Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,989
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Katavi kimejipanga kutekeleza kufanya maandamano ya amani yanayotarajiwa kufanyika Januari 24, 2024.
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Katavi, Roda Kunchela ameyasema hayo akiwa katika ofisi ya chama hicho mkoani humo ambapo amesema agiza la Mwenyekiti Taifa, Freeman Mbowe la kufanya maandamano ya amani nchi zima ni tamko la Kikatiba katika mstakabali wa kudai haki ya maoni ya Wananchi.
Roda amewaomba Wananchi wa Katavi kushiriki ipasavyo katika maandamano ya amani yatakayofanyika tarehe Januari 24, 2024.
Elizabeth Kasela ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana katika Chama hicho Mkoa wa Katavi amewaomba vijana kujitokeza katika kutekeleza maandamano ya amani huku Wanawake na wazee wakiombwa kujitokeza siku ya maandamano ya amani.
Roda amewaomba Wananchi wa Katavi kushiriki ipasavyo katika maandamano ya amani yatakayofanyika tarehe Januari 24, 2024.
Elizabeth Kasela ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana katika Chama hicho Mkoa wa Katavi amewaomba vijana kujitokeza katika kutekeleza maandamano ya amani huku Wanawake na wazee wakiombwa kujitokeza siku ya maandamano ya amani.