Kulingana na utafiti wangu nilioufanya kwa kuangalia samples za maprofesa mbalimbali waliopewa majukumu serikalini wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo kitu kinachonifanya ni-conclude kuwa sio uprofesa unaoongoza bali kipaji, moyo wa uzalendo, na uadilifu wa mtu. Kwa muda mrefu na kwa...
Siku ya jana tarehe 26 Novemba 2014 taifa letu limeandika historia nyingine mbaya kutokea katika uongozi wa awamu ya nne ya utawala wa nchi hii. Historia hii iliandikwa wakati taarifa ya Kamati ya PAC iliposomwa bungeni kufuatia matokeo ya ukaguzi maalum wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za...
Ule usemi wa "nyani haoni kundule" umedhihirika pale Katibu Mkuu wa CCM, Abdallahaman Kinana alipowachana wanachama wa CCM katika mkutano alioufanya hapo jana mjini Kigoma kwa kuwaambia wanachama wa chama hicho waache kupendeleana wala kubebana kwani kwa kufanya hivyo tutazalisha makundi mengi...
Nimeshtushwa na kushangazwa sana baada ya kusoma katika GAZETI LA RAIA TANZANIA la leo tarehe 27 Machi 2014 kuwa Waziri wa Utalii na Maliasili katika serikali ya Tanzania, Mh. Lazaro Nyalandu amezindua ndege mbovu itakayotumika katika vita dhidi ya ujangili hapa nchini. Na kwamba ndege hiyo...
Wana JF,
Salaam aleikum. Nimeguswa sana na zile documentary (kwenye You Tube) zilizopostiwa na Kurugenzi ya Habari ya Chadema. Zile documentary zinaonesha hali halisi na matatizo yanayowakabili watanzania wengi. Katika kuelekea katika chaguzi ndogo cha ubunge katika majimbo ya Kalenga na...
Jamani huu ni utabiri wangu japo mie sio mtaalam wa mambo ya nyota! Hakika mtaniambia humu kama utabiri wangu huu ni kweli au uongo. Ni kwamba, namuona Ridhiwan Kikwete, kijana wa rais, mgombea wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Chalinze. Namuona huyu kijana akiwaza na kuweka mikakati...
Mwanasiasa mkongwe nchini, Mateo Qaresi ambaye amewahi kushika nyadhifa mbalimbali katika Serikali ya Awamu ya Pili na Tatu, ikiwamo uwaziri na ukuu wa mkoa, amesema Tanzania kama taifa halina dira wala mwelekeo na matokeo yake mambo yake yamekuwa yakienda bila utaratibu huku akishauri...
MAHAKAMA ya Rufaa Dar es Salaam imetupilia mbali rufaa iliyokatwa na aliyekuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kasulu Vijijini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Nsanzugwako, aliyekuwa akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora uliotolewa Mei 3,2012.
Nsanzugwako alifungua kesi ya...
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikijiuliza mikataba mingi ambayo Serikali hii ya Awamu ya Nne kupitia chama cha mapinduzi na Rais Kikwete imeingia na inaendelea kuingia na mataifa mbalimbali ya nje inavyomnufaisha mtanzania wa kawaida lakini sipati jibu. Naweza kusema Serikali hii imevunja rekodi...
Leo magazeti mengi yamebeba vichwa vya habari kuwa CCM inapinga tozo la simu la shilingi 100 kila mwezi kwa kila simu iliyosajiliwa. Kwangu mimi huu ni usanii, unafiki na hadaa kubwa kwa watanzania.
Naongea haya kwa sababu CCM, chama kilicho na wabunge wengi katika bunge letu ndio waliopitisha...
Katika kile kinachoonesha kuwa kuwa kuna mkakati kabambe wa kukwamisha upinzani bungeni, hivi punde Spika Makinda ame-withdraw uwasilishwaji wa hotuba ya Wiziri kivuli, Katiba na Sheria, Mheshimiwa Tundu Lissu kwa madai kuwa wamechelewa kuileta mezani kwake.
Nadhani CHADEMA wamefanya hivyo ili...
Nipo kwa shughuli zangu za biashara hapa jijini Mbeya na kwa bahati nzuri leo nimeona nisali katika Kanisa kuu la Katoliki la Mtakatifu Antony wa Padua. Wakati wa mahubiri tumesomewa tamko lililosainiwa na viongozi wakuu wa makanisa hapa nchini kufuatia kikao cha dharula kilichokutana hivi...
Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na lawama mbalimbali kutoka kwa wananchi dhidi ya udhaifu wa Serikali ya awamu ya nne hususan kwa Wizara ya Mambo ya Ndani. Watafiti wa mambo wanasema kuwa udhaifu huu ndio unaopelekea mauaji mengi yanayoendelea hivi sasa dhidi ya wananchi wasiokuwa na hatia...
Kitendo cha Mheshimiwa Hamisi Kigwangala (kama inavyojulikana kuwa ni mwizi wa jina) cha kuacha hoja yake ya msingi ya ajira kwa vijana na kujikita katika mambo binafsi kimenifanya nizidi kumdharau, licha ya kumuona kuwa amejidhalilisha mwenyewe na kudhalilisha chama chake. Nawaonea huruma sana...
Hivi punde katika Kongamano ya miaka 51 baada ya uhuru, mwasiasa machachari na mbuge wa Ludewa Mh. Deo Filikunjombe ametoboa ukweli kuwa kuna kasumba na dhana potofu miongoni mwa watanzania wakidhani kuwa nchi hii (Tanzania) ni mali ya CCM. Hii nchi si mali ya CCM bali ya watanzania. Nimeipenda...
"Mimi sioni kama gazeti la Mwanahalisi linaandika habari za uchochezi kama zinavyo daiwa lakini hiyo ni njama ya mtu ambaye analengo la kutaka kuwafunga mdomo waandishi wa habari ili wasieleze mambo ya kweli jambo ambalo halikubaliki," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Hali halisi...
Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) tukiwa ni sehemu ya wadau wa sekta ya habari nchini, tunaunga mkono maandamano ya amani mliyoitisha ya kupinga hatua ya serikali kulifungia gazeti la MwahaHALISI.
Tunawapongeza wahariri kwa mshikamano wenu katika kipindi hiki cha majaribu...
Wana-JF,
Nimekuwa nikijiuliza mwenyewe hili wimbi la migomo lilivyoanza hapa nchini pasipokupata majibu. Fikiria walivyogoma madaktari hapa nchini na matokeo ya mgomo huo. Fikiria wanavyogoma walimu muda huu na matokeo ya mgomo huo. Jaribu kufikiria pia kuwa endapo utakuja kutokea mgomo wa...
Mbunge machachari, msema ukweli na muwazi, mheshimiwa Tundu Lissu amesema bungeni jioni hii kuwa madaktari hwakupaswa kufukuzwa bila kuwapa nafasi ya kujitetea kama inasema sheria. Huu ni uonevu mkubwa. Aidha Lissu ameponda kitendo cha kufukuza madaktari hao ambao wamesomeshwa kwa kiasi kikubwa...
Wana- JF,
Hivi punde katika kipindi cha maswali na majibu Waziri Mkuu, Pinda ameulizwa swali na Mh. Mchungaji Msigwa kuwa huko Zanzibar kuna tamko limetolewa na kiongozi mmoja kuwataka wafanyabiashara wote wa mahoteli kutokuuza chakula hasa wakati wa mchana kwa vile waislamu wako katika mfungo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.