Zungu: Miamala ya M-Pesa kwa mwaka ni trilioni 50, wananchi tulipe kodi tuache kulia

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,961
Mbunge wa Ilala Azzan Zungu ameunga mkono kodi ya makato kwenye mihamala ya simu na kusema serikali inapoteza mapato makubwa sana, amedai makampuni yana lobby kuwa wananchi wataumia kumbe watakoumia ni wao, amewataka wananchi kuacha kulalamikia kodi kwani serikali inategemea kodi kufanya shughuli zake.

Pia amezungumzia fedha zinazopotea kwenye madini kwa makampuni ya madini kudanganya thamani ya mzigo, na wasimamimizi kukosa uelewa, amesema serikali imepoteza trilioni 18 kutoka 2002 mpaka 2011 kutokana na kudanganya bei na ameshauri hiki ni chanzo kingine kikubwa ambacho serikali inaweza ikatumia kama ikisimamiwa vizuri.

Namnukuu (kama alivyonukuliwa kwenye Hansard za Bunge):

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali wai-revisit hii kodi mpya kwa kutazama namna gani ajira zitaathirika katika nchi yetu. Yako malalamiko wananchi wanasema sisi Wabunge tunasema kodi hii ya simu, mimi nasema ni sahihi iwepo na ndiyo njia peke yake ya Serikali ya kupata mapato ya ziada. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, transaction ya M-PESA nchini mwetu kwa mwaka ni trilioni 50, trilioni 50 transaction ya pesa zinazozunguka kwa mwananchi na mwananchi mwenzio ni fifty trilioni kwa mwaka. Makampuni haya yana-lobby kuona kuwa wanaoumia ni maskini, si kweli watakaoumia ni wao. Kwa hiyo, kodi hii naiunga mkono, Serikali iendelee na kodi zingine na kukamata mapato kwenye simu, we are losing a lot of revenue kwenye maeneo haya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye simu kuna non voice revenue, haya ndiyo maeneo Serikali inatakiwa ikae iyatazame. Pesa nyingi sana zinapatika kwenye non voice revenue ambayo sheria zetu hai-capture, inafanya makampuni haya yanaondoka na hela nyingi. Mfano mdogo, Kenya walilalamikia wananchi, lakini Kenya they put their foot down kodi ile ye transfer imewekwa na leo M-PESA, Safari com peke yao wameongeza wateja 21 percent kama hii inaumiza wananchi Kenya wangesema.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wetu na sisi tubadilishe minding setting zetu, Waheshimiwa Wabunge tusiwe na tabia ya kizamani ya kuona tukilipa kodi watu wanaumia, bila kodi Serikali hii haichapishi note. Simu hizi unakaa Dar es Salaam unapeleka pesa Jimboni within second hivi kulipa hata shilingi 400, 500 kwa kila transaction tatizo liko wapi? Ukienda Ulaya Dollar to Pound shilingi ngapi tunakatwa, ukienda Ulaya Dollar to Euro shilingi ngapi tunakatwa, commission za bureau de change, kwa nini tunaogopa kulipa kodi za Serikali? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Kenya, Safari com peke yake imepata faida ya six hundred billions kampuni moja, sisi Makampuni yetu miaka yote yanapata hasara. Kwa hiyo, Serikali put your foot down, kamata hizi kodi ili wananchi wapate huduma. Pia regulator TCRA lazima wajue teknolojia inavyobadilika business as usually imekwisha, wawe on their toes kuhakikisha makampuni haya yanalipa hizi kodi. (Makofi)

======
UPDATE:

Zungu amerudia kauli hii 2021: Azzan Zungu ataka uwepo wa kodi ya uzalendo itakayokatwa kwenye Mitandao ya simu kwa kila Mtanzania
 
wangenyimwa posho na kupeqa mahahara wa laki mbili na nuau ndio wangeelewa zaidi kwa nini wananchi wanalalamika.
 
Mbunge Azzan Zungu ameunga mkono kodi ya makato kwenye simu akidai serikali inapoteza pesa nyingi sana na kuwataka wananchi waache kulia kwenye kulipa kodi.
 
Sawa sisi tunakubali kulipa japo kishingo upande kutokana na kuminywa kwa demokrasia, basi na nyie wabunge mkubali kukatwa ile kodi kwenye mafao yenu.

Poor advice. Kuna pesa nyingi sana zaidi ya hizo za wabunge kiinua mgongo. Kuna madini kodi hazikusanywi kama inavyotakiwa, vitalu vya uwindaji wanyama wanawindwa kwa bei ya kutupwa, ufisadi wa kutisha kwny uuziji wa vitalu, makusanyo hafifu mazao ya baharini etc
 
Poor advice. Kuna pesa nyingi sana zaidi ya hizo za wabunge kiinua mgongo. Kuna madini kodi hazikusanywi kama inavyotakiwa, vitalu vya uwindaji wanyama wanawindwa kwa bei ya kutupwa, ufisadi wa kutisha kwny uuziji wa vitalu, makusanyo hafifu mazao ya baharini etc
Mkuu, mkubwa hasemwi utaambiwa huna nidhamu. Sisi acha tubanane nao hapa bampa tu bampa
 
Hii kodi ndio ilitumika kununulia yale makarandinga? magari ya kuwashawasha?

HATURIDHISHWI NA JINSI WANAVYOPANGILIA MATUMIZI YA FEDHA ZA KODI ZETU.

Halafu leo wanataka kuyabadilishia kazi na kuyafanya yawe yanazima moto ,sijui ni nani alitoa wazo la kununua haya maduduwasha mengi namna hii wakati fujo sio kipaumbele kwa Watanzania!!!??

...
 
Hiyo kodi anayoongelea ilikuwepo toka zamani hamna kipya hapo, tatizo ni hili la 280 kwa kila 1000 ambalo tunahisi Zitto alijichanganya. Kama mtandao utaendelea kula 7000 kwa kila milioni serikali ikakata humohumo hakuna ubaya. Ila huwezi kata laki tatu kwenye milioni ni upuuzi hata kim jong eun hawezi fanya hivo na ugumu wake wote. Tilioni 50 transactions haimaanishi serikali ingepatamo 10%, hizo ni transaction tu sio income ya kukaba tax.

Huyu anataja matatizo bila kutoa solution, hiyo serikali wanayosema iangalie ni ipi hasa? Ndio maana akina Zitto wakiongea bunge linatetemeka, wakitaja matatizo wanataja na solution ambayo imekaa na kufikiriwa vizuri. Huyu hizo hadithi utasema kaambiwa jana kwenye dinner leo anakuja kumwaga.
 
Poor advice. Kuna pesa nyingi sana zaidi ya hizo za wabunge kiinua mgongo. Kuna madini kodi hazikusanywi kama inavyotakiwa, vitalu vya uwindaji wanyama wanawindwa kwa bei ya kutupwa, ufisadi wa kutisha kwny uuziji wa vitalu, makusanyo hafifu mazao ya baharini etc
AH AH hatutaki kodi za huko! kama wao wameona sehemu kuu ya kukusanyia mapato ni kwenye sigara, vinywaji na miamala ya simu, si tunaona sehemu kuu ni kwenye viinua mgongo vyao basi mengine sisi hatuyajui
 
Back
Top Bottom