Yathibitika: Baadhi ya wanaume hupata mzio (allergy) baada ya kujamiiana!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Daktari mmoja wa Kiholanzi amesema, hivi sasa ana uhakika kwamba, kuna homa ya mapenzi ambayo huwapata baadhi ya wanaume, mara wanapomaliza kufanya mapenzi. Amesema wanaume wanaopatwa na homa hiyo ni wale wa umri wa kati, yaani miaka 35 hadi 50.

Dk. Marcel Waldinger wa hospitali ya Leyenburg jijini Hague, Uholanzi amesema, huenda tatizo hilo limekuwepo kwa siku nyingi lakini wanaume wanaohusika walikuwa hawajui kwamba, linatokana na tendo la kujamiiana. Alisema wenye tatizo hilo, baada ya kumaliza kufanya mapenzi, hupata mafua ya aina fulani, ambayo huweza kudumu hata kwa wiki moja.

Hii ina maana kwamba. Mwanaume mwenye tatizo hili , kila akifanya mapenzi , mafua hayo humjia na hivyo, kama anafanya mapenzi zaidi ya mara moja kwa wiki atakuwa na mafua yasiyoisha. Dk. Marcel ambaye ameongoza utafiti kuhusu maradhi hayo , ambayo ameyaita post-orgasmic illness syndrome, amesema yeye mwenyewe hadi sasa ameshakutana na wanaume watano wenye tatizo la aina hii.

Amebainisha dalili nyingine zenye kuambatana na maradhi hayo ni pamoja na vidonda vya koo, kutoka sana jasho baada ya tendo, kuchoka kupita kiasi baada ya tendon a kuwashwa na macho.

Wale walionijia walisema walihisi mafua dakika chache tu baada ya kumaliza kushiriki tendo. Inakuwa kama vile mtu amepata mafua ya nguvu sana kwa ghaflana hutokea mara tu baada ya kumaliza haja yake. Alisema Dk. Marcel.
Inaonekana kama ni maradhi mapya au ya zamani ambayo watu walikuwa hawajayazingatia. Aliongeza kusema Dk. Marcel.

Akieleza uwezekano wa sababu za tatizo hili, mtaalamu huyo alisema, huenda ni tatizo la kimwili linalotokana na mzio (Allergy) wa aina fulani au ni majibu ya mfumo wa kinga ya mwili kwa kitendo cha kemikali kutolewa mwilini baada ya tendo.

Ni kwamba, mtu anapokuwa kwenye tendo la ndoa na hasa wakati anapofika kileleni, homoni kadhaa huingizwa kwenye mfumo wa fahamu. Kwa hiyo, inawezekana baaadhi ya wanaume wanapata mzio kutoka kwenye homoni hizo.

Kwa kuwa ndiyo kwanza maradhi haya yamebainika, taarifa ya kile kinachoyasababisha na aina ya watu ambao wanaweza kukabiliwa nayo, zinapatikana kwa kadiri siku zinavyoenda kutokana na tafiti nyingi kufanyika.

Binafsi naamini hata rafiki yangu Bujibuji anaweza kutupa ushuhuda wa jambo hili
 
Last edited by a moderator:
Atakuwa amefanya utafiti kwa wanaume wa kizungu as miili yao ni dhoofu;
Wanaume wa Kiafrika sidhani kama wanaweza kuwa na tatizo kama hilo as wako very strong.

Hapana, ukweli ni tatizo ambalo lipo hata kwa wanaume wa KiAfrika. Mara nyingi hutokea unapo jamiiana na partner ambaye ni mpya (inakuwa kama damu zimekataana hivi) au particularly unapo jamiiana na partner fulani tu (na wengineo halikutokei). Na mara nyingi inapotokea mki kiss na kulishana maudenda:) ndo inakauwa 'kosa' kabisa siku ya pili yake homa hiyooo!.

Biinafsi nimekuwa nikionelea kuwa ni tatizo linalo sababishwa na udhaifu wa kinga za mwili (immune) zaidi mwanamme anapojamiiana na baadhi ya partner. Maana kama ndio ulispendi weekend nzima na demu halafu J'matu,J''nne wewe hoi unaaanza kuhisi... hee heee duh!.. demu ameniachia 'ngoma' nini:) teh teh!
 
Atakuwa amefanya utafiti kwa wanaume wa kizungu as miili yao ni dhoofu;
Wanaume wa Kiafrika sidhani kama wanaweza kuwa na tatizo kama hilo as wako very strong.
Mamndenyi, sio kila mwanaume wa ki Afrika yuko strong kama mimi. Wengine wako dhaifu sana, si unamuona jirani yetu Mwita Maranya alivyo? Yaani yale makelele ya mwaJ anayopiga usiku yakiisha, kesho yake Mwita Maranya anaamka akiwa mgonjwa, hoi bin taaban hata kunyanyua mswaki anakuwa hawezi.
 
Last edited by a moderator:
I had similar problem nilipokuwa na miaka 20 ila muda ulivyoenda iliisha yenyewe.. so kwa ujumla nakubaliana na huu utafiti kasoro kwenye umri tu
 
Mmmmh
asante kwa kuniambia,
thatha wale wa kuvaa nguo mpya kila siku
kama akina Mtambuzi na wenzie si ni wagonjwa wa mafua ya kudumu kabisa, looooh.

Hapana, ni tatizo ambalo lipo hata kwa wanaume wa KiAfrika. Mara nyingi hutokea unapo jamiiana na partner ambaye ni mpya (inakuwa kama damu zimekataana hivi) au particular unapo jamiiana na partner fulani tu na si wengineo. Na mara nyingi inapotokea mka kiss na kulishana maudenda:) ndo inakauwa 'worse' kabisa siku ya pili yake homa hiyooo!. Mimi binafsi nimekuwa nikionelea kuwa ni tatizo linalo sababishwa na udhaifu wa kinga za mwili (immune) zaidi mwanamme anapojamiiana na baadhi ya partner. Maana kama ndio ulispendi weekend na demu halafu J'matu,J''nne wewe hoi unaaanza kuhisi... hee heee duh!.. demu ameniachia 'ngoma' nini:) teh teh!
 
Last edited by a moderator:
kelewuiiiiiiiii Bujibuji
ha ha haaaa haaaaa
unaniua mie jamani,
Daaaah, Mwita Maranya nimjuaye au ni mwingine
mmmmh sikuwezi aise.

Mamndenyi, sio kila mwanaume wa ki Afrika yuko strong kama mimi. Wengine wako dhaifu sana, si unamuona jirani yetu Mwita Maranya alivyo? Yaani yale makelele ya mwaJ anayopiga usiku yakiisha, kesho yake Mwita Maranya anaamka akiwa mgonjwa, hoi bin taaban hata kunyanyua mswaki anakuwa hawezi.
 
Last edited by a moderator:
I had similar problem nilipokuwa na miaka 20 ila muda ulivyoenda iliisha yenyewe.. so kwa ujumla nakubaliana na huu utafiti kasoro kwenye umri tu
Mtambuzi hajakosea, wengi wanaopatwa na maradhi haya ni wale wa umri alioutaja Mtambuzi, lakini hata wa umri mwingine waweza kupatwa na tatizo hili ila ni kwa uchache
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
Hebu m - Google huyu Professor ana mautafiti ya ngono ya kufa mtu...

Marcel%20Waldinger.jpg


Dk. Marcel Waldinger

Mana nikawa nafikiria labda ile kitu inakula nini?ndo maana too much hunger
 
Ha,ha,ha,ha,ha,ha,ha,ha,haaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Watu wapunguze kupiga gem au wafanyeje?

Tiba yake nini????
 
Back
Top Bottom