25.
Staki kueleza juu ya miguno na kazi ya mikono bali ni kupagawa na hisia za mahaba wote tunaonekana kuzidiwa huku Jesca jicho limemlegea lilionekana kama nusu mwezi, anaonekana kuwa fundi zaidi yangu mpaka nikajiuliza mtoto wa Ikulu kajifunzia wapi hivi vitu?. Kiukweli staki kueleza kilichotokea ila Ilikuwa ni zaidi ya raha.
Baada ya mambo kuwa mambo Jesca aliomba tutoke eneo lile na sasa alinishika mkono tukapandisha ngazi na kuifikia lifuti iliyotupeleka golofa ya kwanza tulitoka huku tukiwa tumeshikana mikono mpaka kwenye chumba kimoja alichokifungua na kunivutia ndani.
Alinibana kwenye ukuta na kuanza kubusu na kutomasana ilikuwa ni kutupa nguo bila mpangilio. Na hatimaye nilimurusha juu ya kitanda kizuri kilichotandikwa kwa ustadi na manjonjo ya kila aina. Mashuka meupe yenye mvuto wa ajabu yalivutia kuyatizama,blanketi na mito mizuri laini ya thamani ilikipamba kitanda kile. Ukiniuliza lilikuwa ni godoro la aina gani stakujibu nitakwambia nililala kwenye kitanda maridhawa kuwahi kutokea duniani, kiukweli kile kitanda ni kitanda kizuri hakuna mfano, godoro laini lakunesanesa, nilihisi niko peponi.
Marashi ya chumbani yalizivutia pua zangu na kunifanya nihisi niko mbinguni, kiukweli kitanda kile kinasahaulisha uwepo wa shida katika ulimwengu huu, nahapo ndipo nilijiuliza kama hiki ni kitanda cha mtoto cha baba kikoje? “Haki ya Mungu ndo maana watu hawataki kuachia madaraka Afrika” nilijisemea kimoyomoyo.
Basi ukawa ni utani juu ya kitanda kukimbizana na kurushiana mito wakati mwingine tulishuka na kuizunguka ile nyumba kwa furaha. “Hakika sihitaji mke zaidi ya huyu katika maisha yangu” nilijisemea. Nilijiona nimechelewa kumjua, nilijuta kutokumueleza mapema kuwa nampenda pengine hizi raha ningeanza kuzipata mapema zaidi ya hapa.
Hisia zilionekana kumuelemea Jesca akiwa kajilaza juu ya kifua changu huku akipumua kwa hisia kali, nilikuwa nikizidi kumbembeleza kwa maneno matamu ili kuufurahisha moyo wake. Jesca ndiye msichana niliyemchagua, ndiye mpenzi wangu wa pekee, nilikuwa najiona kidume na mwanaume aliyekamilika, nilijiona mwanaume pekee mwenye bahati katika dunia hii, leo hatimaye nafanikiwa kuwanaye huyu mrembo katika kitandana cha kifahari ndani ya jumba la Kitawala la Ikulu.
Tukiwa tumelala Jesca kakiweka kichwa chake juu ya kifua changu, tulianza mazungumzo juu ya mahusiano yetu. Tuliaongea mengi sana nilimuuliza Jesca itakuwaje iwapo Rais angejua juu ya mahusiano ya mwanaye? Jesca aliniambia Rais ni mtu muelewa na anamheshimu mwanaye kuliko kawaida na pia anampenda sana hivyo atamsikiliza maana ndiye mwanaye wakike pekee. Pia kama hato elewa basi mama yake Jesca angeingilia kati swala hilo na lingeisha. Kwa upande wake hakuliona kama ni tatizo alinisihi nisiogope. “Nakupenda sana Jamie handsome wangu inakuwaje unakuwa na mashaka juu yangu, mambo ya familia yangu niachie mimi” ni maneno mazuri ya kunifariji yalivutia kuyasikia na pia yalitia moyo.
Jesca aliendelea kunipa faraja kuwa hakuna mtu wakumuamulia ampende nani katika maisha yake, pia akasema hali ya mtu huamliwa na Mungu, hakuna mwanadamu apangaye juu ya maisha yake isipo kuwa muumba peke yake. Jesca alizidi kunifariji sana na kunitia moyo kuwa nisiwe na uoga kwani kila lipangwalo na Mungu hakika hakuna binadamu wakulipangua ni maneno ya faraja yaliyonifanya nijione nimezaliwa upya ndani ya hilo jumba la kifalme. Basi baada ya hayo maneno matamu tuliendelea kuliwadhana juu ya kitanda chetu tulichokichagua kwa siku hiyo natamani ungetuona bila shaka ungetamani kuwa wewe mana furaha ilitawala nyuso zetu.
Hii ilikuwa ni siku niliyoitamani toka siku ya kwanza nakutana na Jesca na leo niko naye kwa karibu zaidi, niko naye katika kitanda kimoja, niko naye tukiwa watupu, nilikuwa nikiutafakari uzuri wake na siupatii picha, ngozi yake laini kila nilipoitomasa ilinitia hamasa, staki kukizungumzia kifua chake kilicho umbwa kikaumbika, Jesca ni binti mwenye mikono laini yenye mbinu katika mapenzi.
JE HUU NI MWISHO???
ITAENDELEA