisha Sata baadae wakakivaa wao).Sasa CUF wanaitukana Chadema kuliko chama kinginw chochote na wana alliance na CCM kule Zanzibar

-Pia kiongozi wa UPND kabla ya uchaguzi mkuu alikua akiongoza kutoa maneno ya kejeli kwa Sata na viongozu wa PF(kama alivyofanya Mtatiro kule Ubungo kwenye kampeni za ubunge mwaka juzi na anavyofanya Juma Haji Duni na Ismail Jusda leo hii) na kukatisha wananchi Tamaa kuwa Upinzani hauwezi kushinda kwa kuwa hawajakomaa na wana safu nyembamba.Baadae na yeye akagombea ili kupunguza kura za upinzani.Nani angempigia kura mwanasiasa ambaye hata yeye mwenyewe aliamini hatashinda?Hillarious....

-Baada ya Uchaguzi wa mwaka jana ambao upinzani ulishinda ameendelea kuungana na chama tawala cha zamani chini ya Rupiah Banda na kumtetea juu ya kashfa yake ya ufisadi yeye na watoto wake akisahau alikua anawatuhumu zamani na sasa ameungana nao kama ambavyo CUF inaungana na CCM dhidi ya CHADEMA na dhidi ya matakwa ya umma

-Hoja ya alliance ni nzuri but opportunism,illusions and evasions is not a recipe for building a strong opposition

-What Tanzania need is a wise,Matured,orderely and courageous opposition in building their confidence for future

-Kuungana na watu wenye narrow agenda ni kufifisha harakati hizi na kukatisha tamaa.Kumbuka aina ya alliance ambayo mtu anafanya inatoa taswira ya commitment yako .Wapinzani tunamalizana wenyewe kwa ujinga.

Ningemshauri kijana mwenzetu Julius Mtatiro ajitazame,akiangalie chama chake na ajenda zake na kufanya wise desicion ili asijikute upande wa UPND tutakaposhinda uchaguzi

Naamini CUF ikibadilika na CHADEMA vikawa na lengo moja kuondoa CCM itawezekana hata kule Zambia Hakaende Hichilima kama sio unafiki na kutojipanga angekua mwanasiasa mzuri na kuiongoza Zambia Siku moja baada ya akina Michael Satta.Ni lazima abadili mtazamo sasa wa wazambia wengi dhidi yake.

Kuungana na CUF ya sasa katika mazingira ya kurushiana vijembe ni kupoteza muda na kuturudisha enzi za chama kimoja na kuipa CCM nguvu .Single state party is a recipe for tyranny.Hatutaki kurudi huko! Tujipange Upya!
 
Kwani lengo ni nini kuiondoa CCM madarakani, Kwenda Ikulu au kuwaletea wananchi maendeleo? Saidieni maendeleo bila hata kuiondoa CCM madarakani na hapo wananchi wenyewe wataona umuhimu wenu. CCM haiwezi kuondoka madarakani kwa kupnga kuungana bila kujua mnataka kuwafanyia nini wananchi.

Maendeleo hayaletwi na vyama kutumia fedha za vyama husika. Huletwa na serikali inayotokana na chama kilichochaguliwa kushika dola. Hivyo kuwa na uhalali wa kutekeleza sera kwa mujibu ya ilani ya chama hicho iliyouzwa kwa wapiga kura kupitia kampeni za uchaguzi. Chama ambacho hakikuchaguliwa kinakosa uhalali wa kutekeleza sera zake . Kwa kuwa hakina uhalali wa kutumia fedha inayotokana na jasho la Wananchi wote wa Tanzania kwa kukusanya kodi na mapato mengine ya serikali kama gesi, madini, na mashirika ya umma ,pia hakina dola ya kusimamia sheria nk. Kwa hiyo ni imani potofu kuwa vyama vya upinzani vianze kuleta maendeleo kabla ya kuchaguliwa. Hata CCM HAITEKELEZI SERA YOYOTE ILITUMiA FEDHA YAKE wenyewe!
 
Mtatiro hana hoja hapa zaidi ya kujaribu kuimba wimbo wa ccm. Kila siku Jusa, Duni na yeye mwenyewe wamekuwa wakitoa maneno mengi ya shutuma na matusi dhidi ya Chadema na viongozi wetu. Sasa hii akili ya kutaka kuunganisha nguvu nasi ameitoa wapi? Bila shaka anatambua nguvu ya Chadema na kukubalika kwetu kwa watanzania kwani kila tunapokwenda kwenye hizi chaguzi ndogo mafanikio yanazidi kuonekana wakati wao cuf wanazidi kupotea.

Siwezi kuunga mkono kamwe Chadema kuungana na cuf katika mazingira ya sasa ya kisiasa ambayo cuf ni mshirika wa karibu sana na ccm. Kama wanataka alliance wanapaswa kujitanabahisha waziwazi kwamba wao ni wapinzani wa ccm na kwamba wako pamoja na Chadema, sio kila siku wanaishambulia Chadema na wanapoona hakuna mafanikio yoyote ya kuishambulia zaidi ya wao wenyewe kuporomoka ndipo sasa wanakuja na ngonjera za kutaka alliance. Hiyo haipo tuatkwenda wenyewe hivi hivi vinginevyo tupate mpinzani mwingine anayeaminika tunaweza kuunganisha nae nguvu.
 
Mtatiro na CUF yake are very Opportunisty,,,wanaona kwa siku zijazo hasa 2015 hata hivyo vi kura wanavyosema wamegawana vitahamia CHADEMA...waliwahi kuambiwa na CHADEMA waachiane sehemu ambazo kila mmoja ana mvuto CUF wakagoma,,,CHADEMA ikaingia kwa nguvu, sasa wameona matokeo Mtatiro analalama, tena hizo sehemu ambazo CCM imeshinda ilibidi CUF washinde kama wangezingatia ushauri wa CHADEMA mapema.

Kwa CHADEMA huu ni ushindi mkubwa kama ilivokuwa Igunga, maana sehemu nyingine hakukuwa na mtaji kabisa hasa Pwani....hebu wewe fikiria CHADEMA inashinda Sikonge hili si balaa jamani...Tujiandae for 2015
 
MTATIRO kusema hayo sioni ajabu. Yeye ni 'JASUSI la MAGAMBA' ndani ya vyama. Unaona "ANAVYOWANYIZA" CUF?
 
Haya ni maneno ya busara sana kutoka kwa mtatiro, bila vyama vya upinzani kubadili startegy zao za kupambana na CCM wasahau kushika dola, watabaki kujipa moyo na mahudhurio kwenye mikutano ya hadhara huku wakipoteza chaguzi
 
Kweli mfa maji haachi kutapatapa. Vipi ule mgogoro wao wa kuchapana makonde kule Arusha umekwisha na sasa wanataka kuungana? Huyu Mtatiro kweli sasa nimeona anataka kuhamia CDM. Nataka kuwa kama mtabiri, miezi miwili haitapita tutamsikia kule kwa vidole viwili kwani kauli hii ni mpya kabisa kutoka kwa huyu mkiristo.
Kutokana na hiyo red, nadiriki kukuita wewe poyoyo! Kichwa chako hakina kitu kabisa. Hivi hii mitizamo ya ukristo na uislamu mmeitoa wapi watanzania wenzangu? Mbona hili tatizo linakua kwa kasi ya kutisha?

Sioni ubaya katika hoja nzima ya Mtatiro. Kwani ni lazima kuungana? Kuna maeneo ambayo ni wazi kwamba CHADEMA wanakubalika zaidi na maeneo mengine ambayo CUF wanakubalika, mengine TLP, na mengine NCCR mageuzi. Ufike wakati upinzani wakubaliane kusimamisha na kumuunga mkono mtu mmoja kulingana na maeneo. Ukanda wa mwambao mwa Tanzani ni dhahiri kwamba CHADEMA haiwezi kuvuna kitu huko, sasa kuna haja gani ya kupoteza resources kupigia kampeni mtu huko, kwanini asisimame wa CUF ambaye anakubalika na akaungwa mkono na vyama vyote?

Kule kigoma kuna majimbo ambayo NCCR mageuzi inakubalika, waachieni NCCR majimbo hayo, similary maeneo ya kaskazini na kusini. Mwisho wa siku, kama upinzani utashinda nafasi ya urais, basi chama chenye wabunge wengi ndiyo kiunde serikali. Kwani tatizo liko wapi? sasa inasaidia nini kuendelea kugawana kura na kuiacha CCM iendelee kuwanyonya watanzania?

Kama kweli vyama vya upinzani vina nia ya dhati ya kumkomboa mtanzania kama vinavyojinasibu, basi hili wazo la Mtatiro lisipuuzwe, kaeni pamoja mkubaliane namna nzuri ya kuing'oa CCM maeneo ilikoweka mizizi. Acheni ubinafsi nyie wapinzani.

Najua wengi mtachukulia kwamba kwa kuwa CUF inaelekea kufa, ndiyo maana wameanza kutafuta muungano, lakini hapa mimi siongelei CUF peke yao bali naongelea vyama vyote vya upinzani, viwe na dira moja. CUF ijitoe kwenye muungano wake na CCM na iamua kuwe chama cha ukweli cha upinzani.
 
Muda huu CCM inaogelea kwenye starehe la utawala kutokana na mifumo duni ya kiuongozi ndani ya vyama vya upinzani, Kuungana kwa CCM na CUF katika GNU huko Zanzibar kumetoa nafasi kubwa kwa CCM kupumua sana bila tatizo, aidha kwa CHADEMA kutokuwa na mipango madhubuti ya kufikia wananchi kwa sera zinazoeleweka kwa urahisi huku Tanzania bara, kunaisidia CCM kuwatumia Wananchi wa Vijijini kupata Ushindi.

Iwapo CUF itarudisha ungangari wake wa siku za nyuma huo ZANZIBAR na CHADEMA ikaimarisha safu yake mikoani na kuacha kuzunguka ziarani tu bila kusimika misingi imara ya chama huku bara niwazi kabisa CCM itaelemewa na na itakuwa ni muda mwafaka kwa wao kuachia.
 
Kweli Vita ya Panzi furaha ya kunguru....
Ukisoma comments hapa utagundua watu siasa hawazijui au wanajifanya hawazijui....
Mwisho wa siku CCM Watatawala kwa Miaka 100 ijayo kama wanavyodai....
 
Sema tatizo ni Uamsho maana bora CCM waongoze milele kuliko Uamsho waongoze dakika kumi zenji!!Alafu hao CUF kwani unataka wakaze kitu gani maana wao na CCM ni chama kimoja so sijakuelewa wakazeje
 
Tatizo lako Mtatiro unaangalia factor moja tu katika mkakati wako wa kuiondoa CCM.Unaangalia idadi ya kura tu na ndipo unathibitisha upeo mdogo ulionao ambao labda Chadema wanaweza kuufanyia kazi ! Maana CHADEMA nao hampishani nao sana kuanzia viongozi wao,mwanachama wao na hata mashabiki wao!

Ebu wewe Mtatiro na wanasiasa uchwara wenzako ndani ya CUF na CHADEMA mbona hamjiulizi kuwa kwa nini pamoja na kelele zenu nyingi mnazotoa huku mapovu meupe yakiwatoka mdomoni kuhusu ubaya wa CCM na bado WATZ hawawapi kura?Ukiangalia haraka haraka hapo kwenye takwimu za matokea bado maeneo mengi hata ukiunganisha CUF ,CHADEMA na NCCR bado hamwezi kuishinda CCM! Mtakimbilia kutoa majibu mepesi kama vilivyo vichwa vyenu kuwa CCM inatoa Rushwa kwa wananchi! POINT ni kwamba hamna sera wa hoja madhubuti za kuiondoa CCM mnachotafuta ni kuganga njaa tu!

Wananchi wanajua hilo vizuri ,kama unabisha ebu compare shavu la John Mnyika wa sasa ,Kafulila wa sasa na wakati wa mchakato majimboni! NIPE JIBU HARAKA MTATIRO,Nanyi mnatafuta KULA tu ndo maana unadhani kuunganisha vyama ni sawa na kuunganisha mbao kwa msumari! Angalia kwanza kama vision na mission ya vyama vyenu ni sawa!? Mnazo sera au masela!? na mwisho mna vibrate vipi kwenye public domain?
 
Hakuna kuungana hapo. CDM TUKIUNGANA NA CUF NI SAWA NA KUCHANGANYA MAFUTA NA MAJI. CUF HAWANA SERA ZAIDI YA KUKATI NA KUPESTI SERA. BADO TU WATAKATI NA KUPESTI SERA ZA UAMUSHO. CDM TUKO MAKINI NA TUTASIMAMISHA MTU MAKINI MAANA TUNAO WENGI (SIO DR PEKE YAKE) KAMA UNAVOFIKIRI WEWE.
 
Muda huu CCM inaogelea kwenye starehe la utawala kutokana na mifumo duni ya kiuongozi ndani ya vyama vya upinzani, Kuungana kwa CCM na CUF katika GNU huko Zanzibar kumetoa nafasi kubwa kwa CCM kupumua sana bila tatizo, aidha kwa CHADEMA kutokuwa na mipango madhubuti ya kufikia wananchi kwa sera zinazoeleweka kwa urahisi huku Tanzania bara, kunaisidia CCM kuwatumia Wananchi wa Vijijini kupata Ushindi.

Iwapo CUF itarudisha ungangari wake wa siku za nyuma huo ZANZIBAR na CHADEMA ikaimarisha safu yake mikoani na kuacha kuzunguka ziarani tu bila kusimika misingi imara ya chama huku bara niwazi kabisa CCM itaelemewa na na itakuwa ni muda mwafaka kwa wao kuachia.
Cuf zanzibar haijaungana na ccm bali wamegawana madaraka tu,bado cuf ipo pale pale,kilichofanyika ni kuwaletea maendeleo wananchi.

Watu wanasema kuwa adui wake ukimweka mbali ndipo anapopata mashambulizi zaidi ya kukudhuru,ili uweze kufanikiwa adui wako kuwa nae karibu kula nae sambamba utamwisha nguvu tu.

CDM kama watakuwa ni maadui wa ccm hawatashinda abadani na wala hawataitoa ccm madarakani,mchombeze choka pangoni atatoka mwenyewe.
 
Cuf wakaze wakati wao wameolewa na magamba?...nawewe nae kuingilia ndoa za watu,acha cuf aendelee kumkatikia mumewe magamba
 
Back
Top Bottom