Yanga katika mtihani wa Afrika, APR, Gor Mahia na Mafunzo kazi ngumu

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
Yanga SC.jpg

WAKATI ambapo Yanga ya Tanzania na Vital’O ya Burundi zinacheza nyumbani Jumamosi hii Februari 27, 2016 zikihitaji sare tu kutokana na ushindi katika mechi zao za kwanza za Ligi ya Mabingwa Afrika, klabu za APR ya Rwanda, Gor Mahia ya Kenya na Mafunzo ya Zanzibar ziko katika wakati mgumu.

Gor Mahia ilikubali kipigo cha nyumbani Nairobi cha mabao 2-1 kutoka kwa CNaPS Sports ya Madagascar katika mechi ya kwanza ya raundi ya awali, na sasa inahitaji miujiza ili isonge mbele wakati zitakaporudiana mjini Antananarivo.

Mafunzo yenyewe ina wakati mgumu Zaidi wa kuvuka mbele ya AS Vita Club baada ya kipigo cha mabao 3-0 mjini Unguja na kuwang’oa wakongwe hao wa soka Afrika ni sawa na kupanda mlima Kilimanjaro wakikimbia.

Yanga wao wanacheza nyumbani kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam dhidi ya Cercle de Joachim wakijivunia ushindi wao wa bao 1-0 mjini Curepipe, lakini kama hawatakuwa makini, wanaweza kuadhiriwa na mabingwa hao wa Mauritius.
ZAIDI CHEKI HUKU...
 
Nategemea yanga itafuzu raundi inayofuata bila shaka kutokana na historia inayombeba anapocheza mechi zake uwanja wa taifa.

Natambua pia itapata upinzani wa kuzomewa na baadhi ya mashabiki uchwara wasiotanguliza utaifa mbele na ambao watawashangilia wageni kisa tu eti ni ushabiki na utani wa jadi usio na tija.

Jambo la msingi tu ni kwamba yanga isijaribu kumdharau mpinzani wake kama ilivyofanya kwa jkt mlale. Ikifanya hivyo basi itawashangaza mashabiki wake.
 
Yanga timu yangu ina mambo ya kizamani Sana. Kubana kuonesha mechi wakati tuna mashabiki nchi nzima ni jipu. Michuano mikubwa hii, hakuna sababu nzuri ni kwa nini isioneshwe
 
Yanga hawajiamini.Ndiyo maana wamewanyima washabiki wao wa mikoani kuona mechi.
 
Hawa viongozi wa yanga bhana! yaani akili zao zinawatuma kwamba mashabiki wote wa timu wanaishi dar! haya ndio matatizo ya kuishi kwa kutegemea mapato ya uwanjani. mnafikiri mtamaliza shida zenu zote kupitia mechi hii!

Mmeshindwa hata kuwaiga watani wenu wa jadi kuuza vifaa vya michezo kupunguza utegemezi? sishangai mnaposhindwa kuitisha uchaguzi na badala yake mkiendelea kumsudia huyo mungu wenu wa kihindi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom