Tayana-wog
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 23,144
- 26,651
Mchungaji Msigwa hana hata haki kisheria kufungisha ndoa kwa hiyo hilo kanisa lake analomiliki sijui ni kanisa la wafuasi gani, hata hivyo kama Msigwa na yeye ni Mxhungaji basi Mungu ana kazi ngumu
Sent using Jamii Forums mobile app
Msgwa ni kiongozi wa dini au dhehebu lipi? Kwa maelezo tuliopewa, walioalikwa siyo kila mchungaji/padre/katekista/shehe nk. Waliitwa viongozi wanaoongoza dini au madhehebu yao. Wengi waliofika ni viongozi wenyewe wenye huduma zao kama vile akina Kakobe, Mwingira, Gwajima, nk, au wawakilishi waliotumwa na viongozi wanaoongoza madhehebu mfano Bakwata, RC, KKKT, nk.
Mchungaji Msigwa sijawahi kuisikia huduma yake inayojitegemea. Labda swahi hili lingemhusu mama Lwakatare ambaye ni mbunge na ana huduma yake anayoiongoza.
Bila shaka na babako akiitisha soda na ubwabwa watamsifiaNatumaini mheshimiwa rais aliwapa soda na ubwabwa.
Baada ya kushiba ilikuwa ni lazima wafanye ibada ya kusifu na kuabudu
Sent using Jamii Forums mobile app
Unaweza kuodherasha madhila na matatizo mbali mbali ambayo waumini dini mbali mbali wanayo ?Ni jana tu viongozi wa dini walikutana na Rais ikulu, kwa mwaliko wa Rais. Viongozi hawa wa dini wanaishi na watanzania, kwa fikra za watu wengi, ni kuwa viongozi hawa wa dini wanayajua matatizo ya waumini wao kwa undani.
Waumini wengi walitarajia kuwa matatizo na madhira yao mengi yangelifikia sikio la Mh. Rais kwa kupitia wao. Nina imani Mh. Rais aliwaalika viongozi akiwa na dhamira ya kusikia mapungufu yaliyopo kwenye utawala wake ili aweze kuyafanyia kazi.
Waumini wengi walivunjika moyo pale ambapo viongozi wao wengi wa dinia walipoonekana kuitumia nafasi waliyopewa, kuacha kutoa maoni kuhusiana na matatizo ya waumini wao, na zaidi wakaitumia nafasi hiyo kutafuta recognition kwa Rais.
Wengine wakatumia nafasi hiyo kuelezea jinsi wao walivyo muhimu katika uongozi wa nchi.
Baadhi walienda mbali zaidi na kutamka kuwa Rais alikuwa amechelewa mno kuwaalila, alitakiwa awaalike wakati alipochukua madaraka ili wapange kwa pamoja namna ya kuongoza nchi!
Kwa maoni yangu, mahusiano ya viongozi wa dini kwa serikali yanaishia kwenye kushauri na kuonya. Na pia ni jambo jema kukiwepo mahusiano mazuri kati ya serikali na taasisi za dini lakini siyo kutengeneza urafiki wa kuongoza nchi.
Viongozi wa dini wana majukwaa yao mahekaluni, misikitini na makanisani ambako wanaweza kuwahubiria waumini wao, wakiwemo watawala na watumishi wa serikali. Huko wanaweza kuonya, wanaweza kukemea, wanaweza kushauri, na kusiwepo wa kuwaingilia. Kualikwa na Rais kwaajili kusikia maoni yao, ni matakwa ya Rais, na siyo wajibu.
Viongozi wa dini wasitafute urafiki na watawala wala wasitafute kuwa sehemu ya watawala. Kama watakuwa marafiki wa watawala au watajiingiza kwenye serikali, watapoteza ihalali wao wa kukemea, kushauri na kuonya.
Zaidi ya kutafuta recognition, viongozi wa dini walitumia muda wao mwingi kupongeza juhudi na mambo mema anayofanya Rais. Kupongeza siyo jambo baya kama kuna jambo jema linafanywa. Lakini kupongeza tu bila kushauri kwenye kasoro, hasa zile kubwa, nadhani hata Rais mwenyewe hatakuwa amefaidika chochote toka kwenye hekima ya hawa viongozi wa dini maana siamini kama Rais aliwaalika kwa nia ya kumpongeza.
Kinachoshangaza zaidi, ni viongozi hawa hawa wa dini, ndio wanaotoa kasoro nyingi za utawala wa Mh. Rais Magufuli wakiwa mbali naye. Ni hawa hawa ndio wanaoandika nyaraka kali kali dhidi ya serikali na watawala. Lakini baada ya kuitwa wanachoweza kutamka ni pongezi tu! Tunachojiuliza, yale malalamiko kwenye nyaraka ilikuwa ni tuhuma za uwongo au chuki ya kitotambulika kuwa na wao ni muhimu? Au wanashindwa kunena KWELI kwa sababu ya woga mbele ya mtawala? Au viongpzi hawa ni wanafiki, wanatamka uale wanayodhani aliywewaalika atapenda kusikia? Au pengine yawezekana yale malalamiko ya kwenye nyaraka yalikwishafanyiwa kazi yote?
Kama viongozi wa dini ni waoga, ni nani atakuwa jasiri?
Kama viongozi wa dini ni wanafiki, wanawafundisha nini waumini wao? Rais atawaheshimu vipi viongozi wanafiki?
Au viongozi wa dini wanawashutumu watawala kwa vile watawala hawataki kuonesha kuwa viongozi wa dini ni muhimu sana katika kuongoza nchi?
Au viongozi wa dini hawakujua Rais alikuwa amewaitia nini, pamoja na ukweli kuwa aliwaeleza mwanzoni mwa mkutano wao?
Viongozi wa dini tumewasikia. Tutawadharau kama baada ya kutoka ikulu ndimi zenu zikanena tofauti na tulovyowasikia mkinena mlipokuwa mbele ya Mh Rais.
Sent using Jamii Forums mobile app
...kwa mfano ujasiri gani walikosa !?Ni jana tu viongozi wa dini walikutana na Rais ikulu, kwa mwaliko wa Rais. Viongozi hawa wa dini wanaishi na watanzania, kwa fikra za watu wengi, ni kuwa viongozi hawa wa dini wanayajua matatizo ya waumini wao kwa undani.
Waumini wengi walitarajia kuwa matatizo na madhira yao mengi yangelifikia sikio la Mh. Rais kwa kupitia wao. Nina imani Mh. Rais aliwaalika viongozi akiwa na dhamira ya kusikia mapungufu yaliyopo kwenye utawala wake ili aweze kuyafanyia kazi.
Waumini wengi walivunjika moyo pale ambapo viongozi wao wengi wa dinia walipoonekana kuitumia nafasi waliyopewa, kuacha kutoa maoni kuhusiana na matatizo ya waumini wao, na zaidi wakaitumia nafasi hiyo kutafuta recognition kwa Rais.
Wengine wakatumia nafasi hiyo kuelezea jinsi wao walivyo muhimu katika uongozi wa nchi.
Baadhi walienda mbali zaidi na kutamka kuwa Rais alikuwa amechelewa mno kuwaalila, alitakiwa awaalike wakati alipochukua madaraka ili wapange kwa pamoja namna ya kuongoza nchi!
Kwa maoni yangu, mahusiano ya viongozi wa dini kwa serikali yanaishia kwenye kushauri na kuonya. Na pia ni jambo jema kukiwepo mahusiano mazuri kati ya serikali na taasisi za dini lakini siyo kutengeneza urafiki wa kuongoza nchi.
Viongozi wa dini wana majukwaa yao mahekaluni, misikitini na makanisani ambako wanaweza kuwahubiria waumini wao, wakiwemo watawala na watumishi wa serikali. Huko wanaweza kuonya, wanaweza kukemea, wanaweza kushauri, na kusiwepo wa kuwaingilia. Kualikwa na Rais kwaajili kusikia maoni yao, ni matakwa ya Rais, na siyo wajibu.
Viongozi wa dini wasitafute urafiki na watawala wala wasitafute kuwa sehemu ya watawala. Kama watakuwa marafiki wa watawala au watajiingiza kwenye serikali, watapoteza ihalali wao wa kukemea, kushauri na kuonya.
Zaidi ya kutafuta recognition, viongozi wa dini walitumia muda wao mwingi kupongeza juhudi na mambo mema anayofanya Rais. Kupongeza siyo jambo baya kama kuna jambo jema linafanywa. Lakini kupongeza tu bila kushauri kwenye kasoro, hasa zile kubwa, nadhani hata Rais mwenyewe hatakuwa amefaidika chochote toka kwenye hekima ya hawa viongozi wa dini maana siamini kama Rais aliwaalika kwa nia ya kumpongeza.
Kinachoshangaza zaidi, ni viongozi hawa hawa wa dini, ndio wanaotoa kasoro nyingi za utawala wa Mh. Rais Magufuli wakiwa mbali naye. Ni hawa hawa ndio wanaoandika nyaraka kali kali dhidi ya serikali na watawala. Lakini baada ya kuitwa wanachoweza kutamka ni pongezi tu! Tunachojiuliza, yale malalamiko kwenye nyaraka ilikuwa ni tuhuma za uwongo au chuki ya kitotambulika kuwa na wao ni muhimu? Au wanashindwa kunena KWELI kwa sababu ya woga mbele ya mtawala? Au viongpzi hawa ni wanafiki, wanatamka uale wanayodhani aliywewaalika atapenda kusikia? Au pengine yawezekana yale malalamiko ya kwenye nyaraka yalikwishafanyiwa kazi yote?
Kama viongozi wa dini ni waoga, ni nani atakuwa jasiri?
Kama viongozi wa dini ni wanafiki, wanawafundisha nini waumini wao? Rais atawaheshimu vipi viongozi wanafiki?
Au viongozi wa dini wanawashutumu watawala kwa vile watawala hawataki kuonesha kuwa viongozi wa dini ni muhimu sana katika kuongoza nchi?
Au viongozi wa dini hawakujua Rais alikuwa amewaitia nini, pamoja na ukweli kuwa aliwaeleza mwanzoni mwa mkutano wao?
Viongozi wa dini tumewasikia. Tutawadharau kama baada ya kutoka ikulu ndimi zenu zikanena tofauti na tulovyowasikia mkinena mlipokuwa mbele ya Mh Rais.
Sent using Jamii Forums mobile app
...anawakilisha Taasisi gani ? Je, hiyo Taasisi yake haikualikwa ?Ni sawa na kuuliza Kwanini sheikh Ponda hakualikwa?
Automatically wanakuwa WAPUUZI
Alilalamikia wachungaji wake kuwekwa ndani mara kwa mara na maDC. Mwingira ana tuhuma za kupora ardhi wa wanakijiji na kuhodhi eneo kubwa sana. Ameweka askari/walinzi ambao mara kwa mara hujichukulia sheria mkononi.next time hata Mwingira hatoalikwa, anataka wanaomsifia tu.
Pengo alikuwemo na maskofu wa baraza walikuwepo.Hao viongozi wa dini utakuta ndio Wakina Kakobe, Mwingira, Gwajima, Sheikh yule lakini huwezi kuwaona wakatoliki.
Si kwamba kila kanisa unaloliona linayo haki ya kufungisha ndoa inayotambuliwa kisheria,mengine haki hiyo hayana likiwemo kanisa la Msigwa. Fuatilia