Zitto Kabwe: Taifa lina nyufa

Olaigwanani lang

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2012
Posts
547
Reaction score
183
Akiwa mtu wa mwisho kuchangia katika hotuba ya wizara/mambo ya ndani bwana Zitto Kabwe alisema watanzania wanaishi kwa umoja na wanashirikiana katika kila jambo kwani wanashirikiana katika mambo mengi na wanaochochea udini ni viongozi hasa wanasiasa kwani mtu huzungumzia udini katika majukwaa ya siasa huku watu elfu tano wakiwa mbele yao na kama ilivo bungeni mtu anazungumzia suala la udini na anaona fahari kwa manufaa yake binafsi.

Akaongeza kuwa, serikali haipo tayari kuchukua hatua kwa yoyote anayesemwa anatumia udini kwa manufaa yake...huku wakiwa na uwezo huo.Pia akaiasa serikali kuchukua hatua sasa badala ya matamko tuu.

Kweli hili ni la kweli kabisa.
 
Hatua ilikuwa ni kuifungia radio iman kifungo cha milele na sio miezi kadhaa tu, dhambi yao haivumiliki lakini kwa uislamu wa zitto hawezi kutamka hilo
 
udini ulianzia pale yule mtoto mdogo alipokojolea msahafu bila kujua analofanya lina madhara gani-- reaction iliyotokea pale kwa waumini na shuluhisho la viongozi wetu; udini ukakua kuhusu sakata la uchinjaji kitoweo abapo mchungaji mmoja akapoteza maisha on the process suruhisho lililotolewa pale na viongozi wetu ndiyo tatizo. tusitafute mchawi, nyumba ikiteteleka basi lawama zote lazima ziende kwa wazazi hasa baba mwenye nyumba.
 


UKIJARIBU KUANGALIA HEKIMA iliyopo katika mchango wa ZZK jana bungeni!! unaweza usifikirie kama anatoka katika chama kilekile na mbumbumbu GODBLESS LEMA... kaongea ukweli mchungu,ambao hakuna aliye na uwezo wa kuusimamia wala kuuongea. katoa lawama kwa kila anayestahili na hata yeye amukuwa tayari kubeba lawama kwa nafasi yake.. na kwa sababu ni watz wachache walio na uzalendo na ukweli kama ZZK, basi tutarajie matusi na kejeli juu yake bila uchambuzi wa mantiki toka kwa wachangiaji.
this guyzzk is presidential material no wonder hata adui zake wanamkubali
 
Zito kasema ukweli kwa mfano huyu mwenyekiti wa wazazi wa CCM taifa amekuwa anatoa matamshi ya hatari sana jukwaani kuhusu CDM kuwa ni chama cha kikabila na cha kidini, mimi binafsi kama mwana CCM sikubaliani na viongozi wa hulka za hatari kama hawa kwani ndizo zinazoleta chuki na kujenga matabaka ndani ya nchi yetu. Nawasihi viongozi wa kisiasa waache tabia na kauli zinazochochea chuki kwa watanzania bila sababu. Na tuwakatae viongozi wa sampuli hii.
 
CHADEMA inanufaika na mgawanyiko wa kidini ndio maana wanashadidia!
 
Ndoa ya BAKWATA NA SERIKALI IVUNJWE ILI WAISLAM TUUNDE CHOMBO CHETU HURU AMBACHO KITAKUWA NA BARAKA KUTOKA KWA WAISLAM WOTE KULIKO HII BAKWATA AMBAYO NI KAMA TAASISI YA CCM. Kwahl nampongeza Zitto.
 
Hatua ilikuwa ni kuifungia radio iman kifungo cha milele na sio miezi kadhaa tu, dhambi yao haivumiliki lakini kwa uislamu wa zitto hawezi kutamka hilo

Ndio maana dhambi ya udini itaendelea kuitafuna nchi hii.Mbona humsemi Mh.Mkosamali ambae nae aliongea kama Mh.Zito?Kwa kua Mkristu mwenzio sio.Au ndo yale yale .....Mfumo Kristu.Kwamba Ukristu kwanza Tanzania baadae.Ww na Nivea lenu moja,na mpo wengi humu.Mnalishwa maneno,mnafikirishwa.Ama kweli watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.Tenda haki ndugu yangu na ufanye Uadilifu."Jitieni nira yangu,MJIFUNZE kwangu kwa maana mm ni MNYENYEKEVU wa moyo......".Haya unayosema bila ushahidi unajifunza kwa nani?
 

Kuna tofauti kubwa kati yao.
 
"dini zipo lakini udini haupo"
"makabila yapo lakini ukabila haupo"

hizi ni baadhi ya kauli zinazotolewa na watu katika kujiridhisha kana kwamba fikra za binadamu hazikui bali zinabakia kama zilivyokuwa sijui miaka 50 iliyopita ambapo tukikubaliana hivyo basi tutakuwa watu wa ajabu. Humanity is growing!
Hali halisi iliyopo sasa inadhihirisha kuwa ukabila, udini, upendeleo nk vinaanza kujitokeza ...ina maana ni kama mbegu zilizokuwa hazijamwagiwa maji na sasa zimepata 'unyevunyevu' na zinaanza kuchipua na kukaa kimya au kutoyaongelea haya haina maana ndio yanaisha!
Katiba ya nchi, za vyama vya siasa na taasisi nyingine hakuna zinapoonyesha kuwa haya mambo yawepo lakini yapo. Kwa maana hiyo kuyashinda sio kutoyaongelea bali kusimamia misingi ya uwepo wetu kama taifa (katiba) na kuwa strict kwa atakayeivunja.
Kwa maana kama sheria zisipofanya kazi ni wazi masheikh watayaongelea misikitini, maaskofu watayaongelea makanisani, wanasiasa watayaongelea majukwaani, wafanyabiashara watayaongelea kwenye biashara zao nk. Suala ni kuyaongelea kwa msimamo na misingi ipi kwa maana hata hapo Mh. anaongelea hilo hilo na tunamsikia.
'busara' za kukaa kimya zitapelekea hata wale wenye nia nzuri ya kulinusuru taifa wasijue kinachoendelea au wasipate pa kutolea ushauri wao.
 
CHADEMA inanufaika na mgawanyiko wa kidini ndio maana wanashadidia!

Subili uchaguzi ukifika uone madhara ya kuingia kwenye uchaguzi ukiwa na mgogoro na jamii fulani, 2005 CUF walikua na kashfa kama hiyo CCM waliposimamisha muilsam mambo yalikua magumu kwa CUF. Kama CDM hawajaanza kuangalia hili suala kwa undani subiri 2015 CCM wasimamishe mgombea wao uje uone mambo yatakavyokua.
 
Hatua ilikuwa ni kuifungia radio iman kifungo cha milele na sio miezi kadhaa tu, dhambi yao haivumiliki lakini kwa uislamu wa zitto hawezi kutamka hilo

Redio imani imeanzishwa lini na kelele za waislam kunyanyaswa, kubaguliwa na kukandamizwa kumeanza lini? Toa mfano wa uchochezi au uzushi wake usikurupuke
 

Uko sahihi pamoja na ZZK, ni ukumbusho kwa wenye akili tu
 
jf siku hizi ni kama BUNGE la TANZANIA watu mizigo ni wengi sana by Ndygai
CC: maranduhussein
 
Kwa hiyo mmeona mnapiga kelele na hakuna anayewasikiliza upuuzi wenu so mmeamua kuua mapadri, kuchoma makanisa na kumwinda balozi wa papa! du! Uislamu na ugaidi ni chanda na pete

Unakumbuka mauaji ya Mwembechai waliuawa viongozi wangapi wa kiislamu? Unakumbuka misikiti imewahi chomwa Tunduru? Unakumbuka Qur'ani imechanwa na kukojolewa mara ngapi? Unakumbuka waislamu Zanzibar 2001 waliuwawa wangapi na Mkiristo mwenzenu? Yatosha kwa leo. Inabidi kila mmoja aangalie matukio haya kama mtanzania na si kama muislamu ama mkiristo.
 

Hayo yalikuwa matokeo ya udini uliokuwa unajengeka kimya kimya ndani ya jamii. Siku zote tusilaumu tulipoangukia,mtulaumu tulipojikwaa ili kisiki tulichojikwaa tuking'oe
 
baadhi ya makada wa ccm ambao ni wabunge na mawaziri hawapo tayari kukemea mtu yoyote wa chanma chao anapotoa kauli za udini au kukiuka maadili, husubiri mtu kutoka upande wa kushoto aongee ndipo uone wanatoa kauli za kusema na kulaani alichosema mtu wa upande wa kushoto, mfano nchimbi anapomzungumzia mh.lema kule arusha wakati wengi wa chama chake huongea mara nyingi majukwaani na hawamkosoi.....!
 
Ukweli huwa ni mgumu sana kukubalika, lakini time will tell!
 

Mauaji ya mwembechai na Zanzibar ni waislamu dhidi ya nguvu za dola. hakuna kanisa limewahi kutuma waumini wake kwenda kuua waislamu. Hili limetokea kwa waislamu tu, kuwatuma waumini wake kwenda kuua padri, na kumwinda balozi wa papa! Na hata quran inapokojolewa, huwa mnaitoa wenyewe mkidai mkojoleaji atageuka kuku! Sasa vitoto vya kikristu ni vijiniasi na huwa vinawaaibisha na uongo wenu maana kama ingekuwa kweli vingeshageuka mijusi
 
Hasa baba dhaifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…