"""Dah Zuchi, Mungu amlaze mahala pema peponi 🙏 nakumbuka wakati na Show ya #ThePlaylist ikabidi nitafute mtu mkali wa kufanya nae Professional Photoshoot nikakutana na Zuchi kipindi iyo anajitafuta na Studio yake Mwenge ndani ndani!
Akawasha midude hatari sana na kutokea apo ikawa kila kazi...
Mwanahabari Kazimbaya Makwega ambaye alikamatwa na Askari Polisi akiwa Chuo cha Mallya, Kwimba (Mwanza), Februari 22, 2024 kisha kusafirishwa hadi Dodoma kwa tuhuma za kuandika maneno ya uchechezo dhidi ya Chuo Kukuu cha Dodoma (UDOM) kupitia tovuti yake ya ‘Mwanakwetu’, ameachiwa kwa dhamana...
Stakabadhi zilizokutwa kwenye laptop zaonysha hawa waandishi wa Aljazeera ambao ni magaidi wa dini, yaani mimi siku hizi huwa sitazami chochote cha Aljezeera, mimi huwaona kama wote magaidi wa dini, ukishajiunga kwenye uzombi wa ile dini yaani wewe na ugaidi mnakua kama pete na chanda...
Kama mada ilivyo hapo juu kwa kuwa inadaiwa kuna 4R (Reconciliation, Resilience, Reforms and Rebuilding)
kwamba zinatibu vidonda vya kuumizwa kiakili, kimwili, kiuchumi na kijamii basi nafasi hiyo ifunguliwe kwa mwandishi mkongwe Cyprian Musiba ili kuchangamsha zaidi myambuliko wa siasa za...
Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam imeifuta Kesi Namba 407 ya 2022 ya Kimtandao katika Kundi la WhatsApp iliyokuwa ikimkabili Mwandishi wa Habari za Afya na Uchunguzi wa Gazeti la Raia Mwema, Mary Victor na wenzake wawili, Asha Mahita na Rogers Simeo.
Uamuzi huo wa...
Mamlaka nchini Burkina Faso inapaswa kurejesha agizo la kuwajumuisha kijeshi waandishi wa habari Issaka Lingani na Yacouba Ladji Bama na kuhakikisha usalama wa mwandishi wa habari Boureima Ouedraogo kutokana na vitisho vya kutekwa nyara, Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari ilisema Jumatano...
Mchakato wa kesi Namba 407 ya 2022 ya Kimtandao katika Kundi la WhatsApp inayokambili Mwandishi wa Habari za afya na uchunguzi wa Gazeti la Raia Mwema, Mary Victor na wenzake wawili, Asha Mahita na Rogers Simeo inatarajiwa kuendelea Novemba 29, 2023.
Usikilizaji wa mashahidi katika kesi hiyo...
Abdifatah Moalim Nur maarufu kwa jina la Qeys aliyekuwa Mkurugenzi wa Somali TV amefariki kwa shambulio la bomu wakati alipokuwa kwenye mgahawa katika Mji Mkuu, Mogadishu.
Anakuwa Mwanahabari wa kwanza kuuawa ndani ya Mwaka 2023 Nchini Somalia.
Kundi la Wanamgambo wa Al-Shabab limekiri...
Marina Ovsyannikova ambaye alishiriki katika maandamano katika Matangazo mubashara (live) ya kwenye TV kupinga vita ya Taifa lake la Urusi dhidi Ukraine, amehukumiwa adhabu hiyo akiwa hayupo Mahakamani.
Amekutwa na hatia ya "Kusambaza hadharani habari za uongo licha ya kuwa na ufahamu kuhusu...
Kisa kingine cha kweli acha niwashirikishe kuhusu JPM kipindi alipokuwa W UJ.
Kama sikosei ilikuwa mwaka 2013 kipindi hicho miradi miwili ya barabara kuanzia Songea mjini hadi Namtumbo na Likuyu hadi Mbinga ilikuwa inatekelezwa kwa ufadhili wa MCC.
Songea - Namtumbo Mkandarasi wake ilikuwa...
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameahidi kuendelea kuwasomesha Watoto wa aliyekuwa mwandishi wa Habari wa Channel Ten, Abdul -Aziz Ahmed ambaye amefariki Dunia Machi 13, 2023 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Majaliwa ametoa ahadi hiyo wakati wa ibada ya...
Mamlaka zinamshikilia Mir Ali Koçer, Mwandishi, wa Habari wa Kujitolea anayetuhumiwa kuweka Mtandaoni taarifa za Uokoaji na hali za Majeruhi wa Tetemeko la Ardhi lililoua takriban watu 50,000 Februari 6, 2023.
Mir Ali Koçer ni kati ya Waandishi 4 waliokuwa wakichunguzwa kwa kuripoti taarifa za...
Sakata la Mwanahabari Luqman Maloto ambaye amefungua kesi ya jinai No. 5/2023 dhidi ya DCI na DPP katika Mahakama Kuu, Dar es Salaam limeendelea leo Februari 9, 2023 ambapo imefikishwa Mahakamani kwa ajili ya kutajwa.
Wakili Hekima Mwasipu anaelezea kilichotokea ikiwemo Mkurugenzi wa Makosa...
Mwanahabari Luqman Maloto, amefungua kesi ya jinai No. 5/2023 dhidi ya DCI na DPP Mahakama Kuu, Dar es Salaam, akiiomba itamke ofisi hizo zimeshindwa kuchunguza matukio yaliyofanywa na wasiojulikana ikiwemo kushambuliwa Tundu Lissu, kupotea Azory Gwanda na Ben Saanane.
Chanzo: MwanaHalisi...
Mashahidi 9 na vielelezo 10 vitatumika katika kesi namba 407 ya 2022 ya kimtandao katika Kundi la WhatsApp inayokambili mwandishi wa habari za afya na uchunguzi wa Gazeti la Raia Mwema, Mary Victor na wenzake wawili, Asha Mahita na Rogers Simeo.
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala...
Mwandishi wa habari wa Raia Mwema wamemkalia kooni kisa hapendi vitisho.
Yeye anafanya kazi zake kwa weledi bila woga. Mfumo unataka kumtoa roho. Wakati ana kesi ya mahakamani ya 2020 aloandika kuhusu Tanzania kuwa na wagonjwa wa Corona, leo nyumba yake inataka kuuzwa na mahakama kufidia deni...
Nyumba hii ambayo ni mali ya Mary Victor Mahundi, mwandishi wa habari wa Gazeti la Raia Mwema la Dar es Salaam imepigwa mnada kwa Tsh. Milioni 30 ili kufidia deni la benki la Tsh. Milioni 5.2 ambalo alikuwa akidaiwa mume wa mwanahabari huyo.
Inaelezwa kuwa nyumba hiyo iliyopo Tabata, Kata ya...
Katika taarifa yake Jeshi hilo limeahidi kufanya uchunguzi na kuchukua hatua zinazostahili kwa wahusika waliompiga risasi Arshad Shariff.
Mwandishi huyo alipigwa risasi kichwani baada maafisa kumfananisha na majambazi waliokuwa wakiwatafuta kwa madai ya kuiba gari jijini Nairobi.
Kifo chake...
Shirika la kijasusi la Urusi (FSB) limembaini raia wa Ukraine aliyetega bomu kwenye gari Urusi na kumuua binti mwanadishi wa habari aitwaye Darya Dugina.
Chombo hicho cha upelelezi cha Urusi kimechapisha video iliyokusanya matukio kadhaa ikimuonesha raia wa Ukraine wa kike kwa jina la Natalya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.