Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,156
- 13,267
Kwa mujibu wa taarifa za ndani ambazo mtandao huu umezipata zinaeleza kwamba jina la Mwenyekiti wa Yanga Yusuf Manji inasemekana limeenguliwa kwenye kinyanganyiro cha kuwania Udiwani Kata ya Mbagala Kuu.
Vyanzo vinaeleza kuwepo kwa mchezo mchafu figisufigisu katika kulikata jina lake, wakati alishinda kwa kishindo kwenye kura za maoni akiomba kuteuliwa na chama chake cha CCM kugombea nafasi hiyo.
Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) leo walijazana kwenye ofisi ya chama hicho mkoa wa Dar es Salaam wakisemekana kukipinga kuenguliwa kwa Manji, huku wakitaka ufafanuzi wa kina juu ya sababu zilizotumika kuliondoa jina lake mpendwa wao.
Hata hivyo mpaka sasa Chama Cha CCM hakijatoa tamko juu ya sakata hilo.
Mtandao huu ulijaribu kufanya mazungumzo na Manji lakini alidai hayuko katika hali yake ya kawaida kutokana na kusumbuliwa na maradhi hivyo hakuwa tayari kuzungumza chochote kwa muda huo na kuomba akimilishe kile kilichompeleka kwenye ofisi za CMM Mkoa.
Baada ya zoezi la kuzungumza na Manji kukwama, mtandao huu ukaona ni vyema kuzungumza na baadhi ya wanachama ambao walikuwa wamepiga kambi kwenye ofisi hizo kusubiri hatma ya mgombea wanaedai ndiye chaguo lao.
Chanzo: ShaffihDauda