A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

Na bado watafuataia na wengine hakuna mtu atakaye ishinda serikali mkono wake ni mrefuuu wewe hapo hata ukikimbilia chooni kwenye nnya(headhunt movie) tunakupata tuu!

Hao wanatumiwa na mabeberu wa kiarabu na masultani kuleta fujo nchini wenzao wenye uzalendo kule Zanzibar wanapata mshahara chini ya mara5 wa huo wanaoupata lakini hawalalamiki

Dawa ni kuwashughulikia tu hawa wanaojaribu kumrudisha sultani
 
That's why some people become martyrs and others snipers, yet others freedom fighters and more other guerrillas. (And the state in turn labels them as TERRORISTS!!!!)
 
Hivi mbona tunakua kama majuha. Nashangaa watu wanasema tamko tamko, Zombe nawenzake walifanya haya wako wapi sasa. Tunangoja tamko gani la Sirikali. Ni sisi wananchi tutoe tamko kwa serikali!
 
that's why some people become martyrs and others snipers, yet others freedom fighters and more other guerrillas. (and the state in turn labels them as terrorists!!!!)

hao ni vibaraka wa masultani na waarabu , pengine ndio uamsho wenyewe ; serikali itawashughulikia vizuri
 
Binafsi, kama nilivyochangia hapo mwanzo ninasikitika sana na hili! Lakini najaribu kujiuliza, wale waliokufa kwa ule mgomo wa kwanza na wa sasa nani anawalilia? wale waliopoteza ndugu zao kwa mgomo wa sasa na ule wa mwanzo watafurahia tena huu mgomo? Nachelea kusema, kama hayajakukuta ni rahisi kusema na kulaumu!
 
Ajitokeze mtu upande wa wanasiasa na wana-ccm atoe hoja za ni kwa nini huduma za afya zisiboreshwe sambamba na maslahi ya watumishi wa sekta hiyo kuboreshwa kama wanavyodai madaktari; kisha na mimi nitapinga kwa kuweka sababu za uungaji wangu mkono wa mgomo wa madaktari II

Kuna watu wanapotosha kwa makusudi suala la mgomo huu. Wanatoa cheap and inconsistent reasons as if madaktari ni wakatili, wabinafsi na vitu kama hivyo. Lakini hawajiulizi uhalali na mazingira ya madai ya hawa madktari. Hawataki kufikiri kuwa kwa huduma hizo mbovu mamia ya watu wanakufa kila kona systematically.

Zomba na wenzako kweli mtakuja juta kukubali kuuza nafsi (human integrety) kwa mlo wa siku chache.
 
Kwanza nashukuru kw huyo dogo aliyechapwa hapo hsp na hii ishu Pinda tumemsoma number what ever goes arround came arround atakuja kwenye kumi nane tu sikumoja........................nani asiye ugua dunia hiiiiiiiiiiii
 
Sasa rais ajiuzulu kwa kipi hasa?

Mimi nadhani ingekuwa busara mheshimiwa kiongozi wa madaktari Dr Ulimboka ajiuzulu mara moja kwa sababu wakati anafanya mazungumzo na hao jamaa kama alizungumza nao kama mwakilishi wa madaktari bila kupata idhini ya chama cha madaktari ni makosa makubwa!!
Wakati huu wa crisis Jumuiya ya madaktari ilitoa full mandate kwa kamati kuu kuendelea kunegotiate na serikali hivyo Ulimboka alikuwa anatekeleza majukumu aliyopewa na Madaktari. Wakat mwingine it is better to remain silent and let people doubt you instead of talking and letting people clearing their doubt @ Maundumla and Pinda!!!
 
Tatizo langu na wasiwasi wangu ni hapo hospitali, I hope he is safe...wasije wakammalizia bure..them traitors.
 
Ng'wanambula one saa,ubhange ngika si,aliekuambia dr Ulimboka alikuwa peke yake ni nani,na aliekuambia alikwenda kukutana na watu asiemjua ni nani?fuatilia vizuri upate kuhabarika,
Mhola ahene.Nimesema hivyo kwa sababu kuna post humu inaonyesha kuwa alipigiwa simu na mtu asiyemfahamu akaenda peke yake.Sasa inashangaza aliendaje peke yake
 
Ni u.................vu wa serikali hivi inashindwa kuunganisha dots au hata kuelewa logic ya uunganishaji wa dots hizo? Yaani walitegemea watz wako wavivu wa kufikiri kiasi hiki hata washindwe kulink matukio?? Nadhani wanatu-underestmate sana aisee.
 
"Ndugu zangu,

Najaribu kutuliza mawazo ili angalau niweze kuwapa kidogo tulipofikia na tunakoelekea juu ya suala hili. Kwa kweli haivumiliki ukimwona ulimboka kwa jinsi alivyotendewa na hali aliyonayo; kwa wale wanaojua hali za kitabibu, "this is a very unstable condition that demands permanent watch 24/7".

Kwa taarifa tulizokusanya, ulimboka na mwenzake waliitwa na Afisa mmoja (Jina linahifadhiwa) ili kuzungumza mambo (fulani) na wakiwa wanaendelea na mazungumzo bila kuwa na mwelekeo wa muafaka, jamaa akawasiliana na watu (fulani) kwa simu. Ghafla wakajitokeza "ASKARI" wakawataka yule (Afisa) na Dr (aliyeongozana na Ulimboka) waendelee na shughuli zao na kuwambia "Tunamtaka huyu". Wakatumia nguvu, wakamburuta na kumtia kwenye gari jeusi na kuondoka naye wakidai wanampeleka Polisi.

Huku wakiwa wanamtesa, walimlazimisha mambo kadhaa (kwa sasa tusiyataje) wakaenda naye asikokujua, wakampiga sana kwa ngumi, mateke na magongo na wakati mwengine wakitumia Bunduki zao. Wakiwa wanampiga pia walikuwa wakisema kuwa amewatesa/wasumbua sana na kuwa anajifanya mjanja mbele ya (Srk) na hivyo wanamalizana naye; akapoteza fahamu...

Wakamtupa eneo la mapori huko Tegeta hadi alipookotwa na wananchi asubuhi na kukabidhiwa mikononi mwa Wanaharakati waliompeleka Hospitali Muhimbili.

Wakati akipokelewa MOI tayari baadhi ya wanaharakati walishafika eneo lile, kumbe kati ya walimpokea alikuwamo kijana anayesadikiwa kuwa ni "Askari". Huyu aligundulika baada ya mda mfupi akiwa amejificha chooni akiwasiliana kwa simu na watu aliokuwa akiwaambia " Hajafa. Bado anahema.... na maneno mengine yaliyoashiria kuwa waliofanya 'kazi' ile hawakukamilisha 'maagizo'. Vijana wakamfundisha adabu kwa hasira na kumkuta akiwa na Redio Call, ambayo baada ya muda mfupi Polisi FFU walifika na gari na vifaa vya vurugu wakiisaka ile Radio.


Nashindwa kuendelea....."
NB: Haya ni maelezo ya mwanaharakati Albanie Marcossy aliyehusika kumsaka kama nilivyoyanukuu Mabadiliko Group.


Nina wasi wasi na usalama wake hadi sasa, kwa sababu wasije wakammalizia.
 
naandika haya kwa hasira na machozi yakinitoka kama kweli yupo mungu wa eliya mungu wa ibrahimu, isaka na yakobo hii serikali inatakiwa kung'oka madarakani kwa nguvu ya umma mapema iwezekanavyo haiwezekani kila sauti itakayonyanyuka kutetea wanyonge wao wanaizimisha. Kwa hili hatuwezi kulikubali hata kidogo. Watanzania kama mtalinyamazia hakika damu ya watu hawa itakuwa juu ya vichwa vyenu na uzao wenu. Yuko wapi captain kombe? Wapi horas kolimba? Sokoine na wengine?
 
Hii hatari sana maana nchi yetu ni ya amani lakini kuna matukio huwa yanatokea ukiyaangalia yanatia kichefuchefu, hii yote ni kutokana na nchi yetu bado watu wake wengi si waumini wa kutofautiana hoja ndio maana hata katika maisha yetu ya kwaida huwa mtu akiwa mbishi sana kwenye jamii huwa anachukuliwa kama adui badala ya kumkusanyia vielelezo ili aache kubisha vivyo hivyo kwenye serikali yetu nako ni yaleyale mtu anafanya kosa ambalo linaleta madhara kwa taifa akiambiwa wakati na yeye anajua amefanya kosa anawaona wale waliogundua uovu kama ni maadui. Kiukweli tumeshuhudia mashaidi wa kesi mbalimbali wanakufa katika mazingira ya utata wakati kesi zipo katika hatua ngumu na huwezi sema wameuliwa kwa kuwa hakuna ushahidi. Hii ni sawa na Kubenea alivyomwagiwa tindikali kutokana na kusema ukweli
This is old communist style(tactics) hivi kweli dunia ya sasa unaweza kufanya vitu kwa staili hii ya kizamani ?huwezi kufunga mtu mdomo kwa kutumia mbinu hii ya kizamani dunia iko macho na mambo hayo ya kibabe ya kizamani hayakubaliki
 
Back
Top Bottom