Mimi nadhan kwa serikali hii, hata mkirudisha hizo fedha haisaidi, hata watanzania wengi bado hawajajua magnitude ya tatizo hili la Posho.
Sasa ingekuwa busara, kama CDM wangeanzisha Community Fund ili hizo Posho wanazopinga lakin wanapewa, waziweke huko kisha kuzitumia kwa maslah ya Jamii. Hii ingewaamsha wananchi kupinga posho tofauti na kurudisha. Mfano, wabunge 48 wa CDM ni sawa na 48M. Hapa tungepata madawati mangapi? Je vijana wangapi wangeacha kukalia mawe darasani?