Ni bora kuchukua hatua Na kufanya maamuzi kuliko kutofanya maamuzi. Kinachoendelea ni kuwasimamisha watendaji wanaoshutumiwa Na ubadhirifu wa Mali Au madaraka serikalini ilikupisha uchunguzi. Nadhani nijambo Jema nasi lakubezwa.
Daah! Hii Habari kweli inatia uchungu. Kweli nchi ilikua imeoza. Hatunabudi watanzania wote kushikamana kwapamoja dhidi ya haya magenge ya mafisadi. Hima tumsaidie raisi wetu.
Hii safari inatija Kwa nchi! Mahusiano bana ya Tz na Kigali yalisuasua hapo nyuma na kusababisha mahusiano mabaya ya kibiashara. Uamuzi anaouchukua Magufuli utarudisha mahusiano mazuri na hivyo kukuza ushirikiano wetu wa kibiashara hususani matumizi ya mandari yetu ya Dar es salaam. #justthinking
Siro japo sifaham historia yake kiundani ila nimekuwa nikimsikia kwenye vyombo vya habari na kwakweli anachosema mleta mada ndicho nilichokuwa nakiona kutoka Kwa huyu kamanda. Siro kweli ni jembe.
Kwenye speech yake Makonda aliweka wazi na kusema serikali haikuchangia pesa za matangazo. Pesa imetolewa na wadau mbalimbali ambao pia hakuwataja. Nimemsikiliza Kwa kipindi chote cha masaa 3 na kwakweli anamipango mizuri. Big up Makonda.
Watanzania wengi wenye mitaji midogomidogo hutumia kampuni yake kusafirisha mizigo yao kutoka China mpaka Tanzania. Wafanyabishara wengi wakariakoo wanalitambua hilo ( ukiwa na muda pita kariakoo kuulizia). Lingine nikwamba Kampuni yake imekuwa ikiwasaidia watanzania wanapopatwa na matatizo...
Watanzania tuache kuwa na chuki binafsi! Kampuni yake huko China imekuwa ikiwasaidia watanzania wengi sana kuanzia wafanyabiashara wanaosafirisha mizigo mpaka, watanzania wanaoishi mjini Guangzhou nahata viongozi wanaotembelea China marakwamara. Nimchango anaotoa kwa watubinafsi hata viongozi...
kumekua na maendeleo makubwa kwenye nyanja ya technolojia wenzetu huko marekani kwani hivi karibuni wameweza kutengeneza robot mfano wa wadudu wadogo wenye kuweza kuruka angani nakufuata masharti. Hii ni habari njema sana kwani wanaweza kutumiwa katika mambo mbalimbali kama ujenzi wa madaraja...
Hivi karibuni kumekuwa na maandamano ya vikundi vyakidini kupinga mpango wa serikali ya Ujerumani kupitisha sheria ya kutofanya tohara kwawatoto wakiume nchi humo. Jambo hili limepingwa vikali na vikundi hivyo vikisisitiza nikinyume na taratibu za dini zao. fatilia zaidi kwenye hii link hapa...
Siku chache zilizopita kumetokea mgomo wa madaktari huko nchini Portugal nakusababisha kusitishwa kwa huduma muhimu kama za upasuaji. Jambo ambalo hapa kwetu Tanzania limetokea na kuibua gumzo kubwa ikionekana ni kitendo cha kinyama. Fatilia zaidi kwenye hii link hapa chini
Portugal...
Hapa kwetu Tanzania tumeshuhudia raia wakigeni kutoka kenya akipoteza maisha katika vurugu za kisiasa zilizotokea huko Arusha. hali inayofanana na hii imetokea na wenzetu wanakabiliwa na kesi itakayo wagharimu kiwango kikubwa cha pesa. serikali inabidi kujiandaa kwahili na sikubaki rushiana...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.