Zitto yuko Live Mlimani TV now, huenda ameanza tangu zaa mbili unusu, hadi sasa amekuwa akizungumzia swala la posho za wabunge na kusema lazima wabunge wawe wa kwanza kupinga sitting allowances then wafanyakazi wa serikali wafuate
Sasa anazungumzia posho mpya za wabunge na kusema zinatakiwa kulipwa baada ya rais kutoa masharti ya kazi kwa wabunge na kwa sasa hakuna masharti mapya hivyo malipo yaliyoelezwa na spika kuwa yametolewa sasa ni batili na Dr Kashililah yuko right, rais hajasaini masharti mapya ya kazi za wabunge
anasema spika anaogopa kung'olewa ndio maana kakubali kuvunja taratibu na kuwalipa wabunge posho mpya bila rais kuidhinisha, anasema yeye na wenzake wachache wako tayari kumsaidia spika asing'olewe na wabunge njaa wanaoshinikiza posho kuongezwa
awashutumu pia wajumbe wa kamati ya uongozi wa bunge (makamishna) katika kuongeza posho hizo kwa kukubali pressure za wabunge kwenye nyongeza hiyo, huyu mtangazaji hajamuuliza swali kuhusu ugonjwa wake nadhani kama amepona kabisa au badobado
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.