Yuwapi David Kafulila wa Adani?

Mnatumia mbinu za kizamani, kufungua ID kibao kuanzisha thread na kujijibu kafulila hivi kafulila vile. Hakuna positive impact yoyote kwenye hili

Swali rahisi toka mmeanza kufanya hivi faida ni ipi?
 
Huyo/hao wana kazi ya kila siku kufungua ID kafulila hivi kafulila vile alafu hakuna lolote wamefanikisha
 
Ameshakua siku hizi,ni nyani
Nadhani hata nyani ana busara..., tumbili ndio muharibifu anaharibu shamba zima na kututia hasara sisi walimaji hata mwaka ujao tutakuwa tumekufa hivyo kushindwa kulima na yeye kukosa mlo.....

Ni akili finyu sana kuchukua kitu kidogo (hata kama ni kikubwa) kwa kucheza na kitu kama Nishati ambayo ni Moyo wa Uzalishaji / Taifa zima (Impact yake ni kwenye kila sekta)

(Kwahio kama ni kweli on that token kumuita nyani ni kumsifia, bora useme kamekuwa katumbili kajizi na sio vinginevyo); I repeat kama ni kweli amechukua mlungula ili kuliingiza Taifa matatani (At best kwake tuseme alikuwa hajui anachofanya na ni mzembe wa kufuatilia)
 
Sidhani kama unaweza kuja na tathmini ya thamani ya ardhi ya magorofa yaliyovunjwa hapo, watu walioamishwa kwa lazima. Minus social and environmental auditing ya project.

Ni mataahira tu mnaweza shabikia huo ujinga ndio maana wengine atutaki hata ku-comment kwenye mada husika unless tuwe quoted kama hivi.

Ni taahira tu anaeweza shadadia wapangaji wa muda mrefu kuenguliwa na majizi kujenga project za kipuuzi kama hizo.

Zitto aliwahi kituonya huko nyuma huyo jamaa ni mtu wa maslahi kwenye sakata la mafuta ya wese Kigoma.

Kafulila ni chawa mzuri na mwenye kutumia nguvu kuji-promote ujinga ni kusikiliza ujinga wake na kuamini kweli ana kitu kichwani.
 
Atoke kwenye kiota.aje.na.takwimu.zake.za.google amtetee Gautam Adani kenya.wamekataa kumpa.airport yao
 
Sasa Mnataka ufafanuzi gani wabongo?
Mambo ya Adani na Marekani yanawahusu?
Halafu Adani kwani keshapewa huo mradi?
Adani sifa anayopoteza ni Uaminifu kwenye kupata kazi ila sio kwenye kufanya kazi.
Sioni tatizo la huyu muhindi
Kanjibai hajawahi kuwa na ufanisi mzuri hata siku moja bora mchina.
 
Tanzania hata kusema nani anachukia rushwa kwa uhakika ni vigumu, kwa sababu viwango vyetu vya uwazi viko chini sana. Watu wanakwenda kwa ujanjaujanja tu.

Mara ngapi umesikia kiongozi wa umma kapata matatizo kwa sababu mali alizoziandika katika fomu za Tume ya Maadili ya Viongozi ni tofauti na mali zake halisi?

Kuna jamaa mmoja tu yule aliyekuwa mnikulu Gurumo ndiye alipata tabu kwa issue hii, tena kwa sababu ya hela za Rugemalira.

Tena aliondolewa kazini tu, hata hakufungwa.

Sijawahi kusikia mtu mwingine yeyote mtumishi wa umma akiwajibishwa kwa sababu hii.

Na viongozi kama wote tu wamejaza fomu mambo ya uongo mtupu hata kwa kuangalia wanavyoishi tu.

Sasa unaposema Kafulila anachukia rushwa unajiridhisha vipi?

Kama Kafulila anachukia rushwa hivyo kweli, ina maana hakumjua Adani ni mtoa rushwa anayejulikana dunia nzima?
 
Hahaha Tanzania huwa tuna sera yetu ya KUTOKUFUNGAMANA NA UPANDE WOWOTE. Akilazimishwa kusema, atasema HILO NI LAO HALITUHUSU.

Sasa mtu aliisha toa kishika uchumba , halafu ukala, binti unaye unakuja kugundua ni jambazi utafanyaje? unalipa Jambazi mtoto kwa shingo upande, lakini mwali lazima aende hivyo hivyo kishongoupande.

Hizi pesa zinawafikia wao tu duh, kwanini nisiwe rais hata kwa nusu mwaka tu?
 
Hahaha Jambazi hawezi kumkagua Jambazi mwenzake. CCM/Serikali ni wale wale, halafu wote wezi tu.

Unadhani kwanini wanag'ang'ania Madaraka, au unadhani wantupenda saaana wadanganyika?

Ni wizi tu unawaweka pale.
 
Marehemu Magufuli angekuwa hai, angemwambia azinye hizo pesa za Adani.
 
Hahaha Jambazi hawezi kumkagua Jambazi mwenzake. CCM/Serikali ni wale wale, halafu wote wezi tu.

Unadhani kwanini wanag'ang'ania Madaraka, au unadhani wantupenda saaana wadanganyika?

Ni wizi tu unawaweka pale.
Naam,

Unafikiri Kafulila akiambiwa na Rais huyu Adani ni mtu wetu, atatupa mpunga wa kutusaidia kufanyia uchaguzi, Kafulila anaweza kukataa deal?

Unafikiri Kafulila akiambiwa anatakiwa achangishe kiasi fulani kwenye kampeni ya CCM atazitoa mfukoni mwake?

Hivi mnajua CCM huwa inazunguka kwenye taasisi za umma kuchangisha pesa za uchaguzi?
 
Ataanzia wapi kukataa, Kupewa nafasi tu ndani ya CCM ni msaada kwake. Tunafahamu miaka yote CCM hutumia pesa za umma kufanya kampeni na uchaguzi, kununua wapinzani wao na uchafu kama huo. Ndio maana unakuta wateuliwa wa Taasisi za Umma wako very Royal kwa CCM na viongozi wa Serikali kwasababu ya kulinda matumbo yao na familia zao.

Ndio maana watu wanapoimba KATIBA mpya CCM wanaona kama kelele za mbu, wanaingia ndani ya vyandarua wana mute.

Kikwete Alipojaribu akapelekewa Rasimu iliyopitishwa na Bunge la katiba, aliwadanganya wananchi kwamba sasa wataenda kuipitisha Bunge la JMT, mpaka leo, licha ya wao kuichakachua still wanaiogopa kuileta hivyo hivyo. Kwasababu ilikuwa inawapora silaha zao za kukaa madarakani.

Rais anateuwa kila mtu serikalini, hata wajumbe wa bodi ambao huteuliwa na Mawaziri bado hawapiti bila kuangaliwa na Rais, kwasababu Rais ndiye huteuwa mawaziri, ndio maana wajumbe wa tume ya mawasiliano alio wateuwa Nape akiwa waziri, alipopigwa chini, nawao wakapigwa chini na Rais.

Kafulila akiambiwa achangishe anawafuata wadau wote walioko chini ya ofisi yake, Ukumbuki Nape alivyokuwa Bukoba alisema " Naweza kuyafuata makampuni ya simu yakanipa pesa, kwasababu yako chini ya wizara yangu", the same applied kwa watawala wote walioko Serikalini na ndani ya CCM, na hakuna atakaye kataa.

Zamaani walikwa wakiwakamua Wahindi, siyo kwamba wameacha lakini, wao ndio walikuwa wanajulikana wanapesa, lakini siku hizi wafanya biashara wote ndio mtaji wao, ukikataa TRA, Brela, NIDA na taka taka zote wanakufuata kama kifaranga anavyo shukiwa na mwewe au kipanga.
 
Watu wana akili! Unaweza kuwa na mkataba usokuwa na ‘content’!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…