Zarina Madabida alishukia gazeti la Nipashe

Zarina Madabida alishukia gazeti la Nipashe

Haaaahahah..., majinga ya humu ni pamoja na wewe? Sasa tulia mkuu toa hoja yako basi, huku jf kila mtu anateleza tu.

Ahsante kwa ushauri mkuu, hapa jukwaani kunaweza kuwa na hoja nzuri lakini wachangiaji wengi wamekaa kisiasa zaidi, wakati mwingine unaweza ukatoa mchango mzuri lakini cha ajabu utaambiwa nenda kalipwe Lumumba Elf 7000/- ofisi zenyewe sijui zilipo, mimi niko Mwanza.
 
wakuu TFDA IS THE TOOTHLESS DOG.
 
Chama na interest yake binafsi wapi na wapi. Labda ameingia bungeni kama mahakama kujitetea... Bungeni ni mahali pa kutetea maslahi ya wananchi, ukiona mbunge anajitetea bungeni ujue wananchi wamekosea kumchagua.
bahati mbaya ni mbunge wa kuteuliwa!
 
Sio mapungufu ya TFDA tu hata TBS na EWURA nako pia kuna malugaluga kibao.
 
Kama ni uongo kwanini Kiwanda chao ( TPI ) kimefungiwa ? Hawa viti maalum ni bora Wafutiliwe mbali kabisa , tena Mwambieni aishie hapohapo kabla hatujafumua Mauchafu mengine mubaki midomo wazi !

Mkuu weka hayo mauchafu ya TPI kwa maslahi ya umma. Tambua kile kiwanda kinaformulate pharmaceticals ambayo hutumiwa na umma wa watanzania, huenda hayo mauchafu mengine ni pamoja na kutengeneza madawa yaliyo chini ya viwango (substandard drugs), kutumia adjuvants (innert ingredients) ambayo ni sumu kwa binadamu, kutumia viambato amilifu (active ingredients) ambayo ni sumu na yamepigwa marufuku sehemu zingine duniani (isipokuwa Asia; India na Uchina??), kuingiza sokoni madawa ambayo havijahakikiwa ubora (quality verification) au kusajiliwa (registered) na mamlaka ya kitaifa; TFDA au TPI yenyewe kutokuwa na quality control chain in the drugs manufacturing process. Mambo ni mengi, tafadhali fafanua hayo mauchafu!
 
Muuaji mkubwa huyu. Ingekuwa utetezi wake ni wa kweli, si angekwenda mahakamani? Kwani Bunge ni mahakama? Y. Makamba aliwahi kusema, ukitaka mambo yako yakunyokee jiunge CCM. Sijui hii inadhihirisha usemi wa Makamaba!!!
 
kwa jinsi alivyoeleza leo ina maana TFDA wana chuki na kiwanda chake(serikali inamiliki 40%)

Hapo sijamwelewa huyu Madabida kwa nini TFDA iwe na chuki na kiwanda ambacho partly ni mali ya serikali ilhali TFDA yenyewe ni chombo cha serikali (chini ya wizara ya afya)? TPI might be running pharmaceutical business dubiously with the expense of super profit bila kufuata drugs manufacturing standards! We never know!!
 
Haaaahahah..., majinga ya humu ni pamoja na wewe? Sasa tulia mkuu toa hoja yako basi, huku jf kila mtu anateleza tu.

Huyu mama amethibitisha hujuma na ubadhilifu wake na kiwanda chake, anatumia Ubunge kujiwakilisha yeye na Kiwanda chake. Nilimuuona jana akitoka povu ndicho alichotumwa na mumewe kusema bungeni. Sasa tfda mnatakiwa kumfikisha mahakani kwa tuhuma nzito alizowatuhumu maana amesema ana ushahidi ingawa pale hapakuwa mahala pa kuwatuhumu kwa ushahidi aliothibitisha. Muda wote kwanini hakufungua kesi mahakani kushitaki gazeti la nipashe na tfda kama yeye ni Mtanzania mwenye uchungu na nchi yake. Hana lolote ni Fisadi ndani ya dimbwi la mafisadi wenzake na wauaji kwa kutumia mwavuli wa chama cha majambazi.
 
Kama ni uongo kwanini Kiwanda chao ( TPI ) kimefungiwa ? Hawa viti maalum ni bora Wafutiliwe mbali kabisa , tena Mwambieni aishie hapohapo kabla hatujafumua Mauchafu mengine mubaki midomo wazi !
Pengine hawa Tfda wangekuja kujibu hoja muhimu alizotoa na kama wewe mkuu unajua kitu unachoita'mauchafu' yake na bado hutaki kuyasema tukueleweje?au hayana public interest?Kuficha mauchafu yanayohusu biashara zake za kutengeneza dawa ni udhaifu mkubwa na kukosa uzalendo!Hoja zake nilizisikia ni hizi hapa;
1. Tfda inashirikiana na wafanyabiashara wa nje ya nchi kuua viwanda vya ndani na tayari wameua viwanda karibu sita au saba na vimebaki vinne tu! 2.Tfda walipotangaza kuwa kuna ARV feki zilizotoka TPI walikosea kwani walipofanya uchunguzi zikaonekana zimetoka India(jina la kiwanda silikumbuki).Je hayo ni kweli?na kama ni kweli kwa nini hawakuja kwenye vyombo vya habari kumsafisha?Wao wametuhumiwa bungeni,basi waje watuambie kama amelidanganya Bunge! 3.Je kama kweli serikali inamiliki hisa 40%,haina mwakilishi wake kwenye menejimenti ya kiwanda ambaye pia angepaswa kulaumiwa kwa kuruhusu kutengenezwa ARV feki?na walifanya hivyo ili iweje?kwani wao biashara wanafanya na serikali hata wakiipandishia bei italipa tuu! 4.Mhariri wa gazeti la Nipashe,aliambiwa na nani kuwa sukari iliyokamatwa ikiwa imekwisha muda wake wa matumizi inakusudiwa kutengeneza ARV?au hao Tfda ndio walimweleza hayo? 5.Pia alidai ana majina ya viongozi wa Tfda wanaomiliki mafamasi yanayowauzia dawa za jumla wamiliki wa maduka ya dawa muhimu('mradi ulioanzishwa kwa akili na kutekelezwa kijanja janja na Tfda' haya yaliyo kwenye mabano ni maneno yangu)Je ni kweli?Kama ni kweli hamuoni kuwa mlianzisha mradi huo ku serve interest zenu badala ya umma?


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Ahsante kwa ushauri mkuu, hapa jukwaani kunaweza kuwa na hoja nzuri lakini wachangiaji wengi wamekaa kisiasa zaidi, wakati mwingine unaweza ukatoa mchango mzuri lakini cha ajabu utaambiwa nenda kalipwe Lumumba Elf 7000/- ofisi zenyewe sijui zilipo, mimi niko Mwanza.
Pole mkuu, usijali sana ndio mambo za huku jf
 
Kwanini nyinyi MODS mnaanza ku-censor habari? Nimeweka hapa comments zangu kuhusu Zarina Madabida mmeziondoa! Kwenye thread ya Mungi inayohusi kijana wa bodaboda kukamatwa kama mlipuaji wa kanisa pia comments zangu mmeziondoa! Why? Hebu acheni huo U-SOCIALIST/FASCIT!
 
Badala ya kushambulia gazeti anatakiwa aeleze ile sukari iliyoisha muda wake alikuwa anataka
kuipeleka Arusha kuifanyia nini??na huko ndiko kiliko kiwanda chao na mumewe cha kutengeneza
ARV feki!!!! Kwa nini waliendelea kumtumia diwani na meya kuwatishia maafisa Afya waliokamata hiyo sukari?!!!
 
amenishangaza zaidi aliposema haungi mkono hoja na akawa anawaponda wapinzani

haeleweki yuko upande upi zaidi haelezi bayana kwa kujenga hoja za kwa nini anaikataa hoja ya serikali

nahisi labda anatetea hoja so si lazima kukubaliwa na wapinzani au serikali....sampuli hizi ndo tunataka kwa faida ya watanzania, mambo ya kushabikia vyama yanatupeleka pabaya!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom