Yamenikutaaa ndugu zangu

Hamjui mnachotaka ktk mahusiano.

Kama ni mapenzi kuweni makini ongeeni kama watu wazima,je umewahi kuongea naye serious?
 
Hiyo window ina virus piga chin weka nyingine.wako wengi ni pm nikupe namba ya dem mmoja anaadabu.
 
Mwanamume kama rijali,unajiamini na unapiga game vizuri hukosi penalti kwa nini ulie lie demu anaposema muachane?achana naye labda kama una weakness zingine.
 
soma alama za nyakati mapema.iyo ni viashiria vibaya sana kama mtakuja anza maisha ya ndoa..pole pambana mwanaume mpaka akuelewe jinsi unavokereka...kama hakusomi piga chini.
 
Mkuu wewe ndo wa kufanya maamuzi magumu! Binafsi nilishawahi kuwa na msichana wa type hiyo. Mkikosona japo kwa jambo dogo, alikuwa anatukana sana kupitia message. Lakini akikaa hasira zikiisha anakuja kuniomba msamaha yanaisha.
Nilijitahidi sana kumuelimisha maana ya safari kimaisha, lakini hakunielewa. Tulifanya mchezo wa kuachana na kurudishiana mara tatu. Nikaja kugundua kumbe alikuwa na uhusiano na mwanaume mmoja mtu mzima ofcn kwao. Japo kazi mi ndo nilimtafutia.
Baada ya hayo nilifanya uamuzi wa kuachana nae, japo alinitukana sana....alifikia hatua hadi ya kuniambia ninaliwa TIGo.
Baada ya miezi mitatu akaanza kunisumbua tena, ati kajifunza kwamba nilikuwa nampenda kweli! Anaomba nimpe chance ya mwisho ( ya nne). Mara ooh we ndo mwanaume ninaekupenda pekee.
Nilihitimisha zoezi kwa shida sana, hadi alipokuja kugundua nimepata mwanamke mwingine.
Ndugu yangu nakushauri achana na huyo mwanamke. Muombe Mungu akupe mwingine, wapo walio tulia kwa aliyetulia pia. All the best!!!!!
 
Kabla ya kuchangia naomba kufahamu
1. Je yeye ni tegemezi kwako?
2. Umewahi kusikia tetesi kama amewahi kua na bwana hapo katikati 2007-date
3. Kabila lake?
4. Umri wake?
Unajua mabinti wengine mnawaweka mjini sana ndo maana wanakua na viburi, lakini kama mmebalance utegemezi wenu its okey

Roughly hakufai, kama hizo kero ni mkabla ya ndoa je utafurahia ndoa yako kweli kwa staili hiyo ya maisha?
 
Huyo dada ananipenda kufa wivu umemzidi mkuu mpaka inakera sana
<br />
<br />
jambo gani linakuonyesha kuwa unapendwa sana,na yote hayo ni wivu 2?kama wewe mkristo soma 1 corinthians 13,utajua upendo ni nini na kama wivu ni upendo,
 
kaka mambo ya mausioano yana mambo mengi sana,ninachoweza kusema kaa chini tafakari, kwetu sisi wakiristo, tunasema marriage is not a word, is a sentence to life, na ndo maana inaitwa pingu za maisha, unaweza kumuoa mambo yakawa magumu sana baadae au mazuri lakini inahitaji ufanye uchunguzi wa kina, ujue kwa nini anasema hivo, kaa na marafki zake, chunguza familia yao, tabia zake kwa ujumla, kama mlikuwa mnakaa vizuri iweje abadilike sasa hivi? kuna mengi sana ambayo yanahitaji moyo wa ujasiri na muda wa kutosha kufanya maamuzi yanayohusu maisha yako yote yaliyobaki hapa duniani!

yangu ni hayo!!!!!!!!
 
Ndugu yangu usisubili inyeshe wakati mawingu unayaona, jitoe katika hayo mausiano, upendo amishia kwa wazazi wako mana wao ndio wanajua thamani yako
 
huyo mwanamke atakutesa saaaaaaana ndani ya ndoa chukua hatua mapema dalili ya mvua ni mawingu!
 
kama yeye ndo anaamua kuwa muachane kwa nini usimwambie tu kuwa unaheshimu maamuzi yake na umwambie imetosha uone kama atathubutu kuendeleza wimbo wake wa tuachane, hata huo wivu hutausikia tena maana anakuchezea akili kwa vile anajua fika kuwa unampenda.
 
Anza mbele. Huyo hakupendi na anakutafutia sababu wewe huelewi. Lazimisha kuingia naye ndani ya ndoa utajaona cha moto.
 
Huyo dada ananipenda kufa wivu umemzidi mkuu mpaka inakera sana

Ulisahasikia wanaume wanasema jamaa anaibiwa mzimamzima sasa ndi hiyo unaibiwa mzimamzima unaona unapendwa... huyo mrembo wako anakuzuga hakuna kitu hapo piga moyo konde aanza maisha upya ingawa ni ngumu kuanza ila inabidi uyafanye hayo usijejijutia huko mbeleni....
 
Za sahizi wanajamii. Ni siku nyingi sijajiunga nanyi lakini leo ninahitaji msaada wenu wa mawazo. Nina uhusiano wa mapenzi na msichana mmoja toka 2007. Ni muda mrefu sana lakini kinachonishangaza moyo wangu unajiuliza mara mbili mbili kumuoa najiuliza sana kwanini. Ila tatizo kubwa ana wivu sanaaa umepitiliza kabisa kiasi kwamba vitu vidogo anasema nimemcheat anataka tuachane bila ushaidi. Kuna kipindi flani nilinyimwa unyumba kwa zaidi ya miezi 8 nikamwambia sitakuja kumuomba unyumba daima.

Kiukweli bado nampenda lakini nakereka sana vitu vidogo anasema tuachane imezidi sana. Kutokana na umbali wa ninapoishi nimejikuta na uhusiano na msichana mwingine ambao si wa mapenzi na huyu dada anatambua kuwa nina msichana. Mwezi wa 7 nilikua nimepanga kumvisha pete huyu mpenzi wangu lakini kabla ya muda kufika akaja ghafla mkoa akakuta msg za yule rafiki yangu ikawa balaa akampigia simu yule dada akamwambia sisi ni marafiki tuu.

Hakutaka kuamini akachukua vitu vyake vyote akaondoka zake. Baada ya siku chache akaanza kupigia simu wasichana wote aliokuta msg zao na kuwaambia vitu vya ajabu ajabu kwamba mimi nina wasichana wengi na mambo mengine machafu sana ambayo siwezi ongea.

Naona story inakua ndefu anyway sasahivi tunawasiliana vizuri ila kila siku napigiwa simu usiku wa manane nikiwa nimelala asubuhi nakutana na messege tuachane kweli nimechoka huu wivu wa hatari. Hebu jamani naombeni msaada huyu dada ananifaa au ndo ntaishia kuchomwa kisu maana ni mcha.....[/QUOTE]

Si afadhali uchomwe kisu ndugu yangu unaweza kuponea chupuchupu. Anaweza akamkata Mr. Kipara huko chini akakuacha huna jinsia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom