CCM Mbeya mjini waijibu CHADEMA

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Jul 17, 2019
322
645
CCM MBEYA MJINI, WAIJIBU CHADEMA

Na Elius Ndabila

Wiki iliyopita Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walifanya mkutano mkubwa wa Kampeni kwenye viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya. Mkutano huo ambao ulikuwa ni wa kuomba kura kwa Mh Lisu anaye gombea Urais ulihudhuriwa na watu wengi kiasi kwamba watu wengi mitandaoni walisema CCM Mbeya itaendelea kuisoma namba.

Wakati watu wakiwa busy kujadili uwingi ule wa watu, mimi nilisema ule Umati ulikuwa ni wa kumpokea Lisu na si Sugu au madiwani wa CDM Mbeya Mjini. Nilienda mbali kwa kusema uwingi wa mahudhurio yale tutaupima na uwingi wa watu watakaompokea JPM atakapo kuja Mbeya. Nilisistiza kuwa kuwa ule mkutano haukuwa wa Sugu bali wa Lisu mgombea Urais. Na kwa tafsiri rahisi ule mkutano ulihudhuriwa na watu wa Wilaya zote. Nilisema ili tujue bado Sugu ana nguvu Mbeya aitishe mkutano wa kwake pale uwanjani ili tuone kama atapata idadi ile ya watu ambayo hata hivyo ilikuwa ndogo kuliko iliyowahi kuhudhuriwa uwanjani hapo wakati wa Dkt Slaa na Mh Lowasa.

Jana Chama cha Mapinduzi kupitia kwa mgombea wao wa Ubunge jiji la Mbeya Dkt Tulia Ackson walifanya uzinduzi kwenye uwanja huo huo ambao CHADEMA walifanyia mkutano wa Kampeni za Urais. Ukweli ni kuwa uwanja ulitapika, Uwanja ulijaa pomoni, Uwanja ulikuwa full park. Mkutano wa jana ambao ni wa Mbunge tu ulikuwa sawa kama si zaidi ya ule wa Mgombea Urais wa CDM. Ni dhahiri uwingi ule unaonyesha kuwa Mbeya wana jambo lao na wameamua kuupumzisha CDM. Idadi ile inawakumbusha CCM Mkoa wa Mbeya kuwa Mh Rais JPM atakapokuja inatakiwa mkutano ukafanyike uwanja wa Sokoine kwani kama tu Mbunge ameujaza Ruanda Nzovwe basi Rais patakuwa hapatoshi.

Wakati Dkt Tulia akifanyia mkutano wake katika eneo la wazi na Uwanjani, Mh Sugu amekuwa anavizia mikutano kwenye Vilabu na kwenda kwenye masoko. Jumatatu alifanyia mkutano wake kwenye soko la Maendeleo Iyela na Jana amefanyia kwenye soko la Isanga. Anafanya hivyo ili kuaminisha watu kuwa mikutano yake inakuwa na watu wakati watu wanakuwa kwenye shughuli zao za kibiashara.

Jana CCM walikuwa wanawasha mitambo, na hakika mitambo iliwashwa na imekubali.
 
CCM wameshindwa kujibu shida za Watanzania, CCM walikuwa busy kununua madiwani na wabunge

Wakati Magufuli anaingia madarakani sukari ilikuwa kati ya 800 na 1200 Kwa Kilo Moja. Mwaka 2016, Magufuli akaingilia Biashara ya sukari na sukari ikapanda hadi 2400.

Mwaka 2016 Magufuli alisema Matajiri wataishi kama Mashetani...alidhamiria watanzania wakose pesa, na hakusema masikini wataishi kama malaika
. Akafanya matendo makuu ya bomoa bomoa kimara bila fidia, akapora fedha za wafanyabishara za Bureu De Change, maelfu ya wafanyakazi wakakosa ajira. Mpaka leo Magufuli hajatoa riporti kwa umma kuwa ni pesa kiasi gani alichukua?

Ukiangalia mikoa Pwani, Kibaha, Chalinze, etc...Sukari ni muhimu na kipato ni kidogo.

Angalia sukari ya Malawi, Brazil, Thailand ni rahisi kuliko ya Tanzania. Why..Mfumo wa kodi ni mbovu

Burundi na Rwanda kuagiza gari ni rahisi zaidi kuliko Tanzania, wakati magari yao yanapita bandari ya Dar es salaam.

Pia ukiangalia Ngome za CCM Chalinze, Morogoro Dodoma, Shinyanga, .., nyumba za tembe ni nyingi...Gharama za ujenzi ni kubwa mno. Cementi ni ghali sana... Hakuna sababu cementi kuwa ghali sana. Maana ni mali ghafi ya hapa hapa nchini...Mfano, Mtu akiagiza Cementi Pakistani, anakuja kuuza bei chini kuliko Simba au Twiga Cementi. Bado cement ya nje kuna usafirishaji, kodi ya taifa lao na VAT ya Tanzania. Kama alivyosema Mh. Tundu Lisu, kuna tatizo TRA.
 
Endeleeni kushindana kujaza viwanja vya kampeni maana ndio siasa mlizobakiwa nazo.
 
Acha kudanganya watu wewe.

Mimi mikutano yote miwili nimehudhuria.

Tulia alikuwa na watu wachache Sana jana Jana ukilinganisha na mkutano wa wiki iliyopita wa chadema.

Mimi si mwanachama wa chama chochote ila kwa hapa Mbeya huyu mama ana wakati mgumu mno.
Huyu mama ni mzuri ila tatizo ni Jimbo analogombea.

IMG-20200909-WA0006.jpg
IMG-20200909-WA0005.jpg


Ona hii ya last week

Kiwanja ni hichohichoView attachment 1564961
 
Acha kudanganya watu wewe

Mimi mikutano yote miwili nimehudhuria.

Tulia alikuwa na watu wachache Sana Jana ukilinganisha na mkutano wa wiki iliyopita wa chadema.

Mimi si mwanachama wa chama chochote ila kwa hapa Mbeya huyu mama ana wakati mgumu mno.View attachment 1564939View attachment 1564940
Mleta mada anadhani zama hizi ni zama za Nyerere! 😁😁,nadhani amejuta huko alipo!
 
CCM wameshindwa kujibu shida za Watanzania, CCM walikuwa busy kununua madiwani na wabunge

Wakati Magufuli anaingia madarakani sukari ilikuwa kati ya 800 na 1200 Kwa Kilo Moja. Mwaka 2016, Magufuli akaingilia Biashara ya sukari na sukari ikapanda hadi 2400.

Mwaka 2016 Magufuli alisema Matajiri wataishi kama Mashetani...alidhamiria watanzania wakose pesa, na hakusema masikini wataishi kama malaika
. Akafanya matendo makuu ya bomoa bomoa kimara bila fidia, akapora fedha za wafanyabishara za Bureu De Change, maelfu ya wafanyakazi wakakosa ajira. Mpaka leo Magufuli hajatoa riporti kwa umma kuwa ni pesa kiasi gani alichukua?


Ukiangalia mikoa Pwani, Kibaha, Chalinze, etc...Sukari ni muhimu na kipato ni kidogo.

Angalia sukari ya Malawi, Brazil, Thailand ni rahisi kuliko ya Tanzania. Why..Mfumo wa kodi ni mbovu

Burundi na Rwanda kuagiza gari ni rahisi zaidi kuliko Tanzania, wakati magari yao yanapita bandari ya Dar es salaam.

Pia ukiangalia Ngome za CCM Chalinze, Morogoro Dodoma, Shinyanga, .., nyumba za tembe ni nyingi...Gharama za ujenzi ni kubwa mno. Cementi ni ghali sana... Hakuna sababu cementi kuwa ghali sana. Maana ni mali ghafi ya hapa hapa nchini...Mfano, Mtu akiagiza Cementi Pakistani, anakuja kuuza bei chini kuliko Simba au Twiga Cementi. Bado cement ya nje kuna usafirishaji, kodi ya taifa lao na VAT ya Tanzania. Kama alivyosema Mh. Tundu Lisu, kuna tatizo TRA....
Acha kupotosha takwimu sukari ilikuwa kwenye 1800 na sio bei uliyoweka
 
Back
Top Bottom