Yondani Mchezaji bora 2012/2013

Yondani Mchezaji bora 2012/2013

Mi nafikiri kipa bora isiishie tu kuangalia magoli machache aliyofungwa.Unaweza kuta kipa kafungwa bao 7 labda,na ligi mpaka inaisha timu yake imeshambuliwa(mashambulizi ya hatari) 10 kwenye mechi alizodaka yeye.Kwa hiyo 70% ya michomo ya hatari ilikuwa magoli kwa timu yake.Huyu kipa sio mzuri ila labda ana mabeki wazuri waliosababisha apate misukosuko michache langoni.

Na mwingine unaweza kuta amefungwa mabao 20 kati ya mashambulizi ya hatari 50 kwenye mechi alizocheza. Kwahiyo amefungwa 40% ya misukosuko yote langoni kwake.Huyu ni kipa mzuri kuzidi yule wakwanza isipokuwa beki yake ni mbovu,inaruhusu sana mashambulizi.

Kwa hiyo tusiishie tu kuangalia magoli machache
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom