WOSIA WA MWISHO (Shairi)

WOSIA WA MWISHO (Shairi)

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
1>laana itaposhuka,nani ataebakia.
Tutaja kumbuka shuka,saa nyumba yaungua.
Wao wameshazinduka,wapi pakukimbilia.
Wangu wosia wa mwisho,kura siyo uadui.
2>ukishindwa we ridhika,tena pembeni tulia.
Mauti yasijefika,taifa kutuchomea.
Eti haki yaitaka,tumbo waliongelea.
Wangu wosia wa mwisho,kura siyo uadui.
3>bila kuruka mipaka,kura yako kuchochea
jivu moto litawaka,kuchoma waso hatia.
Taifa tumelishika,utu tusije achia.
Wangu wosia wa mwisho,kura siyo uadui.
4>kosa tukija lipika,mwiko tutaujutia.
Pishi lilolanika,wanao kuwalishia.
Washiba wataabika,kaa kuwapakulia.
Wangu wosia wa mwisho,kura siyo uadui.
5>jivu litatawanyika,kichwani litaingia.
Kwa mola tutaepuka,njema dua kuombea.
Upendo kutuzunguka,daima milele pia.
Wangu wosia wa mwisho,kura siyo uadui.
Shairi=WOSIA WA MWISHO.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha.
0755519736 Au 0655519736.

eeee mungu mwenyezi mwenye kurehemu,ujalie uchaguzi wa Tanzania uwe wa amani na utulivu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom