Yapi nizingatie kabla sijalipia kiwanja?

Yapi nizingatie kabla sijalipia kiwanja?

haszu

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2017
Posts
1,475
Reaction score
3,538
Ndo tunaanza maisha, nyumba za kupanga zinachosha, ila matapeli ni mishosho zaidi. Ili niwe salama, nini nizingatie kabla sijalipia kiwanja.. ? Msaada
 
Ndo tunaanza maisha, nyumba za kupanga zinachosha, ila matapeli ni mishosho zaidi. Ili niwe salama, nini nizingatie kabla sijalipia kiwanja.. ? Msaada
Kwa dsn kupigwa hakuna mjanja... ila nakushauri nunua kwa yale makampuni ya viwanja then lipa kwa installment hii itakupa nafasi kujua kama kiwanja ni magumashi kabla hujatoa pesa ndefu
 
Pitia hapa labda unaweza kuokota mawili

 
Usinunue viwanja visivyopimwa.sio lazima ununue ndani ya mipaka ya jiji,unaweza ukatoka nje ya mji.
 
Kwa dsn kupigwa hakuna mjanja... ila nakushauri nunua kwa yale makampuni ya viwanja then lipa kwa installment hii itakupa nafasi kujua kama kiwanja ni magumashi kabla hujatoa pesa ndefu
vile vya serikali hali ikoje ?
 
Kwani vilivyopimwa hakuna matapeli unadhani?

Kuna watu wanaishi maeneo hayakupimwa yenye ukubwa na mazingira rafiki kuliko kukariri viwanja vilivyo pimwa mabwepande.
Usinunue viwanja visivyopimwa.sio lazima ununue ndani ya mipaka ya jiji,unaweza ukatoka nje ya mji.
 
1. Jiridhishe kuwa kiwanja anaekiuza ndie mmiliki
2. Siku ya mauziano uwe na mwanasheria akupe mkataba wa kisheria.
3. Piga picha ikiwezekana videos wakati mnapouziana.
4. Wajue majirani zako.
5. Shirikisha serikali ya mtaa.



Kama hakijapimwa weka beacon mapema mara tu baada ya kununua.

Hzo ndizo steps ambazo ht mm huwa nazifuata na hazijawahi niangusha
 
1. Jiridhishe kuwa kiwanja anaekiuza ndie mmiliki
2. Siku ya mauziano uwe na mwanasheria akupe mkataba wa kisheria.
3. Piga picha ikiwezekana videos wakati mnapouziana.
4. Wajue majirani zako.
5. Shirikisha serikali ya mtaa.
Kama hakijapimwa weka beacon mapema mara tu baada ya kununua.
Hzo ndizo steps ambazo ht mm huwa nazifuata na hazijawahi niangusha
shukran mkuu, je wale ma afisa alsi pia wanaweza fanya utapeli ?
 
Pitia hapa labda unaweza kuokota mawili
ahsante mkuu nimepitia, nimepata kadhaa
 
cha kwanza kama utatumia dalali akisha kuonyesha kiwanja usilipie chukua siku hata tatu nne fika tena kwenye eneo husika uliza majirani ikiwezeka tafuta mjumbe na serikali ya mtaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom