Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Rais kwa kawaida ndiye kiongozi hasa anayetazamwa kudumisha amani katika nchi yoyote ile. Kwa Bahati mbaya rais kikwete na CCM wanaonekana kuwa ndio watakuwa wakwanza kuvuruga amani nchini tanzania, sababu ni kwamba
1. Kuna viongozi wengi ambao wameshutumiwa kwenye mambo ya kifisadi ambao mpaka wangekuwa wameshahukumiwa. Kwani mali nyingi za umma zinaibiwa lakini kiongozi wetu ndio kama kinga yao, hasa ukizingatia menono ya Edward Hosea yaliyonukuliwa na Wikileaks. Ni wazi kwamba, Rostam Aziz, Edward Lowassa, Benjamin Mkapa, Karamagi, Ridhiwani Kikwete, Manji Yusuf, Yusuf Makamba na wengine wengi tu ndio vinara wakubwa wa ufisadi pamoja na Kikwete mwenyewe, lakini kama kawaida yake na upuuzi, anaendelea kupuuzia
2. Rais mwenyewe anahusishwa na mambo mengi ya kifisadi pamoja na familia yake. Watoto wake na marafiki zake wamekuwa kama ndio viongozi wa nchi, wakikuchukia ni umekiwsha. Wanawake zake wanagawiwa nyadhifa kama pipi ilhali vijana wengi wenye uwezo wa kufanya hizo kazi wanatembea na vyeti mikononi mwao wakitafuta ajira zisizopatikana
3. Rais Kikwete amekuwa mfujaji mali zetu namba moja. Safari zake za kipuuzi nje ya nchi haziishi, kila kukicha anasafiri na mabillioni ya kodi zetu, kazi ambazo zingefanya na wasaidizi wake hasa waziri wa mbambo ya nje. Serikali ya Kikwete kwa ujumla imekuwa ikifuja pesa zetu kwa anasa za hali ya juu. Familia yake mkewe na watoto wanafanya kila watakalo, wanadiriki hadi kuingia kwenye utawala na uongozi wa nchi, kitu ambacho inatokea katika nchi zinazoongozwa na wafalme na madikteta
Wananchi wanapochoka na utawala wa kihimla, wanakuwa hawana namna tena. Wanafikia hatua ya kuchukua madaraka mikononi mwao, na hapo ni kumlazimisha kiongozi kuondoka madarakani. Rais anapokataa kuwasikiliza, basi machafuko mtindo mmoja. Kikwete ameombwa na CCM yake kushugulikia ufisadi, kuhacha uonevu, lakini nikama vileanawaona wananchi kama wapuuzi. Watanzania wenzangu, atakayechafua amani nchini Tanzania siyo mwingine bali rais Kikwete
Tunamuomba ajiuzulu ili kulinda amani Tanzania. Lasivyo wananchi watamg'oa na hatima yake haitakuwa nzuri na familia yake
1. Kuna viongozi wengi ambao wameshutumiwa kwenye mambo ya kifisadi ambao mpaka wangekuwa wameshahukumiwa. Kwani mali nyingi za umma zinaibiwa lakini kiongozi wetu ndio kama kinga yao, hasa ukizingatia menono ya Edward Hosea yaliyonukuliwa na Wikileaks. Ni wazi kwamba, Rostam Aziz, Edward Lowassa, Benjamin Mkapa, Karamagi, Ridhiwani Kikwete, Manji Yusuf, Yusuf Makamba na wengine wengi tu ndio vinara wakubwa wa ufisadi pamoja na Kikwete mwenyewe, lakini kama kawaida yake na upuuzi, anaendelea kupuuzia
2. Rais mwenyewe anahusishwa na mambo mengi ya kifisadi pamoja na familia yake. Watoto wake na marafiki zake wamekuwa kama ndio viongozi wa nchi, wakikuchukia ni umekiwsha. Wanawake zake wanagawiwa nyadhifa kama pipi ilhali vijana wengi wenye uwezo wa kufanya hizo kazi wanatembea na vyeti mikononi mwao wakitafuta ajira zisizopatikana
3. Rais Kikwete amekuwa mfujaji mali zetu namba moja. Safari zake za kipuuzi nje ya nchi haziishi, kila kukicha anasafiri na mabillioni ya kodi zetu, kazi ambazo zingefanya na wasaidizi wake hasa waziri wa mbambo ya nje. Serikali ya Kikwete kwa ujumla imekuwa ikifuja pesa zetu kwa anasa za hali ya juu. Familia yake mkewe na watoto wanafanya kila watakalo, wanadiriki hadi kuingia kwenye utawala na uongozi wa nchi, kitu ambacho inatokea katika nchi zinazoongozwa na wafalme na madikteta
Wananchi wanapochoka na utawala wa kihimla, wanakuwa hawana namna tena. Wanafikia hatua ya kuchukua madaraka mikononi mwao, na hapo ni kumlazimisha kiongozi kuondoka madarakani. Rais anapokataa kuwasikiliza, basi machafuko mtindo mmoja. Kikwete ameombwa na CCM yake kushugulikia ufisadi, kuhacha uonevu, lakini nikama vileanawaona wananchi kama wapuuzi. Watanzania wenzangu, atakayechafua amani nchini Tanzania siyo mwingine bali rais Kikwete
Tunamuomba ajiuzulu ili kulinda amani Tanzania. Lasivyo wananchi watamg'oa na hatima yake haitakuwa nzuri na familia yake