Kiluuj
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 692
- 278
Hii sio hadithi, yamenikuta hiyo jana.
Ni siku nyingi sijatembea Tanzania haswa Tanga. Kwa kawaida huwa ninatuma kupitia mabasi ya kutoka humu Mombasa hadi Tanga. Jana nikaamua niende mwenyewe.
Nilipofika Tanga mjini kumbe coaster za kwenda Mgwashi, Lushoto kwa wakwe zangu zimehamishiwa stendi mpya, KANGE. Kwa vile stendi yenyewe siijuwi ikabidi niliache gari langu na kupanda la abiria.
Baada ya dakika kama kumi hivi tukaingia Kange. Sasa kule kubanana kwa abiria nilipatwa na kizunguzungu, hivyo wakati wa kushuka mate yangu yakawa hayawekeki kinywani. Nikajaribu kumeza, ndio kikazidi. Ikabidi NITEME!
Ghafla nikashtukia nimebanwa nyuma! "Mbona unachafua mji?" Kumbe kutema mate mjini Tanga ni CRIMINAL CASE!
Ilinibidi nilipe 50,000 Tsh ndio niwachiliwe.
Niligharamika lakini I wish ingekuwa hivyo Kenya. Hongera Tanga.
Ni siku nyingi sijatembea Tanzania haswa Tanga. Kwa kawaida huwa ninatuma kupitia mabasi ya kutoka humu Mombasa hadi Tanga. Jana nikaamua niende mwenyewe.
Nilipofika Tanga mjini kumbe coaster za kwenda Mgwashi, Lushoto kwa wakwe zangu zimehamishiwa stendi mpya, KANGE. Kwa vile stendi yenyewe siijuwi ikabidi niliache gari langu na kupanda la abiria.
Baada ya dakika kama kumi hivi tukaingia Kange. Sasa kule kubanana kwa abiria nilipatwa na kizunguzungu, hivyo wakati wa kushuka mate yangu yakawa hayawekeki kinywani. Nikajaribu kumeza, ndio kikazidi. Ikabidi NITEME!
Ghafla nikashtukia nimebanwa nyuma! "Mbona unachafua mji?" Kumbe kutema mate mjini Tanga ni CRIMINAL CASE!
Ilinibidi nilipe 50,000 Tsh ndio niwachiliwe.
Niligharamika lakini I wish ingekuwa hivyo Kenya. Hongera Tanga.