Yuko wapi Askofu Josephat Gwajima?

Yuko wapi Askofu Josephat Gwajima?

mshale21

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
2,514
Reaction score
6,070
Wakuu , hivi Askofu Gwajima yuko wapi? Toka usiku wa kuamkia leo alipoonekana akitoa update za wasiojulikana wanaojulikana kama polisi hajaonekana tena!

Je, wametembea nae?

Je, alichochora akapita katikati yao akaenda zake ? Ama namna gani ndugu zangu?
 
Matumaini yangu ni kuona Askofu Gwajima yupo Huru kama Ndege.

Kuhoji haki iko wapi ni wajibu wa kila mwananchi !!!

Lolote Baya litakalomkuta Uvumilivu utatushinda 100% . Tusilaumiane!!!
 
Sio watanzania,sema WATANGANYIKA.
Maana Zanzibar huwezi kuwaletea usengerema kama huu.Mnakumbuka kipindi cha hayati Malim Seif.jamaa pasingekarika
 
Sio watanzania,sema WATANGANYIKA.
Maana Zanzibar huwezi kuwaletea usengerema kama huu.Mnakumbuka kipindi cha hayati Malim Seif.jamaa pasingekarika
Mkuu. Hata Zanzibar ni hayo hayo tu, Tanzania ili ipate uhuru kamili kama taifa labda CDF achoke nq dharma, tofauti na hapo hayupo mwanasiasa, hayupo mtu yoyote yule atakaeweza kuwa against na serikali akawa salama
 
Akijionesha tu, watamtia ndani...
 
Nikiwa kama Mwanahistoria nguli! Huwa nikikumbuka Madikteta wakubwa waliowahi kuisumbua dunia kama akina Adolf Hitler, Benito Musolini, Fransisco Franco, Hideki Tojo, Iddi Amini Dada, na wengineo wengi ambao kwa sasa wamebakia tu kuwa mifupa! Huwa ninapata nguvu na matumaini ya kwamba; hata haya nayo yatapita..
 
Back
Top Bottom