Zanzibar na biashara ya utumwa

bilengeh

Senior Member
Mar 31, 2017
135
86
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali. Moja kati ya njia hizo ni utumwa.

Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.

Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa katika vita, kushindwa kulipa deni unalodaiwa, adhabu kufuatia uhalifu uliotenda n.k.

Wazungu ndio waliokuwa wahalifu wakubwa kabisa katika kuendeleza biashara hii ya utumwa kwa niaba ya msalaba. Kati ya makabila yote ya Kizungu waliotia fora walikuwa ni Waingereza na Wamarekani ambao ni Wakristo wa Kiprotestant na Katoliki ambao leo wanajigamba na kujidai ati ni wao walioondosha utumwa.

Kama tulivyotangulia kusema awali kwamba utumwa ulikuwa ni mfumo wa maisha pale Waingereza walipopendekeza kuondoshwa kwa utumwa ulikuwa ni kwa sababu utumwa haukutia faida tena za kiuchumi na ilibidi ubadilishwe na uzalishaji mali mpya wa kibwanyenye nasio kwa sababu kwamba Wazungu walikuwa na huruma sana na Waafrika.

Kwa njia ya kudau kuondosha utumwa Manuwari na Merikebu za Kiingereza zilidiriki kuchoma na kuteketeza kwa moto madai na majahazi ya wafanya biashara yakiwa na watumwa au la, na matendo yao hayo kubainika na watawala wao. Pengine ajenda ambayo imefichwa hadi leo na Waingereza hao juu ya ukatili wao huo ni kuwa lengo kubwa lilikuwa ni kukata mizizi ya biashara baina ya Afrika Mashariki na nchi za Mashariki ya Bahari ya Hindi.

Kwa kutumia njia hii Waingereza waliweza kuhodhi uchumi wa Afrika ya Mashariki na kuua kabisa biashara baina ya Afrika ya Mashariki na Mashariki ya Bahari ya Hindi biashara ambayo ilishadumu kwa karne nyingi. Wakati Muingereza alidai kupiga vita usafirishaji wa watumwa kutoka Afrika ya Mashariki, upande mwingine aliruhusu uuzaji na uzalishaji mali wa watumwa katika bara la Afrika ya Mashariki na kwa kutenda hivyo aliweza kujinufaisha kisiasa na kiuchumi kupitia biashara hiyo ya watumwa.

Kwa vile Zanzibar ilikuwa ndio kitovu cha biashara katika Afrika ya Mashariki na kati Muingereza aliweza kuuwa uchumi wa Zanzibar na hivyo kumuwiya rahisi kutawala sehemu yote ya Afrika ya Mashariki. Zanzibar iligeuzwa bandari na soko mojawapo maalumu la watumwa, vituo vingine vikiwa sehemu za jirani na visiwa hivi kama vile Bagamoyo na Kilwa.

Pamoja na kwamba Zanzibar ilikuwa ni bandari na soko muhimu la watumwa, hakuna Mzanzibari ambaye alifanywa mtumwa bali watumwa hawa walitoka mabara ama kutokana na kusakwa na wachuuzi wa watumwa wa Kiarabu na wa kienyeji au kutokana na kuwa mateka wa vita baina ya machifu, mapigano baina ya makabila mbalimbali kama vile Wamakonde, Wamakua, Wayao n.k. au ni kutokana na kushindwa nguvu na kutekwa na wenzao.

Kufikia mwaka 1873 Zanzibar ilipiga marufuku biashara ya utumwa lakini cha kushangaza ni kwamba Wareno na Wafaransa waliendelea na biashara hiyo na Muingereza hakunyanyua mkono wkae kuwakemea.

Ingawa sheria ya kukomesha utumwa ilipitishwa rasmi 1873 cha kustaajabisha ni kwamba hadi leo wanasiasa wetu wamekuwa wakiwadanganya wananchi na wageni wanaofika Zanzibar kwamba utumwa uliondoshwa na mapinduzi ya Januari 1964.

Kama neno lenyewe linavyoonyesha, utumwa ni njia mojawapo ya uzalishaji mali ambayo ni kashfa kubwa mtu kunasibishwa nayo na kwa mujibu wa sifa za ubinadamu anayekashifika zaidi ni yule muuzaji wa watumwa hao kuliko watumwa wenyewe, kwani yeye huwa ndio kaonyesha upungufu mkubwa wa kibinadamu kwa kukubali kumuuza binadamu mwenziwe.

Pengine kwa kutambua hili ndio maana Sultan hakutaka kuwaona raia wake wa Zanzibar wakifanywa watumwa. Nchi za Ulaya ambazo leo zinajipa au kupewa sifa za utu bora ndio zinazotumia uzalishaji mali kupitia njia za watumwa na kuyawezesha matabaka ya juu yaliyokuwa yakitawala kujinufaisha kwa kiasi kikubwa. Mfano mzuri wa Waafrika wa Kimarekani (Black American) waliojenga uchumi wa Marekani kwa jasho na damu yao wakati tabaka lao likisehelea katika umasikini.

Wakoloni wote wakiongozwa na Waingereza wamekuwa wakifanya njama za siri na dhahiri za kujifanya wao ni wazuri na kuja kwao Afrika kulikuwa na madhumuni ya kuleta kheri na mafanikio kwa Waafrika pasi na kuwa na lengo jingine lolote.

Njia moja kubwa waliyoitumia ni Makanisa na Mapadri. Wazungu hao walidai kwamba wamekuja kupiga vita ushenzi na kuleta staarabu.

Wakoloni wa Kiingereza mara tu baada ya kuwanyang’anya hatamu wazalia wa Zanzibar na kuuhifadhi utawala wa Kibuu Said walimpa jina ambalo lililokuwa na dhamira ya kuwapa faida zaidi wao.

Waingereza kwa sababu zao waliuita utawala huo kuwa ni wa Waarabu. Lengo la kuuita utawala huo kuwa ni wa Kiarabu lilikuwa ni kuufanya Uislamu uonekane ni mbaya na umekandamiza Waafrika na Wazungu na Ukristo ndio mzuri kwa vile unapiga vita biashara ya watumwa.

Bahati mbaya sana watu wengi hadi hii leo wamenasa katika mtego huo wa Waingereza na wengine pamoja na kusoma kwao kote basi wameshindwa kulielewa lengo na dhamira hii ya Muingereza. Ukweli ni kwamba utumwa ulikuwepo Afrika ya Mashariki hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (as) kwa hiyo hata kabla ya kuja Mtume Muhammad (saw) utumwa ulikuwa umeshaota mizizi ulimwenguni, lakini Waingereza na wakoloni wenzao wa Kizungu kwa kutumia Kanisa wakaufanya utumwa umeletwa na Waarabu kwa lengo lile lile la kuonyesha kwamba Uislamu ndio ulioleta utumwa.

Wakati ambao utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar, Wareno na Wafaransa walishughulika na biashara ya utumwa katika nchi za Mashariki ya Afrika na kazi hiyo walifanya bila ya kuingiliwa kati na Manowari za Kiingereza zilizowekwa maalum kulinda usafirishaji wa watumwa.

Ukweli huu hausemwi na Muingereza wala vibaraka wake wa Kikristo ingawaje wanafahamu kwamba kulikuwa na Waingereza hapa hapa Zanzibar ambao walikuwa wakifaidika kutokana na jasho la watumwa hao na ndio maana utaona kwamba kilichopigwa marukufu na Wazungu ni usafirishaji wa watumwa na si kumiliki watumwa.

Jambo jingine ambalo Waingereza na vibaraka wao wamesahau kulisema ni kwamba huko kwao pia kulikuwa na utumwa ingawaje hakukuwa na Uislamu. Katika hili Waingereza wanajifanya hawatambui juu ya maafa ya Waafrika wa Afrika Magharibi (Nigeria, Ghana, Liberia) waliopelekwa Marekani ya Kaskazini, Kusini na Caribbean ambako nako hakukuwa na Uislamu. Wazungu walipokwenda Marekani waliwenda kwa niaba ya jina takatifu la Ukristo na kwa niaba ya jina la Msalaba, wakawateketeza wenyeji wa huko na kuwafanya watumwa, lakini hilo leo hawalisemi badala yake wanasingizia Uislamu ndio ulioleta biashara ya utumwa.

Njama za kuufanya Uislamu uonekane mbaya Afrika ilikuwa ni kuleta chuki za kugonganisha vichwa baina ya Wazanzibari kwa Wazanzibari, Watanganyika kwa Watanganyika ili kuweza kuwatawala kwa urahisi na kuweza kusambaza dini yao ya Kikristo.

Hilo ndilo lilikuwa na linaendelea kuwa lengo maalumu la kampeni hiyo, ingawa wengi wa Wazungu hao walikuwa na wanaendelea kuwa hata huyo Mungu mwenyewe hawamuamini bali hutumia Ukristo kuwatawala kimawazo na kiuchumi Waafriak tu. Waingereza hawa na vibaraka wao wamesahau kwamba Christopher Columus aliwateketeza Wahindi Wekundu kwa niaba ya Ukristo na kazi hiyo ovu ikaendelezwa na Waingereza mkoloni hadi leo hajatuambia ni kwa nini aliwateketeza wenyeji wa Australia na New Zealand kwa maradhi mbalimbali. Je, wakati wakifanya hayo nao walikuwa ni Waislamu?

Ni bahati mbaya sana kwamba Wazanzibari badala ya kuamka na kuzitamka mbinu za mkoloni za kutugonganisha vichwa Waislamu kwa Waislamu badala ya kukaa kitako na kujaribu kutatua tofauti zetu za kisiasa na nyingine za kijamii, tumezama katika kuendeleza mifarakano.

Jambo jingine ambalo Muingereza na Kanisa wamesahau kuwaambia Waafrika ni kwamba katika biashara ya utumwa Zanzibar Waislamu hawakufanywa watumwa na wale ambao walisimu walitolewa utumwani. Lakusikitisha ni kuona hata wale waandishi na wataalamu wanaodaiwa kuwa wameendelea wametekwa nyara na tafsiri potofu ya utumwa kama ilivyotolewa na Kanisa.

Uislamu hadi leo unapigwa vita sehemu zote ulimwenguni ingawaje leo hazitumiki sababu za utumwa lakini bado kwa kiasi kikubwa zinanasibishwa na matukio ya utumwa. Ni budi Wazanzibari tukumbuke kwamba kwa kutumia Uislamu badala ya tafsiri ya kitabaka aliyoiandaa yeye mwenyewe Muingereza alifanikiwa kuleta chuki na uhasama baina ya wakazi wa visiwa hivi, wakati mwenyewe akishirikiana na kuuhifadhi utawala huo aliouita wa Kiarabu.

Kwa njia hiyo Muingereza alifaulu kutufanya tukabane roho wenyewe kwa wenyewe na kusahau kumpiga vita adui yetu mkubwa ambaye ni yeye na Kanisa lake, kama alivyofanikiwa leo kutugonganisha vichwa kwa masuala ya kisiasa na kuwaacha maadui wetu wakubwa ukizidi kuiangamiza jamii yetu kwa kasi ya kutisha.
 
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali. Moja kati ya njia hizo ni utumwa.

Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.

Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa katika vita, kushindwa kulipa deni unalodaiwa, adhabu kufuatia uhalifu uliotenda n.k.

Wazungu ndio waliokuwa wahalifu wakubwa kabisa katika kuendeleza biashara hii ya utumwa kwa niaba ya msalaba. Kati ya makabila yote ya Kizungu waliotia fora walikuwa ni Waingereza na Wamarekani ambao ni Wakristo wa Kiprotestant na Katoliki ambao leo wanajigamba na kujidai ati ni wao walioondosha utumwa.

Kama tulivyotangulia kusema awali kwamba utumwa ulikuwa ni mfumo wa maisha pale Waingereza walipopendekeza kuondoshwa kwa utumwa ulikuwa ni kwa sababu utumwa haukutia faida tena za kiuchumi na ilibidi ubadilishwe na uzalishaji mali mpya wa kibwanyenye nasio kwa sababu kwamba Wazungu walikuwa na huruma sana na Waafrika.

Kwa njia ya kudau kuondosha utumwa Manuwari na Merikebu za Kiingereza zilidiriki kuchoma na kuteketeza kwa moto madai na majahazi ya wafanya biashara yakiwa na watumwa au la, na matendo yao hayo kubainika na watawala wao. Pengine ajenda ambayo imefichwa hadi leo na Waingereza hao juu ya ukatili wao huo ni kuwa lengo kubwa lilikuwa ni kukata mizizi ya biashara baina ya Afrika Mashariki na nchi za Mashariki ya Bahari ya Hindi.

Kwa kutumia njia hii Waingereza waliweza kuhodhi uchumi wa Afrika ya Mashariki na kuua kabisa biashara baina ya Afrika ya Mashariki na Mashariki ya Bahari ya Hindi biashara ambayo ilishadumu kwa karne nyingi. Wakati Muingereza alidai kupiga vita usafirishaji wa watumwa kutoka Afrika ya Mashariki, upande mwingine aliruhusu uuzaji na uzalishaji mali wa watumwa katika bara la Afrika ya Mashariki na kwa kutenda hivyo aliweza kujinufaisha kisiasa na kiuchumi kupitia biashara hiyo ya watumwa.

Kwa vile Zanzibar ilikuwa ndio kitovu cha biashara katika Afrika ya Mashariki na kati Muingereza aliweza kuuwa uchumi wa Zanzibar na hivyo kumuwiya rahisi kutawala sehemu yote ya Afrika ya Mashariki. Zanzibar iligeuzwa bandari na soko mojawapo maalumu la watumwa, vituo vingine vikiwa sehemu za jirani na visiwa hivi kama vile Bagamoyo na Kilwa.

Pamoja na kwamba Zanzibar ilikuwa ni bandari na soko muhimu la watumwa, hakuna Mzanzibari ambaye alifanywa mtumwa bali watumwa hawa walitoka mabara ama kutokana na kusakwa na wachuuzi wa watumwa wa Kiarabu na wa kienyeji au kutokana na kuwa mateka wa vita baina ya machifu, mapigano baina ya makabila mbalimbali kama vile Wamakonde, Wamakua, Wayao n.k. au ni kutokana na kushindwa nguvu na kutekwa na wenzao.

Kufikia mwaka 1873 Zanzibar ilipiga marufuku biashara ya utumwa lakini cha kushangaza ni kwamba Wareno na Wafaransa waliendelea na biashara hiyo na Muingereza hakunyanyua mkono wkae kuwakemea.

Ingawa sheria ya kukomesha utumwa ilipitishwa rasmi 1873 cha kustaajabisha ni kwamba hadi leo wanasiasa wetu wamekuwa wakiwadanganya wananchi na wageni wanaofika Zanzibar kwamba utumwa uliondoshwa na mapinduzi ya Januari 1964.

Kama neno lenyewe linavyoonyesha, utumwa ni njia mojawapo ya uzalishaji mali ambayo ni kashfa kubwa mtu kunasibishwa nayo na kwa mujibu wa sifa za ubinadamu anayekashifika zaidi ni yule muuzaji wa watumwa hao kuliko watumwa wenyewe, kwani yeye huwa ndio kaonyesha upungufu mkubwa wa kibinadamu kwa kukubali kumuuza binadamu mwenziwe.

Pengine kwa kutambua hili ndio maana Sultan hakutaka kuwaona raia wake wa Zanzibar wakifanywa watumwa. Nchi za Ulaya ambazo leo zinajipa au kupewa sifa za utu bora ndio zinazotumia uzalishaji mali kupitia njia za watumwa na kuyawezesha matabaka ya juu yaliyokuwa yakitawala kujinufaisha kwa kiasi kikubwa. Mfano mzuri wa Waafrika wa Kimarekani (Black American) waliojenga uchumi wa Marekani kwa jasho na damu yao wakati tabaka lao likisehelea katika umasikini.

Wakoloni wote wakiongozwa na Waingereza wamekuwa wakifanya njama za siri na dhahiri za kujifanya wao ni wazuri na kuja kwao Afrika kulikuwa na madhumuni ya kuleta kheri na mafanikio kwa Waafrika pasi na kuwa na lengo jingine lolote.

Njia moja kubwa waliyoitumia ni Makanisa na Mapadri. Wazungu hao walidai kwamba wamekuja kupiga vita ushenzi na kuleta staarabu.

Wakoloni wa Kiingereza mara tu baada ya kuwanyang’anya hatamu wazalia wa Zanzibar na kuuhifadhi utawala wa Kibuu Said walimpa jina ambalo lililokuwa na dhamira ya kuwapa faida zaidi wao.

Waingereza kwa sababu zao waliuita utawala huo kuwa ni wa Waarabu. Lengo la kuuita utawala huo kuwa ni wa Kiarabu lilikuwa ni kuufanya Uislamu uonekane ni mbaya na umekandamiza Waafrika na Wazungu na Ukristo ndio mzuri kwa vile unapiga vita biashara ya watumwa.

Bahati mbaya sana watu wengi hadi hii leo wamenasa katika mtego huo wa Waingereza na wengine pamoja na kusoma kwao kote basi wameshindwa kulielewa lengo na dhamira hii ya Muingereza. Ukweli ni kwamba utumwa ulikuwepo Afrika ya Mashariki hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (as) kwa hiyo hata kabla ya kuja Mtume Muhammad (saw) utumwa ulikuwa umeshaota mizizi ulimwenguni, lakini Waingereza na wakoloni wenzao wa Kizungu kwa kutumia Kanisa wakaufanya utumwa umeletwa na Waarabu kwa lengo lile lile la kuonyesha kwamba Uislamu ndio ulioleta utumwa.

Wakati ambao utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar, Wareno na Wafaransa walishughulika na biashara ya utumwa katika nchi za Mashariki ya Afrika na kazi hiyo walifanya bila ya kuingiliwa kati na Manowari za Kiingereza zilizowekwa maalum kulinda usafirishaji wa watumwa.

Ukweli huu hausemwi na Muingereza wala vibaraka wake wa Kikristo ingawaje wanafahamu kwamba kulikuwa na Waingereza hapa hapa Zanzibar ambao walikuwa wakifaidika kutokana na jasho la watumwa hao na ndio maana utaona kwamba kilichopigwa marukufu na Wazungu ni usafirishaji wa watumwa na si kumiliki watumwa.

Jambo jingine ambalo Waingereza na vibaraka wao wamesahau kulisema ni kwamba huko kwao pia kulikuwa na utumwa ingawaje hakukuwa na Uislamu. Katika hili Waingereza wanajifanya hawatambui juu ya maafa ya Waafrika wa Afrika Magharibi (Nigeria, Ghana, Liberia) waliopelekwa Marekani ya Kaskazini, Kusini na Caribbean ambako nako hakukuwa na Uislamu. Wazungu walipokwenda Marekani waliwenda kwa niaba ya jina takatifu la Ukristo na kwa niaba ya jina la Msalaba, wakawateketeza wenyeji wa huko na kuwafanya watumwa, lakini hilo leo hawalisemi badala yake wanasingizia Uislamu ndio ulioleta biashara ya utumwa.

Njama za kuufanya Uislamu uonekane mbaya Afrika ilikuwa ni kuleta chuki za kugonganisha vichwa baina ya Wazanzibari kwa Wazanzibari, Watanganyika kwa Watanganyika ili kuweza kuwatawala kwa urahisi na kuweza kusambaza dini yao ya Kikristo.

Hilo ndilo lilikuwa na linaendelea kuwa lengo maalumu la kampeni hiyo, ingawa wengi wa Wazungu hao walikuwa na wanaendelea kuwa hata huyo Mungu mwenyewe hawamuamini bali hutumia Ukristo kuwatawala kimawazo na kiuchumi Waafriak tu. Waingereza hawa na vibaraka wao wamesahau kwamba Christopher Columus aliwateketeza Wahindi Wekundu kwa niaba ya Ukristo na kazi hiyo ovu ikaendelezwa na Waingereza mkoloni hadi leo hajatuambia ni kwa nini aliwateketeza wenyeji wa Australia na New Zealand kwa maradhi mbalimbali. Je, wakati wakifanya hayo nao walikuwa ni Waislamu?

Ni bahati mbaya sana kwamba Wazanzibari badala ya kuamka na kuzitamka mbinu za mkoloni za kutugonganisha vichwa Waislamu kwa Waislamu badala ya kukaa kitako na kujaribu kutatua tofauti zetu za kisiasa na nyingine za kijamii, tumezama katika kuendeleza mifarakano.

Jambo jingine ambalo Muingereza na Kanisa wamesahau kuwaambia Waafrika ni kwamba katika biashara ya utumwa Zanzibar Waislamu hawakufanywa watumwa na wale ambao walisimu walitolewa utumwani. Lakusikitisha ni kuona hata wale waandishi na wataalamu wanaodaiwa kuwa wameendelea wametekwa nyara na tafsiri potofu ya utumwa kama ilivyotolewa na Kanisa.

Uislamu hadi leo unapigwa vita sehemu zote ulimwenguni ingawaje leo hazitumiki sababu za utumwa lakini bado kwa kiasi kikubwa zinanasibishwa na matukio ya utumwa. Ni budi Wazanzibari tukumbuke kwamba kwa kutumia Uislamu badala ya tafsiri ya kitabaka aliyoiandaa yeye mwenyewe Muingereza alifanikiwa kuleta chuki na uhasama baina ya wakazi wa visiwa hivi, wakati mwenyewe akishirikiana na kuuhifadhi utawala huo aliouita wa Kiarabu.

Kwa njia hiyo Muingereza alifaulu kutufanya tukabane roho wenyewe kwa wenyewe na kusahau kumpiga vita adui yetu mkubwa ambaye ni yeye na Kanisa lake, kama alivyofanikiwa leo kutugonganisha vichwa kwa masuala ya kisiasa na kuwaacha maadui wetu wakubwa ukizidi kuiangamiza jamii yetu kwa kasi ya kutisha.
Kusudio lako lilikuwa jema kabisa .... but maelezo yako yamedhihirisha wazi kabisa kuwa ulikusudia kujikita zaidi katika UTETEZI WA KIDINI .... KUTETEA HUKU na KUPONDA KULE ....
USHAURI: If you want to be a GOOD WRITER with an IMPRESSIVE STORY for anyone to CONTRIBUTE FREELY then just try to BALANCE your STORY ..... MZANI wako USIEGEMEE UPANDE MMOJA ...... It's just a piece of advice ... you may take it or leave it ...
 
Kusudio lako lilikuwa jema kabisa .... but maelezo yako yamedhihirisha wazi kabisa kuwa ulikusudia kujikita zaidi katika UTETEZI WA KIDINI .... KUTETEA HUKU na KUPONDA KULE ....
USHAURI: If you want to be a GOOD WRITER with an IMPRESSIVE STORY for anyone to CONTRIBUTE FREELY then just try to BALANCE your STORY ..... MZANI wako USIEGEMEE UPANDE MMOJA ...... It's just a piece of advice ... you may take it or leave it ...
a.
Bravo mjibu hoja. Hivi kalne ya 13 nani mzungu alishafika afrika. Kumbuka Mzungu wa kwanza kuiona Afrika ni kalne ya 14 wakati huo waarabu walishafika na walishaanza chukua watu kwao. Ni wakati huo ndugu zetu walishaanza uzwa uhindini na humu ndani kwa kulipizana visasi. Waarabu hawa ndo waliovunja tawala nyingi za kikabila humu nchini na kuweka watu waliowapa bunduki.
Kalne ya 19 wakati speek anakuja ukisoma kitabu chake utaona jinsi waarabu walivyotamaraki mpaka Uganda. Unaweza kujiuliza kwanini waganda walichukia kiswahili? Lugha ya watumwa. Walie waliotoka pwani wakiitwa waungwana, ni wale wale waliochukuliwa zamani kama watumwa baadaye wakapandishwa vyeo na kuja kuchukua watumwa. Hapo Mjerumani, mwingereza wala mfaransa hajakanyaga. Kumbuka wavumbuzi waliopitia costal kama akina vasco dagama walichukua watu wakufanya kazi kwenye meli wakipewa na watemi lakini wakati huo hawana habari za utumwa ili hali wenzetu waarabu walishajikusanyia watumwa kila wakati. Waliwahasi ndo maana hatuna mazalio kama yalivyo marekani. Mwarabu alikuwa kuadi wa kunununa na kuuza kwa wazungu. Read documents kwenye vitabu vya wachungzi na wale waliopitia East Africa wakati ule. Hata kijijijini kwetu kuna mwembe ambapo waarabu walikuwa wakinununua watumwa toka kwa watemi wale waliowakamata au kuwateka.
 
Kusudio lako lilikuwa jema kabisa .... but maelezo yako yamedhihirisha wazi kabisa kuwa ulikusudia kujikita zaidi katika UTETEZI WA KIDINI .... KUTETEA HUKU na KUPONDA KULE ....
USHAURI: If you want to be a GOOD WRITER with an IMPRESSIVE STORY for anyone to CONTRIBUTE FREELY then just try to BALANCE your STORY ..... MZANI wako USIEGEMEE UPANDE MMOJA ...... It's just a piece of advice ... you may take it or leave it ...
kwahiyo mkuu umeweza kusoma hili gazeti lote!?
 
Ni mjinga tu ndie anaweza kuhusisha utumwa na dini manake historia inaonesha biashara ya utumwa imefanywa na wajasiriamali wa dini zote!!

Kwa Afrika Mashariki, ndio waliendesha biashara ya utumwa lakini ukienda Afrika Magharibi, through Transatlantic Slave Trade ilifanywa na wazungu.
 
kwahiyo mkuu umeweza kusoma hili gazeti lote!?
Yes I did ... nilitamani kusoma hadi mwisho ili NIHABARIKE zaidi juu ya hiyo issue ya WATUMWA na masahibu yalowapata ... mana history naipenda sana ... but on the contrary NAUJUTIA MUDA wangu niloutumia ...
 
a.
Bravo mjibu hoja. Hivi kalne ya 13 nani mzungu alishafika afrika. Kumbuka Mzungu wa kwanza kuiona Afrika ni kalne ya 14 wakati huo waarabu walishafika na walishaanza chukua watu kwao. Ni wakati huo ndugu zetu walishaanza uzwa uhindini na humu ndani kwa kulipizana visasi. Waarabu hawa ndo waliovunja tawala nyingi za kikabila humu nchini na kuweka watu waliowapa bunduki.
Kalne ya 19 wakati speek anakuja ukisoma kitabu chake utaona jinsi waarabu walivyotamaraki mpaka Uganda. Unaweza kujiuliza kwanini waganda walichukia kiswahili? Lugha ya watumwa. Walie waliotoka pwani wakiitwa waungwana, ni wale wale waliochukuliwa zamani kama watumwa baadaye wakapandishwa vyeo na kuja kuchukua watumwa. Hapo Mjerumani, mwingereza wala mfaransa hajakanyaga. Kumbuka wavumbuzi waliopitia costal kama akina vasco dagama walichukua watu wakufanya kazi kwenye meli wakipewa na watemi lakini wakati huo hawana habari za utumwa ili hali wenzetu waarabu walishajikusanyia watumwa kila wakati. Waliwahasi ndo maana hatuna mazalio kama yalivyo marekani. Mwarabu alikuwa kuadi wa kunununa na kuuza kwa wazungu. Read documents kwenye vitabu vya wachungzi na wale waliopitia East Africa wakati ule. Hata kijijijini kwetu kuna mwembe ambapo waarabu walikuwa wakinununua watumwa toka kwa watemi wale waliowakamata au kuwateka.
Wewe sema tu kwamba huku Afrika Mashariki players wakubwa wa biashara ya utumwa walikuwa ni Waarabu lakini kusema eti Vasco da Gama, kama kiwakilishi cha Wazungu hakufahamu masuala ya utumwa si kweli kwa sababu wakati biashara ya utumwa inashamiri Afrika Mashariki, tayari Wareno walishakuwa magwiji wa biashara ya utumwa through transatlantic slave trade.

Look, wakati biashara ya utumwa Afrika Mashariki ilishamiri baada ya kuhamia kwa Sultan wa Oman kati kati ya 1800's, historia inaonesha convoy ya kwanza ya watumwa kwenda Brazil ilifanyika somewhere in 1526 na Wareno!!!
 
Wewe sema tu kwamba huku Afrika Mashariki players wakubwa wa biashara ya utumwa walikuwa ni Waarabu lakini kusema eti Vasco da Gama, kama kiwakilishi cha Wazungu hakufahamu masuala ya utumwa si kweli kwa sababu wakati biashara ya utumwa inashamiri Afrika Mashariki, tayari Wareno walishakuwa magwiji wa biashara ya utumwa through transatlantic slave trade.

Look, wakati biashara ya utumwa Afrika Mashariki ilishamiri baada ya kuhamia kwa Sultan wa Oman kati kati ya 1800's, historia inaonesha convoy ya kwanza ya watumwa kwenda Brazil ilifanyika somewhere in 1526 na Wareno!!!
MPAMBANO MKALI kati ya bara la ULAYA na ASIA waendelea .... yetu macho ...
 
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali. Moja kati ya njia hizo ni utumwa.

Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.

Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa katika vita, kushindwa kulipa deni unalodaiwa, adhabu kufuatia uhalifu uliotenda n.k.

Wazungu ndio waliokuwa wahalifu wakubwa kabisa katika kuendeleza biashara hii ya utumwa kwa niaba ya msalaba. Kati ya makabila yote ya Kizungu waliotia fora walikuwa ni Waingereza na Wamarekani ambao ni Wakristo wa Kiprotestant na Katoliki ambao leo wanajigamba na kujidai ati ni wao walioondosha utumwa.

Kama tulivyotangulia kusema awali kwamba utumwa ulikuwa ni mfumo wa maisha pale Waingereza walipopendekeza kuondoshwa kwa utumwa ulikuwa ni kwa sababu utumwa haukutia faida tena za kiuchumi na ilibidi ubadilishwe na uzalishaji mali mpya wa kibwanyenye nasio kwa sababu kwamba Wazungu walikuwa na huruma sana na Waafrika.

Kwa njia ya kudau kuondosha utumwa Manuwari na Merikebu za Kiingereza zilidiriki kuchoma na kuteketeza kwa moto madai na majahazi ya wafanya biashara yakiwa na watumwa au la, na matendo yao hayo kubainika na watawala wao. Pengine ajenda ambayo imefichwa hadi leo na Waingereza hao juu ya ukatili wao huo ni kuwa lengo kubwa lilikuwa ni kukata mizizi ya biashara baina ya Afrika Mashariki na nchi za Mashariki ya Bahari ya Hindi.

Kwa kutumia njia hii Waingereza waliweza kuhodhi uchumi wa Afrika ya Mashariki na kuua kabisa biashara baina ya Afrika ya Mashariki na Mashariki ya Bahari ya Hindi biashara ambayo ilishadumu kwa karne nyingi. Wakati Muingereza alidai kupiga vita usafirishaji wa watumwa kutoka Afrika ya Mashariki, upande mwingine aliruhusu uuzaji na uzalishaji mali wa watumwa katika bara la Afrika ya Mashariki na kwa kutenda hivyo aliweza kujinufaisha kisiasa na kiuchumi kupitia biashara hiyo ya watumwa.

Kwa vile Zanzibar ilikuwa ndio kitovu cha biashara katika Afrika ya Mashariki na kati Muingereza aliweza kuuwa uchumi wa Zanzibar na hivyo kumuwiya rahisi kutawala sehemu yote ya Afrika ya Mashariki. Zanzibar iligeuzwa bandari na soko mojawapo maalumu la watumwa, vituo vingine vikiwa sehemu za jirani na visiwa hivi kama vile Bagamoyo na Kilwa.

Pamoja na kwamba Zanzibar ilikuwa ni bandari na soko muhimu la watumwa, hakuna Mzanzibari ambaye alifanywa mtumwa bali watumwa hawa walitoka mabara ama kutokana na kusakwa na wachuuzi wa watumwa wa Kiarabu na wa kienyeji au kutokana na kuwa mateka wa vita baina ya machifu, mapigano baina ya makabila mbalimbali kama vile Wamakonde, Wamakua, Wayao n.k. au ni kutokana na kushindwa nguvu na kutekwa na wenzao.

Kufikia mwaka 1873 Zanzibar ilipiga marufuku biashara ya utumwa lakini cha kushangaza ni kwamba Wareno na Wafaransa waliendelea na biashara hiyo na Muingereza hakunyanyua mkono wkae kuwakemea.

Ingawa sheria ya kukomesha utumwa ilipitishwa rasmi 1873 cha kustaajabisha ni kwamba hadi leo wanasiasa wetu wamekuwa wakiwadanganya wananchi na wageni wanaofika Zanzibar kwamba utumwa uliondoshwa na mapinduzi ya Januari 1964.

Kama neno lenyewe linavyoonyesha, utumwa ni njia mojawapo ya uzalishaji mali ambayo ni kashfa kubwa mtu kunasibishwa nayo na kwa mujibu wa sifa za ubinadamu anayekashifika zaidi ni yule muuzaji wa watumwa hao kuliko watumwa wenyewe, kwani yeye huwa ndio kaonyesha upungufu mkubwa wa kibinadamu kwa kukubali kumuuza binadamu mwenziwe.

Pengine kwa kutambua hili ndio maana Sultan hakutaka kuwaona raia wake wa Zanzibar wakifanywa watumwa. Nchi za Ulaya ambazo leo zinajipa au kupewa sifa za utu bora ndio zinazotumia uzalishaji mali kupitia njia za watumwa na kuyawezesha matabaka ya juu yaliyokuwa yakitawala kujinufaisha kwa kiasi kikubwa. Mfano mzuri wa Waafrika wa Kimarekani (Black American) waliojenga uchumi wa Marekani kwa jasho na damu yao wakati tabaka lao likisehelea katika umasikini.

Wakoloni wote wakiongozwa na Waingereza wamekuwa wakifanya njama za siri na dhahiri za kujifanya wao ni wazuri na kuja kwao Afrika kulikuwa na madhumuni ya kuleta kheri na mafanikio kwa Waafrika pasi na kuwa na lengo jingine lolote.

Njia moja kubwa waliyoitumia ni Makanisa na Mapadri. Wazungu hao walidai kwamba wamekuja kupiga vita ushenzi na kuleta staarabu.

Wakoloni wa Kiingereza mara tu baada ya kuwanyang’anya hatamu wazalia wa Zanzibar na kuuhifadhi utawala wa Kibuu Said walimpa jina ambalo lililokuwa na dhamira ya kuwapa faida zaidi wao.

Waingereza kwa sababu zao waliuita utawala huo kuwa ni wa Waarabu. Lengo la kuuita utawala huo kuwa ni wa Kiarabu lilikuwa ni kuufanya Uislamu uonekane ni mbaya na umekandamiza Waafrika na Wazungu na Ukristo ndio mzuri kwa vile unapiga vita biashara ya watumwa.

Bahati mbaya sana watu wengi hadi hii leo wamenasa katika mtego huo wa Waingereza na wengine pamoja na kusoma kwao kote basi wameshindwa kulielewa lengo na dhamira hii ya Muingereza. Ukweli ni kwamba utumwa ulikuwepo Afrika ya Mashariki hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (as) kwa hiyo hata kabla ya kuja Mtume Muhammad (saw) utumwa ulikuwa umeshaota mizizi ulimwenguni, lakini Waingereza na wakoloni wenzao wa Kizungu kwa kutumia Kanisa wakaufanya utumwa umeletwa na Waarabu kwa lengo lile lile la kuonyesha kwamba Uislamu ndio ulioleta utumwa.

Wakati ambao utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar, Wareno na Wafaransa walishughulika na biashara ya utumwa katika nchi za Mashariki ya Afrika na kazi hiyo walifanya bila ya kuingiliwa kati na Manowari za Kiingereza zilizowekwa maalum kulinda usafirishaji wa watumwa.

Ukweli huu hausemwi na Muingereza wala vibaraka wake wa Kikristo ingawaje wanafahamu kwamba kulikuwa na Waingereza hapa hapa Zanzibar ambao walikuwa wakifaidika kutokana na jasho la watumwa hao na ndio maana utaona kwamba kilichopigwa marukufu na Wazungu ni usafirishaji wa watumwa na si kumiliki watumwa.

Jambo jingine ambalo Waingereza na vibaraka wao wamesahau kulisema ni kwamba huko kwao pia kulikuwa na utumwa ingawaje hakukuwa na Uislamu. Katika hili Waingereza wanajifanya hawatambui juu ya maafa ya Waafrika wa Afrika Magharibi (Nigeria, Ghana, Liberia) waliopelekwa Marekani ya Kaskazini, Kusini na Caribbean ambako nako hakukuwa na Uislamu. Wazungu walipokwenda Marekani waliwenda kwa niaba ya jina takatifu la Ukristo na kwa niaba ya jina la Msalaba, wakawateketeza wenyeji wa huko na kuwafanya watumwa, lakini hilo leo hawalisemi badala yake wanasingizia Uislamu ndio ulioleta biashara ya utumwa.

Njama za kuufanya Uislamu uonekane mbaya Afrika ilikuwa ni kuleta chuki za kugonganisha vichwa baina ya Wazanzibari kwa Wazanzibari, Watanganyika kwa Watanganyika ili kuweza kuwatawala kwa urahisi na kuweza kusambaza dini yao ya Kikristo.

Hilo ndilo lilikuwa na linaendelea kuwa lengo maalumu la kampeni hiyo, ingawa wengi wa Wazungu hao walikuwa na wanaendelea kuwa hata huyo Mungu mwenyewe hawamuamini bali hutumia Ukristo kuwatawala kimawazo na kiuchumi Waafriak tu. Waingereza hawa na vibaraka wao wamesahau kwamba Christopher Columus aliwateketeza Wahindi Wekundu kwa niaba ya Ukristo na kazi hiyo ovu ikaendelezwa na Waingereza mkoloni hadi leo hajatuambia ni kwa nini aliwateketeza wenyeji wa Australia na New Zealand kwa maradhi mbalimbali. Je, wakati wakifanya hayo nao walikuwa ni Waislamu?

Ni bahati mbaya sana kwamba Wazanzibari badala ya kuamka na kuzitamka mbinu za mkoloni za kutugonganisha vichwa Waislamu kwa Waislamu badala ya kukaa kitako na kujaribu kutatua tofauti zetu za kisiasa na nyingine za kijamii, tumezama katika kuendeleza mifarakano.

Jambo jingine ambalo Muingereza na Kanisa wamesahau kuwaambia Waafrika ni kwamba katika biashara ya utumwa Zanzibar Waislamu hawakufanywa watumwa na wale ambao walisimu walitolewa utumwani. Lakusikitisha ni kuona hata wale waandishi na wataalamu wanaodaiwa kuwa wameendelea wametekwa nyara na tafsiri potofu ya utumwa kama ilivyotolewa na Kanisa.

Uislamu hadi leo unapigwa vita sehemu zote ulimwenguni ingawaje leo hazitumiki sababu za utumwa lakini bado kwa kiasi kikubwa zinanasibishwa na matukio ya utumwa. Ni budi Wazanzibari tukumbuke kwamba kwa kutumia Uislamu badala ya tafsiri ya kitabaka aliyoiandaa yeye mwenyewe Muingereza alifanikiwa kuleta chuki na uhasama baina ya wakazi wa visiwa hivi, wakati mwenyewe akishirikiana na kuuhifadhi utawala huo aliouita wa Kiarabu.

Kwa njia hiyo Muingereza alifaulu kutufanya tukabane roho wenyewe kwa wenyewe na kusahau kumpiga vita adui yetu mkubwa ambaye ni yeye na Kanisa lake, kama alivyofanikiwa leo kutugonganisha vichwa kwa masuala ya kisiasa na kuwaacha maadui wetu wakubwa ukizidi kuiangamiza jamii yetu kwa kasi ya kutisha.
Wewe ata historia hujui, mpuuzi muongereza mwenyewe katawaliwa, nenda ujifunze old history utaelewa maana wamarekani wenyewe ni waingereza, wayahudi, waaustralia, wazawa kabisa wa marekani ni red indians ambao ata wao waligeuzwa watumwa na muingereza badae.

Kuna taifa linaitwa,Italia(romani) karibu limetawala dunia nzima ata misri limefika, rudi darasani usituletee historia ya madarasa upuuzi mtupu..!
 
Nimefika mahali nikaona pameandikwa " wazungu na vibaraka wao wa kristo" nikaanzakusoma kwa kuruka ...nikakuta tena "uislam unapigwa vita"....
Niakawa nimeshajua mwandishia ni aina ya watu wanapoona sadaqa imepungua misikitini, wanasema hila za dini fulani, watoto wa kiislam wakifeli shule..hila, majambazi ya kibiti yakitajwa kwa majina ya kiarabu...hila tu hizo..


Nikamuonea huruma sana mwandishi, kwaluwa ninauhakika ataishi maisha yake yote kwa kulalamika! Badala ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yake na hiyo dini yake anayoipenda mnoo!

Cha ajabu hadi siku anakufa atashangaa hao anawalalamikia wanaendelea kustawi....!
 
Kumbe kuna wakati unaweza jitoa ufaham kiasi hiki halafu ukajiaminisha upo sahihi kabisa? Unaweza kuongea uongo mpaka wewe mwenyewe ukaanza kuuamini. Mwandishi anaonesha kuandika kishabiki na kihisia hasa leo hii ni mwendawazimu tu atakayepinga utumwa kuhusishwa na waarabu. Tunakoelekea hata mapinduzi ya zanzibara itakuja sema walipinduliqa wazungu.... Nyie subirini tu.
 
Kumbe kuna wakati unaweza jitoa ufaham kiasi hiki halafu ukajiaminisha upo sahihi kabisa? Unaweza kuongea uongo mpaka wewe mwenyewe ukaanza kuuamini. Mwandishi anaonesha kuandika kishabiki na kihisia hasa leo hii ni mwendawazimu tu atakayepinga utumwa kuhusishwa na waarabu. Tunakoelekea hata mapinduzi ya zanzibara itakuja sema walipinduliqa wazungu.... Nyie subirini tu.
Kwa hiyo mistari minne (4) ya mwisho ... really you've made my day ... yaani nimejikuta nacheka mwenyewe
 
Mleta mada nikuulize!! Je huu utumwa unaoendelea Libya leo nao unasababishwa na makanisa na wazungu??!!! Una defend nini!! Mwarabu au Uislaamu?!

Dunia imepitia history zingine nzuri na zingine mbaya kabisa. Kati ya mbaya iliodhalilisha utu wa mwaafrika ni UTUMWA. Na mnyama aliehusika na biashara hiyo EA ni mwarabu. Huwezi kuwasafisha kwa namna yeyote, kwa kutumia mgongo wa dini. Woote waarabu na wazungu ni washenzi na vibaraka waafrica walioshirikiana nao.

Hizi dini nazo ukizichunguza vizuri ndio zimeendeleza utumwa wa kifikra kwa mwafrika, hata awe tayari kumtoa uhai mwaafrika mwenzie kisa dini.
 
a.
Bravo mjibu hoja. Hivi kalne ya 13 nani mzungu alishafika afrika. Kumbuka Mzungu wa kwanza kuiona Afrika ni kalne ya 14 wakati huo waarabu walishafika na walishaanza chukua watu kwao. Ni wakati huo ndugu zetu walishaanza uzwa uhindini na humu ndani kwa kulipizana visasi. Waarabu hawa ndo waliovunja tawala nyingi za kikabila humu nchini na kuweka watu waliowapa bunduki.
Kalne ya 19 wakati speek anakuja ukisoma kitabu chake utaona jinsi waarabu walivyotamaraki mpaka Uganda. Unaweza kujiuliza kwanini waganda walichukia kiswahili? Lugha ya watumwa. Walie waliotoka pwani wakiitwa waungwana, ni wale wale waliochukuliwa zamani kama watumwa baadaye wakapandishwa vyeo na kuja kuchukua watumwa. Hapo Mjerumani, mwingereza wala mfaransa hajakanyaga. Kumbuka wavumbuzi waliopitia costal kama akina vasco dagama walichukua watu wakufanya kazi kwenye meli wakipewa na watemi lakini wakati huo hawana habari za utumwa ili hali wenzetu waarabu walishajikusanyia watumwa kila wakati. Waliwahasi ndo maana hatuna mazalio kama yalivyo marekani. Mwarabu alikuwa kuadi wa kunununa na kuuza kwa wazungu. Read documents kwenye vitabu vya wachungzi na wale waliopitia East Africa wakati ule. Hata kijijijini kwetu kuna mwembe ambapo waarabu walikuwa wakinununua watumwa toka kwa watemi wale waliowakamata au kuwateka.
Usikurupuke. Karne ya 13 mwarabu bunduki anaitoa wapi. Tangu lini mwarabu anatengenwza bunduki.
Tafuta kitabu kinaitwa the Portuguese period in East Afrika uone ushenzi uliofanywa Na wazungu Na huyo Vasco dagama wako.
 
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali. Moja kati ya njia hizo ni utumwa.

Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.

Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa katika vita, kushindwa kulipa deni unalodaiwa, adhabu kufuatia uhalifu uliotenda n.k.

Wazungu ndio waliokuwa wahalifu wakubwa kabisa katika kuendeleza biashara hii ya utumwa kwa niaba ya msalaba. Kati ya makabila yote ya Kizungu waliotia fora walikuwa ni Waingereza na Wamarekani ambao ni Wakristo wa Kiprotestant na Katoliki ambao leo wanajigamba na kujidai ati ni wao walioondosha utumwa.

Kama tulivyotangulia kusema awali kwamba utumwa ulikuwa ni mfumo wa maisha pale Waingereza walipopendekeza kuondoshwa kwa utumwa ulikuwa ni kwa sababu utumwa haukutia faida tena za kiuchumi na ilibidi ubadilishwe na uzalishaji mali mpya wa kibwanyenye nasio kwa sababu kwamba Wazungu walikuwa na huruma sana na Waafrika.

Kwa njia ya kudau kuondosha utumwa Manuwari na Merikebu za Kiingereza zilidiriki kuchoma na kuteketeza kwa moto madai na majahazi ya wafanya biashara yakiwa na watumwa au la, na matendo yao hayo kubainika na watawala wao. Pengine ajenda ambayo imefichwa hadi leo na Waingereza hao juu ya ukatili wao huo ni kuwa lengo kubwa lilikuwa ni kukata mizizi ya biashara baina ya Afrika Mashariki na nchi za Mashariki ya Bahari ya Hindi.

Kwa kutumia njia hii Waingereza waliweza kuhodhi uchumi wa Afrika ya Mashariki na kuua kabisa biashara baina ya Afrika ya Mashariki na Mashariki ya Bahari ya Hindi biashara ambayo ilishadumu kwa karne nyingi. Wakati Muingereza alidai kupiga vita usafirishaji wa watumwa kutoka Afrika ya Mashariki, upande mwingine aliruhusu uuzaji na uzalishaji mali wa watumwa katika bara la Afrika ya Mashariki na kwa kutenda hivyo aliweza kujinufaisha kisiasa na kiuchumi kupitia biashara hiyo ya watumwa.

Kwa vile Zanzibar ilikuwa ndio kitovu cha biashara katika Afrika ya Mashariki na kati Muingereza aliweza kuuwa uchumi wa Zanzibar na hivyo kumuwiya rahisi kutawala sehemu yote ya Afrika ya Mashariki. Zanzibar iligeuzwa bandari na soko mojawapo maalumu la watumwa, vituo vingine vikiwa sehemu za jirani na visiwa hivi kama vile Bagamoyo na Kilwa.

Pamoja na kwamba Zanzibar ilikuwa ni bandari na soko muhimu la watumwa, hakuna Mzanzibari ambaye alifanywa mtumwa bali watumwa hawa walitoka mabara ama kutokana na kusakwa na wachuuzi wa watumwa wa Kiarabu na wa kienyeji au kutokana na kuwa mateka wa vita baina ya machifu, mapigano baina ya makabila mbalimbali kama vile Wamakonde, Wamakua, Wayao n.k. au ni kutokana na kushindwa nguvu na kutekwa na wenzao.

Kufikia mwaka 1873 Zanzibar ilipiga marufuku biashara ya utumwa lakini cha kushangaza ni kwamba Wareno na Wafaransa waliendelea na biashara hiyo na Muingereza hakunyanyua mkono wkae kuwakemea.

Ingawa sheria ya kukomesha utumwa ilipitishwa rasmi 1873 cha kustaajabisha ni kwamba hadi leo wanasiasa wetu wamekuwa wakiwadanganya wananchi na wageni wanaofika Zanzibar kwamba utumwa uliondoshwa na mapinduzi ya Januari 1964.

Kama neno lenyewe linavyoonyesha, utumwa ni njia mojawapo ya uzalishaji mali ambayo ni kashfa kubwa mtu kunasibishwa nayo na kwa mujibu wa sifa za ubinadamu anayekashifika zaidi ni yule muuzaji wa watumwa hao kuliko watumwa wenyewe, kwani yeye huwa ndio kaonyesha upungufu mkubwa wa kibinadamu kwa kukubali kumuuza binadamu mwenziwe.

Pengine kwa kutambua hili ndio maana Sultan hakutaka kuwaona raia wake wa Zanzibar wakifanywa watumwa. Nchi za Ulaya ambazo leo zinajipa au kupewa sifa za utu bora ndio zinazotumia uzalishaji mali kupitia njia za watumwa na kuyawezesha matabaka ya juu yaliyokuwa yakitawala kujinufaisha kwa kiasi kikubwa. Mfano mzuri wa Waafrika wa Kimarekani (Black American) waliojenga uchumi wa Marekani kwa jasho na damu yao wakati tabaka lao likisehelea katika umasikini.

Wakoloni wote wakiongozwa na Waingereza wamekuwa wakifanya njama za siri na dhahiri za kujifanya wao ni wazuri na kuja kwao Afrika kulikuwa na madhumuni ya kuleta kheri na mafanikio kwa Waafrika pasi na kuwa na lengo jingine lolote.

Njia moja kubwa waliyoitumia ni Makanisa na Mapadri. Wazungu hao walidai kwamba wamekuja kupiga vita ushenzi na kuleta staarabu.

Wakoloni wa Kiingereza mara tu baada ya kuwanyang’anya hatamu wazalia wa Zanzibar na kuuhifadhi utawala wa Kibuu Said walimpa jina ambalo lililokuwa na dhamira ya kuwapa faida zaidi wao.

Waingereza kwa sababu zao waliuita utawala huo kuwa ni wa Waarabu. Lengo la kuuita utawala huo kuwa ni wa Kiarabu lilikuwa ni kuufanya Uislamu uonekane ni mbaya na umekandamiza Waafrika na Wazungu na Ukristo ndio mzuri kwa vile unapiga vita biashara ya watumwa.

Bahati mbaya sana watu wengi hadi hii leo wamenasa katika mtego huo wa Waingereza na wengine pamoja na kusoma kwao kote basi wameshindwa kulielewa lengo na dhamira hii ya Muingereza. Ukweli ni kwamba utumwa ulikuwepo Afrika ya Mashariki hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (as) kwa hiyo hata kabla ya kuja Mtume Muhammad (saw) utumwa ulikuwa umeshaota mizizi ulimwenguni, lakini Waingereza na wakoloni wenzao wa Kizungu kwa kutumia Kanisa wakaufanya utumwa umeletwa na Waarabu kwa lengo lile lile la kuonyesha kwamba Uislamu ndio ulioleta utumwa.

Wakati ambao utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar, Wareno na Wafaransa walishughulika na biashara ya utumwa katika nchi za Mashariki ya Afrika na kazi hiyo walifanya bila ya kuingiliwa kati na Manowari za Kiingereza zilizowekwa maalum kulinda usafirishaji wa watumwa.

Ukweli huu hausemwi na Muingereza wala vibaraka wake wa Kikristo ingawaje wanafahamu kwamba kulikuwa na Waingereza hapa hapa Zanzibar ambao walikuwa wakifaidika kutokana na jasho la watumwa hao na ndio maana utaona kwamba kilichopigwa marukufu na Wazungu ni usafirishaji wa watumwa na si kumiliki watumwa.

Jambo jingine ambalo Waingereza na vibaraka wao wamesahau kulisema ni kwamba huko kwao pia kulikuwa na utumwa ingawaje hakukuwa na Uislamu. Katika hili Waingereza wanajifanya hawatambui juu ya maafa ya Waafrika wa Afrika Magharibi (Nigeria, Ghana, Liberia) waliopelekwa Marekani ya Kaskazini, Kusini na Caribbean ambako nako hakukuwa na Uislamu. Wazungu walipokwenda Marekani waliwenda kwa niaba ya jina takatifu la Ukristo na kwa niaba ya jina la Msalaba, wakawateketeza wenyeji wa huko na kuwafanya watumwa, lakini hilo leo hawalisemi badala yake wanasingizia Uislamu ndio ulioleta biashara ya utumwa.

Njama za kuufanya Uislamu uonekane mbaya Afrika ilikuwa ni kuleta chuki za kugonganisha vichwa baina ya Wazanzibari kwa Wazanzibari, Watanganyika kwa Watanganyika ili kuweza kuwatawala kwa urahisi na kuweza kusambaza dini yao ya Kikristo.

Hilo ndilo lilikuwa na linaendelea kuwa lengo maalumu la kampeni hiyo, ingawa wengi wa Wazungu hao walikuwa na wanaendelea kuwa hata huyo Mungu mwenyewe hawamuamini bali hutumia Ukristo kuwatawala kimawazo na kiuchumi Waafriak tu. Waingereza hawa na vibaraka wao wamesahau kwamba Christopher Columus aliwateketeza Wahindi Wekundu kwa niaba ya Ukristo na kazi hiyo ovu ikaendelezwa na Waingereza mkoloni hadi leo hajatuambia ni kwa nini aliwateketeza wenyeji wa Australia na New Zealand kwa maradhi mbalimbali. Je, wakati wakifanya hayo nao walikuwa ni Waislamu?

Ni bahati mbaya sana kwamba Wazanzibari badala ya kuamka na kuzitamka mbinu za mkoloni za kutugonganisha vichwa Waislamu kwa Waislamu badala ya kukaa kitako na kujaribu kutatua tofauti zetu za kisiasa na nyingine za kijamii, tumezama katika kuendeleza mifarakano.

Jambo jingine ambalo Muingereza na Kanisa wamesahau kuwaambia Waafrika ni kwamba katika biashara ya utumwa Zanzibar Waislamu hawakufanywa watumwa na wale ambao walisimu walitolewa utumwani. Lakusikitisha ni kuona hata wale waandishi na wataalamu wanaodaiwa kuwa wameendelea wametekwa nyara na tafsiri potofu ya utumwa kama ilivyotolewa na Kanisa.

Uislamu hadi leo unapigwa vita sehemu zote ulimwenguni ingawaje leo hazitumiki sababu za utumwa lakini bado kwa kiasi kikubwa zinanasibishwa na matukio ya utumwa. Ni budi Wazanzibari tukumbuke kwamba kwa kutumia Uislamu badala ya tafsiri ya kitabaka aliyoiandaa yeye mwenyewe Muingereza alifanikiwa kuleta chuki na uhasama baina ya wakazi wa visiwa hivi, wakati mwenyewe akishirikiana na kuuhifadhi utawala huo aliouita wa Kiarabu.

Kwa njia hiyo Muingereza alifaulu kutufanya tukabane roho wenyewe kwa wenyewe na kusahau kumpiga vita adui yetu mkubwa ambaye ni yeye na Kanisa lake, kama alivyofanikiwa leo kutugonganisha vichwa kwa masuala ya kisiasa na kuwaacha maadui wetu wakubwa ukizidi kuiangamiza jamii yetu kwa kasi ya kutisha.
VERY TRUE.
 
Ni mjinga tu ndie anaweza kuhusisha utumwa na dini manake historia inaonesha biashara ya utumwa imefanywa na wajasiriamali wa dini zote!!

Kwa Afrika Mashariki, ndio waliendesha biashara ya utumwa lakini ukienda Afrika Magharibi, through Transatlantic Slave Trade ilifanywa na wazungu.
Ni muhimu sana kujua kila anayeandika kitabu au historia Fulani ni nani na ana lengo gani.. Na c kukubali kila kinachoandikwa.
 
Wewe ata historia hujui, mpuuzi muongereza mwenyewe katawaliwa, nenda ujifunze old history utaelewa maana wamarekani wenyewe ni waingereza, wayahudi, waaustralia, wazawa kabisa wa marekani ni red indians ambao ata wao waligeuzwa watumwa na muingereza badae.

Kuna taifa linaitwa,Italia(romani) karibu limetawala dunia nzima ata misri limefika, rudi darasani usituletee historia ya madarasa upuuzi mtupu..!
We ndo mpuuzi Na umelishwa sumu. Husikii wala huoni.
 
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali. Moja kati ya njia hizo ni utumwa.

Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.

Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa katika vita, kushindwa kulipa deni unalodaiwa, adhabu kufuatia uhalifu uliotenda n.k.

Wazungu ndio waliokuwa wahalifu wakubwa kabisa katika kuendeleza biashara hii ya utumwa kwa niaba ya msalaba. Kati ya makabila yote ya Kizungu waliotia fora walikuwa ni Waingereza na Wamarekani ambao ni Wakristo wa Kiprotestant na Katoliki ambao leo wanajigamba na kujidai ati ni wao walioondosha utumwa.

Kama tulivyotangulia kusema awali kwamba utumwa ulikuwa ni mfumo wa maisha pale Waingereza walipopendekeza kuondoshwa kwa utumwa ulikuwa ni kwa sababu utumwa haukutia faida tena za kiuchumi na ilibidi ubadilishwe na uzalishaji mali mpya wa kibwanyenye nasio kwa sababu kwamba Wazungu walikuwa na huruma sana na Waafrika.

Kwa njia ya kudau kuondosha utumwa Manuwari na Merikebu za Kiingereza zilidiriki kuchoma na kuteketeza kwa moto madai na majahazi ya wafanya biashara yakiwa na watumwa au la, na matendo yao hayo kubainika na watawala wao. Pengine ajenda ambayo imefichwa hadi leo na Waingereza hao juu ya ukatili wao huo ni kuwa lengo kubwa lilikuwa ni kukata mizizi ya biashara baina ya Afrika Mashariki na nchi za Mashariki ya Bahari ya Hindi.

Kwa kutumia njia hii Waingereza waliweza kuhodhi uchumi wa Afrika ya Mashariki na kuua kabisa biashara baina ya Afrika ya Mashariki na Mashariki ya Bahari ya Hindi biashara ambayo ilishadumu kwa karne nyingi. Wakati Muingereza alidai kupiga vita usafirishaji wa watumwa kutoka Afrika ya Mashariki, upande mwingine aliruhusu uuzaji na uzalishaji mali wa watumwa katika bara la Afrika ya Mashariki na kwa kutenda hivyo aliweza kujinufaisha kisiasa na kiuchumi kupitia biashara hiyo ya watumwa.

Kwa vile Zanzibar ilikuwa ndio kitovu cha biashara katika Afrika ya Mashariki na kati Muingereza aliweza kuuwa uchumi wa Zanzibar na hivyo kumuwiya rahisi kutawala sehemu yote ya Afrika ya Mashariki. Zanzibar iligeuzwa bandari na soko mojawapo maalumu la watumwa, vituo vingine vikiwa sehemu za jirani na visiwa hivi kama vile Bagamoyo na Kilwa.

Pamoja na kwamba Zanzibar ilikuwa ni bandari na soko muhimu la watumwa, hakuna Mzanzibari ambaye alifanywa mtumwa bali watumwa hawa walitoka mabara ama kutokana na kusakwa na wachuuzi wa watumwa wa Kiarabu na wa kienyeji au kutokana na kuwa mateka wa vita baina ya machifu, mapigano baina ya makabila mbalimbali kama vile Wamakonde, Wamakua, Wayao n.k. au ni kutokana na kushindwa nguvu na kutekwa na wenzao.

Kufikia mwaka 1873 Zanzibar ilipiga marufuku biashara ya utumwa lakini cha kushangaza ni kwamba Wareno na Wafaransa waliendelea na biashara hiyo na Muingereza hakunyanyua mkono wkae kuwakemea.

Ingawa sheria ya kukomesha utumwa ilipitishwa rasmi 1873 cha kustaajabisha ni kwamba hadi leo wanasiasa wetu wamekuwa wakiwadanganya wananchi na wageni wanaofika Zanzibar kwamba utumwa uliondoshwa na mapinduzi ya Januari 1964.

Kama neno lenyewe linavyoonyesha, utumwa ni njia mojawapo ya uzalishaji mali ambayo ni kashfa kubwa mtu kunasibishwa nayo na kwa mujibu wa sifa za ubinadamu anayekashifika zaidi ni yule muuzaji wa watumwa hao kuliko watumwa wenyewe, kwani yeye huwa ndio kaonyesha upungufu mkubwa wa kibinadamu kwa kukubali kumuuza binadamu mwenziwe.

Pengine kwa kutambua hili ndio maana Sultan hakutaka kuwaona raia wake wa Zanzibar wakifanywa watumwa. Nchi za Ulaya ambazo leo zinajipa au kupewa sifa za utu bora ndio zinazotumia uzalishaji mali kupitia njia za watumwa na kuyawezesha matabaka ya juu yaliyokuwa yakitawala kujinufaisha kwa kiasi kikubwa. Mfano mzuri wa Waafrika wa Kimarekani (Black American) waliojenga uchumi wa Marekani kwa jasho na damu yao wakati tabaka lao likisehelea katika umasikini.

Wakoloni wote wakiongozwa na Waingereza wamekuwa wakifanya njama za siri na dhahiri za kujifanya wao ni wazuri na kuja kwao Afrika kulikuwa na madhumuni ya kuleta kheri na mafanikio kwa Waafrika pasi na kuwa na lengo jingine lolote.

Njia moja kubwa waliyoitumia ni Makanisa na Mapadri. Wazungu hao walidai kwamba wamekuja kupiga vita ushenzi na kuleta staarabu.

Wakoloni wa Kiingereza mara tu baada ya kuwanyang’anya hatamu wazalia wa Zanzibar na kuuhifadhi utawala wa Kibuu Said walimpa jina ambalo lililokuwa na dhamira ya kuwapa faida zaidi wao.

Waingereza kwa sababu zao waliuita utawala huo kuwa ni wa Waarabu. Lengo la kuuita utawala huo kuwa ni wa Kiarabu lilikuwa ni kuufanya Uislamu uonekane ni mbaya na umekandamiza Waafrika na Wazungu na Ukristo ndio mzuri kwa vile unapiga vita biashara ya watumwa.

Bahati mbaya sana watu wengi hadi hii leo wamenasa katika mtego huo wa Waingereza na wengine pamoja na kusoma kwao kote basi wameshindwa kulielewa lengo na dhamira hii ya Muingereza. Ukweli ni kwamba utumwa ulikuwepo Afrika ya Mashariki hata kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (as) kwa hiyo hata kabla ya kuja Mtume Muhammad (saw) utumwa ulikuwa umeshaota mizizi ulimwenguni, lakini Waingereza na wakoloni wenzao wa Kizungu kwa kutumia Kanisa wakaufanya utumwa umeletwa na Waarabu kwa lengo lile lile la kuonyesha kwamba Uislamu ndio ulioleta utumwa.

Wakati ambao utumwa ulipigwa marufuku Zanzibar, Wareno na Wafaransa walishughulika na biashara ya utumwa katika nchi za Mashariki ya Afrika na kazi hiyo walifanya bila ya kuingiliwa kati na Manowari za Kiingereza zilizowekwa maalum kulinda usafirishaji wa watumwa.

Ukweli huu hausemwi na Muingereza wala vibaraka wake wa Kikristo ingawaje wanafahamu kwamba kulikuwa na Waingereza hapa hapa Zanzibar ambao walikuwa wakifaidika kutokana na jasho la watumwa hao na ndio maana utaona kwamba kilichopigwa marukufu na Wazungu ni usafirishaji wa watumwa na si kumiliki watumwa.

Jambo jingine ambalo Waingereza na vibaraka wao wamesahau kulisema ni kwamba huko kwao pia kulikuwa na utumwa ingawaje hakukuwa na Uislamu. Katika hili Waingereza wanajifanya hawatambui juu ya maafa ya Waafrika wa Afrika Magharibi (Nigeria, Ghana, Liberia) waliopelekwa Marekani ya Kaskazini, Kusini na Caribbean ambako nako hakukuwa na Uislamu. Wazungu walipokwenda Marekani waliwenda kwa niaba ya jina takatifu la Ukristo na kwa niaba ya jina la Msalaba, wakawateketeza wenyeji wa huko na kuwafanya watumwa, lakini hilo leo hawalisemi badala yake wanasingizia Uislamu ndio ulioleta biashara ya utumwa.

Njama za kuufanya Uislamu uonekane mbaya Afrika ilikuwa ni kuleta chuki za kugonganisha vichwa baina ya Wazanzibari kwa Wazanzibari, Watanganyika kwa Watanganyika ili kuweza kuwatawala kwa urahisi na kuweza kusambaza dini yao ya Kikristo.

Hilo ndilo lilikuwa na linaendelea kuwa lengo maalumu la kampeni hiyo, ingawa wengi wa Wazungu hao walikuwa na wanaendelea kuwa hata huyo Mungu mwenyewe hawamuamini bali hutumia Ukristo kuwatawala kimawazo na kiuchumi Waafriak tu. Waingereza hawa na vibaraka wao wamesahau kwamba Christopher Columus aliwateketeza Wahindi Wekundu kwa niaba ya Ukristo na kazi hiyo ovu ikaendelezwa na Waingereza mkoloni hadi leo hajatuambia ni kwa nini aliwateketeza wenyeji wa Australia na New Zealand kwa maradhi mbalimbali. Je, wakati wakifanya hayo nao walikuwa ni Waislamu?

Ni bahati mbaya sana kwamba Wazanzibari badala ya kuamka na kuzitamka mbinu za mkoloni za kutugonganisha vichwa Waislamu kwa Waislamu badala ya kukaa kitako na kujaribu kutatua tofauti zetu za kisiasa na nyingine za kijamii, tumezama katika kuendeleza mifarakano.

Jambo jingine ambalo Muingereza na Kanisa wamesahau kuwaambia Waafrika ni kwamba katika biashara ya utumwa Zanzibar Waislamu hawakufanywa watumwa na wale ambao walisimu walitolewa utumwani. Lakusikitisha ni kuona hata wale waandishi na wataalamu wanaodaiwa kuwa wameendelea wametekwa nyara na tafsiri potofu ya utumwa kama ilivyotolewa na Kanisa.

Uislamu hadi leo unapigwa vita sehemu zote ulimwenguni ingawaje leo hazitumiki sababu za utumwa lakini bado kwa kiasi kikubwa zinanasibishwa na matukio ya utumwa. Ni budi Wazanzibari tukumbuke kwamba kwa kutumia Uislamu badala ya tafsiri ya kitabaka aliyoiandaa yeye mwenyewe Muingereza alifanikiwa kuleta chuki na uhasama baina ya wakazi wa visiwa hivi, wakati mwenyewe akishirikiana na kuuhifadhi utawala huo aliouita wa Kiarabu.

Kwa njia hiyo Muingereza alifaulu kutufanya tukabane roho wenyewe kwa wenyewe na kusahau kumpiga vita adui yetu mkubwa ambaye ni yeye na Kanisa lake, kama alivyofanikiwa leo kutugonganisha vichwa kwa masuala ya kisiasa na kuwaacha maadui wetu wakubwa ukizidi kuiangamiza jamii yetu kwa kasi ya kutisha.
Nonsense aka upupu....mnatetea vitu visivyo exist. Uislam unafundisha roho mbaya na ndio maana wazee waliopelekwa utumwani uarabuni walihasiwa wasizae na waarabu.
 
Waliwahasi ndo maana hatuna mazalio kama yalivyo marekani. Mwarabu alikuwa kuadi wa kunununa na kuuza kwa wazungu. Read documents kwenye vitabu vya wachungzi na wale waliopitia East Africa wakati ule. Hata kijijijini kwetu kuna mwembe ambapo waarabu walikuwa wakinununua watumwa toka kwa watemi wale waliowakamata au kuwateka.
Hivi kwanini mnapenda kutumia kigezo cha kufahamu some black americans kama ndio kigezo cha kwamba hawa waliwahasi watumwa na wale hawakuwahasi watumwa?!

Hivi leo nikikuuliza unitajie wacheza soka wa nchi za Kiarabu bila ku-Google; utaweza?!

Haya mambo mengine tunatakiwa kutumia common sense kwa sababu hatuwezi kuyapata darasani. Huo uwepo wa black americans tunaotumia kama kigezo ni kwavile tunafuatilia sana habari za Marekani na Ulaya compared na Middle East.

Aidha, huko Ulaya na Marekani ndiko wabobezi kwenye tasnia ya burudani ambayo blacks ni washiriki wazuri na sisi ni wafuatiliaji wazuri!!

Ni kutokana na ushiriki mkubwa wa Blacks kwenye tasnia ya burudani na sisi kufuatilia sana burudani za huko ndicho kinachotufanya leo hii tuwafahamu akina Michael Jackson, Mike Tyson, Eddie Murphy, Whitney Houston n.k!!! Period!

Lakini leo hii hata ukiambiwa utaje waigizaji 3 ambao ni Waarabu kutoka UAE si ajabu utahitaji msaada wa Google lakini unaweza kutaja waigizaji hata 50 ambao ni black americans bila msaada wa Google kwa sababu tunafuatilia filamu za US.

Nini logic ya hiyo hoja?!

In short ni kwamba, hayo mazalio unayoyaona US ni kwa sababu Marekani ipo juu in social activities na Blacks ni major players wa hizi social activities.

Kutokana na hilo, ni lazima utawaona tu!! Ni lazima utawafahamu na kuwasikia! LAZIMA!

In contrast, leo hii ukiambiwa utaje Waarabu 10 tu kutoka Oman bila kujali wanajishughulisha na nini; sidhani kama utaweza unless kama una access to Oman!!!

Sasa ikiwa hata Waarabu wenyewe si ajabu huwafahamu, so, how do you expect kuwafahamu blacks in Arab countries?!

Ukweli ni kwamba, Saudi Arabia ni wabaguzi sana even among Arabs themselves. Hata hivyo, hapa chini ni timu ya soka ya taifa ya Saudi Arabia.
Arabs.png

My first time kuona timu ya soka ya Saudi Arabia ilikuwa 1994... I was very surprised manake zaidi ya nusu ya wachezaji walikuwa 100% BLACK!!!

Hapo juu kuna wengine ni weusi tii... 100% BLACK! But who gives the fvck about Saudi Arabian football? Hii picha hata tukiipeleka kule jukwaa la michezo, kuna uwezekano mkubwa football fans wakashindwa kutaja majina ya hao wachezaji... WHY? Because no one cares about Saudi Arabia soccer!!!

So, if no one cares, unatarajia vipi ufahamu blacks waliopo kule ikiwa hata Waarabu wenyewe hatuwajui?!

Hapa chini ni Saudi Arabia Basketball National Team.

Arabs02.png

Unawaona Wamatumbi wenzetu hao ambao wengine ukikutana nao pale Kariakoo unaweza kudhani wanatoka Kolomije!!!

But ni wangapi wanaweza kutaja any of above players hususani hao Waaabu?! No one cares about Saudi Arabia basketball!!!

Sasa kama tunashindwa kuwafahamu hata national team players ambao ni Waarabu, how do you expect kuwafahamu Blacks?

The problem, for decades now tumekuwa tukilishwa propaganda za Wazungu na ndio maana, mtu anaweza kudhani biashara ya utumwa imefanywa sana na Waarabu kuliko Wazungu wakati ukweli ni kwamba Wazungu wamefanya biashara kubwa sana ya utumwa tena pengine kuliko hata hao Waarabu!!

Above argument is based on the fact that, Transatlantic slave trade was the largest slave trade route na biashara hii iilifanywa na Waafrika wenyewe pamoja na wazungu ambapo watumwa walipelekwa US, Europe na Carribean!

Niliwahi kusoma kitabu kimoja ambacho sikikumbuki ambacho mwandishi aliandika "Waafrika wenyewe walikuwa wanajisikia furaha sana kuuzwa utumwani!" Mwandishi huyo alikuwa anatetea European Slave Traders...

Sasa unaweza kupata picha hawa watu wamebananga mangapi katika kuelezea participation ya wazungu kwenye slave trade?!

Tukiweka unafiki pembeni ukweli ni kwamba Wazungu, Waarabu, Waislamu, Wakristo na jamii zingine; hawa wote wamehusika kwenye slave trade kwa viwango vikubwa sana!!!

Lakini kwavile historia nyingi zimeandikwa na Wazungu, walikuwa wanaandika kwa kuji-favor zaidi huku wakikandamiza upande mwingine!!!

Kwa mfano, watumwa waliokuwa wanapelekwa Mashariki ya Kati wanaandika "Slaves sold to Muslim countries by Muslim Traders!"

Kinyume chake, watumwa waliokuwa wanapelekwa North America, South America, Europe na Carribean katu huwezi kukuta wameandika "Slaves sold to Christian countries by Christian Traders!"

Sana sana kwa wale wanaotaka kupunguza bias ndo wataandika "...sold to European countries by European traders!"

Hiyo ni kuonesha ni namna gani kumekuwa na double standard kwenye uandishi wa historia ya biashara ya utumwa!!!

Na kwa hili, wamefanikiwa manake hata mimi kabla sijawa na uwezo wa kutafuta ukweli mwenyewe; niikuwa nawachukia sana Waarabu lakini baadae nikagundua Waarabu na Wazungu wote ni washenzi tu linapokuja suala la biashara ya utumwa!

Je, America wali-castrate watumwa?!

Hata kama hakuna maandishi yanayothibitisha kwamba Watumwa walikuwa castrated, lakini upo ushahidi unaoonesha moja ya adhabu ambazo ziliwekwa dhidi ya watumwa ni castration. Kwamba, ukileta fyoko fyoko tu, adhabu yako ni kuhasiwa!

That's one but two, according to Encyclopedia of American Race Riots Vol. 1; wazungu hawakuwahasi wenzetu si kwa sababu ni Waznungu walikuwa ni wema sana ukilinganisha na Waarabu bali walitaka kuwa-utilize waliopo!!

Black01.png


Transatlantic slave trade route was very expensive in terms of time and mortality rate. Malaki kwa malaki ya Watumwa walikuwa wanakufa njiani kabla hawajafika America.

Kutokana na hilo, Wajasiriamali wanaotumia akili waliona watumwa ambao tayari walishafika America wawe ndio mbegu ya kuzalishia watumwa wengi zaidi wa kuendelea kuwatumia miongo kwa miongo!!!

Lakini hawakufanya hayo eti kwa sababu Wazungu walikuwa ni watu wazuri!!!
 
Back
Top Bottom