Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

hatuwezi wote kuwa polotician ila ni wajibu wetu wote kuleta maendeleo. Siku moja niliwaza kwanini James Carville au Paul Begala Wasigombee urais wenyewe badala yake wanampa akili zao zote president Clinton au Karl Christian Rove asingekuwa yeye president badala ya Bush kwa mtizamo wangu huyu jamaa ni ten time clever than bush pia David Axelrod badala ya obama mzee wa teleprompter guess who is writing.

Jibu nililolipata ni kwamba si lazima wote tungombee uraisi au ubunge bali nijukumu letu wote kuhakikisha kile tunachoamini kinafanikiwa (kwa watu wa kyela ni shule, maji afya na watu kuacha uvivu).

Badala ya kumchukia mbunge wako na kutaka ukagombee wewe (ni haki yako) akikisha amepewa muda wa kutosha kutekeleza majukumu, Ili miaka mitano( bila kumchomolea tairi za gari hakuna uchaguzi mwingine) ingalau kitu kifanyike ukimkwamisha kabisa kwanza miaka mitano inakwenda bure na pili huna uhakika wa kufanikiwa na tatu unkuwa umetesa maelfu kwa ubisfsi wako.

Mbunge wetu angefanya mambo mengi na makubwa sana kama watu wangetofautisha muda wa kampeni na muda wa kufanya kazi. sasa hata asipo deliver ana sababu kubwa ya kutuambia. Na uchaguzi wa kyela hautakuwa wa issues hata siku moja bali utakuwa wa events tu. Tutasikia hata siku moja kura zikiombwa kwa "nimeleta maji kwa vijiji 4 kata ya saba nipeni muda nimalizie vilivyobaki " bali itakuwa "mimi ninaungwa mkono na raisi"
Acha propaganda zako, mtu kuandika hapa JF atamkwamisha vipi mbunge ku deliver? kwahiyo JK akishindwa ahadi zake ni kwasababu anaandamwa JF? Kuandamwa ndiko kunaweza kuwa chachu ya kukufanya uongeze juhudi na sio vinginevyo.

Mbona Dr. Slaa kazungukwa na CCM kila upande na anachapa kazi?

Acha kutafuta scapegoats wa kila failure, haikusaidi wewe wala haimsaidii huyo mbunge wako. Kama watu wamechomoa tyre ya gari lake toa ushahidi, vinginevyo unakuwa kama Yahaya Hussein.

Hakuna aliyemkwamisha mbunge kufanya kazi zake Kyela; kama unaamini hilo basi akina Zitto wasingefanya kazi yoyote kule kwenye majimbo yao.

Mkuu usipotoshe watu; tuna mifano mingi tu ya kuonyesha kwamba anayekwamisha maendeleo ni yeye mwenyewe kwa hofu ya kwamba kila anayefanya jambo la maana Kyela anataka kumwondoa kwenye ubunge. Tulimwunganisha hata na watu wa kusaidia baadhi ya mambo Kyela lakini hata siku ya appointment hatokei; watu tukapata aibu kweli kweli; mtu kama huyo utamsaidia vipi?

Kweli sio kila mtu anaweza kuwa mwanasiasa na sio kila mwanasiasa anaweza ku deliver na ndio maana kuna uchaguzi kila baada ya miaka mitano ili wale walioshindwa kazi kuwe na njia ya kuwaondoa. Hata ningetaka kugombea ubunge ni haki ya raia yeyote wala haiwezi kumfanya mbunge aliyepo ashindwe kufanya kazi.

Kama mtu anashindwa ku deliver ni kwasababu hana uwezo; mengine yote ni visingizio tu.
 
Wakuu Fataki na, Kapela na Shalom; Nilisimama kwa muda mrefu kuchangia mijadala ya kyela baada ya kubaini hicho mlichokibainisha, kwamba watu wako kwenye kampeni hapa JF. Hutumia kila fursa wanayoipata kuingiza kampeni hata kwenye hoja isiyohusiana na siasa za Kyela.

Hebu angalia mjadala wa ajali ya Dr Mwakyembe ulivyobadilishwa na kina Mtanzania na engineer, kutoka ajali umehamishiwa kwenye personal attacks zao kwa dk. na katika kuzugu eti kyela kwenye matatizo wanakuwa pamoja, unafiki mtupu.

Ushauri mliowapa ni mzuri sana waende kyela wakajinadi, kwa nini wanaogopa kuwakabili wananchi kisha wanakimbilia hapa JF kuendesha kampeni zao za ubunge wa kyela, inachosha sana kwa kweli.

Utawatambua tu hapa JF, wakiguswa hawasiti kuwatukana wanaowapinga hapa na kukimbilia kudai kwamba hao wanaowapinga kutokana na fitina na uongo wao hawazijui siasa za kyela, bali ni wao tu ndio wanaozifahamu siasa za huko.

Kwa mtazamo wao huyo mbunge wao hana alichofanya, kwamba anakwamisha hata uwekezaji wilayani Kyela kwa kuwazuia wenye nia hiyo!

Jamani kwa ambaye hajafika kyela hebu ajaribu kutembelea wilaya hiyo, alinganishe na maeneo mengine nchini kisha atupe tathmini yake, naamini kwa kufanya hivyo tutapata maelezo yaliyo sahihi, lakini kupitia hawa kina Mtanzania tutaendela kulishwa pumba tu hapa.
 
Wakuu Fataki na, Kapela na Shalom; Nilisimama kwa muda mrefu kuchangia mijadala ya kyela baada ya kubaini hicho mlichokibainisha, kwamba watu wako kwenye kampeni hapa JF. Hutumia kila fursa wanayoipata kuingiza kampeni hata kwenye hoja isiyohusiana na siasa za Kyela.

Hebu angalia mjadala wa ajali ya Dr Mwakyembe ulivyobadilishwa na kina Mtanzania na engineer, kutoka ajali umehamishiwa kwenye personal attacks zao kwa dk. na katika kuzugu eti kyela kwenye matatizo wanakuwa pamoja, unafiki mtupu.

Ushauri mliowapa ni mzuri sana waende kyela wakajinadi, kwa nini wanaogopa kuwakabili wananchi kisha wanakimbilia hapa JF kuendesha kampeni zao za ubunge wa kyela, inachosha sana kwa kweli.

Utawatambua tu hapa JF, wakiguswa hawasiti kuwatukana wanaowapinga hapa na kukimbilia kudai kwamba hao wanaowapinga kutokana na fitina na uongo wao hawazijui siasa za kyela, bali ni wao tu ndio wanaozifahamu siasa za huko.

Kwa mtazamo wao huyo mbunge wao hana alichofanya, kwamba anakwamisha hata uwekezaji wilayani Kyela kwa kuwazuia wenye nia hiyo!

Jamani kwa ambaye hajafika kyela hebu ajaribu kutembelea wilaya hiyo, alinganishe na maeneo mengine nchini kisha atupe tathmini yake, naamini kwa kufanya hivyo tutapata maelezo yaliyo sahihi, lakini kupitia hawa kina Mtanzania tutaendela kulishwa pumba tu hapa.

Kwi kwi kwi!!! wanaogopa kuwakabili wananchi? Na wewe hapa JF unafanya nini? Wengine tuko kwenye vijiwe kabla hata Mwakyembe hajawa mbunge labda mkilielewa hilo mtajua kwamba huwezi kuzuia watu wasijadili.

Kama ni uchaguzi ni 2010 wanaotaka watagombea na sisi tunaoandika JF tutaendelea kuandika.

Ya Kyela hamuwezi kuyaficha maana data zote tunazo. Hata hao vijana mnaowakwamisha tunawajua. Tutaendelea kuwafichua wanafiki bila kuogopa kelele zenu.

Kama mnataka kuchangia ya kwetu, changieni tu na mko huru; leteni data lakini hili la kutafuta motives za watu halitawasaidia.

Kama mbunge wenu ni popular, mna haja gani ya kuogopa watu kama sisi? msubirini na ushindi wa kishindo 2010.

Wewe ondoka rudi utatukuta tupo tu; ukipata kichefuchefu katapike na rudi tuendelee kumkoma nyani giladi.
 
Jiulize waliomwunga mkono Mwakyembe 2005 wako wapi? kwanini anakosana na kila mtu anayekaribiana naye?
Kwa sababu attitude yake toward people ina stinki.

Hata kama polisi wamekukera namna gani huwezi kutamka eti the whole of police force in Tanzania hakuna anaejua kuchambua mambo/sheria kuliko wewe. Hiyo sio kauli ya kiongozi. Hata uwe umesoma namna gani haipendezi kutoa written statement unasema polisi wamekuja ``kupiga ramli`` eneo la ajali.

Kumbe ndo maana hata NBC aligombana na wenzake akatimka. Attitude yake ina stinki. Hata ukimsiliza alipokuwa anaongea na waandishi wa habari, anawachagua wenye shahada eti ndio watamuelewa, anasema ``mimi nimesoma sana bwana.`` Mara akasema Bungeni anasikita wanasheria wanakaa Gongo la Mboto, na Kwa Mfuga Mbwa Manzese. Kama vile kule hawaishi binadamu. Amejaa dhihaka na dharau.

Nadhani yule Mwandosya ambae hapayuki payuki majisifa yake ovyo ndio watu wanamuheshimu zaidi.
 
Mkuu Mtanzania,

Usidangaye watu kwa kujifanya unaielewa zaidi kyela kuliko mtu mwingine, tunafahamu kila kiunachoendelea ndio maana tunakwambia nenda kajiuze kwa wananchi kwani hao ndio wapiga kura wao sio sisi hapa JF.

Nakutakia kila la heri, kwani uzuri wa kyela huwa hawana mtu wa kudumu pale!!!!!!
 
Nadhani yule Mwandosya ambae hapayuki payuki majisifa yake ovyo ndio watu wanamuheshimu zaidi.
Dilunga,

Huko nyuma wengine tulikuwa tunaandamwa hapa JF kwamba ni watu wa prof. Mwandosya au tunashabikia ukabila. Jamaa ni makini ndio maana wengine tulijitolea kuwa wapiga debe bila kuombwa.

Kama kulikuwa na mpango wa kumdhibiti mtu Mbeya basi angekuwa ni profesa. Lakini yeye anachanganyikana na watu wote; umesikia hata siku moja kuna mtu anamwandika vibaya?

Huo ndio usomi wa kweli ambao wengine tunauunga mkono; usomi wa kuelewa jamii zetu na kuwa tayari kuzisaidia.

Dr. Mwakyembe angeiga tabia za kakake Mwandosya na ambaye ni mtu wake wa karibu; hii migogoro ya kila siku Kyela isingelikuwepo au ingepungua sana. Mbona hatuoni malumbano kati ya Mwakipesile na Mwandosya wakati watu wanaamini RC aliachwa pale ili kumdhibiti profesa?
 
Mkuu Mtanzania,

Usidangaye watu kwa kujifanya unaielewa zaidi kyela kuliko mtu mwingine, tunafahamu kila kiunachoendelea ndio maana tunakwambia nenda kajiuze kwa wananchi kwani hao ndio wapiga kura wao sio sisi hapa JF.

Nakutakia kila la heri, kwani uzuri wa kyela huwa hawana mtu wa kudumu pale!!!!!!

Mkuu Nsesi,

Nikisema ninaielewa Kyela kuliko mtu mwingine yeyote nitakuwa nakudanganya na hakuna mahali niliposema hivyo. Ila naelewa mambo ya Kyela hilo halina swali.

Nakubaliana na wewe Kyela hawana mtu wa kudumu; ukivurunda unatolewa! Hilo naamini ni jambo zuri, ingefaa nchi nzima iwe hivyo.

Nikitaka kwenda kujiuza sitasubiri nitumwe na Nsesi; siku nikitaka na muda muafaka ukifika basi nitaenda mwenyewe. kwasasa naona ni bora niendelee kubeba boksi zangu na kuchangia maendeleo ya Kyela kwa njia zingine.
 
Badala ya kumchukia mbunge wako na kutaka ukagombee wewe (ni haki yako) akikisha amepewa muda wa kutosha kutekeleza majukumu, Ili miaka mitano( bila kumchomolea tairi za gari hakuna uchaguzi mwingine) ingalau kitu kifanyike ukimkwamisha kabisa kwanza miaka mitano inakwenda bure na pili huna uhakika wa kufanikiwa na tatu unkuwa umetesa maelfu kwa ubisfsi wako.

Mbunge wetu angefanya mambo mengi na makubwa sana kama watu wangetofautisha muda wa kampeni na muda wa kufanya kazi. sasa hata asipo deliver ana sababu kubwa ya kutuambia. Na uchaguzi wa kyela hautakuwa wa issues hata siku moja bali utakuwa wa events tu. Tutasikia hata siku moja kura zikiombwa kwa "nimeleta maji kwa vijiji 4 kata ya saba nipeni muda nimalizie vilivyobaki " bali itakuwa "mimi ninaungwa mkono na raisi"

Shalom,
kumbe wee mbishi kama dagaa. Umeanza kwa point nzuri sana ila unapomalizia duu. Niliandika juzi kuwa mwanaume wa kweli utamfahamu anapomaliza, ila ujumbe ukafutwa. Maliziaji zako huwa zinaniacha hoi.

Sasa hapa unataka kusema nini? Kuwa JF ndiyo ilimchomolea matairi ili afe? Kuwa JF ndiyo ilimwambia dereva wake aende speed ya 140km/hr kwa barabara za Tanzania? Hata Ulaya hizo barabara ziko chache sana na zimewekewa uzio. Kuwa ni JF imemwambia awe anagombana na watu? Kuwa JF ndiyo ilimchagua hadi awe anaisikiliza JF? JF ikimsifia au ikimlaani, inauhusiano gani na wana-Kyela? Au Kyela ni part ya JF? JF ikisimama unataka kusema kuwa Kyela imesimama? Unafikiri mwakani Mwakyembe atakuja hapa JF kujitetea na kuomba kura au ataenda Kyela kwenda kusulubiwa? JF ni kelele za chura tu na kioo cha jamii. Ukiona wafagiliwa hapa kama Dr. Slaa (ingawa naye wapinzani wapo pia) basi ujuwe unafanya kazi vizuri.

Amini usiamini hata mie mwanzo nilikuwa MPINZANI mkubwa wa Mtanzania hasa linapokuja swala la Dr. Nilipigwa datas na sikuamini sana. Zilipoanza vurugu za Kyela hadi watu kupigwa, bado kuna watu walimpinga Engineer na kesho yake, habari hizohzo zikaandikwa magazetini. Hapo ukweli wotee aliokuwa akiusema Mtanzania ukaanikwa juani.

Sasa nyie ni kipi hadi leo mmekisema kuonyesha kuwa Mtanzania au Engineer walidanganya? Juzi umepigwa DATAS za shule hadi umekimbia na ukweli juu yako sasa tunaufahamu ingawa habari zilifutwa. Leo unalialia eti Mods wazirudishe ingawa moyoni unaombea zifutwe kabisa ili AIBU usiipate.

Kubali tu UMEISHIWA na kama ni ngumi, basi umepata GUMI LA KWENYE INI, umehesabiwa hadi 10, mchezo kwisha na ini haliumi tena. Ila sasa unaamka na kusema "niachieni, niko fit sana, niachieni niko fit. Watu weweeee ahhhh!!!!

Shalom, time to move one with new datas.

Eti Mwakyembe hawezi fanya kazi kisa JF/Mtanzania na wapambe wake wanamwandama. Yaani unaweza kwenda LOW Kiasi hicho?
 
Dilunga,

Huko nyuma wengine tulikuwa tunaandamwa hapa JF kwamba ni watu wa prof. Mwandosya au tunashabikia ukabila. Jamaa ni makini ndio maana wengine tulijitolea kuwa wapiga debe bila kuombwa.

Kama kulikuwa na mpango wa kumdhibiti mtu Mbeya basi angekuwa ni profesa. Lakini yeye anachanganyikana na watu wote; umesikia hata siku moja kuna mtu anamwandika vibaya?

Huo ndio usomi wa kweli ambao wengine tunauunga mkono; usomi wa kuelewa jamii zetu na kuwa tayari kuzisaidia.

Dr. Mwakyembe angeiga tabia za kakake Mwandosya na ambaye ni mtu wake wa karibu; hii migogoro ya kila siku Kyela isingelikuwepo au ingepungua sana. Mbona hatuoni malumbano kati ya Mwakipesile na Mwandosya wakati watu wanaamini RC aliachwa pale ili kumdhibiti profesa?

Mtanzania rudi nyumbani, usiongelee mambo ya Tz kutoka Uingereza! Ndo maana unaongea utumbo. Mwakipesile hawezi kulumbana na Mwandosya kwa kuwa aliyemwondoa Mwakipesile Kyela si Mwandosya ni Mwakyembe! Simple! Inashangaza kuwa hulielewi hilo halafu unalilia ubunge Kyela through JF!
 
Mtanzania rudi nyumbani, usiongelee mambo ya Tz kutoka Uingereza! Ndo maana unaongea utumbo. Mwakipesile hawezi kulumbana na Mwandosya kwa kuwa aliyemwondoa Mwakipesile Kyela si Mwandosya ni Mwakyembe! Simple! Inashangaza kuwa hulielewi hilo halafu unalilia ubunge Kyela through JF!

Kwa taarifa yako leo niko Kyela. Kama unataka kuja kuniona unakaribishwa.

Hivi unayeongelea mambo ya Kyela ukiwa Dar, je unaona ni sawa! Au mtu akiwa nje tu ndio hawezi kuongelea mambo ya TZ? Mawazo mufilisi hayo!

Hilo la RC hiyo ni tafsiri yako; tafsiri ya wengi ni kwamba alipewa kuwa RC ili kumkabili Mwandosya. Kama ni kweli mbona hata siku moja hatujaona wakilumbana na Mwandosya?
 
Kama kweli Mtanzania unahamu ya ubunge Kyela, basi mwaga dataz zako hapa tuone kama unaviweza viatu vya shujaa Mwakyembe. Hilo brother wetu au dada yetu Mtanzania unayeishi Uingereza huwezi kulikwepa: Mwakyembe is a house-hold name in Tanzania whether you or RC Mwakipesile likes it or not! Lete dataz hapa tukuone na tukupe support au tukutose mapema uokoe fedha zako hizo unazozisotea Uingereza kwenye baridi na maisha magumu! Ikiwa CV yako ni ya ki-Nchimbi Nchimbi na doctorate za vyuo feki, count me out! Vilevile kama uko Uingereza na unaosha dishes mahotelini ili kusurvive na kuwekeza huku nyumbani, vilevile count me out!
 
Zito na Slaa wanasapoti kubwa kwenye vyama vyao na inawasaidia. lakini karatu pamoja na slaa waliweza kuweka mfumo mzuri sana wa wa maji lakini aliyekuja kuuharibu unajua nani ndugu yenu babu jinga(muulize mtikira) akahakikisha ameharibu kabisa kile kitu na sijui kama wameweza kuinuka. hivyo ni kwamba chama chako kina uwezo mkubwa wa kuharibu maendeleo ya sehemu kama hawamtaki mtu.

Tofauti iko kubwa sana kati ya wananchi anakotoka Dr slaa na zitto na huko unakotaka kwenda kugombea umbunge. wanacnhi wa karatu na kigoma usiwafananishe na sisi watu wa kyela ingekuwa kyela ni karatu wasingepokea hivyo vizadi vyako wangekuambia kuwa sisi sio omba omba bali ni watu tunaotaka maisha ya uhakika. tafadhali pamoja na mimi kuwa mnyakyusa lakini wenzetu hao wametuacha kwa kujiamini na kufanya wanacho amini na ndio maana wabunge wao wanaweza kuwaletea maisha.

Na mfano umetoa wewe mwenyewe kuhusu huyo ndugu yako mwezi wa kumi na mbili yuko kwenye kampeni za mwakyembe na ndiyo mtu wa mbele, mwezi wa kwanza mwakipesile anaukwaa ukuu wa mkoa kaenda kuomba msamaha( wewe unaita alikwenda kutaka yaishe)- Huyu ndiyo tyipical mnyakyusa- mambo ya kujiuliza

i. Alipokuwa kambi ya ya mwakyembe laikwenda kwa maslahi fulani au itikadi fulani ilimsukuma ya kutaka mabadiliko
ii. kwa nini alienda kuomba msamaha baada ya mwakipesile kupata ukuu wa mkoa na siyo baada ya uchaguzi kwisha
iii. na mwandosya aliyekuwa anamfanyiakampeni ashindwe uchaguzi na yule kjana naye anadharaukama za dokta

Mbona husemi aliyosema baba yake mwanjala baada ya dokta kwenda kushtaki siku alipokwenda kama hujui baba yake alisema hivi nanukuu " nasikia wewe na mwenzio Mwaka..... mnataka kugombea ubunge? ndiyo baba akajibu baba yake akasema " ukamwambie na mwenzio kuwa hatuwataki pelekeni matumbo yenu huko huko" huyu ni baba mzazi anayesema hivyo ( kama unabisha mpigie simu umuulize) na jamaa tangia siku hiyo ni mpole. Siku ya msiba kwa dokta alikuwa naahangaika wenziwe wametulia tu yanini sasa saiku zote fanya kitu unachojiamini nacho siyo kuiga.
Jiulize waliomwunga mkono Mwakyembe 2005 wako wapi? kwanini anakosana na kila mtu anayekaribiana naye -
ndiyo wale waliotaka kuandamana kumpongeaza wakati wa richmond na mkafanya kila njia na babu yako lisitokee.
Hayo ya kwamba jamaa analalamika kwasababu ya mashemeji ni kwenda chini kwa mtu kama wewe kuamini hivyo. Tafuta simu ya Mwanjala na ongea naye na upate upande wa pili wa shilingi, hata mimi naweza kukupatia ukiitaka.
mimi nimesikia kutoka kwenye modo wake akitoa hiyo sababu sasa wewe unadai nimuulize tena unashangaza simu simpigii namfuta stereo au mandela nikimtaka ni rafiki yangu na ndugu yangu pia
At last hata wana Kyela walio wengi wameshagundua tatizo liko wapi na watatoa hukumu yao 2010.
- hiyo haitamaanisha kuwa akishindwa ni kwa sababu ya sababu zako wangapi wazuri wameshindwa? rwakatare. njelu na wengi tu.
 
Kwa taarifa yako leo niko Kyela. Kama unataka kuja kuniona unakaribishwa.

Hivi unayeongelea mambo ya Kyela ukiwa Dar, je unaona ni sawa! Au mtu akiwa nje tu ndio hawezi kuongelea mambo ya TZ? Mawazo mufilisi hayo!

Hilo la RC hiyo ni tafsiri yako; tafsiri ya wengi ni kwamba alipewa kuwa RC ili kumkabili Mwandosya. Kama ni kweli mbona hata siku moja hatujaona wakilumbana na Mwandosya?

Mkuu, wewe si mwanasiasa, una jazba na huna subra. Ungelikuwa Kyela leo hii, usingekuwa busy toka ahsubuhi hadi jioni kwenye JF badala ya kutembelea vijiji ujulikane angalau kidogo! Pili, Wanyakyusa ni wacha Mungu sana. Ungelitakiwa sasa hivi kumwombea Dk. apone haraka badala ya kuendesha midahalo JF ya kumponda na kumwombea atokomee kabisa! Kwa njia hiyo sahau ubunge TZ! Tatu, unadai Mwakipesile alipewa uRC ili kumkabili Mwandosya. Kumkabili kwenye nini? Hii ndo shida ya kuishi Ulaya na kutegemea dataz za wapambe uchwara. Ikiwa Kikwete hamtaki Mwandosya na amemweka RC wa kumdhibiti, asingemteua Waziri, tena kwenye wizara nyeti sana ya Maji! Brother, rudi nyumbani, achana na alinacha. Mwakyembe humshindi kwa kukaa kwenye kompyuta na kuchonga hoja JF! Pole sana.
 

Kama kweli Mtanzania unahamu ya ubunge Kyela, basi mwaga dataz zako hapa tuone kama unaviweza viatu vya shujaa Mwakyembe. Hilo brother wetu au dada yetu Mtanzania unayeishi Uingereza huwezi kulikwepa: Mwakyembe is a house-hold name in Tanzania whether you or RC Mwakipesile likes it or not! Lete dataz hapa tukuone na tukupe support au tukutose mapema uokoe fedha zako hizo unazozisotea Uingereza kwenye baridi na maisha magumu! Ikiwa CV yako ni ya ki-Nchimbi Nchimbi na doctorate za vyuo feki, count me out! Vilevile kama uko Uingereza na unaosha dishes mahotelini ili kusurvive na kuwekeza huku nyumbani, vilevile count me out!

Mtanzania hawezi kugombea ubunge wa Kyela kwa kuweka data zake hapa kwa sababu ni sawa na Professor Shayo kuweka thesis zake kwa MICHUZI. Wanaopiga kura Kyela wengi hawako hapa, na waliopo ndio kama wewe ambae hutambui values za hardscrabble work ethics, unadhani credentials za uongozi ni shahada.

Shahada, bila shahada, nadhani katika kuelimika Mtanzania anakuzidi we mtu mara elfu lela ulela. Ijabu!
 
kumbe wee mbishi kama dagaa. Umeanza kwa point nzuri sana ila unapomalizia duu. Niliandika juzi kuwa mwanaume wa kweli utamfahamu anapomaliza, ila ujumbe ukafutwa. Maliziaji zako huwa zinaniacha hoi
. - No comment!!!
Sasa hapa unataka kusema nini? Kuwa JF ndiyo ilimchomolea matairi ili afe? Kuwa JF ndiyo ilimwambia dereva wake aende speed ya 140km/hr kwa barabara za Tanzania? Hata Ulaya hizo barabara ziko chache sana na zimewekewa uzio. Kuwa ni JF imemwambia awe anagombana na watu? Kuwa JF ndiyo ilimchagua hadi awe anaisikiliza JF? JF ikimsifia au ikimlaani, inauhusiano gani na wana-Kyela? Au Kyela ni part ya JF? JF ikisimama unataka kusema kuwa Kyela imesimama? Unafikiri mwakani Mwakyembe atakuja hapa JF kujitetea na kuomba kura au ataenda Kyela kwenda kusulubiwa? JF ni kelele za chura tu na kioo cha jamii. Ukiona wafagiliwa hapa kama Dr. Slaa (ingawa naye wapinzani wapo pia) basi ujuwe unafanya kazi vizuri
sijasema chochote kuhusu JF labda umenielewa vibaya. nilikuwa namaanisha kuwa uchaguzi haukuisha watu wameunganisha mpaka leo. sasa wakati wa uchaguzi kazi hazifanyiki.

Amini usiamini hata mie mwanzo nilikuwa MPINZANI mkubwa wa Mtanzania hasa linapokuja swala la Dr. Nilipigwa datas na sikuamini sana. Zilipoanza vurugu za Kyela hadi watu kupigwa, bado kuna watu walimpinga Engineer na kesho yake, habari hizohzo zikaandikwa magazetini. Hapo ukweli wotee aliokuwa akiusema Mtanzania ukaanikwa juani.
Hongera mtz kwa kukubadili lakini wengine bado hatujakubali kama kweli huyu jamaa anaipenda kyela kuliko mwenyewe
Kubali tu UMEISHIWA na kama ni ngumi, basi umepata GUMI LA KWENYE INI, umehesabiwa hadi 10, mchezo kwisha na ini haliumi tena. Ila sasa unaamka na kusema "niachieni, niko fit sana, niachieni niko fit. Watu weweeee ahhhh!!!!-
haya mambo nilityafanya darasa la saba kajunjumele nimekwachia mwenyewe uyamalize pengine ndiyo maana mtz alikupata kirahisi

Shalom, time to move one with new datas-
Tukiweka data hapa mnafuta. wengine hata mkilog hamonekani sawa hii niyo TZ bwana- tunaona post imeinga bali hatuwaoni mkining'inia

 
Mtanzania hawezi kugombea ubunge wa Kyela kwa kuweka data zake hapa kwa sababu ni sawa na Professor Shayo kuweka thesis zake kwa MICHUZI. Wanaopiga kura Kyela wengi hawako hapa, na waliopo ndio kama wewe ambae hutambui values za hardscrabble work ethics, unadhani credentials za uongozi ni shahada.

Shahada, bila shahada, nadhani katika kuelimika Mtanzania anakuzidi we mtu mara elfu lela ulela. Ijabu!

Mkuu, naona na wewe una matatizo kama ya huyo Mtanzania unayemtetea faithfully. Nimesema dataz, sikusema shahada! Dataz ni pamoja na ujumbe wa nyumba kumi kumi, udiwani, ukatibu kata na hata hizo shahada! Kama hizo dataz hatituhusu hapa JF, basi afunge mdomo. Tumechoka na porojo za Kyela utadhani ni wilaya pekee Tanzania. Tena Mtanzania amshukuru sana Mwakyembe kwa kuiweka Kyela kwenye chati nchini. Ijabu
 
tafsiri ya wengi ni kwamba alipewa kuwa RC ili kumkabili Mwandosya. Kama ni kweli mbona hata siku moja hatujaona wakilumbana na Mwandosya?
Kumakbili siyo kulumbana bali nikufanya obstruction lakini wapi wanyaki wa Tukuyu (conservative)siyo sawa na wa kyela (flip flop) mfano ni rafiki aliyekwenda kuomba msamaha kisa eti mimi n mfanyabiashara bwana na magari yangu yanapita mbeya!
 
Mkuu Jabu,

Ni kweli inachosha watu kutumwagia majungu kwenye forum inayotegemewa kujadili mambo ya maana, eti kisa wanataka ubunge huko kwao kyela!

Kyela leo hii watu wako huru kuwekeza tofauti na ilivyokuwa miaka mitatu tu iliyopita, kina Mtanzania wamekalia majungu tu hapa, eti Mwakyembe anawazuia, ajabu sana.

Huyo Mwanjala ambaye Mtanzania amekazana kumtolea mfano, anakimbia kivuli chake mwenyewe baada ya kuona amejirahisi mno, mbona hatuelezwi kwa nini ameikimbia hata nyumba yake ya kunduchi mtongani iliyo jirani na ya mjomba wake huyo, Mwakyembe, au nako alimfukuza!

Pale MECCO ni kampuni ya ujenzi, sasa kama halipi ushuru wa maegesho wamuangalie tu kwa sababu ni mpwa wa mwakyembe, Mtanzania acha ubabaishaji na kudanganya watu hapa.

Kama kweli leo hii uko kyela basi ni vema ukaenda vijijini kwa wananchi kufanya kampeni zako badala ya kutumia nguvu nyingi hapa JF kwani hapatakusaidia, wenzio hawakuwahi kuwa na mazingira murua kama hayo wanapoingia kwenye ubunge, wala kuwekeza, leo mnao huo uhuru ndio maana mnabwabwaja hapa, pole sana!
 
Back
Top Bottom