Chadema kutokubali uchaguzi mdogo Arusha Mjini kunazua maswali!

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
NI zaidi ya miezi minne sasa wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini, hawana mbunge wa kuwawakilisha katika vikao vya mikutano ya shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyo kwa majimbo karibu yote ya Tanzania Bara.

Jimbo lingine, ambalo halina mbunge kwa kipindi kama hicho, ni Sumbawanga Mjini, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, kutengua ubunge wa Khalfan Aeshi (CCM).

Aesh alitiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 uliompa ushindi.

Jimbo la Arusha Mjini, ambalo ndiyo mada yangu ya leo, halina mbunge kwa sababu kuu mbili. Ya kwanza, ni hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha. Hukumu hiyo ilitengua ubunge wa Godbless Lema (Chadema) aliyekuwa akiliwakilisha jimbo hilo bungeni tangu mwaka 2010.

Hukumu hiyo ilitolewa Aprili 5, mwaka huu, na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila, baada ya kujiridhisha kuwa Lema alitumia kashfa, kejeli na udhalilishaji katika mikutano yake ya kampeni, kinyume cha kanuni, taratibu na sheria ya maadili ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Sababu ya pili inayofanya jimbo hilo likose mbunge hadi sasa, ni rufaa iliyokatwa na Chadema kupinga hukumu hiyo ya Jaji Rwakibarila. Sheria inazuia kuitishwa uchaguzi hadi rufaa hiyo itakapoamuliwa.

Rufaa hiyo ndiyo kwanza imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Kesi iliyotengua ubunge wa Lema, ilifunguliwa na wanachama watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliodai kuwa wakati wa kampeni Lema alimdhalilisha aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian, ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania, nchini Kenya.

Baada ya hukumu ile, Lema alionekana kutokuwa na wazo kabisa la kukata rufaa. Kwani siku ileile saa chache baada ya hukumu kutolewa, alikaririwa akisema hatakata rufaa kwa kuwa hataki kuwa mbunge wa rufaa.

Msimamo huo wa Lema ulioana sawia na ule aliokuwa nao Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

Mwigamba pamoja na mambo mengine, alikaririwa akisema haoni sababu ya kukata rufaa. Bali kujiandaa na kuingia kikamilifu katika uchaguzi wa marudio jimboni humo.

Alisema kukata rufaa ni kupoteza muda, kwani kinachotakiwa ni kujiandaa kikamilifu kuiangusha tena CCM katika uchaguzi wa marudio kwa kura nyingi tofauti na zile zilizopita.

Ni wazi kuwa kauli hiyo ya Lema inadhihirisha imani yake kwa Chadema kwamba, ina uwezo mkubwa wa kulirejesha jimbo hilo wakati wowote na saa yoyote kama atasimamishwa tena kulitetea.

Naweza kusema Lema hapo yuko sahihi. Kwamba, kwa hakika Jimbo la Arusha Mjini bado ni ngome ya Chadema. Vipo vigezo vingi vinavyoweza kuthibitisha ukweli huo.

Cha kwanza, ni matokeo halisi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 yaliyompa ushindi Lema. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa Lema alimwangusha Dk. Burian kwa kumshinda karibu kura 20,000.

Kigezo cha pili, ni mchuano mkali uliopo katika idadi ya madiwani waliovunwa na Chadema dhidi ya madiwani, ambao CCM ilipata katika uchaguzi huo katika Manispaa ya Arusha.

Katika manispaa hiyo, CCM ilipata madiwani 16, Chadema 15 na Chama cha Tanzania Labour (TLP) wawili. Takwimu hiyo ni kabla ya madiwani watano wa Chadema kuvuliwa uanachama kwa kukiuka maamuzi na maelekezo ya chama.

Kigezo cha tatu, ni mwitikio wa watu, ambao umekuwa ukionekana katika mikutano ya hadhara, maandamano na shughuli nyingine za kisiasa na kijamii zinazoandaliwa na Chadema jimboni humo.

Kigezo cha nne, ni ushindi, ambao Chadema iliupata katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

Ni ukweli usiopingika kuwa ushindi huo alioupata aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chadema, Joshua Nassari, ulichangiwa na ushawishi mkubwa wa wananachi kutoka Jimbo la Arusha Mjini.

Kigezo cha tano, ni namna mwitikio wa wananchi ulioonekana mahakamani siku ya hukumu na katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na uongozi wa Chadema mjini Arusha baada ya hukumu hiyo.

Yawezekana vigezo hivyo ndivyo vilivyomfanya Lema aamini kuwa kushindwa kwake kesi si kwa sababu chama chake nay eye mwenyewe hawaungwi mkono na wananchi. La!

Bali aliamini na kudiriki kutamka kwamba, kulitokana na shinikizo la Ikulu, madai ambayo yalinushwa vikali na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu kwamba, ni ya upuuzi na ni ukosefu mkubwa wa adabu na heshima uliofanywa na Lema kwa mahakama na serikali.

Ni wazi kuwa hatua ya Lema kukata rufaa hiyo, haikuwa ni hiari yake. Bali ilikuwa ni kutekeleza uamuzi ya chama chake. Na pengine ulitokana na kuhofia yasije yakamkuta yaliyowakuta madiwani wale watano wa Chadema.

Uamuzi wa Chadema wa kukata rufaa, ulitangazwa na Mbowe katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya NMC, mjini Arusha, Aprili 8, mwaka huu.

Mbowe alisema licha ya Chadema kuwa na uhakika wa kushinda uchaguzi katika jimbo hilo, wameshauriana na wanasheria pamoja na viongozi wenzake.

Wameona ni vema wakakata rufaa kwa sababu ya jaji kutafsiri kuwa Lema alitukana, alibagua kijinsia na aliendesha kampeni zisizo za kistaarabu, jambo ambalo alidai kuwa halikuwa kweli na halikutokea.

Hata hivyo, uamuzi wa Chadema wa kutokubali kwenda kwenye uchaguzi mdogo jimboni humo ili kumrudisha mbunge wake, bado unazua maswali!

Mosi, kauli ya Lema kwamba, hataki kuwa mbunge wa rufaa, je, ilikuwa ni ya kukurupuka?

Pili, shinikizo la Ikulu lililodaiwa na Lema kuingilia kesi yake Mahakama Kuu na kutengua ubunge wake, je, haliwezi ‘kupenya’ pia katika Mahakama ya Rufaa, ambako chama kimekimbilia huko, rufaa yake ikatupwa?

Tatu, ikiwa viongozi wakuu wa Chadema, Lema mwenyewe na wananchi, wana uhakika wa chama kushinda Arusha Mjini hata kama watasimamisha jiwe kugombea, kwanini basi wasikubali kuingia kwenye uchaguzi badala ya kupoteza muda wa rufaa?
 
Swala hapa sio kushinda, Chadema ina uhakika wa kushinda jimbo la AR wakati wowote uchaguzi ukiitiswa.
Kilichozingatiwa ni kulinda heshima ya chama na Lema mwenyewe, kwani kukubali hukumu na kwenda kwenye uchanguzi ni kukubali yale yote yaliyoainishwa kwenye kesi wakati si kweli.
Kesi ilivyoendeshwa hata wale mashidi wa ccm ilionekana wazi ni wakupandikiza. mashahidi muhimu upande wa ccm wahakufikishwa mahakamani kutoa ushahidi na hoja muhimu za CDM zilitupiliwa mbali.
Kwa hayo yote ulitaka CDM wakubaliane nayo kwamba ni sahihi ilimradi waende kwenye uchaguzi na kushinda?
CDM ni chama makini zaidi ya watu wengi wanavyofikiri, wanasimamia haki na ukombozi wa kweli, sio swala la kushinda tu!
 
Mtoa mada kakurupuka tu. sababu kubwa ya CDM kukata rufaa Arusha ni kwamba katika hukumu ya mahakama Kuu haikuelezwa kwa bayana kabisa kuhusu suala la rushwa - iwapo Lema alitoa hongo etc na hivyo kutogombea tena ubunge kwa kipindi fulani. Hukumu haikuwa wazi, nadhani iliachwa hivyo kimakusudi tu katika hilo.

Hivyo Lema angegombea tena, CCM wangeweza kuweka pingamizi kwa Tume ya uchaguzi - NEC -kumuengua wakati wa uteuzi na kufanikiwa, na hivyo kuiwezesha CCM kulichukuwa jimbo kwa ulaini. Si unajua tena mara nyingi Tume ya Uchaguzi siyo huru.

Hilo ndilo walikuwa wanahofia CDM na ndiyo maana wamekata rufaa, na katika rufaa hiyo CDM wanaomba Mahakama ya Rufaa ifafanue pia kuhusu suala la rushwa.
 
Mtoa mada from 2day ur out'f ma mind,.huwa nakuamini kamanda ila huna hoja at all.OSOKONI= GAMBA
 
NI zaidi ya miezi minne sasa wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini, hawana mbunge wa kuwawakilisha katika vikao vya mikutano ya shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyo kwa majimbo karibu yote ya Tanzania Bara.

Jimbo lingine, ambalo halina mbunge kwa kipindi kama hicho, ni Sumbawanga Mjini, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, kutengua ubunge wa Khalfan Aeshi (CCM).

Aesh alitiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 uliompa ushindi.

Jimbo la Arusha Mjini, ambalo ndiyo mada yangu ya leo, halina mbunge kwa sababu kuu mbili. Ya kwanza, ni hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha. Hukumu hiyo ilitengua ubunge wa Godbless Lema (Chadema) aliyekuwa akiliwakilisha jimbo hilo bungeni tangu mwaka 2010.

Hukumu hiyo ilitolewa Aprili 5, mwaka huu, na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila, baada ya kujiridhisha kuwa Lema alitumia kashfa, kejeli na udhalilishaji katika mikutano yake ya kampeni, kinyume cha kanuni, taratibu na sheria ya maadili ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Sababu ya pili inayofanya jimbo hilo likose mbunge hadi sasa, ni rufaa iliyokatwa na Chadema kupinga hukumu hiyo ya Jaji Rwakibarila. Sheria inazuia kuitishwa uchaguzi hadi rufaa hiyo itakapoamuliwa.

Rufaa hiyo ndiyo kwanza imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Kesi iliyotengua ubunge wa Lema, ilifunguliwa na wanachama watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliodai kuwa wakati wa kampeni Lema alimdhalilisha aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian, ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania, nchini Kenya.

Baada ya hukumu ile, Lema alionekana kutokuwa na wazo kabisa la kukata rufaa. Kwani siku ileile saa chache baada ya hukumu kutolewa, alikaririwa akisema hatakata rufaa kwa kuwa hataki kuwa mbunge wa rufaa.

Msimamo huo wa Lema ulioana sawia na ule aliokuwa nao Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

Mwigamba pamoja na mambo mengine, alikaririwa akisema haoni sababu ya kukata rufaa. Bali kujiandaa na kuingia kikamilifu katika uchaguzi wa marudio jimboni humo.

Alisema kukata rufaa ni kupoteza muda, kwani kinachotakiwa ni kujiandaa kikamilifu kuiangusha tena CCM katika uchaguzi wa marudio kwa kura nyingi tofauti na zile zilizopita.

Ni wazi kuwa kauli hiyo ya Lema inadhihirisha imani yake kwa Chadema kwamba, ina uwezo mkubwa wa kulirejesha jimbo hilo wakati wowote na saa yoyote kama atasimamishwa tena kulitetea.

Naweza kusema Lema hapo yuko sahihi. Kwamba, kwa hakika Jimbo la Arusha Mjini bado ni ngome ya Chadema. Vipo vigezo vingi vinavyoweza kuthibitisha ukweli huo.

Cha kwanza, ni matokeo halisi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 yaliyompa ushindi Lema. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa Lema alimwangusha Dk. Burian kwa kumshinda karibu kura 20,000.

Kigezo cha pili, ni mchuano mkali uliopo katika idadi ya madiwani waliovunwa na Chadema dhidi ya madiwani, ambao CCM ilipata katika uchaguzi huo katika Manispaa ya Arusha.

Katika manispaa hiyo, CCM ilipata madiwani 16, Chadema 15 na Chama cha Tanzania Labour (TLP) wawili. Takwimu hiyo ni kabla ya madiwani watano wa Chadema kuvuliwa uanachama kwa kukiuka maamuzi na maelekezo ya chama.

Kigezo cha tatu, ni mwitikio wa watu, ambao umekuwa ukionekana katika mikutano ya hadhara, maandamano na shughuli nyingine za kisiasa na kijamii zinazoandaliwa na Chadema jimboni humo.

Kigezo cha nne, ni ushindi, ambao Chadema iliupata katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

Ni ukweli usiopingika kuwa ushindi huo alioupata aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chadema, Joshua Nassari, ulichangiwa na ushawishi mkubwa wa wananachi kutoka Jimbo la Arusha Mjini.

Kigezo cha tano, ni namna mwitikio wa wananchi ulioonekana mahakamani siku ya hukumu na katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na uongozi wa Chadema mjini Arusha baada ya hukumu hiyo.

Yawezekana vigezo hivyo ndivyo vilivyomfanya Lema aamini kuwa kushindwa kwake kesi si kwa sababu chama chake nay eye mwenyewe hawaungwi mkono na wananchi. La!

Bali aliamini na kudiriki kutamka kwamba, kulitokana na shinikizo la Ikulu, madai ambayo yalinushwa vikali na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu kwamba, ni ya upuuzi na ni ukosefu mkubwa wa adabu na heshima uliofanywa na Lema kwa mahakama na serikali.

Ni wazi kuwa hatua ya Lema kukata rufaa hiyo, haikuwa ni hiari yake. Bali ilikuwa ni kutekeleza uamuzi ya chama chake. Na pengine ulitokana na kuhofia yasije yakamkuta yaliyowakuta madiwani wale watano wa Chadema.

Uamuzi wa Chadema wa kukata rufaa, ulitangazwa na Mbowe katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya NMC, mjini Arusha, Aprili 8, mwaka huu.

Mbowe alisema licha ya Chadema kuwa na uhakika wa kushinda uchaguzi katika jimbo hilo, wameshauriana na wanasheria pamoja na viongozi wenzake.

Wameona ni vema wakakata rufaa kwa sababu ya jaji kutafsiri kuwa Lema alitukana, alibagua kijinsia na aliendesha kampeni zisizo za kistaarabu, jambo ambalo alidai kuwa halikuwa kweli na halikutokea.

Hata hivyo, uamuzi wa Chadema wa kutokubali kwenda kwenye uchaguzi mdogo jimboni humo ili kumrudisha mbunge wake, bado unazua maswali!

Mosi, kauli ya Lema kwamba, hataki kuwa mbunge wa rufaa, je, ilikuwa ni ya kukurupuka?

Pili, shinikizo la Ikulu lililodaiwa na Lema kuingilia kesi yake Mahakama Kuu na kutengua ubunge wake, je, haliwezi ‘kupenya' pia katika Mahakama ya Rufaa, ambako chama kimekimbilia huko, rufaa yake ikatupwa?

Tatu, ikiwa viongozi wakuu wa Chadema, Lema mwenyewe na wananchi, wana uhakika wa chama kushinda Arusha Mjini hata kama watasimamisha jiwe kugombea, kwanini basi wasikubali kuingia kwenye uchaguzi badala ya kupoteza muda wa rufaa?

Hoja kuu hapa ni HAKI INATAFUTWA na siyo Lema alisema nini au jimbo halina mbunge.
 
Pia kwa mtazamo wangu, CDM walikata rufaa ili hukumu ile isitumiwe kama precedence (kwa wataalamu wa sheria kama niko sahihi), katika kesi zingine.
 
Kwanza ikumbukwe kuwa Mhe.Lema hakushtakiwa kwa makosa ya Rushwa.. Kwenye Judgement Jaji alitumia kifungu cha rushwa kumtia hatiani (Kinyume cha sheria).. Na kifungu hicho kiliwekwa kimtego ili CHADEMA wakubali kumrudisha Mhe.Lema kugombea na CCM wamuondoe kwa Pingamizi waweze kushinda Ubunge wa Hila Arusha Mjini. Hilo CHADEMA ililiona. Pili ni Vigumu sana kwa Chama kama CHADEMA kinachohubiri kila siku Uongozi Bora (Si Utawala Bora) kukubali sheria ivunjiwe miguuni pake! Naamini uamuzi wa CHADEMA ni wa busara hata sasa.

Pengine chukua muda upitie kurasa za Judgement ya Mhe.Lema inaweza kulipasua kaniki unaloliona mbele yako.
 
Swala hapa sio kushinda, Chadema ina uhakika wa kushinda jimbo la AR wakati wowote uchaguzi ukiitiswa.
Kilichozingatiwa ni kulinda heshima ya chama na Lema mwenyewe, kwani kukubali hukumu na kwenda kwenye uchanguzi ni kukubali yale yote yaliyoainishwa kwenye kesi wakati si kweli.
Kesi ilivyoendeshwa hata wale mashidi wa ccm ilionekana wazi ni wakupandikiza. mashahidi muhimu upande wa ccm wahakufikishwa mahakamani kutoa ushahidi na hoja muhimu za CDM zilitupiliwa mbali.
Kwa hayo yote ulitaka CDM wakubaliane nayo kwamba ni sahihi ilimradi waende kwenye uchaguzi na kushinda?
CDM ni chama makini zaidi ya watu wengi wanavyofikiri, wanasimamia haki na ukombozi wa kweli, sio swala la kushinda tu!
Haki gani wanaisimamia wakati wanawanyima wananchi wa jimbo la Arusha haki ya kuwakilishwa bungeni?
 
NI zaidi ya miezi minne sasa wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini, hawana mbunge wa kuwawakilisha katika vikao vya mikutano ya shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyo kwa majimbo karibu yote ya Tanzania Bara.

Jimbo lingine, ambalo halina mbunge kwa kipindi kama hicho, ni Sumbawanga Mjini, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, kutengua ubunge wa Khalfan Aeshi (CCM).

Aesh alitiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 uliompa ushindi.

Jimbo la Arusha Mjini, ambalo ndiyo mada yangu ya leo, halina mbunge kwa sababu kuu mbili. Ya kwanza, ni hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha. Hukumu hiyo ilitengua ubunge wa Godbless Lema (Chadema) aliyekuwa akiliwakilisha jimbo hilo bungeni tangu mwaka 2010.

Hukumu hiyo ilitolewa Aprili 5, mwaka huu, na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila, baada ya kujiridhisha kuwa Lema alitumia kashfa, kejeli na udhalilishaji katika mikutano yake ya kampeni, kinyume cha kanuni, taratibu na sheria ya maadili ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Sababu ya pili inayofanya jimbo hilo likose mbunge hadi sasa, ni rufaa iliyokatwa na Chadema kupinga hukumu hiyo ya Jaji Rwakibarila. Sheria inazuia kuitishwa uchaguzi hadi rufaa hiyo itakapoamuliwa.

Rufaa hiyo ndiyo kwanza imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Kesi iliyotengua ubunge wa Lema, ilifunguliwa na wanachama watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliodai kuwa wakati wa kampeni Lema alimdhalilisha aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian, ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania, nchini Kenya.

Baada ya hukumu ile, Lema alionekana kutokuwa na wazo kabisa la kukata rufaa. Kwani siku ileile saa chache baada ya hukumu kutolewa, alikaririwa akisema hatakata rufaa kwa kuwa hataki kuwa mbunge wa rufaa.

Msimamo huo wa Lema ulioana sawia na ule aliokuwa nao Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

Mwigamba pamoja na mambo mengine, alikaririwa akisema haoni sababu ya kukata rufaa. Bali kujiandaa na kuingia kikamilifu katika uchaguzi wa marudio jimboni humo.

Alisema kukata rufaa ni kupoteza muda, kwani kinachotakiwa ni kujiandaa kikamilifu kuiangusha tena CCM katika uchaguzi wa marudio kwa kura nyingi tofauti na zile zilizopita.

Ni wazi kuwa kauli hiyo ya Lema inadhihirisha imani yake kwa Chadema kwamba, ina uwezo mkubwa wa kulirejesha jimbo hilo wakati wowote na saa yoyote kama atasimamishwa tena kulitetea.

Naweza kusema Lema hapo yuko sahihi. Kwamba, kwa hakika Jimbo la Arusha Mjini bado ni ngome ya Chadema. Vipo vigezo vingi vinavyoweza kuthibitisha ukweli huo.

Cha kwanza, ni matokeo halisi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 yaliyompa ushindi Lema. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa Lema alimwangusha Dk. Burian kwa kumshinda karibu kura 20,000.

Kigezo cha pili, ni mchuano mkali uliopo katika idadi ya madiwani waliovunwa na Chadema dhidi ya madiwani, ambao CCM ilipata katika uchaguzi huo katika Manispaa ya Arusha.

Katika manispaa hiyo, CCM ilipata madiwani 16, Chadema 15 na Chama cha Tanzania Labour (TLP) wawili. Takwimu hiyo ni kabla ya madiwani watano wa Chadema kuvuliwa uanachama kwa kukiuka maamuzi na maelekezo ya chama.

Kigezo cha tatu, ni mwitikio wa watu, ambao umekuwa ukionekana katika mikutano ya hadhara, maandamano na shughuli nyingine za kisiasa na kijamii zinazoandaliwa na Chadema jimboni humo.

Kigezo cha nne, ni ushindi, ambao Chadema iliupata katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

Ni ukweli usiopingika kuwa ushindi huo alioupata aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chadema, Joshua Nassari, ulichangiwa na ushawishi mkubwa wa wananachi kutoka Jimbo la Arusha Mjini.

Kigezo cha tano, ni namna mwitikio wa wananchi ulioonekana mahakamani siku ya hukumu na katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na uongozi wa Chadema mjini Arusha baada ya hukumu hiyo.

Yawezekana vigezo hivyo ndivyo vilivyomfanya Lema aamini kuwa kushindwa kwake kesi si kwa sababu chama chake nay eye mwenyewe hawaungwi mkono na wananchi. La!

Bali aliamini na kudiriki kutamka kwamba, kulitokana na shinikizo la Ikulu, madai ambayo yalinushwa vikali na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu kwamba, ni ya upuuzi na ni ukosefu mkubwa wa adabu na heshima uliofanywa na Lema kwa mahakama na serikali.

Ni wazi kuwa hatua ya Lema kukata rufaa hiyo, haikuwa ni hiari yake. Bali ilikuwa ni kutekeleza uamuzi ya chama chake. Na pengine ulitokana na kuhofia yasije yakamkuta yaliyowakuta madiwani wale watano wa Chadema.

Uamuzi wa Chadema wa kukata rufaa, ulitangazwa na Mbowe katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya NMC, mjini Arusha, Aprili 8, mwaka huu.

Mbowe alisema licha ya Chadema kuwa na uhakika wa kushinda uchaguzi katika jimbo hilo, wameshauriana na wanasheria pamoja na viongozi wenzake.

Wameona ni vema wakakata rufaa kwa sababu ya jaji kutafsiri kuwa Lema alitukana, alibagua kijinsia na aliendesha kampeni zisizo za kistaarabu, jambo ambalo alidai kuwa halikuwa kweli na halikutokea.

Hata hivyo, uamuzi wa Chadema wa kutokubali kwenda kwenye uchaguzi mdogo jimboni humo ili kumrudisha mbunge wake, bado unazua maswali!

Mosi, kauli ya Lema kwamba, hataki kuwa mbunge wa rufaa, je, ilikuwa ni ya kukurupuka?

Pili, shinikizo la Ikulu lililodaiwa na Lema kuingilia kesi yake Mahakama Kuu na kutengua ubunge wake, je, haliwezi ‘kupenya' pia katika Mahakama ya Rufaa, ambako chama kimekimbilia huko, rufaa yake ikatupwa?

Tatu, ikiwa viongozi wakuu wa Chadema, Lema mwenyewe na wananchi, wana uhakika wa chama kushinda Arusha Mjini hata kama watasimamisha jiwe kugombea, kwanini basi wasikubali kuingia kwenye uchaguzi badala ya kupoteza muda wa rufaa?
Nashikwa na kigugumizi kuchangia mada hii, Hivi majaji wa Kesi ya LEMA na wale walioamua kezi za Igunga na Sumbawanga tofauti zao nini, CDM wakishinda, jaji mzuri, wakishindwa, jaji wa CCM. Haya mambo yanakuaje? si tuachane na haya mambo ya vyama vingi? Haya mambo ya wazungu bwana, Afrika tunadandia gari kwa mbele.
 
mkuu rufaa ilikua ni muhimu sana kwasababu
1.hukumu hiyo ingeachwa bila kukatiwa rufaa,kesi zingine zingeweza kujudgiwa kwa kutumia hukumu hiyo(wataalam wa sheria mtanisaidia hapo)
2.hukumu ile ilikua inamtaka lema asigombee kwa miaka mi 5,ambapo kwa kosa lema alilohukumiwa nalo ambapo kisheria haikutakiwa kuwa hivyo.
3.uchaguzi ungerudiwa bila ya kukata rufaa ingehesabika kwamba ni kweli lema alikua na hatia
4.reason nyingine mbowe aliyoisema pale nmc ni kwamba hizi chaguzi ndogo zinaigarimu serekali na vyama vya siasa pesa nyingi sana,kwahiyo wao hawaoni sabab ya kurudia uchaguzi kwa hukumu ya kipuuzi namna ile.
CHADEMA NI CHAMA MAKINI CHENYE VIONGOZI MAKINI HAKIKURUPUKI.
 
NI zaidi ya miezi minne sasa wananchi wa Jimbo la Arusha Mjini, hawana mbunge wa kuwawakilisha katika vikao vya mikutano ya shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyo kwa majimbo karibu yote ya Tanzania Bara.

Jimbo lingine, ambalo halina mbunge kwa kipindi kama hicho, ni Sumbawanga Mjini, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, kutengua ubunge wa Khalfan Aeshi (CCM).

Aesh alitiwa hatiani na mahakama kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 uliompa ushindi.

Jimbo la Arusha Mjini, ambalo ndiyo mada yangu ya leo, halina mbunge kwa sababu kuu mbili. Ya kwanza, ni hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha. Hukumu hiyo ilitengua ubunge wa Godbless Lema (Chadema) aliyekuwa akiliwakilisha jimbo hilo bungeni tangu mwaka 2010.

Hukumu hiyo ilitolewa Aprili 5, mwaka huu, na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila, baada ya kujiridhisha kuwa Lema alitumia kashfa, kejeli na udhalilishaji katika mikutano yake ya kampeni, kinyume cha kanuni, taratibu na sheria ya maadili ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Sababu ya pili inayofanya jimbo hilo likose mbunge hadi sasa, ni rufaa iliyokatwa na Chadema kupinga hukumu hiyo ya Jaji Rwakibarila. Sheria inazuia kuitishwa uchaguzi hadi rufaa hiyo itakapoamuliwa.

Rufaa hiyo ndiyo kwanza imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Kesi iliyotengua ubunge wa Lema, ilifunguliwa na wanachama watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliodai kuwa wakati wa kampeni Lema alimdhalilisha aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian, ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania, nchini Kenya.

Baada ya hukumu ile, Lema alionekana kutokuwa na wazo kabisa la kukata rufaa. Kwani siku ileile saa chache baada ya hukumu kutolewa, alikaririwa akisema hatakata rufaa kwa kuwa hataki kuwa mbunge wa rufaa.

Msimamo huo wa Lema ulioana sawia na ule aliokuwa nao Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.

Mwigamba pamoja na mambo mengine, alikaririwa akisema haoni sababu ya kukata rufaa. Bali kujiandaa na kuingia kikamilifu katika uchaguzi wa marudio jimboni humo.

Alisema kukata rufaa ni kupoteza muda, kwani kinachotakiwa ni kujiandaa kikamilifu kuiangusha tena CCM katika uchaguzi wa marudio kwa kura nyingi tofauti na zile zilizopita.

Ni wazi kuwa kauli hiyo ya Lema inadhihirisha imani yake kwa Chadema kwamba, ina uwezo mkubwa wa kulirejesha jimbo hilo wakati wowote na saa yoyote kama atasimamishwa tena kulitetea.

Naweza kusema Lema hapo yuko sahihi. Kwamba, kwa hakika Jimbo la Arusha Mjini bado ni ngome ya Chadema. Vipo vigezo vingi vinavyoweza kuthibitisha ukweli huo.

Cha kwanza, ni matokeo halisi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 yaliyompa ushindi Lema. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa Lema alimwangusha Dk. Burian kwa kumshinda karibu kura 20,000.

Kigezo cha pili, ni mchuano mkali uliopo katika idadi ya madiwani waliovunwa na Chadema dhidi ya madiwani, ambao CCM ilipata katika uchaguzi huo katika Manispaa ya Arusha.

Katika manispaa hiyo, CCM ilipata madiwani 16, Chadema 15 na Chama cha Tanzania Labour (TLP) wawili. Takwimu hiyo ni kabla ya madiwani watano wa Chadema kuvuliwa uanachama kwa kukiuka maamuzi na maelekezo ya chama.

Kigezo cha tatu, ni mwitikio wa watu, ambao umekuwa ukionekana katika mikutano ya hadhara, maandamano na shughuli nyingine za kisiasa na kijamii zinazoandaliwa na Chadema jimboni humo.

Kigezo cha nne, ni ushindi, ambao Chadema iliupata katika uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki.

Ni ukweli usiopingika kuwa ushindi huo alioupata aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chadema, Joshua Nassari, ulichangiwa na ushawishi mkubwa wa wananachi kutoka Jimbo la Arusha Mjini.

Kigezo cha tano, ni namna mwitikio wa wananchi ulioonekana mahakamani siku ya hukumu na katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na uongozi wa Chadema mjini Arusha baada ya hukumu hiyo.

Yawezekana vigezo hivyo ndivyo vilivyomfanya Lema aamini kuwa kushindwa kwake kesi si kwa sababu chama chake nay eye mwenyewe hawaungwi mkono na wananchi. La!

Bali aliamini na kudiriki kutamka kwamba, kulitokana na shinikizo la Ikulu, madai ambayo yalinushwa vikali na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu kwamba, ni ya upuuzi na ni ukosefu mkubwa wa adabu na heshima uliofanywa na Lema kwa mahakama na serikali.

Ni wazi kuwa hatua ya Lema kukata rufaa hiyo, haikuwa ni hiari yake. Bali ilikuwa ni kutekeleza uamuzi ya chama chake. Na pengine ulitokana na kuhofia yasije yakamkuta yaliyowakuta madiwani wale watano wa Chadema.

Uamuzi wa Chadema wa kukata rufaa, ulitangazwa na Mbowe katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya NMC, mjini Arusha, Aprili 8, mwaka huu.

Mbowe alisema licha ya Chadema kuwa na uhakika wa kushinda uchaguzi katika jimbo hilo, wameshauriana na wanasheria pamoja na viongozi wenzake.

Wameona ni vema wakakata rufaa kwa sababu ya jaji kutafsiri kuwa Lema alitukana, alibagua kijinsia na aliendesha kampeni zisizo za kistaarabu, jambo ambalo alidai kuwa halikuwa kweli na halikutokea.

Hata hivyo, uamuzi wa Chadema wa kutokubali kwenda kwenye uchaguzi mdogo jimboni humo ili kumrudisha mbunge wake, bado unazua maswali!

Mosi, kauli ya Lema kwamba, hataki kuwa mbunge wa rufaa, je, ilikuwa ni ya kukurupuka?

Pili, shinikizo la Ikulu lililodaiwa na Lema kuingilia kesi yake Mahakama Kuu na kutengua ubunge wake, je, haliwezi ‘kupenya’ pia katika Mahakama ya Rufaa, ambako chama kimekimbilia huko, rufaa yake ikatupwa?

Tatu, ikiwa viongozi wakuu wa Chadema, Lema mwenyewe na wananchi, wana uhakika wa chama kushinda Arusha Mjini hata kama watasimamisha jiwe kugombea, kwanini basi wasikubali kuingia kwenye uchaguzi badala ya kupoteza muda wa rufaa?

Hapo kwenye bold! Sababu ya kukata rufaa haikuwa moja, nimeamini wewe ni Gamba; Sababu ilikuwa 1. Kuweka record sahihi ya hukumu. 2.Kupinga kubambikizwa kwa makosa ya rushwa ambayo Lema hakushitakiwa kwayo. 3. Kupinga kuzuiwa kwa Lema kushiriki uchanguzi kwa miaka mitano. 4. Kulinda Heshima ya Mahakama.

Msimamo: Chadema hatuogopi uchaguzi wowote, mahali popote, muda wowote; we have the moral authority kusimama mbele ya watanzania na kuwaomba kura!
 
Mtoa Mada uwe na uhakika kuwa wanachama wa chadema huwa tunafuatilia matamko ya viogozi wetu kwa umakini, huwezi kutudanganya. Kimsingi wananchi wa Arusha tulikuwa tunataka uchaguzi mpaka pale viongozi wetu walipo tuelimisha na tukaelewa, tunaweza kuishi bila mbunge na shughuli zitaendela kama kawaida, kwani kuwa na mbunge wa ccm ni sawa na kutokuwa na mbunge tu! Haki ni bora zaidi kuliko barabara za Lami!
 
Back
Top Bottom