Zero 65,000.. Maghembe unatupeleka wapi?

Inakatisha tamaa kwa kweli. Serikali ilitilia nguvu ujenzi wa shule za kata na kusahau walimu wenye taaluma watatoka wapi, sasa mijengo ipo pasipo walimu wenye taaluma. Ni bora kabisa kuwepo na walimu wenye taaluma na kufundishia chini mbuyu kuliko walimu wa UPE kufundishia mijengoni.... tunaenda wapiiiiiiiii TZzzzzzzz !!!!
 
Tatizo ni wale wenye kutoa maamuzi ya msingi kuhusu mwelekeo wa elimu,ni wazi katika karne hii ya sci& tech lazima kuwe na watu wenye mitizamo na muelekeo huo,jinsi ya kufundisha,vifaa vya kufundisha,ni nini unafundisha,watu unaowafundisha,walimu wenyewe,mazingira yao,kipato chao,vyuo etc.Kwa sasa ni kama hamna direction kiukweli.kibinafsi sijawahi sikia katika historia shule kama ilboru inakuwa na zero na div nyingi kama this time
 
.....ukipitia ile website ya NECTA then ukajaribu kuangalia randomly matokeo....unaweza ukalia kama kweli ni mzalindo wa TZ.......! mi nadhani ni more than 82% wamepata div zero na four! hata wachache waliopata div 3 combinations za waliowengi zinagoma?

What are we doing to end this? kwa nini hawa mawaziri bado tunawachekea tuuuuuu.....? can't we do something for our young brothers' future?
 
Sasa ndo tumeelewa kwa nini ex-dc mnali na Makweta walikuwa sahihi!

Wakati fulani waziri makweta alishauri watoto wanaopata div zero wafikishwe mahakamani kwa uzembe na kuisababishia hasara serikali, nadhani niwakati mwafaka kulifanyia kazi hili wazo.

Kwaupande wa walimu nashauri uanzishwe mpango wa "performance contract" mwalimu atakaefelisha afutwe kazi na ikiwezekana apandishwe kizimbani kwa kuisababishia serikali hasara kwani kalipwa mshahara ili afundishe kazi ambayo hakuitimiza. Walimu wengi vijijini wanachukua mikopo NMB na kununua pikipiki then wanaanza kazi ya kubeba abiria na kusahau majukumu yao.

Madc wapewe jukumu la kufatilia mahudhuio ya walimu na wapewe mamlaka ya kuwafuta kazi watumishi wa umma walevi wazururaji na watoro.

Uwekwe mpango wa kutenganisha majukumu ya utawala na taaluma kwani walimu wakuu sasa wamekuwa "supplies officers" kutwa nzima wako na Quotation kwenye mikoba watasimamia taaluma saa ngapi?
 
Hii batch ndio wale wa darasa la saba 2005. Mwaka huo asilimia 62 (kama 400,000) kati ya watihaniwa 700,000 walifaulu. Kwahiyo mwaka huo kuna kama vijana 300,000 walioachwa nyuma (walifeli). Sasa basi, wale 400,000 waliofaulu na kuendelea na O level, ndio matokeo yao tumeyaona majuzi na kati yao wengine ndio wameachwa nyuma. Walioachwa ni 200,000 ambao wamepata daraja la 4 na 0. Ukijumlisha hawa wa kidato cha nne mwaka 2009, na wenzao kiumri ambao walifeli darasa la saba 2005, jumla tuna kama vijana laki 700,000 nchini kwa sasa ambao system ya elimu ya Tanzania imewashinda.

Hypothetically, tunaweza kusema kuna vijana kama Laki Saba wenye umri kati ya 16-19 ambao academically ni failures. This is easily 2% of Tanzania's population.

Sasa, kila mwaka tukiwa tunafelisha wanafunzi, baada ya miaka kumi nchi yetu itakuwa inazidi kuwa ni nchi ya wasio na elimu ya kutosha. Imagine tukiendelea na rate hii hii ya vijana kufeli mitihani, huko mbele tutapata kweli nguvu kazi ya kutusaidia kusonga?
 
Sasa ndo tumeelewa kwa nini ex-dc mnali na Makweta walikuwa sahihi!
Wakati fulani waziri makweta alishauri watoto wanaopata div zero wafikishwe mahakamani kwa uzembe na kuisababishia hasara serikali, nadhani niwakati mwafaka kulifanyia kazi hili wazo.
Kwaupande wa walimu nashauri uanzishwe mpango wa "performance contract" mwalimu atakaefelisha afutwe kazi na ikiwezekana apandishwe kizimbani kwa kuisababishia serikali hasara kwani kalipwa mshahara ili afundishe kazi ambayo hakuitimiza. Walimu wengi vijijini wanachukua mikopo NMB na kununua pikipiki then wanaanza kazi ya kubeba abiria na kusahau majukumu yao.

Madc wapewe jukumu la kufatilia mahudhuio ya walimu na wapewe mamlaka ya kuwafuta kazi watumishi wa umma walevi wazururaji na watoro.

Uwekwe mpango wa kutenganisha majukumu ya utawala na taaluma kwani walimu wakuu sasa wamekuwa "supplies officers" kutwa nzima wako na Quotation kwenye mikoba watasimamia taaluma saa ngapi?

Hiyo pointi ya wanaofeli kupelekwa mahakamani imenichekesha.

Mi sielewi tatizo ni nini. Mbona fom foo mtihani ni mrahisi? Yaani mtu unashindwa kupata zaidi ya 35% kati ya masomo 7?
 
Back
Top Bottom