Polisi hawamtafuti tena aliyemuua Mushi, bali wanatafuta wanaosema Mushi ameuawa

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,512
37,829
Ukitaka vichekesho bila gharama soma Taarifa za Polisi. Katika tukio la hivi karibuni la kupote na Kuuawa kijana Robert Mushi na kishà maiti yake kukutwa Mortuary ya hospitali ya rufaa ya Polisi Kilwa road, Jeshi la Polisi limetoa Taarifa ya kuumizwa na maneno wanayoyaita ya uzushi wa taharuki toka Kwa wanaharakati G.J Malisa na Boniface Jacob na kamwe hutaona mahali walipoumizwa na kifo cha Robert Mushi.

Mbali ya Taarifa yao kutoa hitimisho la chanzo cha kifo kuwa ajali ya kugongwa na gari lililokimbia (Hit & Run), hakuna sentensi hata moja inayoonyesha gari Hilo linatafutwa au limeshakamatwa.

Hiki ni kichekesho kinachohuzunisha. Watu wakiwatuhimu Polisi kuhusika ni vigumu kukwepa. Haiwezekani Polisi ishughulike na kesi ya kukashifiwa wao binafsi kuliko kuwasaka waliomuua Mushi iwe ni Kwa ajali au ajali ya kutengeneza.

Leo utawaambia nini watu huusiki wakati lugha ya matusi/kashifa ni kosa kubwa kwako kuliko kifo cha Mtanzania masikini?

Kwanini Polisi haitumii nguvu hiyo hiyo kuwasaka wauaji wa Robert kama inavyotumia nguvu na gharama kubwa kuwasaka WAZUA TAHARUKI. Kipi kina thamani Kati ya UHAI wa Robert na HESHIMA ya Polisi?

Polisi mnashindwa kujeshimika sababu ya maamuzi ya ovyo kama haya. Yaani heshima yenu ni muhimu kuliko uhai wa mtu?

Pia soma:

-
Kamanda Muliro: Malisa GJ, Boniface Jacob wakamatwe kwa tuhuma za kupotosha taarifa za kifo cha Robart Mushi
- Utata sakata la ndugu wa Boniface Jacob: Kupotea mpaka kukutwa mochwari ya polisi, Amana wapigilia msumari!
- Boniface Jackob afika kituo cha Polisi cha Oysterbay ili akamatwe kama alivyoagiza RPC
- Jeshi la Polisi lapekua nyumba ya Boniface Jacob, laenda na GJ Malisa Moshi kupekua nyumba yake
 
Hii ndio Tanganyika ya KIZIMKAZI.YY Yuko zake majuu hata mvua wanafanya kumsimulia tu kua uku kunanyesha.watanganyika tujipange
 
Huyu marehemu anamiburuzo ya kuumizwa na lami, mgongoni, usoni, sijui mnataka mufafanuliwe kwa jinsi gani, na aliyemgonga alikimbia hapo Buguruni, nadhani labda ripoti sasa itolewe na madaktari wachunguza maiti. (ili tufike final)
Ajali gani dunia nzima haijashuhudia. Hakuna gata sisimizi anayema alishuhudia ajali.

Mtu ametangazwa anatafutwa hadi wiki baadae ndo anapatikana. Tena ukisikiliza maelezo ya polisi ndo unachoka zaidi.

Kwa nini iwe huyu tu? Smelling uovu hapa either party.
 
Ajali gani dunia nzima haijashuhudia. Hakuna gata sisimizi anayema alishuhudia ajali.

Mtu ametangazwa anatafutwa hadi wiki baadae ndo anapatikana. Tena ukisikiliza maelezo ya polisi ndo unachoka zaidi.

Kwa nini iwe huyu tu? Smelling uovu hapa either party.
Mwamuzi hapa ni ni madaktari wanaochunguza maiti, watupe final conclusions, it's over!
 
Huyu marehemu anamiburuzo ya kuumizwa na lami, mgongoni, usoni, sijui mnataka mufafanuliwe kwa jinsi gani, na aliyemgonga alikimbia hapo Buguruni, nadhani labda ripoti sasa itolewe na madaktari wachunguza maiti. (ili tufike final)
Kwahiyo akikimbia muuwaji polisi hawatakiwi kumtafuta?

Wiki nzima dogo anatafutwa na watu wameenda hadi vituo vya polisi kuulizia wanaambiwa jeshi halina taarifa zake kisha unambiwa alikuwa mortuary ya polisi wiki nzima! Kwahiyo hata watu walio katika mortuary zao hawajui?
 
Huyu marehemu anamiburuzo ya kuumizwa na lami, mgongoni, usoni, sijui mnataka mufafanuliwe kwa jinsi gani, na aliyemgonga alikimbia hapo Buguruni, nadhani labda ripoti sasa itolewe na madaktari wachunguza maiti. (ili tufike final)
Nashukuru Kwa Taarifa yako. Ila nisaidie wapi Polisi wamesema wanamtafuta? Hit and run ni kesi rahisi Sana kama ni gari limehisika.
 
Ajali gani dunia nzima haijashuhudia. Hakuna gata sisimizi anayema alishuhudia ajali.

Mtu ametangazwa anatafutwa hadi wiki baadae ndo anapatikana. Tena ukisikiliza maelezo ya polisi ndo unachoka zaidi.

Kwa nini iwe huyu tu? Smelling uovu hapa either party.
Smelling uovu...!
 
Kwahiyo akikimbia muuwaji polisi hawatakiwi kumtafuta?

Wiki nzima dogo anatafutwa na watu wameenda hadi vituo vya polisi kuulizia wanaambiwa jeshi halina taarifa zake kisha unambiwa alikuwa mortuary ya polisi wiki nzima! Kwahiyo hata watu walio katika mortuary zao hawajui?
Wao KASHFA imewaudhi zaidi ya mauaji.
 
Huyu marehemu anamiburuzo ya kuumizwa na lami, mgongoni, usoni, sijui mnataka mufafanuliwe kwa jinsi gani, na aliyemgonga alikimbia hapo Buguruni, nadhani labda ripoti sasa itolewe na madaktari wachunguza maiti. (ili tufike final)
Buguruni ipi na aligongwa mda gani, maana kwa foleni ya pale sidhani kama kuna speed ya mpaka mtu kugonga na kuua papo hapo.
 
Ukitaka vichekesho bila gharama soma Taarifa za Polisi. Katika tukio la hivi karibuni la kupote na Kuuawa kijana Robert Mushi na kishà maiti yake kukutwa Mortuary ya hospitali ya rufaa ya Polisi Kilwa road, Jeshi la Polisi limetoa Taarifa ya kuumizwa na maneno wanayoyaita ya uzushi wa taharuki toka Kwa wanaharakati G.J Malisa na Boniface Jacob na kamwe hutaona mahali walipoumizwa na kifo cha Robert Mushi. Mbali ya Taarifa yao kutoa hitimisho la chanzo cha kifo kuwa ajali ya kugongwa na gari lililokimbia (Hit & Run), hakuna sentensi hata moja inayoonyesha gari Hilo linatafutwa au limeshakamatwa.
Hiki ni kichekesho kinachohuzunisha. Watu wakiwatuhimu Polisi kuhusika ni vigumu kukwepa. Haiwezekani Polisi ishughulike na kesi ya kukashifiwa wao binafsi kuliko kuwasaka waliomuua Mushi iwe ni Kwa ajali au ajali ya kutengeneza.
Leo utawaambia nini watu huusiki wakati lugha ya matusi/kashifa ni kosa kubwa kwako kuliko kifo cha Mtanzania masikini? Kwa nini Polisi haitumii nguvu hiyo hiyo kuwasaka wauaji wa Robert kama inavyotumia nguvu na gharama kubwa kuwasaka WAZUA TAHARUKI. Kipi kina thamani Kati ya UHAI wa Robert na HESHIMA ya Polisi?
Polisi mnashindwa kujeshimika sababu ya maamuzi ya ovyo kama haya. Yaani heshima yenu ni muhimu kuliko uhai wa mtu?
Inawezekana wanamjua hivyo wanamtafuta aliyetoa siri.
 
Murillo keshaelezea tukio la ajali lilitokea eneo ambalo kulikuwa na watu bado wanafanyabiashara zao ndio waliita polisi.

Sasa kama unataka kufanya investigation yako kwanini usiende na wewe mida iliyotajwa tukio lilipotokea ukaangalia kweli kuna watu wa biashara mida hiyo na kuwauliza kama kulikuwa na hiyo ajali.

Ukatoka hapo ukaenda hospitali anayodaiwa kupelekwa marehemu kwanza na kuchunguza kweli motuary ilikuwa imejaa, wana records za hizo maiti, je ni kawaida mortuary kujaa na kawaida kupeleka wagonjwa motuary ya hospitali ya polisi.

Unaweza pia muuliza Masauni kama uamini polisi ni utaratibu wa motuary ya polisi kupokea raia.

Hakuna dhambi mbaya kama kumsingizia mtu, polisi wana motive gani za kumuua fundi simu.

Mkiitwa kwa uchochezi mnaanza kulalama mnaonewa. Wakati polisi washaelezea sakata lote.
 
Back
Top Bottom