Ya tume ya uchaguzi UDOM

toghocho

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
1,172
198
Katika Kitivo cha Sayansi za Jamii (Social Science) majina ya waliopitishwa kugombea u-raisi wa kitivo ni;

- Philipo Mwakibinga
- Godwin Gonde
- Israel

Tume ya uchaguzi pia imempitisha mtu mmoja tu kugombea nafasi ya makamu wa raisi Social sciences, japo walikuwa wagombea watatu.


Sifa kubwa ya kupitishwa ni kuwa mwanachuo tu, cha ajabu inaonekana kama kinyume cha demokrasia, au labda kuwekana. Waliopo madarakani ndo huwachagua watu wa tume ya uchaguzi, hivyo kuna hiyo possibility.

Na kuna uwezekano wa kuto tokea uongozi huru na bora UDOM kamwe, kwa upande wa federation pia mambo sio mazuri kwani tume imempitisha

- Mwesiga thobias;
Huyu jamaa ndio yule aliyetoa tamko kwamba CHADEMA waombe msamaha kwa kutoka nje wakati presidaa anahutubia.

- abubakar mohamed;
Huyu ni mdogo wake Bashe yule aliyewahi kuambiwa sio raia, ambaye ni mfanyakazi wa Rostam Aziz na kuna tetesi kuwa kapewa mil 5 na Bashe kwa ajili ya ku-take over uongozi.

- Deborah ( ) ambaye pia amekuwa akionekana katika mikutano mikubwa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) hasa wakati wa kampeni za JK.

Nitazidi kuwapa more news wakubwa but for now ndo hayo kifupi mambo sio mazuri.
 
Kitivo cha Elimu mambo ndio mabaya zaidi maana kuna watu makini wameachwa hasa kwenye Uraisi na wanasema tu eti sio wana CCM..
 
Wanafunzi wa UDOM fikirieni kwanza kabla ya kuainaka hapa JF. Tunawachora tu kwa yote mnayoandika humu. Hapa siyo mahakamani kwani kila kitu mnaleta kushitaki hapa. Sisi tunasoma na kuelewa nyie mkoje.
 
Wanafunzi wa UDOM fikirieni kwanza kabla ya kuainaka hapa JF. Tunawachora tu kwa yote mnayoandika humu. Hapa siyo mahakamani kwani kila kitu mnaleta kushitaki hapa. Sisi tunasoma na kuelewa nyie mkoje.

kwani nani kakwambia utoe hukumu? kuna watu makini wanahitaji habari muhimu kama hizi, na yote yanayoandikwa humu kwani huwa unaambiwa u-judge? kama hutaki kusoma, ukiona udom potezea...
 
Back
Top Bottom