Siku chache baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Mbeya, Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson (CCM) ametoa wito kwa wakazi wa Mbeya kuacha kuhangaika na maneno ya wanasiasa wasiowatakia mema kwa kuwa wakati uliopo sasa ni wa kupelekewa maendeleo na si maneno
Dkt. Tulia ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkurugenzi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya 'Tulia Trust' amezungumza hayo Februari 23.2024 wakati wa hafla ya kukabidhi nyumba kwa Hosea Kalemali ambaye ni mmoja wa wanufaika wa nyumba tisa (9) zilizotolewa na taasisi hiyo kupitia mpango wa 'Tulia Trust na Jamii'
Kuhusu kufana kwa maandamano hayo Dkt. Tulia amesema ameshangazwa kusikia maandamano hayo yalikuwa na muitikio wa watu wengi jambo ambalo amedai si sahihi kwa kuwa wengi waliojitokeza haifahamiki wametokea wapi kwa kuwa hawafahamiki hata na wenyeji yaani wakazi wa Mbeya
Dkt. Tulia pia amekosoa kitendo cha CHADEMA kuwatembeza watu kwa miguu (waandamanaji) umbali mrefu akitolea mfano wa kutoka Mbalizi hadi uwanja wa Ruanda Nzovwe jijini Mbeya kwenda kwenye mkutano jambo ambalo amedai CCM haiwezi kufanya hivyo kwa kuwa ikiwahitaji watu hao itawatumia usafiri wa kuwafikisha kwenye eneo husika.
Credit - JamboTv
Dkt. Tulia ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkurugenzi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya 'Tulia Trust' amezungumza hayo Februari 23.2024 wakati wa hafla ya kukabidhi nyumba kwa Hosea Kalemali ambaye ni mmoja wa wanufaika wa nyumba tisa (9) zilizotolewa na taasisi hiyo kupitia mpango wa 'Tulia Trust na Jamii'
Kuhusu kufana kwa maandamano hayo Dkt. Tulia amesema ameshangazwa kusikia maandamano hayo yalikuwa na muitikio wa watu wengi jambo ambalo amedai si sahihi kwa kuwa wengi waliojitokeza haifahamiki wametokea wapi kwa kuwa hawafahamiki hata na wenyeji yaani wakazi wa Mbeya
Dkt. Tulia pia amekosoa kitendo cha CHADEMA kuwatembeza watu kwa miguu (waandamanaji) umbali mrefu akitolea mfano wa kutoka Mbalizi hadi uwanja wa Ruanda Nzovwe jijini Mbeya kwenda kwenye mkutano jambo ambalo amedai CCM haiwezi kufanya hivyo kwa kuwa ikiwahitaji watu hao itawatumia usafiri wa kuwafikisha kwenye eneo husika.
Credit - JamboTv