Mr RoundAbout,
Habari za asubuhi.
Ziara za Makonda zilihusisha taasisi zote za umma,kwa maana ya magari na watumishi.
Nilishuhudia mwenyewe hapa Arusha magari ya wakurugenzi wa Wilaya zote Monduli,Longido,Karatu ,Arusha DC na Wilaya za mikoa jirani kama Kilimanjaro na Manyara.
Wakuu wa mashirika yote ya umma NHC,TANAPA,NCAA,AICC,TANESCO,AUWSA, KADCO,TFS,TAWA,TANROAD,TARURA,IAA,Nelson Mandela University,CARMATEC,VETA......Hawa wote walitoa magari,fedha na watumishi.
Ukiwa ni mtu makini utabaini kote alikopita
Makonda hata kama wananchi wa sehemu husika wangegoma kuhudhuria mikutano yako bado angepata nyomi la kutosha kwasababu taasisi moja inaweza kama Tanapa ilikuwa inatoa magari 10 mpaka 20 na watumishi wa vitengo mbali mbali kama 100 hivi.Ukijumlisha taasisi zote hakosi nyomi la watu 15,000 ukiweka na makauzu kama elfu 5,000 nyomi lazima litokee la kutosha.
Fuatilia ajili ya msafara wake huko kusini ni magari mangapi yalipata ajali ?.Ni fedha kiasi gani alikusanya huyu mtoto pendwa !.
Ziara za Makonda zililenga zaidi kumjenga yeye na poromosha taasisi zote za umma ikiwemo Mahakama.
Ziara za viongozi wa sasa zinakijenga zaidi chama na si mtu.