Mkimbia kwao huitwa mkimbizi na mdharau kwa hutiwa utumwani. Ukitaka kujua uzuri wa Bongo kumbuka marafiki zako uliocheza nao chandimu au kupikapika, siku za sikukuu kutembelea beach, kula nao lamba lamba, karanga za majambo, wali wa nazi, mtori, ndizi mshale, matoke, ugali na maziwa ya mgando, marafiki zako uliokuwa ukichunga nao ng'ombe na huko machungani kunyonya maziwa ya ng'ombe mnaposikia kiu, pilau siku ya iddi au krismas, nyama choma kwa JF, bia za safari, kilimanjaro na serengeti. Sahau habari za kwenda posta, siku hizi watu wanatumiana sms na e-mails. Kama kuna document muhimu EMS wanakuletea nyumbani kwako. Kila kwenye mjumuiko kuna vyoo vya kulipia kuanzia feri,posta ya zamani, mwenge hadi ubungo mwisho.
Wanasiasa wenye kugushi na kununua vyeti wasubiri wakati wa kampeni, kama anasema ana digrii ya uhandisi akipita anga zao mtwangwe swali la kihandisi. Kisha muulize chuo alichosoma na walimu wake mbele ya kadamsi.
Bado tu bongo si mahala pazuri kwako?