Asante mh. Mbowe kwa kuliona hili,huu mkoa umefanywa shamba la bibi.

Huyu jamaa hakuandaliwa kuja kuwa kiongozi na wala hana sifa za uongozi.Ninahisi hata ukarani BoT alipewa na baba mkwe ex-Governor.Ukiachilia mbali kuitumikia nchi katika maeneo tofauti na kuifahamu nchi sidhani hata kama JKT kwa mujibu wa sheria alipitia.Ukizungumzia watu wanaozunguka mlima kunufaika je wanajeshi wetu wanaolinda mipaka ya nchi usiku na mchana watalipwa nini? leo kama hakuna ulinzi wa mipaka ya nchi ambao askari wake ni wa makabila yote kutoka mikoa yote ya Tanzania kuna Mlima Kilimanjaro? Ni aibu maneno kama haya kutamkwa na mtu anaetajwa kama kiongozi na ni fedheha kwa wafuasi na wanachama wake.
 
Hapo ndipo CDM tunapochnganyana kama hii nchi ni moja na wanachi wake ni wamoja rasilimali zilizopo ni lazima zigawanywe equally.Sitegemei kabisa mtu kama Mbowe ambae tunamfahamu kwa kutema madini mdomoni mwake aje na kioja kama hiki.Au mleta mada kachakachua alichokisema? CDM ongeeni kama wamoja linapoika suala la rasilimali za kitaifa .Je ile mikoa iisiyobalikiwa rasilimali itakuwaje?Please njooni na hoja zenye mashiko wadau.
 
kwanini mimi sina haki ya kuongelea huko?Ukiongea na watu wasio wa kuzimu km avator yako,basi unapswa jifunza switch fikra very fast na kurudi kila mara mifano hai ya pande tofauti ikiletwa. Sijui switching kapability yako ina ukubwa gani ila nadhani haitoshi.Katikaeneo la ajira huitwa "flexibility".

Kaulize kwanini makampuni yana social responsibility kama corporate law and civilizations.Wewe huwa unakula futari ya vida tuu hujui ni kwanini?Serikali ndio wanachukua kodi pale kupitia taasisi ambayo ingekuwa binafsi ingekuwa kampuni na wangepaswa rudisha hela kwa jamii ya eneo lake la kazi ili kuhifadhi mazingira, kuwawezesha wanajamii, n akuwaambia ahsante.


Sometimes uombe kuelemishwa moja kwa moja bila kuansiha ubishi usiokuwa na kichwa wala miguu.

Mambo ya futari yanakujaje sasa.
 
May be tuna different backgrounds and professions. However interms of stylistics and semantics you are quite wrong. Mleta thread ametumia maneno yake kuelezea alichokisikia na Mbowe alitumia semantics kadiri ya hadhira aliyokuwa anahutubia yenye diversity-wasomi wa juu, wa kati na wasio wasomi ili waweze kumwelewa. Asingeweza kutumia sana CSR au terms zenye kufanana na hilo. However, in wide translation that's what he meant to say. Anayevuna sehemu zile anatakiwa aache siginificant contribution for development. Hapana hakuna twist. Sasa wewe unasema katika kupanda mlima hakuna kampuni inamili lakini kuna tour companies. Hizi Tour companies zinafanya kazi in the blue au zina leseni toka mamlaka husika? Je, zinalipa kodi au hazilipi? Zinazalisha au hazizalishi. Jibu ni kwamba zinazalisha la sivyo zingekuwa zishaaondoka. Malipo yanayofanywa yanaenda wapi? Jubu ni kwamba yakwenda serikali kuu na kuacha maeneo yayozunguka mlima huo kuwa hayana kitu. Hayo mapato yanayokuwa generated na tour companies must be deducted and the gains be distributed to the surrounding communities. Hii ndio CSR in the real sense of the term na sio ile ya kusubiri mwezi mtukufu na kuwaadalia watu daku, au sikukuu ya Christmas au IDD na kuwatembelea watoto wa vituoni. Hili linahitaji nguvu za kisheria ili isiwe mapaka makampuni yajisikie kutoa


alichosema ni cheap political point ambayo wewe unataka kujistify kua iko kwenye angle hii...I understand the whole concept ya CSR, na kitu hiki kinaitwa eco tourism ili kulinda mazingira na kusustain bioiversity na kuamsha maisha ya watu wa eneo husika ili wawe partners katika kutunza mazingira hayo kwa vizazi vingi vijavyo. Lakini paraphrasing Mbowe kwamba 88 bil tsh zilizotengenezwa 2010/2011 zimeenda zote Dar kwa mafisadi, hii maana yake nini?

Jibu la kimanatiki bila kuweka hisia zako binafsi au filosofia ya uelewa wako mwingine ni kwamba alikua anataka zote zibaki hai na siha (au Kilimanjaro kwa ujumla) na serikali isipate kitu kwa kuendeleza shughuli zake ikiwemo kulinda amani inayowafanya tour waoperate na watalii waje.

Tulifundishwa shule ukitaka kujua kitu kivunje vunje kwenye misingi yake ya uhalisi na utakijua tu, ukioverthink kwenye
kitu simple unakosea.Unless ur one of those romantics from the North (thinking of grandeur of that part of the country).
 
Mambo ya futari yanakujaje sasa.

teh teh unapendwa tukanwa sana...ila this time sijakutukana nilitaka kichwa ifunguke ila sijaona tofauti bado.Voda wanatoa kama sehemu ya Social responsibility kwa watu ,kwa kugawanya kwa makundi husika mojawapo likiwa Waislam na hivyo kuelekeza ktk "futari".Povu litakutoka kazi kuhesabu uovu na kutafuta uovu tuu .Ndio maana nikatumia huo mfano ili nikushike.
 
teh teh unapendwa tukanwa sana...ila this time sijakutukana nilitaka kichwa ifunguke ila sijaona tofauti bado.Voda wanatoa kama sehemu ya Social responsibility kwa watu ,kwa kugawanya kwa makundi husika mojawapo likiwa Waislam na hivyo kuelekeza ktk "futari".Povu litakutoka kazi kuhesabu uovu na kutafuta uovu tuu .Ndio maana nikatumia huo mfano ili nikushike.

Wewe jamaa kwa kweli binafsi yangu huwa sikuelewi kabisa unachoandika, kama hapa sijui unataka kusema nini.
 
Wewe jamaa kwa kweli binafsi yangu huwa sikuelewi kabisa unachoandika, kama hapa sijui unataka kusema nini.

mbona mimi nakuelewa na kukuelewesha?Uliuliza kuhusu Futari kitaka kujua nini?Kwanza sidhani kama kun amtu unamwelewa humu ndani.
 
Tangu aanze kuzunguka mikoa ya Tanzania Kilimanjaro pekee ndo ameona kivutio ambacho kinafaa kuwanufaisha wananchi wa eneo hilo? mbona sijawahi kusikia hayo kuhusu ziwa etu kule mara? Mbona sijawahi kusikia hilo kuhusu
madini ya shinyanga, Mwanza, Mara na kwingineko?
ndo ubaya wa kutohudhuria mikutano na kusimuliwa tu, au kuishi kwa kukariri. Nna uhakika hata vyombo vya habari husikilizi achilia mbali kununua gazeti ukasoma maana haya yamezungumzwa tangu 2005 kwenye uchaguzi mkuu, na raslimali zinazongumzwa ni kwa nchi nzima, changamka kidogo!
 
Huyu jamaa hakuandaliwa kuja kuwa kiongozi na wala hana sifa za uongozi.Ninahisi hata ukarani BoT alipewa na baba mkwe ex-Governor.Ukiachilia mbali kuitumikia nchi katika maeneo tofauti na kuifahamu nchi sidhani hata kama JKT kwa mujibu wa sheria alipitia.Ukizungumzia watu wanaozunguka mlima kunufaika je wanajeshi wetu wanaolinda mipaka ya nchi usiku na mchana watalipwa nini? leo kama hakuna ulinzi wa mipaka ya nchi ambao askari wake ni wa makabila yote kutoka mikoa yote ya Tanzania kuna Mlima Kilimanjaro? Ni aibu maneno kama haya kutamkwa na mtu anaetajwa kama kiongozi na ni fedheha kwa wafuasi na wanachama wake.
ni aibu kwa watu wako wa karibu na mkoa unaotoka, kama ungekuwa unatokea kwetu mi ningekukana..kwanini nasema hivyo? Askari ni wafanyakazi wa serikali na wanalipwa mishahara, kinachozungumzwa hapa ni masuala ya kimaendeleo mfano shule, barabara, hospitali na nk. Hao unaosema polisi kwa kuwa wanaishi eneo hilo moja kwa moja watafaidika na huduma zilizopo. Wenyeji maana yake ni wakazi wa hapo ikiwa na maana hata wewe kama utahamia hapo unakuwa mwenyeji haina maana kwamba wataofaidika ni kabila wenyeji wa hapo. Na hii ina faida nyingi kuliko hasara, tafakari!
 
Msiyaangalie Haya mambo katika Jicho lenye ukungu kiasi hicho na bado mnajiita Great Thinker. Jiulizeni Je ni sahihi KWA wananchi wanaouzunguka mlima Kilimanjaro kukosa Huduma muhimu za kijamii Kama shule, afya etc huko mlima waliokuwa nao miaka nenda rudi unaingiza pesa nyingi. Concept hii ni sawasawa na walio na vizimba kwenye masoko wanaotoa ushuru wa kuuza bidhaa zao pale lakini wanakosa Huduma muhimu za choo, vile vile mazingira yanaowazunguka yakiwa machafu hayatamaniki. Je na hao wasiombe japo kiasi fulani cha ushuru wanaolipa ubakie KWA ajili ya kuboresha mazingira ya soko KWA kuogopa wataitwa WABAGUZI?

Simple and good explanation, labda kwa kutumia mfano huu wa vizimba na vyoo vya soko tutaelewana
 
The government is too central. Thats the end of the story. I get the point of the kili people and it may owe to the fact that they are much into the private sector thats why they dont depend/want the central govt to micromanage e'thing from Dar. In America CDM would be likened to
--the republicans in that they need a limited government that is not so central as it is now and :
--on the other side be likened to the left democrats in that they want more taxation and wellfare programs to help the poor.
(kumbuka cdm ni wa mrengo wa kati)

the whole tz government is run in pretty much the same way ccm people tend to mock here. Mps are chosen from their respective regions (sijawahi ona ccm wanampeleka mbunge asiye mzawa katika jimbo lolote unadhani ni kwa nini? n naturally ndio maana tuna majimbo ya uchaguzi on the first place) the problem starts when these 'our guys' go to mind the 'central government businesses' they become so heavily involved with the central beuracracies(maana ndo madili yako huko) that they can't quite represent the people who chose them on the first place. [ sie tunakuchagua utuwailishe sie on the first place au sio? na ukishindwa tutakuwajibisha!]. Wakati wa mwalimu uwaziri haukuwa dili.

Sasa hapo mbowe ni mbunge wa hai wilaya iliyoko kili au sio? Afanyeje? Ndio maana ccm wakiona unapiga sana kelele kuwakilisha wanakupa uwaziri. ITS MESSY!! MESSY!!

CDM endeleeni kuwabana hawa jamaa kwa sera zao mbovu. Ukiona wao nagomba ujue mepatia!!!!!
 
Hapo sasa na sera za Nchi kujigawa kwa ukanda na majimbo ndo zinaponipa wasiwasi tunakokwenda kubaya kwa kweli.
Hapo ndipo CDM tunapochnganyana kama hii nchi ni moja na wanachi wake ni wamoja rasilimali zilizopo ni lazima zigawanywe equally.Sitegemei kabisa mtu kama Mbowe ambae tunamfahamu kwa kutema madini mdomoni mwake aje na kioja kama hiki.Au mleta mada kachakachua alichokisema? CDM ongeeni kama wamoja linapoika suala la rasilimali za kitaifa .Je ile mikoa iisiyobalikiwa rasilimali itakuwaje?Please njooni na hoja zenye mashiko wadau.
 
Mh.mbowe upo sahihi kabisa,haiwezekani kila mwaka tunasikia mapato m/kilimanjaro yamepanda halafu wazawa wa pale hawanufaiki.
 
Nadhani kuna haja ya kujitahidi kulielezea zaidi jambo hili maana naona limeeeleweka sivyo.
Kwanza hapa hakuna maswala ya ukanda alivyomaanisha ni kuwa sehemu zote za nchi zenye raslimali kuhimu lazima zimilikiwe kwanza na wakazi. The local Authorites should take ownership of the available resources. Bila hivyo hakuna atakayejua upotevu na matumizi mabaya yanayotokea pale.

Nchi nzima kila sehemu ina raslimali muhimu kabisa ni kasi cha kuthubutu tu, Mungu ametupa nchi tajiri sana.

Halafu si kweli kwamba amemaanisha kuwa serikalini kusiende chochote. Ila kinachobakia sehemu zenye hizo raslimali hakitoshelezi wananchi hata kuwezesha wananchi wa eneo kuwajibika kuilinda.

Kingine ambacho pia ni muhimu sana, huenda watu wengi hawafahamu kuwa ule mlima mpaka sasa ukichunguza vizuri sana wanaofaidika zaidi na huo mlima ni waKenya. Ukibahatika kuwa Nairobi kwa muda na ukaangalia jinsi watalii wanavyosafiri ndiyo utaelewa. Kwanza wanaona kama Tanzania hakuna maisha mazuri, miundo mbinu na huduma kwa ujumla ni duni. Hata wakaipata janga au kuugua kwa bahati mbaya ni lazima wakimbilie Nairobi.
Wakishamaliza kutembelea sehemu za vivutio Tanzania wanarudi haraka sana Nairobi kuja sasa kupumzika, na ndipo wanapotumia fedha zao zaidi. Kwa kifupi mtalii akiwa amebajeti $10,000 kuja kutembea kuona Ngorongoro, serengeti nk. anhakikisha ametumia kiasi kidogo sana huku kwetu say $1500 tu the rest anatumia awapo Kenya. Nimekaa Nairobi kwa muda na nililiona hilo.
Kwahiyo kama wananchi wa maeneo watawezeshwa zaidi wakaendeleza na kuwekeza ipasavyo kule Ngorongoro, Serengeti, Mikumi, Selous nk. basi huenda wangevutiwa kukaa zaidi na wangejisikia comfortable.

Wanaodhani ni mambo ya ukanda nawashangaa sana maana wapo watu wa kutoka sehemu zote za Tanzania wanaishi Moshi na kufanya biashara aina zote pale, hakuna anayekatazwa kwa kuwa ametoka kusini au magharibi mwa nchi nadhani ndivyo ilivyo hata sehemu nyingine zenye raslimali kama hizo.

Nadhani inabidi kuangalia kauli hii kwa mapana zaidi. Ukichukulia kuwa ni mbunge wa kichaga kaongea hivyo kwa ajili ya wachaga wenzake unaweza usinufaike na wazo. Lakini ukipenda kuliangalia na kulikuza wazo lake ili liweze kunufaisha Taifa basi unaweza kuliboresha na likapata picha halisi iliyokusudiwa.

Nina hakika wananchi wa eneo walimochukuliwa wale Twiga kinyemela na kurushwa kwa ndege kwenda Arabuni, kama wananchi wa eneo lile wangekuwa wanajua kuwa wale wanyama wanamanufaa gani kwao na wameachiwa dhamana ya kuwalinda, asingechukuliwa hata mmoja.

Mfumo wetu wa kiutawala ni mbovu sana maana huwa tunaiga bila kujiandaa vizuri na kuelewa vitu sawasawa. Mfumo wa kila kitu kuendeshwa na Central Government kidogo uwashinde hata wa China, lakini walipoona mambo yanataka kwenda mrama ndipo walipoanza kupiga watu risasi hadharani. Je waTZ tuna huo ujasiri? Maana leo waliohusika na ununuzi wa Rada, EPA, Wanayama kutoroshwa, MEREMETA, Richmond nk. wangekuwa wamechoka. Lakini Tanzania yetu waziri Mkuu anawaonya wananchi kupitia Bunge kuwa waliohujumu nchi wakiguswa nchi itatikisika.
 
Back
Top Bottom