Zitto Kabwe: Nyerere wangu mimi!

Kama kumbukumbu zangu ziko sawa,
Zitto alisema alikulia kwa babu yake mzaa mama na alijifunza kusoma na kuandika kabla ya kwenda shule ili kumsaidia babu kusoma barua kwani babu hakujua kusoma na kuandika.
Leo anasema alisoma shule ya msingi na alipelekwa na mama yake mzazi,
Sasa hapa kuna mchanganyiko kidogo,kuhusu alisomea kutoka kwa babu au wazazi ?
NB Isije kuwa tunapewa false stories for hidden reasons.
 
You must be stupid questioning someone's vision, ambitions of plans!!

Even kids wants to be pilots, doctors, engineers! whats wrong with that??

please format your brain

Uko sahihi mkuu... mtoto anapolala anaiombea midoli yake ili aikute kesho...yuko sahihi kama zitto tu, na kama wewe tu!! Tatizo lenu ni kulazimisha akili za kitoto wakubwa wazikubali!! Mswahili kutunaka kwa kiingereza mara zote inaonyesha uzembe wa akili ya huyo mtukanaji!! "Mzembe wa akili"!!......
 
Anasema "NJIANI TULIKUWA TUKIJADIRI KITOTO KUWA TUNAJENGA TAIFA",

Sasa hivi "WANAJADIRI KIKUBWA KWAMBA WANAJENGA MATUMBO"!!!!

Safi sana Mh. Zitto nimekuelewa vyema!! Piga dili Mkuu upunguze machungu ya kutembea peku enzi hizo!!
 
Robat0873398 said:
Dah! Sasa nimeanza kuamini yanayosemwa juu ya huyu jamaaa.

Anasema alikua akiangalia picha kimoyomoyo anasema siku moja nitakua kama wewe sasa sijui kuwaje.
 
Mbona kila kitu anamtaja mama Shida Salum pekee? Huyo baba mzee Kabwe vipi? Yeye kama anautaka uongozi wa juu ajue hakuna cha kuficha juu ya maisha yake. Hata kama mzee aliachia ngazi kwa tabia mbovu za mama aweke hapa hadharani.
 
Makala yako imenigusa hata mimi nidhani tupo wengi sana ambao tulisoma bila ya kuvaa viatu tulipokuwa shule ya msingi, ila kwakuwa fursa zilikuwa ni sawa kati ya mtoto wa mwenye cheo na wa maskini(hakukuwa na twisheni wala St schools) ilitufanya tusome kwa uchungu, Mimi nilipenda sana kuwa fundi magari ilinifanya nipende sana somo la sayansi na hesabu, na vilevile nilipenda kujua maeneo mbalimbali ya Tanzania, Afrika na Dunia ilinibidi niibe atlas shuleni nilipokuwa monita darasa la tatu ilimradi tu niweze kusoma maeneo mbalimbali ya dunia hii.
Asante JK Nyerere ulijenga nchi yenye usawa.


 
Nakupenda CHADEMA,nitakupigania na kukueneza popote pale nitakapokuwepo.
Mungu nisaidie.
 
You must be stupid questioning someone's vision, ambitions of plans!!

Even kids wants to be pilots, doctors, engineers! whats wrong with that??

please format your brain
Umetumia kiingera ili kuficha udhaifu wa hoja yako, lini watanzani utumwa wa kichwani utapungua kama sio kuisha? kiingereza chenyewe ulichoandika duh! mlemle na nilivyokuhisi!
 
safi sana zitto
Hatutomtofautisha ZK na mafisadi kwa kutoa simulizi ambazo kila mtu wa makamo yake au aliyemzidi anaweza kuelezea hadithi hizo, Ila tutamtofautisha kwa matendo yake yaliyotofauti na mafisadi!

Hapo safi kwa lipi?? kwa kutambua kuwa enzi hizo kulikuwa na mfumo mzuri uliojengwa na muasisi wa Taifa hili au kwa kushindwa kuishi kama muasisi wa Taifa hili?. Kama ni hadithi kila mtu anaweza kuhadithia, isipokuwa kuna wale wenye fursa hata za kupata sehemu za kusemea kama vyombo vya habari lakini kuna wale ambao ni wazalendo wa kweli hawana hata pakusemea. Kwa mtazamo wako hayo aliyoyaongea hakuna mtu anayeyajua? Unafikiri mafisadi hawayajui?

"Hivi unafikiri chombo cha habari kinapomwalika madharani "Wasira" unazani ni mahitaji ya wasikilizaji na watazamaji kusikia wasira anaongea nini?
 

umeona eeh, mbavu zangu
 
akina Faizafoxy, Bigshow njoo msome mtu mwenye akili zake anavyomwona Nyerere, nyinyi mtabaki peke yenu hata wanenu hawatawaelewa, JK late atabaki kuwa national icon hadi vifo vyenu vinawakuta, u just need to accept that fact or u'll die a hater, kufa una kinyongo na mtu ni kitu kibaya sana.
 
Usituletee unahii wako hapa! Hivyo ni vitu viwili tofauti unavyo vizungumzia wewe.

Sent from my SM-G800H using Tapatalk
 
Mh! Hizi story za mtu kukumbuka details hivyo za darasa la kwanza huwa zinanitia wasiwasi sana. Kuna huyu Zitto Kabwe na January Makamba. Yani hawa wenzetu wanataka kutuaminisha kua wao swala la uongozi walizaliwa nalo kama haki yao na walioteshwa na Mungu na kuandaliwa toka vichanga!

Utakuta story za dhiki na shida, over exaggeration ya truimph over turmoil, overcoming immense obstacles in dire situations to finally emerge the messiahs to lead us to the promised land.


There stories of tribulation and truimph are sure to make the likes of Job, Moses and Jesus envious to say the least.
Wanataka tuwafikire kama wao ni watu pekee sana na waajabu wakati waliyoyapitia kama yana ukweli kuna waTZ wengi sana wamepitia lakini hawatumii kama kete ya kupata kula/kura!

Hehehe ngoja mimi nitakuja na story yangu muone jinsi nilivozaliwa kwenye zizi la ngombe huku nikimsaidia mama yangu kujifungua mimi, nilivoanza kunywa uji wa mchanga na nilipofikisha miaka mi5 nikaanza kulima na kulisha kijiji!
 
Ndugu Zitto, mimi ni mmoja wa wakubwa zako , waliopendezwa na msimamo wako wa kisiasa na how close you are to the public, lakini kitu ambacho mara nyingi kinaniudhi ni wakati unapoleta siasa sa kinafiki za kujikomba na Hayati Mwalimu na kutafuta umaarufu on his legecy.

Kijana Zitto, i will quote you a bit "" Ujamaa haukuwa katika usawa wa elimu tu ambapo kila mtoto alipata elimu bure na bora katika Shule za umma bila ubaguzi bali pia namna jamii iliishi. Mtoto alikuwa analelewa na jamii nzima. Ukifanya makosa mtaani mzazi yeyote anakuadhibu ili kukurekebisha. Ukifanya jambo jema, mzazi yeyote anakupongeza.""

Huo ni uwongo wa hali ya juu sana, tabia za watoto kulelewa na jamii nzima, haikuletwa na UJAMAA wa Nyerere, bali hiyo ndio mila yet toka enzi za kina babu na babu, hata nyerere mwenyewe alilelewa katika mazingara hayo.

Mdogo wangu ZItto napenda kukushauri uwache hii tabia ya kilio cha maish yako ya kusoma kwa taabu, na sifa za ulivyo kuwa na akili shuleni, na namna ulivyokuwa na shida ya viatu. Zitto hiyo ndiyo hali halisi ilivyokuwa kwa watoto wa kitanzania 85% na kama sio 95%, and it was not only unique for you , this story of yours is becoming very boring.

Pia ningekushauri wewe na wengine, tuwe wakweli kuhusu utawala wa Hayati Baba wa Taifa, ni kweli alikuwa na mengi mazuri, na pia halikuwa na mengine mabaya, au siasa yake ya kijamaa zipo sehemu zilizo leta maafa makubwa kwa Umma, mbona hamuzizungumzi ili vizazi vya nyuma wajue ukweli, ile wale watakao taka kuuridisha Ujamaa wawe kujua hayo matatizo na waweze kuutafutia uvumbuzi mzuri.
 
Asante Mkirindi . Unajua hawa jamaa wanaleta siasa za kuiga za kwa akina Obama na kutulisha hapa! Ni hali ya kusikitisha sana wanasiasa wetu vijana kuwa copy cats na kukosa uhalisia wowote. Kwakweli inashtua kuwa hawa watu wanaoiga mpaka hata hotuba, kweli watakua na njia thabiti za kuendelza Taifa au ni uchu tu wa madaraka.

Mzizi wa Mbuyu katoa comment nzito sana ila wasiotafakari hawajamwelewa. Kasema kuwa Nyerere akiwa kijana alikua na ndoto za uhuru na sio kuwa raisi. Hio statement ni nzito sana, kwa mwenye akili atailewa sababu ina maana pana sana nu ku summarize vizuri tofauti ya viongozi wa enzi hizo na hawa wanaotaka uongozi sasa.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…