Zitto aitibua CHADEMA

Kama hajui kisa lake kwa nini asibainishiwe tu akalijua au wanaficha nini
hii inaweza tafsiriwa kuwa alionewa
nadhani ni wakati muafaka wa kumbainishia makosa yake ayajue ili Ayatubie
na kama hana basi Chama kimtubie kwa kumuonea
Huo sasa ndo utakuwa Muafaka (Msamaha) mzuri na Maridhiano Mazuri
na si Kufunika Kombe..,,,
 
..kisiasa tunasema Kitila na Mwigamba hawana wafuasi.

..YES, wametengeneza ilani ya chama, but at the end of the day wananchi wanampigia kura mgombea.

..
Mgombea anakamilishwa na components za chama. Moja ya components zinazowakamilisha wagombea ni Manifesto. Kwa lugha nyingine, watengeneza Manifesto ni sehemu ya mgombea kama ilivyo kwa mgombea ambaye pia ni sehemu ya watengeneza Manifesto.

Hii dhana ya kusema fulani ni muhimu kuliko wengine ndiyo inavijenga vyama katika msingi wa personality badala ya Institution. U-mimi unakuwa ndiyo kioo cha chama. Kama unavyosema hapa kuwa Mhe. Zitto ni muhimu zaidi ya wengine.

Ndiyo maana hata kwenye chaguzi ambazo zinaruhusu wagombea binafsi, ni mara chache sana wagombea binafsi huwa wanachaguliwa.
 

..CDM imejiviringisha ndani ya UKAWA..

..ni vigumu kufanya siasa za upinzani nje ya UKAWA bila kuonekana mbabaishaji, au kibaraka wa CCM.

..suala hapa ni Zitto anataka kuendelea kufanya siasa? Kama ni ndiyo, anataka kufanya siasa ndani ya UKAWA au nje?
 
Wale waona mbali tunasema hivi chadema acha wajipapatue tu lakini ukweli ni kwamba lazima zitto wamrudishe hawana ujanja kuendesha chama bila zitto.
kwii kwii kama ccm hawawezi kuendesha chama bila mafisadi kamwe!
 
Mie binafsi sioni tatizo na hoja ya zitto...kama kweli mwanzo alikosea na kuitwa mzandiki,msaliti,kibaraka wa chama na menginey mengi tuu,...sasa anataka ambiwe makosa yake ili arudi kundini asionekane tena mzandiki,muongo na kibarak wa ccm....kwahiy yupo sahih ambiwe ili aombe radhi wanachama kama hakuna kosa basi waliomwajibisha wawajibike mana ndo demokrasia ya kweli
 
Kiongozi act ahutubia mkutano wa ccm geita tafakari vuteni subira

Nguvu ya pesa ya mafisadi inafanya kazi. Lkn watz sasa wameamua na wanamsemo " Chukua mi hela ya ccm pigia kura chadema" Huu uhuni unamwisho wake ni suala la muda tu
 
mkuu acha uwongo, zitto amewahi kusaliti chama chake zaidi ya mara moja, mwaka 2010 alisaliti msimamo wa chama chake wa wabunge wake kutoka nje ya bunge wakati jk akihubia bunge kwa mara ya kwanza. Zitto alikimbia hakuhudhuria .
 

CC. Joka kuu
 
Mnamrejesha na nyadhifa zake?
 
Vipi kuhusu Lissu na Mnyika walivyomshikia kidedea na kumtukana sana katika majukwaa mbalimbali? Kibaya zaidi, hata Mhe Mbowe alikwenda jimboni kwa Mhe Zitto na kumsimanga live kijijini kwao, we unaona imekaaje hii!

..Zitto naye ana wapambe wake ambao wametoa kauli mbaya ajabu dhidi ya Mbowe na CDM.

..hata kampeni kwamba CDM ni chama cha wachagga na wakristo zinaongozwa na wapambe wa Zitto.

..YES,Mbowe alikwenda mbali kusema maneno yale jimboni kwa Zitto Kabwe. Lakini Zitto naye ni mtu wa ajabu sana kwa fitina zake dhidi ya Mbowe na CDM,ukizingatia fadhila na hisani aliyofanyiwa na Mbowe.

..Unajua Zitto bado kijana anaweza kwenda kwingine na kuanza upya. Lakini Mbowe ndiyo kaisha "losti" ujana wote kautumia kujenga CDM hana pahala pengine pa kwenda.

..Mimi namuona Zitto ni mtu asiyeaminika. Kwanza ni kwa vitimbi alivyomfanyia Mbowe. Pili ni sasa hivi anavyojaribu kuwageuka wenzake waliotangulia kuanzisha ACT.

cc Pasco, mpigilie
 
Last edited by a moderator:
pamoja na maelezo mazuri uliyoandika hapo juu nitawadharau sana cdm kama watamwomba msamaha zitto, chama as a group hakiwezi kujishusha kwa mwanachama mmoja! Mbona ccm haikujishusha kwa samweli sitta pale ilipomtendea hujuma ya wazi kwenye kugombea uspika?
 
Watu humu ndani mnaongea sana.yani hata hukumu mahakanani haitolewi hivi.mtu lazima ajitetee ajue kosa lake kisha Kama kuomba radhi ndio aombe .Na Kama ameonewa je?ndio maana nayeye anataka kuwe na masharti kwenye kurudi.
 


..nilichokueleza mimi ni "POLITICAL REALITY."

..kisiasa Zitto ni muhimu na mtu mzito kuliko Mwigamba na Mkumbo.

..kama unabisha hilo waambie Mwigamba au Mkumbo waendelee na ACT yao bila Zitto Kabwe.

cc Pasco, Ghostryder
 
Last edited by a moderator:
Inaonekana zitto ni nguzo muhimu ndani ya chadema maana waliofukuzwa kwenye Chama ni pamoja Na mkumbo Na mwigamba sasa iweje Leo chadema wanashupaa Na zitto peke yake.?
 
Nijuavyo, mtu kutambuliwa kama mnafiki na msaliti si suala dogo la kusema "yaliyopita si ndwele tugange yajayo". Hapo kuna suala la kuaminika kwa mtu ambako ni lazima kuthibitike bila shaka hasa katika siasa za upinzani zenye hatari nyingi. Kama CHADEMA wanakubali kuwa ZZK hakuwahi kuwa na sifa hizo za usaliti na unafiki basi hawana budi kwanza kumuomba radhi kwa kumzushia mambo ya hatari kisha wamtafadhalishe arudi chamani.

Kama tuhuma za kuwa mnafiki na msaliti zilikuwa za kweli na ZZK anataka kurudi chamani, hana budi kukiri huo mwenendo muovu na kuahidi kuwa ameachana nao na kwamba sasa anataka fursa mpya ya kuendeleza mapambano ya dhati akiwa ndani ya chama.

Lakini kama CHADEMA bado wanaamini kuwa ZZK ni msaliti na mnafiki na yeye hakubali; anaona anasingiziwa tu, basi hizo juhudi za kumrejesha chamani hazina maana yoyote. The parties, that's ZZK himself, the CHADEMA leadership and the party faithful, must be totally convinced that ZZK is still a bonafide CHADEMA cadre; Short-term highlights like the Escrow business shouldn't be misinterpreted and cannot constitute decision-making factors for astute (discerning) leadership - especially in competitive politics.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…