la cezz
JF-Expert Member
- Oct 4, 2013
- 314
- 265
Haya mambo yanafanyika kwa sababu uwanja unaotumika ni mmoja. Kesho Simba au yanga ikimiliki uwanja wake unafikiri kunakomandoo wa Simba au yanga ataenda kulinda uwanja wa mwenzie?Mambo ya Simba na Yanga kama huujui undani wa timu hizi ni afadhali kunyamaza Ndugu yangu...Hivi Ndugu yangu unafikiri kwanini makomandoo wa timu hizi mbili kuhakikisha kuwa 'wanalinda' uwanja siku mbili hivi kabla ya mechi na wakati wa mechi?? unadhani ni masuala au hofu ya vitendo vya ushirikiana peke yake?? Hizi timu usizichezee kabisa...kuna mambo mazito yanafanyika na ambayo ukiambiwa utashangaa...ukizubaa wakati wa halftime wenzako wanakuwahi...Hivi unadhani marefarii huwa wanachezesha fair kwenye timu hizi dhidi ya timu nyingine kwenye ligi kuu??..Chunguza Simba ya sasa inapocheza na timu nyingine za ligi na kama unaujua mpira vizuri utaweza kugundua tatizo lipo wapi...Unadhani kwanini mchezaji wa timu anafanya faulo ya kijinga ya redcard na kutolewa??? Mpira ni fitina ..na hii siyo Tanzania tu bali ni dunia nzima...mkubwa katika soka ana element ya upendeleo kwa asilimia fulani...
Sent using Jamii Forums mobile app